Godbless Lema avuliwa ubunge

Godbless Lema avuliwa ubunge

Status
Not open for further replies.
Acha kauli za kuwatisha watu ww, usicheze na dola na lazima mfuate utawala wa sheria
Sina uhakika kama unajua maana ya utawala wa sheria!!!?
Maana yake ni kwamba hakuna mtu yeyote anayetawala bali sheria (Raia wote ni sawa chini ya sheria)
Hivi kama kina Lowasa na Handrew Chenge wameiba mabilioni ya wananchi lakini bado wanaendelea kupokea posho za ubunge(kodi za watanzania!!, Lema anavuliwa ubunge kwa kutoa lugha za kashfa(si matusi kama LUSINDE) wakati wa kampeni. Hapa ni nani anayefuata utawala wa sheria? wananchi wa arusha tuko tayari kwa mapambano kudai HAKI hata ikibidi kufa.
 
Acha kauli za kuwatisha watu ww, usicheze na dola na lazima mfuate utawala wa sheria
Sina uhakika kama unajua maana ya utawala wa sheria!!!? Maana yake ni kwamba hakuna mtu yeyote anayetawala bali sheria (Raia wote ni sawa chini ya sheria) Hivi kama kina Lowasa na Handrew Chenge wameiba mabilioni ya wananchi lakini bado wanaendelea kupokea posho za ubunge(kodi za watanzania!!, Lema anavuliwa ubunge kwa kutoa lugha za kashfa(si matusi kama LUSINDE) wakati wa kampeni. Hapa ni nani anayefuata utawala wa sheria? wananchi wa arusha tuko tayari kwa mapambano kudai HAKI hata ikibidi kufa. Dume la mbegu+ ccm= UFISADI + UNAFIKI
 
Huyu ndo Namelok Sokoine

namelok sokoine.jpg Mbunge wa Korogwe Mjini Yusuph Nasir (kulia) akiongozana na Mbunge wa viti maalum mkoa Arusha  N.jpg Mbunge wa Korogwe Mjini Yusuph Nasir (kulia) akiongozana na Mbunge wa viti maalum mkoa Arusha Namelok Sokoine
 
Vipi kuhusu Lusinde wakuu? Hii haiwezi kumkumba?

lusinde alikuwa makini yeye hakumgusa kabisa mgombea yaani mheshimiwa mbunge mteule ila kama ccm ingekuwa makini ingelala mbele tena na lema ambaye alimgusa mgombea wao pale arumeru mashariki kwa kumwita sho....
 
kwa wenye data,chaguzi ndogo mfano arumeru inaigharimu serikali sh ngapi?miaka mitano itapita tunakimbizana na chaguzi ndogo tuuu!kodi inapotea,mwananchi haletewi maendeleo wala hatekelezewi ahadi alizopewa,wabunge kutoka vyama vyote watajikuta hawajatekeleza chochote jimboni kwao!hasara kwako,hasara kwangu,hasara kwa kila mmoja wetu,HASARA KWA TAIFA!

kuna wakati msajili wa vyama vya siasa tendwa aliwahi kunukuriwa akieleza kuwa uchaguzi mdogo upiga kiasi kisichopungua shilingi bilioni 19 kutegemeana na ukubwa wa jimbo hivyo kiasi hicho ni kwa jimbo dogo
 
Kuna Mtoto wa Sokoine tayari ni Mbunge; Kuna Mtoto wa Sokoine tayari yuko Ubalozini Canada hataki kukaa bongo Ameishi USA kwa Miaka 6 sasa yuko Canada kwanini Mnawapa hao watoto wa wakubwa; wana Ngo'mbe zaidi ya Elfu, wana nyumba wanasomeshwa na serikali ...

Ni sisi wanyonge tungependa kuwa Wabunge tusaidie wanyonge wenzetu, tusaidie nchi yetu angalau !!!

nnguu007,

..Joseph Sokoine amepigwa marufuku Tanzania na Edward Lowassa.

..adhabu yake ya kuishi nje itaisha pale Edward Lowassa atakapouchoka ubunge wa Monduli.
 
hakuna damu itamwagika Arusha mkuu..........watu wameelewa na tunasubiri kufanya maamuzi yetu kwenye sanduku la kura.....safari hii ni kimya kimya......

Tumuombe Mungu watu wote wa Arusha wawe na mawazo kama ya kwako. Fimbo ya kumuadhibu anayekunyanyasa ni sanduku la kura. Kura ambayo ni siri yako. Kama litafanikiwa hilo bila vurugu nadhani tutakuwa tumefika mahali pazuri sana. Unatoa mkong'oto wa nguvu bila kuonyesha hasira.
 
Sioi Sumari katoka kufiwa juzi tu na Baba yake. Kaachiwa mzigo mkubwa wa kusomesha wadogo zake na kulea familia yake. Ni vema CCM ikaangalia hatima ya Sioi Sumari. Hana kazi jamani! Msaidieni mwenzenu huyu. Arusha ipo karibu na Kenya, ni rahisi kwa sioi kupata kura za wahamiaji.

Acha ile Dada yake alikuwa Miss World Africa Nancy Sumari; Dada Mwingine Mwimbaji kasaini na SONY alikwenda Chadema kugombea Ubunge Chadema hawakumpa sababu alijiunga sababu ya Ubunge akarudi CCM kwa kishindo na kupokelewa na Kikwete pamoja na baba yake kabla hajafariki... sasa wadogo zake gani anasomesha???

Wote wanajitegemea na wana pesa...
 
Acha kauli za kuwatisha watu ww, usicheze na dola na lazima mfuate utawala wa sheria

Hiyo sheria ni ipi? Kama sheria maana yake ni msumeno unaokata kotekote sawia basi ni safi lakini dola inaposaidia kupindisha "Msumeno" ukate upande mmoja. Hiyo nayo utaita kuna sheria ilhali dola inasaidia kupindisha hata yaliyo wazi!!!
Waambia hao wenye dola waangalie Risasi zao zitumike kulinda raia na mali zao siyo kama zilivyotumika Songea, Mahenga na kwingineko ambapo polisi wanaua watu ambao wanapaswa kuwalinda!
 
nnguu007,

..Joseph Sokoine amepigwa marufuku Tanzania na Edward Lowassa.

..adhabu yake ya kuishi nje itaisha pale Edward Lowassa atakapouchoka ubunge wa Monduli.

Kwahiyo atakaa ubalozini kula hela za wananchi wa Tanzania? na Unajua kamtelekeza mkewe kwahiyo ni kusafiri na hela za serikali kila mahali na kinadada mbalimbali

Tatizo ni Lowassa hajui Joseph hataki Ubunge anayetaka Ubunge ni yule anayefanya kazi Ikulu ndio atakechukua kwa Lowassa
 
Sioi Sumari katoka kufiwa juzi tu na Baba yake. Kaachiwa mzigo mkubwa wa kusomesha wadogo zake na kulea familia yake. Ni vema CCM ikaangalia hatima ya Sioi Sumari. Hana kazi jamani! Msaidieni mwenzenu huyu. Arusha ipo karibu na Kenya, ni rahisi kwa sioi kupata kura za wahamiaji.
Siyoi has a super super job that pays him handsomely... Acheni *****
 
Acha ile Dada yake alikuwa Miss World Africa Nancy Sumari; Dada Mwingine Mwimbaji kasaini na SONY alikwenda Chadema kugombea Ubunge Chadema hawakumpa sababu alijiunga sababu ya Ubunge akarudi CCM kwa kishindo na kupokelewa na Kikwete pamoja na baba yake kabla hajafariki... sasa wadogo zake gani anasomesha???

Wote wanajitegemea na wana pesa...
Wale sio dada Zake....... If you don't know just keep kimyakimya
 
Mh, jamani CCM wana mambo yaani nadhani mheshimiwa Hakimu alipata messagi kutoka serikalini kwamba kesi ya lema iishe mara moja ili kuondoa/kujisafisha na aibu ya Arumeru. Sikio la kufa halisikii dawa!:heh:
 
nimepitia threads nyingi na sehemu nyingi ili kuona mawazo ya wanachadema na viongozi wao. nilichoona ni kuwa hawaaamini kama mahakama imetenda haki. bali si hilo tu wamediriki kuhisi kuwa ati mahakama imeamuriwa na ikulu kufikia maamuzi yaliofikiwa


nimesikitishwa sana na watu ambao siku zote hujihesabu makini kwa kauli zao za kuhusisha Ikulu na mahakama katika maamuzi.

inawezekana hukumu haikuwa tamu kwao, na wanahisi hawajatendewa haki, na ndio maana kwenye sheria kukawa na haki ya kukata rufaa ili kuhakikisha haki inatendeka. kwa hio ndugu zangu wa chadema kama mnahisi haki haijatendeka fateni taratibu za kisheria kudai haki zenu badala ya kuhubiri chuki na uongo


ndani ya chadema mna wanasheria wengi tu, watumieni ktk kuhakikisha haki inatendeka. na si kuwa nyny mkishinda tu haki imetendeka mkishindwa haki haijatendeka huko ni kutokuwa watu wa haki.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom