Geita yakubali kuundwa Mkoa wa Chato; Kakonko, Biharamulo na Ngara kumegwa. Sengerema kwenda Geita..

Naunga mkono kabisa kuundwa kwa mkoa wa Chato kwa sababu kuu moja, ... nayo ni kuisogeza serikali karibu zaidi na ukanda huu uliopakana na chanzo kikuu cha migogoro ya nchi za maziwa makuu (TUTSI/HUTU conflict zone)!
👊 :cool:✌️💥☠️☠️☠️💀
 
Wenyewe hawajaomba
Midhali ni kaugonjwa iko siku atakuja mwendawazimu mwingine itagawika... usishangae hii meguamegua iko mikoa au wilaya zitamegwa ili kuongezea maeneo sehemu zingine!!! Siasa zikitawala weledi 'upumbavu hutamalaki!' Ati mzee fulani alitoa ombi... haya shime na butiama iwe mkoa tumuenzi Mwalimu ila tusisahau Liwale, Masasi na... na... na....
 
Ujinga tu kupoteza muda kulalamika kukatwa au kutokatwa eneo. Hizi ramani wazungu walikata hadi kuwa na tanganyika hatukupiga kelele au kwa kuwa tulikuwa nyani na wazungu ni watu?

Nashangaa hata kwanini kibaha isiwe Dar, fikiria mtu anatoka Mukuranga anapita Dar kwenda mkoani kwake kwa shughuli za kiofisi huko kibaha Mkoani.

Zanzibar ni kama mkoa mmoja au miwili leo watu wanataka eneo lisikatwe ubaki mkoa wenye eneo kuuuubwa ni kuchelewesha huduma kuwa karibu na watu.

Labda ingeleta Mashiko kama tungejadili kwa mkutadha wa kuongezeka gharama kwa serkali maana watahitajika watumishi kwa mkoa mpya na wilaya zake.
 
Nijuavyo Mimi maamuzi hufanywa na mabaraza ya madiwani na Si DCC wala RCC. Hizi ni Kamati za kushauri tu ambazo hubariki au kushauri maamuzi ya mabaraza ya Madiwani. Aidha, zoezi hili ngumu na tata ni lazima lipate Baraka za wananchi. Hivyo lazima kiwe na Muhtasari ya Mkutano mikuu ya vijiji/mitaa yote Wilaya zitakazohama na zile zitakaosalia. Kwa Maelezo tunayosoma, nibkwamba mikoa yote athirika Mwanza, KAGERA, Kigoma, na Geita lazima ifanye vikao. Gharama hizi zote za nini? Faida ake ni zipi
 
Geita yaridhia kuanzishwa Mkoa wa Chato. RCC yatoa mapendekezo. Baadhi ya maeneo kutoka mikoa jirani. RC Geita Mhe Rosemary Sitaki awashukuru Wananchi kukubaliana kwa hekima bila ushabiki.

Kikao cha Kamati ya Ushauri ya mkoa - REGIONAL CONSULTATIVE COMMITTEE (RCC), Kilichokaa kama kikao Maalum leo kwaajili ya Mapendekezo ya kuunda Mkoa Mpya wa Chato, Kimependekeza yafuatayo:

1. Mkoa Mama wa Geita ubakiwe na Wilaya tatu ambazo ni Wilaya ya Geita, Mbogwe na Wilaya ya Nyang'hwale.

2. Imependeleza iombwe Wilaya ya Sengerema ambayo ipo Mkoa wa Mwanza, ili iweze kukamilisha Wilaya nne za Geita pamoja na Wilaya Pendekezwa ya Busanda.

3. Mkoa wa Chato imependekezwa kwa iundwe na Wilaya za Geita ambazo ni Chato yenyewe, na Wilaya ya Bukombe.

4. Pia imependekezwa kutoka Kigoma, iombwe eneo kutoka Wilaya ya Kakonko, pia kutoka Kagera imependekezwa ziombwe Wilaya mbili ambazo ni Biharamulo na Wilaya ya Ngara.

Mapendekezo haya yamekamilika na yamekubaliwa na wajumbe wote wa RCC.

Sasa yatapelekwa kwenye Wizara husika ili yaweze kufanyiwa kazi.

Zaidi, soma; Geita: Baraza la Madiwani laukataa Mkoa mpya wa Chato
He!!! Kumbe haijikidhi wanaomba wilaya kutoka mikoa mingine!!!! Ukistaajabu ya Musa...!!!!
 
Bora wangafanya hata Kahama kuwa mkoa ili waipunguzie mzigo Tabora kwa kuimega hasa Nzega kuja Kahama na sehemu zingine

Mbona Chalinze au Butiama hawakuwa na hizi Shobo hii ni dalili ofisi kubwa alikalia mtu wa ajabu sana

Mama wewe wape wanayotaka (Sijui Mikoa) lkn pia wasikuingilie ukianza kuendeleza Zanzibar na Pwani yote , maana wao wameanza wewe maliza tena una njia aliyoionyesha mwenzako (Mwendazake) ya kupendelea kwao na wa makabila ya kwao na wa imani yake (Ndo maana hata porini Dom haupataki huko kwa wa Bara) kutesa kwa zamu
Yes!!! Ne yeye apendelee Zanzibar!!!!
 
Bora wangafanya hata Kahama kuwa mkoa ili waipunguzie mzigo Tabora kwa kuimega hasa Nzega kuja Kahama na sehemu zingine

Mbona Chalinze au Butiama hawakuwa na hizi Shobo hii ni dalili ofisi kubwa alikalia mtu wa ajabu sana

Mama wewe wape wanayotaka (Sijui Mikoa) lkn pia wasikuingilie ukianza kuendeleza Zanzibar na Pwani yote , maana wao wameanza wewe maliza tena una njia aliyoionyesha mwenzako (Mwendazake) ya kupendelea kwao na wa makabila ya kwao na wa imani yake (Ndo maana hata porini Dom haupataki huko kwa wa Bara) kutesa kwa zamu
Ha ha ha!!! Porini Dom mama hapataki!!!! This is great!
 
Mikoa mingine hata ikiwa mikubwa inaweza kuwa vigumu kuikata kwa sababu ya population density kuwa ya chini. Unaweza kukuta mkoa una eneo kubwa lakini wakazi ni wachache kwa hiyo mkiukata mnawabebesha wananchi wachache mzigo mzito wa kulea serikali za wilaya/miji na mitaa.
N geita je?
 
Buriani Geita. Ni ushamba kuna ulazima gani? Mbona Morogoro haigawiki?
Well said, Morogoro tu mbona na. Mkoa wa Tabora nao ni mkubwa sana hatujawahi kusikia mapendekezo ya kuigawa mikoa hiyo - ukiangalia kwa umakini utaguduwa Mikoa mipya iliyo anzishishwa ilitokana na shinikizo la kisiasa za Mawaziri wakuu na baadhi ya mawaziri kutoka mikoa husika,mfano: Mkoa was Manyara,Mkoa wa Katavi, Mkoa wa Geita huyo huyo ndie muhusika mkuu wa kalazimisha uundwaji wa Mkoa wa Chato/Rubondo - mambo gani haya?

Kinacho shangaza zaidi we Mkuu wa Mkoa wa Geita ana interest gani katika uundaji wa Mkoa wa Chato, kama sio kwamba kuna ushinikizaji wa chini chini for some strange reasons ambazo hazina tija kwa Taifa zaidi ya ubinafsi tu uliyo pitiliza mipaka - ushinikizaji wa uundwaji wa Mkoa wa Chato mama Samia hasiuwekee maanani hata kidogo
 
Hivi uwingi wa mamikoa unaleta maendeleo kwa wananchi? Bongo bahati mbaya sana , yaani hatuna vipaumbele kabisa ni mawazo ya kuongeza vyeo tu na madaraka lakini tija kwa wananchi hatujadili kabisaaa
 
Chato ni mkoa ambao hautakuwa na mvuto kabisa.
Harafu wanataka kuipotezea radha kagera kwa kuitolea wilaya zake.
Hivi kwa nini wasikate mikoa mikubwa wanaenda kukata mkoa mdogo? Yaani hii nchi tumepigwa kabisa
Tabora ni eneo kubwa balaa, hebu wapeni mkoa mpya.
 
Mama Samoa huu utopolo piga chini kabisa,yule sadist tayari keshaanza kuliwa na mchwa unahofia nini
 
Geita yaridhia kuanzishwa Mkoa wa Chato. RCC yatoa mapendekezo. Baadhi ya maeneo kutoka mikoa jirani. RC Geita Mhe Rosemary Sitaki awashukuru Wananchi kukubaliana kwa hekima bila ushabiki.

Kikao cha Kamati ya Ushauri ya mkoa - REGIONAL CONSULTATIVE COMMITTEE (RCC), Kilichokaa kama kikao Maalum leo kwaajili ya Mapendekezo ya kuunda Mkoa Mpya wa Chato, Kimependekeza yafuatayo:

1. Mkoa Mama wa Geita ubakiwe na Wilaya tatu ambazo ni Wilaya ya Geita, Mbogwe na Wilaya ya Nyang'hwale.

2. Imependeleza iombwe Wilaya ya Sengerema ambayo ipo Mkoa wa Mwanza, ili iweze kukamilisha Wilaya nne za Geita pamoja na Wilaya Pendekezwa ya Busanda.

3. Mkoa wa Chato imependekezwa kwa iundwe na Wilaya za Geita ambazo ni Chato yenyewe, na Wilaya ya Bukombe.

4. Pia imependekezwa kutoka Kigoma, iombwe eneo kutoka Wilaya ya Kakonko, pia kutoka Kagera imependekezwa ziombwe Wilaya mbili ambazo ni Biharamulo na Wilaya ya Ngara.

Mapendekezo haya yamekamilika na yamekubaliwa na wajumbe wote wa RCC.

Sasa yatapelekwa kwenye Wizara husika ili yaweze kufanyiwa kazi.

Zaidi, soma; Geita: Baraza la Madiwani laukataa Mkoa mpya wa Chato
Kuendeleza ukabila wa Magufuli.
Yule alikuwa si mtu mzuri sana.
Upendeleo wa dhhiri.
Mama Samia akiingia mtego huu, basi kila Rais ajaye atataka kuweka mkoa hata kijiji chake.
 
Kumekuwa na mjadala mkali kuhusu uhalali wa wilaya ya chato kupewa hadhi ya makao makuu ya mkoa mpya , na pia kumegwa wilaya za mikoa mingine ya karbu ili kuunda mkoa huo mpya , jonzi hii ilikuwa ni ya aliyekuwa Raisi wa jamhur wa muungano wa Tanzania hayati J.P.J.Maghufuli.

Kimsingi inakuwa ni ngumu kuizima jonzi hyo hata kama mkoa huo mpya wa chato hasa wilaya ya chato kutokuwa na hadhi hyo ,

Hayati alikuwa ameanza kuwekeza miradi mizito wilayani chato , kiukweli miradi hyo ili iweze kufanya kazi Kwa ufanisi ni lazima chato iwe makao makuu ya mkoa mpya zaidi ya hapo miradi hyo itakuwa dead project ...
Ujenzi wa uwanja wa ndege , hospital kubwa ya kisasa, kufunguliwa Kwa matawi ya huduma za kibank , ujenzi wa barabara ,na hifadhi ya burigi na Bandari pia naskia ipo kule ..N.K .miradi hii yote ingekufa kibudu na ingekuwa bonge la hasara Kama wilaya ya chato haitakuwa mkoa ....

Kupewa hadhi ya mkoa kutavutia shughuli za kiserikali na hii itafanya miardi hyo iwe na tija. ....

Kimsingi jamaa kafariki akiwa ameisogeza chato kwenye point of no return thus why hata viongozi waliopo wameshindwa kupiga U-Turn.
Kashindwa nani kupiga U-Turn? Hivi amuoni yaliyo kumba mji aliozaliwa Mobutu Sseseko - hivi sasa zahama hizo ndio zimeanza kunyemelea mji Chato ambao alizaliwa JPM

Dunia haishangazwi na hilo kwa kuwa Mobutu na JPM wote walikuwa na hulka zinazo randana sana,walikuwa hawataki kukosolewa, walilazimisha kauli zao ziwe final bila kujali athali zinazo weza kusababishwa na baadhi ya mahumuzi yao ya kupendelea wazi wazi Wilaya/Majimbo yao kwa kutumia tax payers money big time kujenga mega infrastructure wilaya/kijiji waliko zaliwa bila aibu!!

Tujaribu kuwa wakweli hapa, upendeleo/blatant nepotism is unethical,Viongozi wetu wa kitaifa wanapashwa kukemea vitendo hivyo kwa nguvu zao zote na ingekuwa vizuri zaidi kama Bunge lingepitisha sheria ya ku- impeach Rais yoyote aliyepo madarakani akionekana anapendelea kupeleka maendeleo yaliyo pitiliza mipaka jimboni mwake,kupendelea ndugu zake na kabila lake - upendeleo huu unarudisha nyuma umoja wa Kitaifa.

Mbona hatukuwahi kushuhudia matendo haya ya ajabu wakati wa Uongozi wa: Baba wa Taifa,Mzee Mwinyi,MzeeMkapa na JPM.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom