Masahibu yalowakumba Dkt. Slaa na Mwabukusi ni moja ya hatua muhimu za udhibiti, kwa kiingereza huitwa "Purge"

Richard

JF-Expert Member
Oct 23, 2006
14,939
20,400
Awali napenda kusema mimi si chawa wala mshabiki wa chawa wa DP world na si mfuasi wa Dr Slaa au Mwabukusi bali natoa maoni yangu kama nilivyochambua masuala yalojitokeza hususan suala la kukamatwa Dr Slaa na Mwabukusi na wenzao na kisha kubadilishiwa makosa kutoka kuwa ya uchochezi hadi kuwa ya uhaini.

Kuna jambo moja ambalo serikali mbalimbali hufanya ili kuwanyamazisha wanasiasa ambao huitwa "firebrand" walopitiliza, hutumia njia ya kukusukuma pembeni au kukutoa kwenye kundi au kwenye ulingo wa siasa.

Neno "Purge" ni neno la kiingereza likimaanisha kutapisha au kuondoa kwa ghafla. Sasa Hapo mtu au kundi fulani huondoshwa ghafla kutoka katika jukwaa la siasa, michezo na maeneo mengine lakini lengo likiwa ni kukumaliza kisiasa, kimichezo na kukupoteza kabisa kwenye macho ya jamii.

Kiongozi yoyote yule ambae hushindwa kuvumilia mijadala, malumbano ya hoja na kuhojiwa ni lazima atumie mbinu hii ya "Purge" ili kumaliza mzozo.

Viongozi wengine hutumia njia hii kwa "level" ingine kabisa ambayo wengine hufikia kuagiza fulani ashughulikiwe kisawasawa na hata nchi kama Marekani sasa hivi raisi wa zamani Donald Trump yuko na msukomsuko kuhakikisha hagombei uraisi wa nchi hiyo ingawa msukomsuko huo wazidi kumuongezea umaarufu na uhakika wa kuwa raisi tena.

Sasa Dr Wilbroad Slaa na wakili Mwabukusi na wengine, ni watu ambao wamekosea namna yao ya uwasilishaji hoja zao. Hoja zao zaweza kuwa sahihi kabisa na hata watu wengi wakaona ni hoja sahihi kabisa kuhusu suala la mkataba wa serikali na DP world, lakini namna au mtindo wa uwasilishaji wake ndo umekuwa tatizo.

Mimi nimeishi ughaibuni na nimeishi na watu mbalimbali na nikajifunza kuwa hata ukiwa watoka Tanzania ukifika ughaibuni ni lazima utabadilika tu katika kuwasilisha hoja zako hata uwe na jazba kiasi gani. Utaweza tu kutumia lugha zisizo na ustaarabu ukiwa mitandaoni lakini katika majukwaa ya kisiasa kamwe hutamsikia mwanasiasa au mtu yoyote akizungumza lugha kali ya vitisho na ya kudharau mamlaka.

Ndo maana ughaibuni hata mbunge akitoa lugha ya ukakasi kama vile kusema mbunge mwenzake ni mwongo, au laghai au apenda kudanganyadanganya, ataamrishwa na spika wa bunge afute kauli yake hiyo vinginevyo ataondolewa bungeni.

Na wakati mwingine mbunge huyo akitoa kauli za kudhalilisha mamlaka hutakiwa kuomba msamaha palepale bungeni na mambo huendelea.

Hapa ndipo nnapokuja kwa mwanasiasa Tundu Lissu ambae kadri muda unavyozidi kwenda amekuwa makini sana na mtindo wa uwasilishaji hoja zake katika hadhira hata kama lugha hiyo pengine yaonekana ni ya dharau. Mara nyingi ametumia maneno makali sana na ya kustua lakini amekuwa ndani ya mistari wa haki yake ya kutoa maoni kikatiba.

Lakini nyuma ya pazia hatufahamu ni kwanini Tundu Lissu atumia mtindo ule wa kisiasa katika kuwasilisha hija zake na ni kwanini akiwa ndani ya Chadema yuko na kinga zaidi kuliko huko nje aliko Dr Slaa na akina Mwabukusi na asipatwe na madhara yoyote kutoka kwenye mikono ya jeshi la polisi?

Lakini Dr Slaa amejiamini kupita kiasi kwa kuzingatia kuwa alikuwa balozi na akadhani kuwa labda alivuka mstari mwekundu huenda akafikiriwa. Hatufahamu ajenda zingine alizonazo Dr Slaa lakini huenda waloamua akamatwe na apachikwe makosa ya uhaini kutoka kwenye makosa ya uchochezi wao wanafahamu mengi likiwamo suala la Dr Slaa kutaka kugombea uraisi mwaka 2025.

Kulikuwa na mada kadhaa za tetesi humu JF kwamba Dr Slaa alikuwa mbioni kujiunga na cha kisiasa au kutaka kupewa nafasi ya kuwa mgombea mahala fulani jambo ambalo litakuwa lilizisha mtafaruku miongozji mwa watesi wake kisiasa wakiwemo wanachama wa CCM. Dr Slaa ni mtu makini na anafahamu kuwa ukivuka mipaka matokeo yake ni nini, lakini kwa hili la sasa lilomkumba baada ya mambo kama haya kumkumba mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe na kisha kuachiwa kwa msamaha maalum kupitia mpango wa maridhiano kuna uwezekani mkubwa kuwa kuna mpango mahsusi wa kumfanyia Dr Slaa kitu hicho kiitwacho "Purge".

Hivyo hii "purge" hatufahamu itakuwa ni ya muda gani na kama itachukua muda zaidi hadi uchaguzi wa 2025, lakini ni sambamba na wakili Mwabukusi ambae aonekana tu kwamba amejiingiza katika eneo ambalo hana uzoefu nalo yaani siasa chafu.

Ni kweli wakili Mwabukusi amesoma tena amesoma kwelikweli kiasi cha kufikia kuwa wakili wa kujitegemea. Lakini siku zote ukiwa msomi ni lazima usome alama za nyakati na pia usome mienendo ya hali mbalimbali khasa siasa. Wakili Mwabukusi kujitoa katika kujadili suala la DP world tayari alijiingiza katika siasa za fitna bila kufahamu. Wengi walijitokeza kutaka kumfahamu, kumrekodi kwa asilimia 100 maneno yake mstari kwa mstari na pia baadhi ya waandishi kumuuliza mara mbilimbili kurudia kauli zake ambao kwa mtindo wa vitisho alikuwa akitoa lugha kali sana kumzidi hata Tundu Lissu.

Lakini wakati Dr Slaa na wakili Mwabukusi wanatoa kauli kali na za vitisho dhidi ya mamlaka hawakutambua kuwa miongoni wa walowazunguka wapo wanafikina mandumilakuwili ambao waliwenda kuketi na kuchambua kauli zile na kisha kuzikabithi kwa wahusika yaani jeshi la pili kwa ajili ya kufanya "analysis" zaidi.

Lengo la serikali kufanya "purge" ni nini?

Serikali kwa sasa imedhamiria kuwatolea mfano Dr Slaa na wakili Mwabukusi ili iwe funzo kwa wale wanotaka kuendeleza mjadala wa DP World. Serikali imetumia Bunge ( ambalo kidemokrasia ni wawakilishi wa wananchi) kama "rubber stamp" kuridhia mchakato wa DP world, hivyo serikali yenyewe na CCM wameamua hivyo na yaonyesha kuwa jambo hilo sasa ni rasmi na kinongojewa tu ni raisi Samia kuweka saini kuwa sheria.

Lakini hapohapo serikali imejipambanua kuwa haijiamini na lolote italosikia itafanya "purge" jambo ambalo ni hatari kwa kuwa lazuia raia kutumia haki yao ya msingi ya kuhoji na kujadili. Pili serikali kupitia mihimili yake ya mahakama na jeshi la polisi imeonyesha kuwa nchi yetu uko nyuma sana katika kuruhusu uhuru wa kusema na kutoa maoni, ingawa katika hili Dr Slaa na wakili Mwabukusi wamevuka mipaka ambayo ni dhahiri kuwa wamekashifu na kutishia mamlaka hivyo kushikishwa makosa ya uhaini.

Serikali chini ya raisi Samia S Hassan bado ina wajibu wa kuurejea mchakato wa DP world na kuangalia wapi pana hitilafu hususan ni bandari zipi zitakuwa chini ya DP World pamoja na maeneo mengine ambayo yamekwishaainishwa. Watanzania hatukatai DP world au hatukatai uwekezaji lakini ni lazima hatua sahihi na kuzingatiwa kwa maslahi ya nchi kwatimiliwa maanani.

Nchi hii ni yetu sote na hakuna mwenye haki miliki ya kudai nchi hii ni ya kwake, hakuna utawala wa kisultan ambao hufanya kila kitu ni mali yake. Pia mali za nchi hii ni mali za taifa na zingine huwa tawaziita nyara za serikali kama wanyama.

Tanzania ilifikia uchumi wa kati kati ya mwaka 2019 na 2020 na leo hii uchumi huo umepotea tena. Sababu kuwa ni usimamizi mbovu wa vyanzo vya mapato na matumizi mabaya ya fedha za umma. Bado serikali ya Tanzania chini ya raisi Samia ina kila sababu na wajibu wa kuhakikisha nchi yetu hii yapata maendeleo kwamba umeme wasambazwa nchi nzima na kuachana na mkaa, maji ya uhakika, elimu bora na watoto kuketi kwenye madawati na huduma bora za afya.

Bado kiu ya wananchi ipo palepale kuona kwamba nchi yawa na viwanda vitavyotoa ajira, kuboresha maisha ya watanzania, na kwa maoni yangu ni kwamba serikali ina kazi kubwa ya kuhakikisha kunakuwepo uwiano sawa kati ya miji na vijiji ili kuharakisha maendeleo ya pamoja jambo ambalo kwa CCM itakuwa imefanya kazi ya maana zaidi kuloko kukamatana na wanasiasa huko mabarabarani na kufanya "purges" ili kuzia hoja na mijadala.
 
Kuna mambo umepotosha,Mbowe hakuachiwa kwa sababu ya maridhiano,wote tunajua namna ambavyo serikali ilijikanyanga kwenye kuleta ushahidi wa Ugaidi aliotuhumiwa Mbowe,Ile kesi ilikosa ushahidi hata serikali ilijua hilo.

Una uhakika gani wamevuka mipaka?mipaka ipi?,Kusema utahamasisha maandamano yasiyo na kikomo mpaka serikali iondoke madarakani ni kosa,kuandamana Tanzania ni kosa?Au kusema PM ni mwongo hapaswi kuaminiwa?

Hio Clip ya Dr.Slaa wala haitoshi kumfanya apewe kesi ya uhaini,hapa serikali ina kazi sana kuleta ushahidi wa hii kesi na ikishindwa itakuwa ndio imekoleza moto zaidi

Wakati kesi ikiendelea serikali inazidi kujichafua huko duniani,maana kinachoonekana ni kwamba wamekamatwa sababu wanatetea bandari isiuzwe hivyo wamewatungia mashtaka ya uongo.
 
Kuna mambo umepotosha,Mbowe hakuachiwa kwa sababu ya maridhiano,wote tunajua namna ambavyo serikali ilijikanyanga kwenye kuleta ushahidi wa Ugaidi aliotuhumiwa Mbowe,Ile kesi ilikosa ushahidi hata serikali ilijua hilo.

Una uhakika gani wamevuka mipaka?mipaka ipi?,Kusema utahamasisha maandamano yasiyo na kikomo mpaka serikali iondoke madarakani ni kosa,kuandamana Tanzania ni kosa?Au kusema PM ni mwongo hapaswi kuaminiwa?

Hio Clip ya Dr.Slaa wala haitoshi kumfanya apewe kesi ya uhaini,hapa serikali ina kazi sana kuleta ushahidi wa hii kesi na ikishindwa itakuwa ndio imekoleza moto zaidi

Wakati kesi ikiendelea serikali inazidi kujichafua huko duniani,maana kinachoonekana ni kwamba wamekamatwa sababu wanatetea bandari isiuzwe hivyo wamewatungia mashtaka ya uongo.
Big brain argues like this, sio yale mapumbavu na makuwadi ya warabu koko dpworld eti unakuna yanakoment wakome yani ni mijitu isiyojielewa mali za umma zinauzwa hovyo watu wanapinga uuzwaji wa hovyo lakin makuwadi na mapuppets yanaibuka kutetea upumbavu.
 
Big brain argues like this, sio yale mapumbavu na makuwadi ya warabu koko dpworld eti unakuna yanakoment wakome yani ni mijitu isiyojielewa mali za umma zinauzwa hovyo watu wanapinga uuzwaji wa hovyo lakin makuwadi na mapuppets yanaibuka kutetea upumbavu.
Wale wamelipwa na madalali wa bandari, pesa walishakula kurudisha imekuwa taabu sasa wanachofanya ni kuhakikisha kila Uzi wapo ili kumridhisha mwarabu,ila safari hii inawatokea puani
 
Kuna mambo umepotosha,Mbowe hakuachiwa kwa sababu ya maridhiano,wote tunajua namna ambavyo serikali ilijikanyanga kwenye kuleta ushahidi wa Ugaidi aliotuhumiwa Mbowe,Ile kesi ilikosa ushahidi hata serikali ilijua hilo.

Una uhakika gani wamevuka mipaka?mipaka ipi?,Kusema utahamasisha maandamano yasiyo na kikomo mpaka serikali iondoke madarakani ni kosa,kuandamana Tanzania ni kosa?Au kusema PM ni mwongo hapaswi kuaminiwa?

Hio Clip ya Dr.Slaa wala haitoshi kumfanya apewe kesi ya uhaini,hapa serikali ina kazi sana kuleta ushahidi wa hii kesi na ikishindwa itakuwa ndio imekoleza moto zaidi

Wakati kesi ikiendelea serikali inazidi kujichafua huko duniani,maana kinachoonekana ni kwamba wamekamatwa sababu wanatetea bandari isiuzwe hivyo wamewatungia mashtaka ya uongo.
Mkuu sipo hapa kutetea DP world wala Dr Slaa na wenzake ila nipo kutafuta kiini cha kesi ya uhaini dhidi ya Dr Slaa na akina Mwabukusi.

Hata hivyo kusema utaandamana hadi serikali itoke madarakani una uwezo huo?

Na kama unao uwezo huo umeupata wapi?

Utaiondoaje serikali ambayo imechaguliwa na wananchi.

Kumbuka, hata kama raisi Samia amechukua nafasi baada ya kifo cha hayati Magufuli lakini nae alichagukliwa akiwa mgombea mwenza.

Nafikiri nimeeleza uzuri hapo juu kuhusu mtindo wa uwasilishaji wa hoja na nikatoa tofauti kati ya Tundu Lissu ambae yeye bado yupo nje na Dr Slaa na Mwabukusi ambao wamekubwa na dhahama za mahakama.
 
Mkuu sipo hapa kutetea DP world wala Dr Slaa na wenzake ila nipo kutafuta kiini cha kesi ya uhaini dhidi ya Dr Slaa na akina Mwabukusi.

Hata hivyo kusema utaandamana hadi serikali itoke madarakani una uwezo huo?

Na kama unao uwezo huo umeupata wapi?

Utaiondoaje serikali ambayo imechaguliwa na wananchi.

Kumbuka, hata kama raisi Samia amechukua nafasi baada ya kifo cha hayati Magufuli lakini nae alichagukliwa akiwa mgombea mwenza.

Nafikiri nimeeleza uzuri hapo juu kuhusu mtindo wa uwasilishaji wa hoja na nikatoa tofauti kati ya Tundu Lissu ambae yeye bado yupo nje na Dr Slaa na Mwabukusi ambao wamekubwa na dhahama za mahakama.
Uwezo wa kuandamana mpaka serikali itoke madarakani unaupimaje, mpaka uulize kama kina Adv. Mwabukusi wana uwezo huo?

Hapa tayari unaonekana una mawazo mfu/uoga, unaamini maandamano ni vurugu, ambapo ndipo unaungana na akili ya Wambura kuwakamata wale waliotaka kuandamana, na kuwapa kesi ya uhaini, yote hiyo kwasababu ya uoga wenu tu!.

Maandamano yameainishwa na Katiba ya JMT kama njia mojawapo ya kufikisha ujumbe kwa watawala, yapo kisheria, tena njia hii inatakiwa itumike baada ya msaliti kusema ametuzibia masikio, hataki kujibu maswali yetu ya msingi kuhusu ule mkataba wa hovyo wa bandari, au wewe ulitaka waendelee kuongea na kiziwi mpaka awasikie?!
 
Uwezo wa kuandamana mpaka serikali itoke madarakani unaupimaje, mpaka uulize kama kina Adv. Mwabukusi wana uwezo huo?

Hapa tayari unaonekana una mawazo mfu/uoga, unaamini maandamano ni vurugu, ambapo ndipo unaungana na akili ya Wambura kuwakamata wale waliotaka kuandamana, na kuwapa kesi ya uhaini, yote hiyo kwasababu ya uoga wenu tu!.

Maandamano yameainishwa na Katiba ya JMT kama njia mojawapo ya kufikisha ujumbe kwa watawala, yapo kisheria, tena njia hii inatakiwa itumike baada ya msaliti kusema ametuzibia masikio, hataki kujibu maswali yetu ya msingi kuhusu ule mkataba wa hovyo wa bandari, au wewe ulitaka waendelee kuongea na kiziwi mpaka awasikie?!
Kuandamana kwa minajili ya kutaka kufikisha ujumbe kwajulikana mwaandamana hadi kwenye "platform" na kisha mwazungumza hoja zenu. Hii Tundu Lissu ndo anayoifanya katika ziara zake na hajapata tatizo.

Kuandamana kwa kusudio la kuleta hamasa ya vurugu na machafuko ambako ndiko wengi wataka iwe, hiyo ni vigumu kufanyika kutokana na serikali (polisi) kuwa tayari wamejipanga maana wao hawawezi kupoima kauli za kuhamasisha maandamano.

Na hiyo pia haitaweza kutokea kutokana na tabia ya uoga wa watanzania ambao wengi kama weye huwezi kuingia "front" ili uandamane kwa minajili ya kuhamasisha vurugu za kuondoa serikali madarakani.

Ili maandamano unotaka weye yenye kuhamasisha wananchi wengi kuiondoa serikali madarakani ni lazima nchi iingie kama ilivyo Libya, Morocco na Misri ambako iliwezekana kwa sababu ya ile "Arab Spring".

Mimi sioni Arab Spring ikitokea Tanzania kutokana na ujinga wa watanzania wengi ambao hushabikia kila kitu bila kutafakari.

Pili, kulitakiwa kuwe na coordination kati ya Tundu Lissu, Dr Slaa, Mwabukusi na wengine ili kuwa na kauli moja na msimamo mmoja kuhusu DP World, jambo ambalo lingeweza kuondoa kutoka nje ya mstari na kuzungumza kauli moja.

Jambo hili si tu ni tatizo kwa akina Dr Slaa, Tundu Lissu na wengine bali ni tatizo la Afrika nzima ambapo tumegawiwa tangu ukoloni hivyo ile "divide and rule" ndo inotumaliza hata kabla ya uhuru.

Hawa walitakiwa kuwa kitu kimoja hivyo kuondoa uwezekano wa polisi na mahakama (kwa niaba ya serikali) kutafuta "weakest links" ndani ya wanaharakati na ndo lilotokea.
 
Fahamu pia hizi njia za kubambika watu kesi za ugaidi na uhaini hushindwa pia na wanaowabambika kesi wenzao kionevu watajibu hapo mbeleni mambo yatakapobadilika (regime changes)

Rais wa sasa wa Uturuki Tayyep Erdogan alishakutana na kadhia kama hizi,waoga pekee na wasioweza kujibu hoja za mahasimu wenzao hukimbilia njia hii ya kijinga kabisa,kwa sababu jamii imeelimika na inajua mbivu na mbichi,usije shangaa jamaa yupo gerezani akashinda uchaguzi
 
Mkuu sipo hapa kutetea DP world wala Dr Slaa na wenzake ila nipo kutafuta kiini cha kesi ya uhaini dhidi ya Dr Slaa na akina Mwabukusi.

Hata hivyo kusema utaandamana hadi serikali itoke madarakani una uwezo huo?

Na kama unao uwezo huo umeupata wapi?

Utaiondoaje serikali ambayo imechaguliwa na wananchi.

Kumbuka, hata kama raisi Samia amechukua nafasi baada ya kifo cha hayati Magufuli lakini nae alichagukliwa akiwa mgombea mwenza.

Nafikiri nimeeleza uzuri hapo juu kuhusu mtindo wa uwasilishaji wa hoja na nikatoa tofauti kati ya Tundu Lissu ambae yeye bado yupo nje na Dr Slaa na Mwabukusi ambao wamekubwa na dhahama za mahakama.
Watakao andamana ni mbuzi,ngombe au ni wananchi ambao ndio wameweka serikali hiyo madarakani?
Kama jibu wananchi ndio watakaoandana elewa wakiamua utawala utaanguka tu,ndio wenye Serikali
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom