Ghala la silaha Gongo la Mboto lalipuka!

Ghala la silaha Gongo la Mboto lalipuka!

Hivi kwani viongozi wa TZ huwa hawawajibiki jamani??? Sijawahi kuuona nchi ambayo viongozi wake hawako respnsible kwa yanayotokea...jana Kova anaanza kulaumu wananchi ..eti wanakimbia hovvyo so inaweza ikaleta madhara makubwa...wananchi wangefanyaje sasa??? hakuna taarifa rasmi ya kuwaelekeza cha kufanya...halfu unaanza kuwalaumu!!! I hate these leaders for what they are doing....:A S 20::A S 20::A S 20:
 
Thanx for the information mkuu Pdidy. Hakika unajitahidi kutujuza mkuu.
 

JESHI LA ULINZI LA WANANCHI WA TANZANIA

Tarehe 16 February, 2011

PRESS RELEASE
Mlipuko wa bomu umetokea katika kambi ya Jeshi iliyopo eneo la Gongolamboto tarehe 16 Februari, 2011 muda wa saa mbili na dakika ishirini usiku. Mlipuko huo wa kwanza umesababisha milipuko mengine. Chanzo chake bado kinachunguzwa. Jeshi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya Ulinzi na Usalama linaendelea kuchukua hatua za usalama katika eneo la ajali. Wananchi wanashauriwa kutokusogea karibu na eneo la tukio wala kugusa kitu wasichokifahamu. Vile vile wanaombwa kutoa ushirikiano kwa Jeshi au vyombo vingine vya Ulinzi na Usalama na kutoa taarifa za mabomu na risasi zitakazoonekana katika maeneo yao. Jeshi linatoa masikitiko kwa madhara na usumbufu uliotokea kwa wananchi wa Dar es Salaam na hasa waliopo karibu na eneo la tukio.


Imetolewa na Kurugenzi ya Habari na Uhusiano, Makao Makuu ya Jeshi, Upanga
SLP 92023, Simu: 0764 7421621
Email:ulinzimagazine@yahoo.co.uk
 
Sidhani kama kuna mtu anatakiwa ajiuzulu huo utakuwa ni uzezeta kutaka kiongozi wa juu ajiuzulu ,mbona sehemu nyingi tu duniani kulipuka kwa maghala ya silaha ni jambo la kawaida.

Mara mbili ndani ya miaka miwili haikubaliki. Lazima tushinikize Waziri wa Ulinzi ajiuzulu tu. Unataka maghala mangapi yalipuke ndio ujue ameshindwa kazi???
 
Hivi kwani viongozi wa TZ huwa hawawajibiki jamani??? Sijawahi kuuona nchi ambayo viongozi wake hawako respnsible kwa yanayotokea...jana Kova anaanza kulaumu wananchi ..eti wanakimbia hovvyo so inaweza ikaleta madhara makubwa...wananchi wangefanyaje sasa??? hakuna taarifa rasmi ya kuwaelekeza cha kufanya...halfu unaanza kuwalaumu!!! I hate these leaders for what they are doing....:A S 20::A S 20::A S 20:
- TBC ILISEMA WALITANGAZA WATU WAONDOKE HARASA SANA
- ITV WATU WAKIMBILIE MABONDENI
- ITV/CHANEL 5 WASIKIMBIE HOVYO
- tv ZINGINE WALIONYESHA MZIKI TUUU!
-TBC GHALA LINALOLIPUKA NI NAMBA 5 LINAUWEZO WA KWENDA 10KM
HALAFU HAWASEMI 10KM ZINAKOVER MAENEO GANI!? NCHI INAMATAAHILA HII!
PUMAVU ZENU SAANA, MNATUCHANGANYA KAMA ILIVYOKUWA DOWANS
 
Ni vizuri mkuu akuna kitu mbaya kama kuwaleta abiria airport ukijua ama kuna dharura ama ndege yako airuki hili limeleeta heshima kwa nchi za wenzetu nahisi ni wakati na sisi kujirekebisha na kujali utu na hela yake anapokulipa...wapo vijibiti vinaajiriwa kuuza tkt lakini ikitokea emergency samahani siwatukan mnakuwa bogas kabisa..na mbaya mnashindwa hata kusachi namba za simu kwenye tkt systemna kumpigia mteja...mnaishia kupiga stiory za umbea na upashu amjui mnaicost kampuni zenu hasa mteja anapojua mlijua tatizo amkumjulisha..ni vyema tubadilike wakati huu wa majonzi tukiwakumbuka wenzetu waliokula valentine pamoja na sasa kila mtu amekufa kivyake

Mwanga wa Milele uwangazie ee bwana Wapumzike kwa amani....na wote tuseme
AMEN
 
watu 200 waliokufa umewatoa wapi?


nakupa kazi ndogo mtafute deo ryunga anijui simjui yeye alikuwepo kwa tukio..ndugu yangu yuko huko kwenye emergency ntakupa namba yake akiniruhusu baada ya kuwatibia akujuze zaidi...

Shika neno

tenda.......
 
Zamani mwalimu J K Nyerere na hata mawaziri wake walipokuwa wakitoa tamko lilikuwa ni amri na utekelezaji wake ulikuwa mara moja. sasa sielewi Tanzania ya leo inaongozwaje. Yalipotokea ya Mbagala matamko mengi tu yalitolewa na wakubwa lakini hakuna hata moja lililotekelezwa hasa hili la kuchukua tahadhali milipuko isijurudie. Tumechoka siasa na sasa ni taaluma tu ndiyo inayotakiwa kutawala, nafikiri wakati wakuingia mitaani umefika. Yamewezekana misri hata huku yatawezekana
 
Kuna mwanajshi tunaishi naye jirani alituambia jana wakati mabomu yakilipuka kuwa, JK alijulishwa hali hiyo tangu mchana ili asaini document kuruhusu yaharibiwe, badala yake akaenda zake Tangu kula Maulid! Jamani huyu kilaza tumfanye nini? Poleni wafiwa na mliojeruhiwa kwa namna yoyote nawatakia mpone haraka tuendelee kulijenga taifa letu!
 
leo asubuhi 12.00am BBC walikuwa wanasema 10 na Radio one saa 1 asubuhi wamesema 13 kutoka Hospital ya Amana

Lakini inawezekana wakafika 200 maana waliokufa kwenye tukio hawajahesabika

Amana saizi wanasema walio kufa wamefika 14
 
Makamba alisema hapa duniani sio peponi, matatizo tuliyonayo ya umeme, matokeo ya form na gharama za maisha kupanda ni ya kawaida tu. Kweli jamani? Hata hili la mabomu yetu kutuua wenyewe? wanajeshi hawana kazi yoyote zaidi ya kulinda vitu ambayo haipo kwa sasa, kila siku wako makambini inakuwaje mabomu yanalipuka ovyo, hapana hii haikubaliki. Lazima tuwawajibishe wahusika.
 
Serikali yetu bado iko enzi za ujima... why 3days ni nini ambacho hawawezi kifanya in one day shughuli zikaendelea kama kawaida.
Ina maana hata wanajeshi wetu ni ovyo tu.
 
"sikilizeni na msome kwa makini.... hii crises imeanzia southen part of Tanzania(Mbagala) inaelekea Southen-North ... katika ukanda huo kuna External, inaelekea Nyumbu maeneo ya kibaha, Changanyikeni ndo inashuka Lugalo.HII NI KWA SABABU WAKOLONI wALIANZIA kuyaweka Mbagala na kuelekea sehemu hizo. so get prepared"

one of my friend nilikuwa nachat naye huko FB kanipa ujumbe huu, yawezekana kuna kaukweli vile!!

Lady N,

There is no such a thing as Southern North.
 
Explosions at an ammunition depot at Mbagala army base in spring 2009 killed at least three people.

hii yakweli au BBC wanapotosha kuhusu 2009? yaani walikufa angalau watu 3 tu??
 
nakupa kazi ndogo mtafute deo ryunga anijui simjui yeye alikuwepo kwa tukio..ndugu yangu yuko huko kwenye emergency ntakupa namba yake akiniruhusu baada ya kuwatibia akujuze zaidi...

Shika neno

tenda.......

Nipe numba yake nitwangie
 

JESHI LA ULINZI LA WANANCHI WA TANZANIA

Tarehe 16 February, 2011

PRESS RELEASE
Mlipuko wa bomu umetokea katika kambi ya Jeshi iliyopo eneo la Gongolamboto tarehe 16 Februari, 2011 muda wa saa mbili na dakika ishirini usiku. Mlipuko huo wa kwanza umesababisha milipuko mengine. Chanzo chake bado kinachunguzwa. Jeshi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya Ulinzi na Usalama linaendelea kuchukua hatua za usalama katika eneo la ajali. Wananchi wanashauriwa kutokusogea karibu na eneo la tukio wala kugusa kitu wasichokifahamu. Vile vile wanaombwa kutoa ushirikiano kwa Jeshi au vyombo vingine vya Ulinzi na Usalama na kutoa taarifa za mabomu na risasi zitakazoonekana katika maeneo yao. Jeshi linatoa masikitiko kwa madhara na usumbufu uliotokea kwa wananchi wa Dar es Salaam na hasa waliopo karibu na eneo la tukio.


Imetolewa na Kurugenzi ya Habari na Uhusiano, Makao Makuu ya Jeshi, Upanga
SLP 92023, Simu: 0764 7421621
Email:ulinzimagazine@yahoo.co.uk

Jamani hata kwenye hii release mnadanganya kuwa mmeichapa jana usiku? nani alikuwa kazini? Kuweni makini hata japo kidogo?
 
Back
Top Bottom