Losambo
JF-Expert Member
- Nov 8, 2011
- 2,611
- 867
Nimepokea sms toka kwa jamaa yangu wa karibu ambaye ni kada mkubwa wa magamba kanidokeza kuwa kuna tetesi chama kimejipanga kumrejesha mgombea mwanamke na chapuo linamwendea Mbunge wa Viti maalumu Ndugu, Dada yetu Nameloki Sokoine. wadau mwasemaje? je huyu dada katolewa kafara ama magamba wanategemea kutumia historia ya baba ya binti huyu, waziri mkuu kipenzi cha watanzania Hayati edward moringe sokoine kwa manufaa yao? sielewi!
Huyo dada namfahamu ni mshenzi sana na sijui alipateje pataje ubunge wa viti maalumu kupitia Monduli!!!!
Akigombea huyo hata kama CDM ikisimamisha kivuli, kivuli kitashinda tu na siyo yeye tu hata JK akija hapa atashindwa maana hata kura zar urais Arusha hazikutosha dhidi ya Dr. Slaa.