Godbless Lema avuliwa ubunge

Godbless Lema avuliwa ubunge

Status
Not open for further replies.
mimi nimeskitika sana hata easter yangu yote imeharibika. ushauri naomba lema asigombee tena badala yake apewe majukumu ya ukatibu mkuu azunguke vijiji vyote kukijenga chama. Dr. slaa akagombee pale arusha mjini kwa hakika atashinda na itakuwa aibu kwa ccm. kwa kuwa 2015 chadema itashinda na kuchukua dola hii mizengwe itakuwa imeisha lema atakuwa na uhakika wa kumiliki arusha ama sehemu yoyote hapa tz. vinginevyo hawa mafisadi wamepanga kuja kuweka pingamizi. hii nchi kikwete ameshaiharibu mkono wa sheria umeegemea upande wa ccm.
 
Post iliyopita kuhusu Polisi nilisema tutalivunja jeshi hilo na kuliunda upya. Kwa haya yanayotokea sasa katika mkondo wa Mahakama, kuna umuhimu wa kuangalia upya uteuzi wa majaji. Hawa wote walioteuliwa kwa kulipa fadhila ya kutetea mazambi ya CCM watapimwa upya na kama wakishindwa waondolewe.

Umuhimu wa katiba mpya ndio unonekana zaidi sasa. Kwamba katiba mpya lazima iainishe namna ya kupata majaji competent wasioteuliwa na Rais.

Wakumbuka mmoja wa wanaotuhumiwa kuhusika na wizi wa EPA sasa ni jaji. Unajua yuko mkoa gani/kanda gani?
 
Nilikuwa na fuatilia kwa umakini kesi hii tangu mwanzo na ingawa si mwanasheria lakini HUKUMU hii ni kama ya Pilato kwa Bwana Yesu,pale ambapo alimtoa Yesu awe kafara kwa ajili ya matakwa tu ya Wayahudi! jaji hakutenda haki hata moyo wake unashuhudia hivyo,Hii ni dalili tosha kwamba tunahitaji katiba mpya ambapo mhimili huu muhimu wa kuleta haki unakuwa Real Independent na sio kiini macho kam wakati huu!

haomajaji wanateuliwa na Mwenyekiti wa CCM na kwa jinsi walivyokamatwa Arusha na CDM na wao hawakupenda ndio wamepitia huko sasa kutekeleza mambo yao.

Peopleeeeeeeeees Powerrrrrrrr-daima tutashinda Arusha
 
Hata CCM wamsimamishe nani, hakuna mtu wakusimama na Lema kwa Arusha Mjini! CDM wasikate rufaa wala nini. Kaka Lusinde, Kuna usemi usemao "The parking spaces infront of bars are for the designated drivers, not the drinkers!" Kama kawa na Arusha mjini kakamue mulemule kama Arumelu tuone. CCM lazima waamini kuwa kila zama na kitabu chake. Huu ni mwanzo tu. nabado 2015 mtashangaaaaaaaaaaa. Wakazi wa Arusha endelezeni mwendo watu wafahamu. Kwataarifa ya CCM baada ya Arusha Kanda ya ziwa inafuatia kwa Mapinduzi. Kama hamuamini subiri utaona 2015 kitakacho wakuta. Hamtaamini.
 
ccm wameanza kuhujum upinzani kupitia mahakama, hata hivyo wanapoteza muda kwani hawana uwezo wa kulitwa hilo jimbo. Kidumu CHADEMA
 
January Makamba.
Wana ccm tumefurahi kuwa uchaguzi wa Arusha utarudiwa....tulijua sisi wanaccm kuwa Lema atashindwa...tumefanya utafiti mitaani na kuona kuwa kesi kwa Bwana Lema angeshindwa..
Walifanya utafiti mitaani na sio kwa wanasheria waliobobea?....... my foot hakuna mzima kichwani CCM nzima, lakini huyu simshangai like father like son!!
 
mwenye habari kamili atupe proceedings za kesi ya Lema . hapa hakuna convinving reportage. naona imeandikwa kimagambamagmba hivi.
 
Nadhani Lema amshukuru Jaji kwani sasa muda wa Ukombozi aliokuwa anausema miaka yote ndio unakaribia kwani Kifo cha CCM kitaanzia Arusha kwenye BY-ELECTION, kwani ARUMERU BADO WAKO MAHUTUTI NA ARUSHA NDIO BYE BYE!!!!!!!! HONGERA KAMANDA KWA KUTOKUWA MBUNGE WA MAHAKAMA AU RUFAA!!!!!!!!!!!!!!
 
UPDATE: Audio imepachikwa hapo baada ya maneno yafuatayo...

Kesi hiyo iliyofunguliwa na makada watatu wa CCM, Mussa Mkanga (55), Happy Kivuyo (49) na Agnes Mollel (44) ambao walikuwa wanamtuhumu Mbunge huyo kwa kutoa kauli za udhalilishaji, matusi na kashifa kwa aliyekuwa mgombea wa Ubunge jimbo hilo kwa tiketi ya CCM, Dkt. Batilda Buriani.

Hukumu hiyo iliyosomwa na Jaji Mfawidhi wa Kanda ya Sumbawanga, Gabriel Rwakibarila.

Katika hukumu hiyo, Lema hakuondolewa haki ya kugombea ubunge huo kwa kuwa kosa lililomtia hatiani ni matumizi mabaya ya lugha tofauti na ilivyodhaniwa kuwa ni vitendo vya rushwa. Uamuzi wa kugombea ama kutokugombea kiti hicho tena utatokana na maamuzi yake mwenyewe na ridhaa ya chama chake ikiwa kitamteua na kumpitisha kugombea.

Taarifa za watu wa karibu zinasema kuwa Lema hatakata rufaa mahakamani juu ya hukumu ya kesi hiyo, bali atakata rufaa kupitia kura ya wananchi wa Arusha Mjini wakati wa kugombea kiti hicho.

Hivyo tutarajie uchaguzi mpya ndani ya siku 90. Tanzania, nchi ya uchaguzi kila uchao...!

Kweli tunahitaji Katiba Mpya yenye kukidhi haja na inayoendana na wakati.
 
kweli ccm inakwenda kufa kifo cha mende pepleeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee poweeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeer
 
Jaji Gabriel Rwakibarila siwezi kuamini umeuza utu wako,taalumu yako kisa Pesa!

Kumbuka Haki haidhulumiwi bali inachelewesha, Damu yeyote itakayomwagika Arusha..itakuwa ya mikono yako!

Kumbuka malipo ni hapa hapa duniani...,leo cheka na mafisadi na hao hao ndio watakaokumaliza, GODBLESS LEMA uliyemdhulumu haki yake ndiye atayekutetea samba samba na mwenzako MAGESSA MULONGO

huna jipya sheria ipo na acha ichukue mkondo wake
 
kisichotakiwa arusha siyo CDM ni Lema ndiye hasiyetakiwa, CDM mnagombanishwa ndani kwa ndani lazima muwe makini zaidi ya mlivyo, hivi leo umwambie Lema asigombee atakubali? na mkampitisha agombee watakuja kumuengua. aisee hii nchi inaongozwa na Mafia
 
nasikia amepigwa marufuku kujiusishana siasa kwa miaka 5
Hapana mkuu, kwa maneno yake Lema mwenyewe, ameseme haki yake ya kugombea Arusha haijatenguliwa na pia hatokwenda mahakamani kuweka pingamizi kwani hakuteuliwa na Mahakama bali alichaguliwa na wananchi. Tamko rasmi la chama litatolewa baadae baada ya kikao cha viongozi wa chama kukaa.
 
Inshalaah wao wameshika serikali, bunge, polisi, jeshi, na wako juu ya sheria lakini LAKINI HAWATAKUWA JUU YA NGUVU YA UMMA HATA SIKU MOJA, KAMANDA LEMA TUKO PAMOJA. Pia chadema fanyeni utaratibu zichangishwe pesa kwa ajiri ya kumsaidia kamanda lema kulipia gharama za kuendesha hiyo kesi, this is M4C until 2015 alwayz.
 
pole sana mb. lema kwani mambo kama haya yanafanyika tz tu. watu wa arusha wamekuchagua lakini wana ccm watatu kwa kushirikiana na mahakama wanaamua kukuondoa!pole sana!
 
Mungu Ibariki Africa,Mungu Ibariki Chadema,Jiwe walilokataa waashi linaenda kuwa jiwe kuu la pemebeni!!
Haki ni haki haihakikiwi na wasio na haki
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom