Gen. Mboma ajaribu kugombea, aangushwa!

Tuna fillibuster bongo? na kwa kiswahili inaitwaje hiyo, filibasta?

Bongo hatuna Fillibuster "Mr. Smith Goes To Washington" style, lakini tuna kutoa shilingi, which revolves areound the same idea but is not exactly the same.

Our Parliament being a Commonwealth/ Westminster offspring I wonder if we inherited this but are just more civilized than the Brits and Americans to descend to this rather low point of parliamentary democracy.
 
Angegombea kwa tiketi ya CHADEMA wengi wa wana JF wasingemsema vibaya.

Mbona anajua kwamba akijaribu kuingia Chadema hatapata nafasi hata ya kuwa mwanachama .So sijui unasemaje ?Ameoza mno kuwa upande wa pili watu wa aina yake huishia CCM tu .
 
Gen Mboma anaingia kwenye siasa ili kujilinda na maovu yake ya nyuma. Wanajeshi wote wasio waadilifu sasa na waliostaafu; wako nyuma yake. Kwa sisi walala hoi hizi ni dalili njema kwamba kweli hawa watu hawana amani huko uraiani. Katika mafisadi wote, imefikia sasa HATA MBONA hana amani uraiani ni dalili nzuri kwa Taifa.

- Mkuu Yebo Yebo, umepiga mpaka Ikulu, jamani JF huyu Mboma ana ........ wake humu anayejifanya anajua sana kurushia mawe viongozi wengine, sasa ninamfahamisha mapema kabisaaa kuwa kazi ndio kwanza imeanza, na mkuki usiwe mchungu kwako this time arround, maana hapa ni JF where we dare!

- Hii topic imeletwa hapa kwa ajili ya kujitayarisha kumkoma nyani, maana ya huyu mkulu yote yanafahamika wazi, mkuu nakuomba kwenye topic zake labda ukae pembeni maana utachukia watu buree!

Woooooh! I love it na hasa this game!
 
Una maana kwa sasa ni MSAFI..are you serious?



Gen Mboma anaingia kwenye siasa ili kujilinda na maovu yake ya nyuma. Wanajeshi wote wasio waadilifu sasa na waliostaafu; wako nyuma yake. Kwa sisi walala hoi hizi ni dalili njema kwamba kweli hawa watu hawana amani huko uraiani. Katika mafisadi wote, imefikia sasa HATA MBONA hana amani uraiani ni dalili nzuri kwa Taifa.


you nailed it..
 
- Mkuu Yebo Yebo, umepiga mpaka Ikulu, jamani JF huyu Mboma ana ........ wake humu anayejifanya anajua sana kurushia viongozi wengine, sasa ninamfahamisha mapema kabisaaa kuwa kazi ndio kwanza imeanza, na mkuki usiwe mchungu kwako this time arround, maana hapa ni JF where we dare!

- Hii topic imeletwa hapa kwa ajili ya kujitayarisha kumkoma nyani, maana ya huyu mkulu yote yanafahamika wazi, mkuu nakuomba kwenye topic zake labda ukae pembeni maana utachukia watu buree!

Woooooh! I love it na hasa this game!

:D:D..phewwwwwwwwwwwww....am just whistling:D:D...ngoja nijitafutie pop corn nianze kujitafunia taratiiiiiibu...maana it looks like hii ni ngoma ya kikubwa,ni lazima ikeshe....bwaa bwaa aaah bwaah....lol
 
Hichi kiti cha Mbeya kitachukuliwa na CCM licha ya kuwa chama tawala popularity yake imeshuka huko Mbeya hata ikafikia JK kulengwa mawe , Chadema na CUF bila ya kusimamisha mgombea mmoja CCM itashinda kama Jimbo la Kilwa ,kwani CCM ilipata kura chache ila iliibuka mshindi kwani kura za Wapinzani zilikatwa katwa kama Kashata na CCm kuibuka kidedea.
It look Chadema wanaamini wao sasa hivi ndio big dog hawataki mashauriano na vyama vyengine vya upinzani ila hiyo ndio itakua bakora ya Wapinzani . Chadema ailiachiwa huko Musoma sasa ni zamu ya wao kuwa Wazalendo kuwa support Wanangangari CUF kwani mwaka 1995 CUF ilishika nafasi ya pili .
Kuna mengi ya kujiuliza nani atabadilisha ramani hii ya matokeo ya Uchaguzi mwaka 2010 kama jimbo la Mbeya tu Wapinzani wameshindwa kukaa kitako na kusimamisha mgombea mmoja na kuiweka CCM pembeni?

Who will change this map in 2010 ?
Tanzania. Presidential Election 2005 | Electoral Geography 2.0
Changes is not too late for Bongo Land.
 
Kikatiba Mbooma ana haki zote kama raia mwingine yeyote kuomba nafasi ya uongozi wa ridhaa ya wanachi. Tatizo ni pale ambapo alishawahi kushika wadhifa wa juu kabisa jeshini. Akastaafu. Mboma anaweza kutumika katika ushauri mbalimbali katika mambo ya ku usalama na ulinzi. Sasa anadhania kuwa pesa na title ya ujenerali basi ni tikiti ya ubunge! mwacheni kama anadhani wapiga kura watapiga saluti ya ndiyo amenoa. Ingawa inategemea amejijenga na kujikita kiasi gani na wapiga kura. Ila asije akarusha ngumi akianikwa hadharani kwa aliyoyafanya Jeshini(ni FISADI).
 
Hi Guys msimsumbue General. Kama Mwanajeshi Mstaafu ni Mahiri sana. Sasa msimzonge kwa sababu hakusema yeye ni Chadema au CUF.

Siamini kama huko Mbeya bado hawajaamka kujua Who is fisadi Mboma. Huu ukoo uangaliwe, kuna kipande cha mti (MUTI) ndani yake.
 
suti safi aliyovaa karibu itamvuka tupate kushuhudia jinsi nguo zake za ndani zinavyonuka!!
 
Siamini kama huko Mbeya bado hawajaamka kujua Who is fisadi Mboma. Huu ukoo uangaliwe, kuna kipande cha mti (MUTI) ndani yake.

Mkuu, watu wa Mbeya wanajua yote: wanajua kuwa MBOMA NI FISADI, tena siyo fisadi tu, bali FISADI NAMBARI MOJA, ambaye jina lake jeshini linanuka kwa rushwa na ubadhirifu.

Mali anazomiliki ni nyingi sana ikiwemo Petrol Station ya Mbeya aliyojengewa na Balhabou wa Morogoro kama asante kwa kuwapa tenda zote za jeshi kuanzia mafuta hata kusupply buti za jeshi! Habari za ukakika ni kuwa anaungwa mkono na mlinzi wa mafisadi ndani ya CCM, MAKAMBA!

Hii ni bahati kubwa kuwa anagombea ili tumwanike hadharani kisawasawa. Hata yule rafiki yake fisadi APSON MWANG'ONDA wa usalama wa Taifa, naye anataka kuwania kiti cha Mbozi Mashariki. Tunamsubiri kwa hamu kumwonesha kuwa yeye ndiye KAGODA nambari wani ambaye kwa sasa anastahili kuwa jela!
 
Ukisha kula nyama ya mtu utaendelea kula tu, ukiacha ujue umekufa tayari.
Watu wanaotamani madaraka kwa uchu kama huu ni kama waliokula nyama ya mtu.
Mh Mboma bado anakumbuka radha na utamu wa madaraka.
Pamoja na kukusanya mabilioni ya wizi, haoni raha kukaa na kuyatafuna kwani hakuna mtu anamwita MH au afande.
Akiukwaa amejianika mwenyewe, uchafu wake wote alofanya akiwa jeshini utawekwa wazi hapa.
Amshauri na Afande Defao(Mahita) naye agombee ubunge ili idadi ya Mishushu, Mimwera na Mijeshi izidi kuongezeka kwenye kilinge cha Bunge.
 
CCM ni kichaka cha mafisadi. People go for CCM sio kwa sababu wana machungu na nchi la hasha na hapana. Wenye machungu na CCM sijawaona, wenye machungu na nchi hii tunawaona. Samahani FMES najua unaipenda CCM but wajuu yako wameshachafua/chafuka. Yeye amesema hajatumwa na yeyote.......

Mboma hana pa kutokea ila kaona being MP atapona ili walau anuse kabla havijakarangizwa. Hakika hapa ni patamu
 
Yebo Yebo, Mwanakijiji; Fataki na Viongozi wa hapa nyumbani JF!

Ningependa mnisaidie kunielimisha kwa uhakika maana kuuliza si ujinga, huyu Ge. Mstaafu Mbona, ana scandal, shida au mapungufu yapi?


Rejea Mradi mzima wa Meremeta (vielelezo vyote vimo humu JF), then ukimaliza angalia tenda nzima ya Radar ya Jeshi, kisha angalia tenda ya Helikpta za Jeshi, ukimaliza kama una swali lingine karibu.
 
Hichi kiti cha Mbeya kitachukuliwa na CCM licha ya kuwa chama tawala popularity yake imeshuka huko Mbeya hata ikafikia JK kulengwa mawe , Chadema na CUF bila ya kusimamisha mgombea mmoja CCM itashinda kama Jimbo la Kilwa ,kwani CCM ilipata kura chache ila iliibuka mshindi kwani kura za Wapinzani zilikatwa katwa kama Kashata na CCm kuibuka kidedea.
It look Chadema wanaamini wao sasa hivi ndio big dog hawataki mashauriano na vyama vyengine vya upinzani ila hiyo ndio itakua bakora ya Wapinzani . Chadema ailiachiwa huko Musoma sasa ni zamu ya wao kuwa Wazalendo kuwa support Wanangangari CUF kwani mwaka 1995 CUF ilishika nafasi ya pili .
Kuna mengi ya kujiuliza nani atabadilisha ramani hii ya matokeo ya Uchaguzi mwaka 2010 kama jimbo la Mbeya tu Wapinzani wameshindwa kukaa kitako na kusimamisha mgombea mmoja na kuiweka CCM pembeni?

Who will change this map in 2010 ?
Tanzania. Presidential Election 2005 | Electoral Geography 2.0
Changes is not too late for Bongo Land.


Mkuu MLEKWA,heshima mbele.

Nakubaliana na wewe kwa asilimia zote,tafadhali chukua tano.
CHADEMA wanahitaji kuelewa na kuelimishwa kwamba ushirikiano na vyama vingine vya upinzani ndiyo njia pekee ya kuiondoa CCM na hatimaye kuleta mabadiliko ya kweli Tanzania.Ushindi wa Tarime umewafanya kujiona wao hawana sababu ya ushirikiano na vyama vingine lakini lazima waelewa kuwa CUF walipata nafasi ya pili 2005.CCM ni chama kikubwa na kikongwe kuitoa madarakani kunahitaji umoja wa vyama vyote yaani CUF,TLP,NCCR Mageuzi na nk.
 
Back
Top Bottom