Geita yakubali kuundwa Mkoa wa Chato; Kakonko, Biharamulo na Ngara kumegwa. Sengerema kwenda Geita..

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,808
11,973
Geita yaridhia kuanzishwa Mkoa wa Chato. RCC yatoa mapendekezo. Baadhi ya maeneo kutoka mikoa jirani. RC Geita Mhe Rosemary Sitaki awashukuru Wananchi kukubaliana kwa hekima bila ushabiki.

Kikao cha Kamati ya Ushauri ya mkoa - REGIONAL CONSULTATIVE COMMITTEE (RCC), Kilichokaa kama kikao Maalum leo kwaajili ya Mapendekezo ya kuunda Mkoa Mpya wa Chato, Kimependekeza yafuatayo:

1. Mkoa Mama wa Geita ubakiwe na Wilaya tatu ambazo ni Wilaya ya Geita, Mbogwe na Wilaya ya Nyang'hwale.

2. Imependeleza iombwe Wilaya ya Sengerema ambayo ipo Mkoa wa Mwanza, ili iweze kukamilisha Wilaya nne za Geita pamoja na Wilaya Pendekezwa ya Busanda.

3. Mkoa wa Chato imependekezwa kwa iundwe na Wilaya za Geita ambazo ni Chato yenyewe, na Wilaya ya Bukombe.

4. Pia imependekezwa kutoka Kigoma, iombwe eneo kutoka Wilaya ya Kakonko, pia kutoka Kagera imependekezwa ziombwe Wilaya mbili ambazo ni Biharamulo na Wilaya ya Ngara.

Mapendekezo haya yamekamilika na yamekubaliwa na wajumbe wote wa RCC.

Sasa yatapelekwa kwenye Wizara husika ili yaweze kufanyiwa kazi.

Zaidi, soma; Geita: Baraza la Madiwani laukataa Mkoa mpya wa Chato
 
Mbona siwaelewi hawa mara vile mara hivi ??

Sent from my Moto E (4) using JamiiForums mobile app
Mkuu itafikia hatua itabidi tujiulize sana hawa wanaokataa sera za majimbo hiki wanachokifanya ni kitu gani? Je hawa wateuliwa wetu wana weledi na wayafanyayo? Je maanguko ya miaka ya sabini hawakujifunza? Je haya majaribio ya mega huku weka kule yana tija gani? Ina maana hatuna watu wabunifu mpaka tutapanye nchi na kuzua migogoro ya ardhi isiyo na ulazima? Je hawajui kuna migogoro toka Ilemela na Nyamagana au Bunda, Serengeti na Butiama zimegawanywa haijaisha mpaka leo?
Anyway tuendelee kutafuta sifa za kijinga historia itaamua
 
Mkuu itafikia hatua itabidi tujiulize sana hawa wanaokataa sera za majimbo hiki wanachokifanya ni kitu gani? Je hawa wateuliwa wetu wana weledi na wayafanyayo? Je maanguko ya miaka ya sabini hawakujifunza? Je haya majaribio ya mega huku weka kule yana tija gani? Ina maana hatuna watu wabunifu mpaka tutapanye nchi na kuzua migogoro ya ardhi isiyo na ulazima? Je hawajui kuna migogoro toka Ilemela na Nyamagana au Bunda, Serengeti na Butiama zimegawanywa haijaisha mpaka leo?
Anyway tuendelee kutafuta sifa za kijinga historia itaamua
Buriani Geita. Ni ushamba kuna ulazima gani? Mbona Morogoro haigawiki?
 
Geita yaridhia kuanzishwa Mkoa wa Chato. RCC yatoa mapendekezo. Baadhi ya maeneo kutoka mikoa jirani. RC Geita Mhe Rosemary Sitaki awashukuru Wananchi kukubaliana kwa hekima bila ushabiki.

Kikao cha Kamati ya Ushauri ya mkoa - REGIONAL CONSULTATIVE COMMITTEE (RCC), Kilichokaa kama kikao Maalum leo kwaajili ya Mapendekezo ya kuunda Mkoa Mpya wa Chato, Kimependekeza yafuatayo:

1. Mkoa Mama wa Geita ubakiwe na Wilaya tatu ambazo ni Wilaya ya Geita, Mbogwe na Wilaya ya Nyang'hwale.

2. Imependeleza iombwe Wilaya ya Sengerema ambayo ipo Mkoa wa Mwanza, ili iweze kukamilisha Wilaya nne za Geita pamoja na Wilaya Pendekezwa ya Busanda.

3. Mkoa wa Chato imependekezwa kwa iundwe na Wilaya za Geita ambazo ni Chato yenyewe, na Wilaya ya Bukombe.

4. Pia imependekezwa kutoka Kigoma, iombwe eneo kutoka Wilaya ya Kakonko, pia kutoka Kagera imependekezwa ziombwe Wilaya mbili ambazo ni Biharamulo na Wilaya ya Ngara.

Mapendekezo haya yamekamilika na yamekubaliwa na wajumbe wote wa RCC.

Sasa yatapelekwa kwenye Wizara husika ili yaweze kufanyiwa kazi.
Chato ni mkoa ambao hautakuwa na mvuto kabisa.
Harafu wanataka kuipotezea radha kagera kwa kuitolea wilaya zake.
Hivi kwa nini wasikate mikoa mikubwa wanaenda kukata mkoa mdogo? Yaani hii nchi tumepigwa kabisa
 
Chato ni mkoa ambao hautakuwa na mvuto kabisa.
Harafu wanataka kuipotezea radha kagera kwa kuitolea wilaya zake.
Hivi kwa nini wasikate mikoa mikubwa wanaenda kukata mkoa mdogo? Yaani hii nchi tumepigwa kabisa

Bigaramuro na ngara hazikufaa kua kagera ukiangalia hAta mila na desturi za watu, kutoka kakonko kwenda mkoani kigoma ni mbali afadhali waende chato rahisi kufika na kupata huduma, , Kagera itabaki na wilaya zifuatazo, Kyerwa, Muleba, karagwe na Bukoba yenyewe hivo sio mbaya
 
Bigaramuro na ngara hazikufaa kua kagera ukiangalia hAta mila na desturi za watu, kutoka kakonko kwenda mkoani kigoma ni mbali afadhali waende chato rahisi kufika na kupata huduma, , Kagera itabaki na wilaya zifuatazo, Kyerwa, Muleba, karagwe na Bukoba yenyewe hivo sio mbaya
Ila hapo wanaharibu ilipaswa mikoa mikubwa mingine ndio wangekata kama Tabora, Morogoro, Tanga au huko Ruvuma
 
Bora wangafanya hata Kahama kuwa mkoa ili waipunguzie mzigo Tabora kwa kuimega hasa Nzega kuja Kahama na sehemu zingine

Mbona Chalinze au Butiama hawakuwa na hizi Shobo hii ni dalili ofisi kubwa alikalia mtu wa ajabu sana

Mama wewe wape wanayotaka (Sijui Mikoa) lkn pia wasikuingilie ukianza kuendeleza Zanzibar na Pwani yote , maana wao wameanza wewe maliza tena una njia aliyoionyesha mwenzako (Mwendazake) ya kupendelea kwao na wa makabila ya kwao na wa imani yake (Ndo maana hata porini Dom haupataki huko kwa wa Bara) kutesa kwa zamu
 
Ila hapo wanaharibu ilipaswa mikoa mikubwa mingine ndio wangekata kama Tabora, Morogoro, Tanga au huko Ruvuma
Mikoa mingine hata ikiwa mikubwa inaweza kuwa vigumu kuikata kwa sababu ya population density kuwa ya chini. Unaweza kukuta mkoa una eneo kubwa lakini wakazi ni wachache kwa hiyo mkiukata mnawabebesha wananchi wachache mzigo mzito wa kulea serikali za wilaya/miji na mitaa.
 
Bigaramuro na ngara hazikufaa kua kagera ukiangalia hAta mila na desturi za watu, kutoka kakonko kwenda mkoani kigoma ni mbali afadhali waende chato rahisi kufika na kupata huduma, , Kagera itabaki na wilaya zifuatazo, Kyerwa, Muleba, karagwe na Bukoba yenyewe hivo sio mbaya
Kwa hiyo sifa ya mkoa ni kujengwa kwa misingi ama viashiria vya ukabila? Makabila mawili au zaidi hayawezi kuwa chini ya mkoa mmoja?

Sioni sababu za msingi za kuugawa mkoa wa Geita wenye idadi ya watu China ya idadi ya 1.8 mln! Huku ni kupoteza rasilimali!
 
Ngara iliwekeza Sana kwenye shule zilizopo bukoba zilipoletwa shule za Kata ikapigwa na sasa unaenda kupigwa ianze moja. Kwani niwemugizi yeye anasemaje
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom