Ghala la silaha Gongo la Mboto lalipuka!

Ghala la silaha Gongo la Mboto lalipuka!

ghala la mabomu kambi ya jeshi gongo imelipuka.soure ninashuhudia live.
 
Jijini kunasikika milipuko mkubwa...taarifa zinasema ni mabomu eneo la Gongo la Mboto. Tupeane taarifa sahihi tafadhali kwa wenye nazo.
 
Yanasikika hata huku Ubungo, pia nimeongea na mtu yupo Jet , hofu ipo kwammba uwanja wa kimataifa wa ndege wa mwalimu nyerere utaathirika. Chanzo bado kujulikana, ni moto na ngurumo kama Afghanistan.
 
Nimepata habari sasa hivi kuwa milio ya milipuko inasikika Dar. Mwenye habari zaidi atujuze tafadhali.
 
jamani, kuna kipande cha bomu kimeingia ndani ya uzio wangu, nimechanganyikiwa hata kukimbia nimeshindwa maana ntaibiwa kila kitu
 
nipo tegeta ... nasikia milio ya ngurumo
 
Hata mie nimesikia hebu tuhabarisheni nasikia ni maeneo ya Mbagala
 
Ni kweli, hata sasa yanaendelea. Nimeambiwa na rafiki yangu aliyeko Buguruni kwa simu kuwa, yanalipukia Gongolamboto mwisho wa lami.
 
Hii nchi inabidi tupigane vita ya wenyewe kwa wenyewe ili haya mabomu yapate matumizi..... Hivi jeshi la wananchi linafanya nini?
Better be careful with ur words. Sidhani kama walio vitani walitamani au walihitaji kutumia stock ya silaha zao.
 
daah jamani hko gongo la mboto,hali inatisha..tuambieni nn kinaendelea.
 
hata hapa mabibo kuna moto unawaka angani kuna mwanga mkali na cheche.nadhan ni kambi ya makuburi
 
Inasemekana ni gongo la mboto, wenye taarifa zaidi tafadhali!!
 
mitandao ya simu iko down....sms haziendi wala simu hazipigiki...kaazi kweli kweli.
 
Milipuko ipo na inasemekana inatoka katika maeneo ya kambi za jeshi, source tbc taifa radio imetangazwa sasa hivi saa 3.02 usiku huu.
CCM watakua wamejipakulia silaha idadi gani kabla ya kuwasha ghala yetu moto??

Maana tunazo taarifa za ndani jinsi wanavyopanga maandalinzi ya kuwapa vikundi vya kihuni kama alivyofanya Dikteta Mubarak Misri kushambulia Nguvu ya Umma wakifanya mapinduzi ya kizalendo????
 
Back
Top Bottom