Ghala la silaha Gongo la Mboto lalipuka!

Ghala la silaha Gongo la Mboto lalipuka!

Matangazo yanaendelea kutolewa TBC na ITV watu waondoke majumbani kwa kuwa haijulikani milipuko itaisha sa ngapi

QN: Waondoke waende wapi?
 
Ni juzi tu tukio kama hili limetokea Mbagala. Ni kwa nini tena ndani ya muda mfupi kiasi hicho? Nchi imekwisha jamani. Tuende wapi? Maisha magumu, bado mnataka kutumaliza na mabomu!!! Na huko gongo la mboto sijui kama kuna umeme sa hizi. Full kukanyagana, watoto kupotea... Oh! Hii ni laana ya kuongozwa na wezi wa kura...
 
Clouds FM wamempigia simu waziri wa ulinzi HUSEIN MWINYI anasema hana taarifa!!!!!!!!1 Anaishi wapi?
Kweli hatuna viongozi, yaani yeye ni mhusika lakini hajui kinachoendelea!
 
Shimbo amethibitisha kutokea kwa milipuko ya mabomu huko Gom's kwenye kambi ya jeshi, ghala no 5 la silaha. Amewaomba wanaoishi jirani wahame kwani hali ni mbaya.

SOURCE TBC TAIFA.
 
Mungu awalinde wote walioko huko...awaepushe na hili janga! Yaani ni mwaka jana Mbagala imetokea...leo Gongo la moto...jamani hata hakuna preventive measures zilizochukuliwa kuepusha haya kutokea tena??!!!!
 
wakuu hali ni mbaya sana huko,kuna jamaaa yangu kaaingia hapa kwangu na familia yake anasema let us pray hard kwa ndugu zetu,Gongolamboto inawaka moto..
 
Jamani the impact is terrible, almost an hour now sijui kwanini wanaweka mabomu mengi hivi mjini?
 
Clouds FM wamempigia simu waziri wa ulinzi HUSEIN MWINYI anasema hana taarifa!!!!!!!!1 Anaishi wapi?

Acha nimemsikia nikatamani niipasue hii redio kwa kweli!! Mungu tuifadhali na utuponye na mabomu haya!!
 
jamani, kuna kipande cha bomu kimeingia ndani ya uzio wangu, nimechanganyikiwa hata kukimbia nimeshindwa maana ntaibiwa kila kitu

Mh we lazima una damu ya kule kwetu yaani u bora ufariki dunia kuliko kuibiwa!!!
Pole lakini
 
Clouds FM wamempigia simu waziri wa ulinzi HUSEIN MWINYI anasema hana taarifa!!!!!!!!1 Anaishi wapi?

hana taarifa maana yake nini? Yeye si ndio waziri wa ulinzi?....familia yangu ikiathirika kwa namna yoyote ile nakuwa suicide bomber halafu nalipuka nae....sh***i taipu.
 
mkuu ... hizi ni nini ..au unaongea huku unakimbia mabomu

Nshaedit mkuu, moyo ulikuwa unanienda mbio hata sikuangalia kabla ya kupost. Wanadamu mko makini kweli. Thanx!
 
we bwan kwan uko wap?km haupo bongo bas bongo yote mtikisiko
nyumba teteme teteme

jamani jamani....take care dear....usije ukaharibika.....nasikia hata huko mitaani hakufai....jam ni ya kufa mtu....ooooh noooo.....Mungu aturehemu Watanzania
 
Hiyo ni main storage ya vifaa vya jwtz na tabia ya kulipuka mabomu stoo ni kwamba linaanza moja linaambukiza jingine kwa hy hapo ni kwamba hadi yaishe yote na joto lipungue ndo usalama. Vingenevyo yataendelea kulipuka hadi yaishe. Nasikitika hapo kuna mali za mabilioni za jeshi hadi magari yote ya akiba yanayowekwa kwa ajili ya emergency. Uzembe umezidi sana hii nchi jamani loh!

Sasa isije ikawa watu wamejitengenezea mazingira ya kuvuta hela...emergency procurement ya Jeshi ku-replenish kilichopotea.....Uchunguzi ni lazima ufanyike kwa makini kuangalia nini haswa chanzo...wasisingizie mvua za hivi karibuni..
 
Back
Top Bottom