Ritz, nakushauri sana kabla yakuandika jambo ufanye utafiti wako japo kidogo.
Nenda kasome historia ya Waingereza wakiwa Nigeria tangu 1922 wakati Nyerere anazaliwa. Halafu angalia Nigeria ilianza na majombo 4 kwanini yameongezeka mara tatu!
Soma harakati za Nigeria katika uhuru mwaka 1960, wakati ambapo Nigeria ilifunika tofauti za kisiasa, kiuchumi na kijamii.
Kwa taarifa yako Nigeria ni taifa lililogawanyika sana katika maeneo ya kiuchumi, kisiasa na kiutamaduni. Hili la Waislam na Wakristo siyo tatizo pekee la Nigeria. Hata waislam katika majimbo yao au wakristo wanatofauti sana.
Haya sisomi wala kusimuliwa nimeyaona mwenyewe na namshukuru mungu.
Then, soma historia ya Nnandi Azikiwe, Balewa, Obafemi Awololo, Yakoub Gown! kabla hujafika 'biafran'.
Ukipata uelewa wa Biafran, enenda zaidi kusoma habari za akina Murtala Mohamed, Obasanjo, Othman Shehu Shagari, Muhamd Buhari, Abdisalaam, Sani Abacha ili uelewe tatizo kubwa la Nigeria ni nini.
Hoja yako kuwa Nyerere aliunga mkono kwasababu ya dini inaweza kuwa sawa kwasababu ukishaaminishwa kuwa Nyerere alikuwa mwanaume kwasababu ya dini hakuna anayeweza kukuzuia kuamini! watu wanaweza kukusaidia kujitambua tu
Jibu la swali lako ni kuwa, Nyerere aliunga mkono Waisrael kwanza. Baada ya wao kuanza kuwafukuza Wapaelstina kwasababu zile zile zilizomfanya aunge mkono, Nyerere akavunja uhusiano na Israel na wala si kulaani tu.
Sijui kama unajua ubalozi wa PLO pale Upanga! Na marehemu Yaser Arafat hakusita kukutana na Nyerere fursa ilipotokea,
Sasa hapo udini uko wapi?
Nyerere alivunja uhusiano na Uingereza mwaka 1965 kwasababu UK ilimtambua Ian Smith ambaye ni mkristo.
Serikali ya Nyerere iliunga mkono wapiganaji wa POLISARIO.
Alikuwa rafiki na mshirika mzuri wa Marehem Huari Boumodiane wa Algeria kwenye waislam.
Aliunga mkono kwa silaha, makazi na askari juhudi za kumuondoa mreno ambaye ni Mkatoliki kweli kweli kule Angola na Msumbiji.
Na mwisho nikumbumbushe maneno ya Nyerere kuhusu Biafra katika bandiko langu lililotangulia. Kwa ufupi amesema sababu zilizomfanya aunge mkono Biafra ni zile zilizomfanya aunge mkono Isreal kuhusu haki ya wanadamu kuishi.
Na ndizo sababu hizo hizo zilimfanya aunge mkono Palestina.
Ritz, kama kuna mtu amekufundisha kumchukia Nyerere bila sababu hiyo ni hiari yako,lakini basi hiari hiyo usiisukimize kooni kwa wengine. Kuna vijana wanataka kuelewa wape nafasi waweze kuchambua na kuwa na fikra zao.