Indume Yene
Platinum Member
- Mar 17, 2008
- 2,948
- 709
MKUU WA MAJESHI NA MNADHIMU NI KAMA MARAIS WASTAAFU WANALELEWA HADI WANAKUFA....LAKINI PIA KITENDO CHA MBOMA KUGOMBEA NI FUNZO KWA SERIKALI....INAWASAHAU SANA HAWA WAKUU WANAKUWA IDLE.....IWATAFUTIE ACTIVITIES.....MBALI YA ZILE WANAZOFANYA MASHAMBANI MWAO...
Mwanzoni mwa thread hii nilichangia kwa kusema ni AIBU kwa Mboma kudai kuwa alilipwa kiinua mgongo kizuri hivyo atakuwa kwenye nafasi nzuri ya kuleta maendeleo kwa wananchi bila ya kuwa na tamaa ya kujitajirisha. Hiyo ilikuwa ni hoja ya KIPUUZI. Kuleta maendeleo kwa wananchi si lazima uwe Mbunge, kama yeye anafikiri kuwa yuko idle sana kwa nini asianzishe hata foundation ya kusaidia KUWALINDA MAALBINO?Kilio cha Maalbino Tanzania kimesikika kila pembe ya DUNIA, kwa nini yeye Mboma kwa kutumia QUALIFICATIONS zake alitumikie Taifa kwa kuhudumia MAALBINO. It's time for him to pay back to Tanzanians huku akiendelea kulelewa kwa KODI ya Watanzania.
AGAIN, MAENDELEO HAYALETWI KWA KUPITIA UBUNGE TU. Askofu, mhubiri maarufu nchini Marekani ambaye vilevile ni mtunzi wa Vitabu Thomas Dexter Sr. (Bis. T.D Jakes) anatumia talent na utajiri wake kutoa misaada kwa ajili ya Maendeleo ya baadhi ya nchi za Afrika kama vile Kenya, Uganda na Afrika Kusini. Amesaidia kujenga baadhi ya visima nchini Kenya. Hiyo inawarahisishia wanawake nchini humo kutembea mwendo mfupi kwenda kuchota maji kwa ajili ya matumizi ya nyumbani. Vilevile jamii inapata maji safi. Lakini yeye si muajiriwa wa serikali yoyote ile lakini anaona umuhimu wa kuhudumia wananchi wenye shida. Wapo watu wengi wenye moyo huo hata hapa nyumbani na mojawapo ni Bw. Mengi na wengineo.
Kama kweli Mboma anataka kueleta maendeleo kwa wananchi huko Mbeya bado ana nafasi hiyo nje ya Ubunge. Maana kipindi chote amekuwa kimya hadi ulipowadia wakati wa kuchukuwa fomu za kugombea jimboni mwake. Miaka 6 yote alikuwa wapi? Watu wataendelea kum-judge kwa matendo yake hasa baada ya kuangushwa kwenye kura za maoni. Wengine wakishaanguka kwenye kura basi hawaonekani tena. Anatakiwa kudhihirisha kwa Wananchi wote kuwa aliyokuwa akisema kuhusu maendeleo ya wananchi ni ya kweli. Aanze kuwahudumia wananchi huku akiendelea kuishi kwa pensheni inayolipwa kwa kodi ya walala puu..