Ghafla chuki na dhihaka dhidi ya waalimu zimeongezeka mitandaoni na mitaani, chanzo ni nini?

Zanzibar-ASP

JF-Expert Member
Nov 28, 2013
10,129
35,148
Huenda labda mambo ni mengi au yako kasi kupita maelezo mpaka yamenipita au nimeshindwa kuyaelewa. Hili la kuibuka ghafla mitandaoni na mitaani, chuki na dhihaka dhidi ya waalimu bado sijalielewa kabisa.

Nimehisi huenda labda limeletwa na mojawapo kati ya haya mambo mawili lakini bado sioni muunganiko wa moja kwa moja.

1. Walimu kuwepo kwenye orodha ya makarani wa sensa huku watu wengi wasiokuwa na kazi kukosa. (Binafsi sioni kama hili lina uzito mnoo, kwa kuwa tangu hapo awali kama jadi miaka yote, zoezi la sensa hufanywa zaidi na walimu kama ilivyo suala la uchaguzi)

2. Nyongeza ya mishahara iliyotangazwa ilivyotumika kuwalaghai watumishi wa umma na mwisho wa siku watumishi wamekuja kugundua kuwa wametapeliwa na serikali! (Sijui walimu kipekee linawagusaje? Labda wao ndio walilishabikia zaidi hapo kabla? Ama huenda walimu wamefaidika na hii nyongeza kuliko kada zingine? Au walimu hawajaona tatizo na wamepongeza hii nyongeza?)

Wenye ufahamu zaidi wanaweza kutusaidia katika hili fumbo, nini chanzo cha kuibuka ghafla kwa chuki na dhihaka dhidi ya waalimu hapa Tanzania?
 
Tunamalizia hasira zetu kwa kutuchapia wanetu kisa hawajanunua visheti vyao. Just kidding 😃😃
 
Huenda labda mambo ni mengi au yako kasi kupita maelezo mpaka yamenipita au nimeshindwa kuyaelewa. Hili la kuibuka ghafla mitandaoni na mitaani, chuki na dhihaka dhidi ya waalimu bado sijalielewa kabisa.
Tupe mtazamo wako🤔
 
Huenda labda mambo ni mengi au yako kasi kupita maelezo mpaka yamenipita au nimeshindwa kuyaelewa. Hili la kuibuka ghafla mitandaoni na mitaani, chuki na dhihaka dhidi ya waalimu bado sijalielewa kabisa.

Nimehisi huenda labda limeletwa na mojawapo kati ya haya mambo mawili lakini bado sioni muunganiko wa moja kwa moja.

1. Walimu kuwepo kwenye orodha ya makarani wa sensa huku watu wengi wasiokuwa na kazi kukosa. (Binafsi sioni kama hili lina uzito mnoo, kwa kuwa tangu hapo awali kama jadi miaka yote, zoezi la sensa hufanywa zaidi na walimu kama ilivyo suala la uchaguzi)

2. Nyongeza ya mishahara iliyotangazwa ilivyotumika kuwalaghai watumishi wa umma na mwisho wa siku watumishi wamekuja kugundua kuwa wametapeliwa na serikali! (Sijui walimu kipekee linawagusaje? Labda wao ndio walilishabikia zaidi hapo kabla? Ama huenda walimu wamefaidika na hii nyongeza kuliko kada zingine? Au walimu hawajaona tatizo na wamepongeza hii nyongeza?)

Wenye ufahamu zaidi wanaweza kutusaidia katika hili fumbo, nini chanzo cha kuibuka ghafla kwa chuki na dhihaka dhidi ya waalimu hapa Tanzania?
Binafsi inaniuma sana nikiona walimu wanasemwa vibaya..

Sijajua Baba wa taifa huko alipo anajisikiaje

Mkombozi wa taifa letu hakuwa daktari,injinia muhasibu,hr n.k isipokuwa mwalimu

Tuwaheshimu sana
 
Huo nimkakati wa team Kazi Iendelee ili kuwachonganisha walimu kwa wananchi iliwaonekane ni waroho wa pesa.
 
Binafsi inaniuma sana nikiona walimu wanasemwa vibaya..

Sijajua Baba wa taifa huko alipo anajisikiaje

Mkombozi wa taifa letu hakuwa daktari,injinia muhasibu,hr n.k isipokuwa mwalimu

Tuwaheshimu sana
Na siyo Tanzania pekee, Walimu au watoto wa Walimu wameongoza harakati za Uhuru kwenye mataifa mengi ya Afrika.Mfano, Dr.Kenneth Kaunda alikuwa mtoto wa Mwalimu.

Ni dunia ya sasa tu isiyo na adabu ndo inaona Walimu ni watu wa hovyo.
 
walimu hufanya kazi kama hizi kwa weledi mkubwa sana kulinganisha na hao jobless ambao wengi huharibu kazi na huna pakuwapata hasa kwa kazi sensitive kama hizi
Tatizo limeanzia kwenye laki tano ya Sensa kugombaniwa na Jobless over employed Ticha
 
Back
Top Bottom