Ritz
JF-Expert Member
- Jan 1, 2011
- 56,734
- 46,262
Ikiwa Nyerere aliwaunga mkono Biafra kwa sababu ya dini, ina maana waliokuwa wakiteswa walikuwa wakristu hivyo kkuwafanya wale walopigana dhidi yao kuwa Waislaam sio?.. Mkuu wangu nyie mnatazama vitu gani?... ndio maana Jasusi na wengine wamewaambia kuwa mnafanya makosa sana kuifikiria udini kwa sababu aliyekuwa rais wakati huo alikuwa Gowon sio Mkandara ama Ustadhi akitetea dini yake, huu udini mkuu wangu unatoka wapi?.
Pia wamekuwepo marais wengine ktk Federation hiyo ya Nigeria ambao ni Waislaam na wakristu lakini wote hadi leo wanapingana na kujitenga kwa Biafra kama tunavyopinga kujitenga kwa Zanzibar, na hivyo usitake kabisa kusema anayewaunga mkono Zanzibar lazima awe Muislaam na anafanya hivyo kwa mapenzi ya Usilaam - huu ni ufinyu wa kufikiri na hufanywa sana na watu wasiokuwa na Ilimu dunia, walopoteza imani na matumaini isipokuwa kumtafuta mchawi. Sitopenda kabisa kuamini kwamba ndivyo Ulivyo, mkuu wangu.
Tatu, labda niongezee kusema tena Biafra haikuwa wala sii sehemu ya wakristu ila ni jimbo la kabila la Waibo ilihali Nigeria kuna makabila mengine mengi tu wakristu ambao hawaishi ktk jimbo hilo la mashariki. Na usije fananisha kabisa Biafra na Sudan ya Kusini maana Wapo Wakristu wengi Nigeria ilobakia ndani ya Federation kuliko walokuwa Biafra, hivyo sielewi hii habari unaipata wapi kuwa Biafra ni ya Wakristu wakati yule Ojukwu hata kanisani alikuwa hapajui isipokuwa msituni kama kina Che. Pengine ukisema Ojukwu alikuwa Mjamaa kwa kutazama magwanda alokuwa akivaa, akitumia mbinu za Che na support kutoka nchi za Kijamaa hapo naweza kubaliana nawe hata kama hakuna ukweli huo maana vitu vingi vinashabihiana na ushabiki wa Ukomunist...
Mengine mkuu wangu nakuachieni kwa sababu sifikirii ndani ya box la udini kila siku. Natumia sana kipimo cha Uhuru, Haki na usawa na pale kimojawapo kinapokosekana huwaunga mkono wale waotoa madai yao na sii watu wanaotaka Uhuru wa nchi kwa jina lake japokuwa wao wenyewe wako huru, na wana haki sawa na wengine.
Mkandara kwa nini Biafra walikuwa wakipinga utawala wa wanajeshi Waislam?
Na yale mauaji ya watu milioni 2 yalisababishwa na nini?
Last edited by a moderator: