Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 20,918
- 30,259
GUNDU LA ADDIS ABABA
Nina bahati mbaya na Ethiopia.
Hili la sanamu halinishangazi
Mara ya kwanza kufika Addis Ababa ilikuwa mwaka wa 1989 mwezi December kuelekea Christmas.
Mwaliko wangu ulikuwa unatokea Nairobi nimetumiwa telex nikachukue tiketi Ethiopian Airways (EA).
Mkosi ulianza siku moja kabla ya safari.
Watu wa Tanga wanaita "gundu."
Tanzania imeshusha thamani ya shilingi.
EA wakanipigia simu kunifahamisha kuwa tiketi yangu inahitaji kuongezwa fedha vinginevyo sitasafiri.
Nikapiga simu Nairobi kuwapa taarifa waongeze fedha kwenye tiketi yangu.
Fedha zenyewe dola ya Mmarekani.
Hii huipata popote ila Benki Kuu na mlolongo wake mrefu sana.
Nairobi ofisi imefungwa kwa ajili ya Christmas.
Safari ikaingia hatihati.
Baba yangu ana travel agency - Sykes Travel.
Nikenda kumweleza tatizo lililonifika.
Palepale akamwamuru Meneja wa Sykes Travel Agent afuatane na mimi hadi AE Mtaa wa Ohio na ahakikishe kuwa naandikiwa tiketi nyingine na yeye atalipa.
Dada yangu Mariam Tewa Allah amrehemu alikuwa akifanya kazi EA dakika tatu hazikufika tiketi ninayo mkononi.
Nilipanda EA kuelekea Khartoum na kulikuwa na transit ya muda mrefu Addis Ababa kutwa nzima hadi siku ya pili mchana ndiyo tunaruka kwenda Khartoum.
Abiria wa daraja la kwanza walishushwa na basi la EA Hilton na si abiria wa kawaida tukapelekwa kulala Wabe Shebele Hotel.
Hii Wabe Shebele ilikuwa hoteli kubwa ya sifa katika wakati wake lakini Mengistu alipompindua Haile Selassie mambo yakaanza kuharibika.
Wabe Shebele ikaporomoka kama ilivyoporomoka nchi nzima.
Kijana wa Kariakoo Hussein Shebe na bendi maarufu The Ashantis walikuwa wakipiga muziki wao hapo Wabe Shebele.
Billy Bandawe alikuwa kiongozi Yanga katika 1980s na mchezaji pia katika miaka ya 1960s alinihadithia kuwa Yanga ilikwenda kucheza na St. Michael ya Ethiopia na timu ilifikia hapo.
Katika wachezaji wa Yanga alikuwa Awadh Gesani.
Awadh Gesani na Hussein Shebe ni ndugu.
Katika moja ya show zake hapo wachezaji wa Yanga walikwenda kumsikiliza Hussein Shebe na Ashantis.
Hussein alipomuona Awadh na wachezaji wengine wameingia hapo ukumbini huku akiimba alishuka kwenye jukwaa akampandisha Awadh na kumtambulisha kwanza kwa Kiingereza kisha akamtambulisha kwa Kiswahili na kuongea maneno mengi ingawa akijua Waethiopia hawajui Kiswahili.
Nilikula chakula cha jioni hapo na nikaliona jukwaa ambalo Hussein Shebe na Ashantis wakipiga muziki wao.
Wabe Shebele imechoka ni kivuli cha hoteli iliyokuwa maarufu.
Nimeletewa Coca-Cola kwenye chupa iliyosagika na kupoteza haiba yake kuwa hii ni chupa ya kinywaji maarufu dunia nzima.
Mkosi ulinikuta barabarani vijana wadogo wa mtaani kama watano hivi walinifuata wakiniomba fedha.
Wakati naingiza mkono mfuko wa nyuma wa suruali mmojawao akachomoa kalamu yangu mfuko wa shati.
Kalamu hii ni Cross ina lifetime guarantee.
Ikiharibika unawarudishia wanakuletea nyingine bure.
Kijana kabla hajanyanyua mguu nikawa nimemdaka.
Safari hii nilikuwa nakwenda ofisi za OAU nikapaone.
Huwezi kuamini.
Ilikuwa mchana wa jua kali.
Nimefika OAU gate ziko wazi.
Naangalia askari.
Hakuna.
Nimepigwa na butwaa.
Nikaona kibanda cha askari pembeni.
Nakakisogelea.
Nikachungulia ndani.
Askari wawili wako ndani wamekaa kwenye viti wamelala fofofo.
Sasa hili la sanamu la Mwalimu Nyerere AU limenikumbusha hawa askari walalavi na mengine.
Nimefika Addis mara tatu na kila safari ina gundu lake la kuhadithia.
University of Khartoum
Nina bahati mbaya na Ethiopia.
Hili la sanamu halinishangazi
Mara ya kwanza kufika Addis Ababa ilikuwa mwaka wa 1989 mwezi December kuelekea Christmas.
Mwaliko wangu ulikuwa unatokea Nairobi nimetumiwa telex nikachukue tiketi Ethiopian Airways (EA).
Mkosi ulianza siku moja kabla ya safari.
Watu wa Tanga wanaita "gundu."
Tanzania imeshusha thamani ya shilingi.
EA wakanipigia simu kunifahamisha kuwa tiketi yangu inahitaji kuongezwa fedha vinginevyo sitasafiri.
Nikapiga simu Nairobi kuwapa taarifa waongeze fedha kwenye tiketi yangu.
Fedha zenyewe dola ya Mmarekani.
Hii huipata popote ila Benki Kuu na mlolongo wake mrefu sana.
Nairobi ofisi imefungwa kwa ajili ya Christmas.
Safari ikaingia hatihati.
Baba yangu ana travel agency - Sykes Travel.
Nikenda kumweleza tatizo lililonifika.
Palepale akamwamuru Meneja wa Sykes Travel Agent afuatane na mimi hadi AE Mtaa wa Ohio na ahakikishe kuwa naandikiwa tiketi nyingine na yeye atalipa.
Dada yangu Mariam Tewa Allah amrehemu alikuwa akifanya kazi EA dakika tatu hazikufika tiketi ninayo mkononi.
Nilipanda EA kuelekea Khartoum na kulikuwa na transit ya muda mrefu Addis Ababa kutwa nzima hadi siku ya pili mchana ndiyo tunaruka kwenda Khartoum.
Abiria wa daraja la kwanza walishushwa na basi la EA Hilton na si abiria wa kawaida tukapelekwa kulala Wabe Shebele Hotel.
Hii Wabe Shebele ilikuwa hoteli kubwa ya sifa katika wakati wake lakini Mengistu alipompindua Haile Selassie mambo yakaanza kuharibika.
Wabe Shebele ikaporomoka kama ilivyoporomoka nchi nzima.
Kijana wa Kariakoo Hussein Shebe na bendi maarufu The Ashantis walikuwa wakipiga muziki wao hapo Wabe Shebele.
Billy Bandawe alikuwa kiongozi Yanga katika 1980s na mchezaji pia katika miaka ya 1960s alinihadithia kuwa Yanga ilikwenda kucheza na St. Michael ya Ethiopia na timu ilifikia hapo.
Katika wachezaji wa Yanga alikuwa Awadh Gesani.
Awadh Gesani na Hussein Shebe ni ndugu.
Katika moja ya show zake hapo wachezaji wa Yanga walikwenda kumsikiliza Hussein Shebe na Ashantis.
Hussein alipomuona Awadh na wachezaji wengine wameingia hapo ukumbini huku akiimba alishuka kwenye jukwaa akampandisha Awadh na kumtambulisha kwanza kwa Kiingereza kisha akamtambulisha kwa Kiswahili na kuongea maneno mengi ingawa akijua Waethiopia hawajui Kiswahili.
Nilikula chakula cha jioni hapo na nikaliona jukwaa ambalo Hussein Shebe na Ashantis wakipiga muziki wao.
Wabe Shebele imechoka ni kivuli cha hoteli iliyokuwa maarufu.
Nimeletewa Coca-Cola kwenye chupa iliyosagika na kupoteza haiba yake kuwa hii ni chupa ya kinywaji maarufu dunia nzima.
Mkosi ulinikuta barabarani vijana wadogo wa mtaani kama watano hivi walinifuata wakiniomba fedha.
Wakati naingiza mkono mfuko wa nyuma wa suruali mmojawao akachomoa kalamu yangu mfuko wa shati.
Kalamu hii ni Cross ina lifetime guarantee.
Ikiharibika unawarudishia wanakuletea nyingine bure.
Kijana kabla hajanyanyua mguu nikawa nimemdaka.
Safari hii nilikuwa nakwenda ofisi za OAU nikapaone.
Huwezi kuamini.
Ilikuwa mchana wa jua kali.
Nimefika OAU gate ziko wazi.
Naangalia askari.
Hakuna.
Nimepigwa na butwaa.
Nikaona kibanda cha askari pembeni.
Nakakisogelea.
Nikachungulia ndani.
Askari wawili wako ndani wamekaa kwenye viti wamelala fofofo.
Sasa hili la sanamu la Mwalimu Nyerere AU limenikumbusha hawa askari walalavi na mengine.
Nimefika Addis mara tatu na kila safari ina gundu lake la kuhadithia.
University of Khartoum