Gavana Balali Ajiuzulu!

Gavana Balali Ajiuzulu!

Jamani wanasheria mko wapi tuungane kumshitaki huyu mtu kwanini tuanalalamika kila wakati tu naombeni email ya Prof.Shivji na mwingie ambaye mnadhani wanaweza kunisaidia mimi naanza tuone , maana kila kitu naona kiko wazi kabisa....

hivi hamtaweza kunichangia nauli kwenda nje ya nchi, maana mimi nakwenda kumfungulia kesi ubelgiji kuna itifaki iliridhiwa na bunge letu kumshtaki mtu kama huyu bunge letu unajua ni wajinga wanaridhia itifaki za kidunia bila hata kujua impact zake.
hata mkapa mnamdekeza tu.

nimeongea na prof mmoja huko Belgium jamaaa yuko fresh na ameniahidi anapitia itifaki za bunge letu ili aone iko vipi halafu tujue cha kuanzia tuonyeshe hasira yetu.

msitegemee ripoti hiyo ni upuuzi tu
 
katika anuani ya gavana katika hii barua kuna kitu hii

Cable:41024 "BENKUU"

what is "BENKUU" ? does it mean "BENKIKUU"?. I'am a little bit suspicious.
 
mshamba wa kijijini
si mnichangie mimi hizo pesa nikakutane na huyo jamaa ubelgiji
 
Mbona haina Muhuri?

Barua ikiwa kwenye letterhead no official haitaji muhuri.

katika anuani ya gavana katika hii barua kuna kitu hii

Cable:41024 "BENKUU"

what is "BENKUU" ? does it mean "BENKIKUU"?. I'am a little bit suspicious.

Zamani kulikuwa na Cables. Siku hizi hazitumiki, lakini letterheads nyingi za Serikali bado ina details za cables.
 
Zakia Meghji. Waziri wa fedha atoa taarifa kuwa wizara yake haina taarifa juu ya kujiuzulu kwa Gavana.
 
Zakia Meghji. Waziri wa fedha atoa taarifa kuwa wizara yake haina taarifa juu ya kujiuzulu kwa Gavana.

Interesting enough, because I just heard the same thing, makes me wonder, sijui hii barua ya Mzee Mwanakijiji bado ina-cross Atlantic ocean ama ni vipi....
 
We utamweza kaka yangu Mwanakijiji..he's on top of of everything....
 
Du!

Ahsante mheshimiwa Mwanakijiji kwa kuileta barua hii hapa jamvini mwa JF.

Barua hii hata ukimpa mtu wa "forensic accounting" hatakuwa na kazi ya kubaini ujumbe hafifu wa barua hii na geresha kubwa ya bwana Balali.

Ni barua fupi yenye ujumbe rahisi kuuelewa na pia ni rahisi kuitilia mashaka kutokana na ujumbe wa mwandishi.

Kwanza anasema amelazwa kwa miezi mitatu sasa. Lakini sisi wananchi hatujui alienda lini huko hospitali na anaumwa nini!

Pili, anasema baada ya "major surgery" pametokea "complications". Ni upasuaji gani alifanyiwa na nini "brief" ya madaktari kwa vyombo vya habari vya TZ au ndio wamelala?

Na mwisho amefikia lini uamuzi wa kujiuzuru na kwa kushauriana na nani na vipi ataishi kwa muda uliobakia kwa maaana ni serikali ndio inalipa gharama yote kama sio pesa yake mwenyewe ya mfukoni?

Mimi kama mtanzania halisi sikubali kabisa upuuzi huu wa bwana Balali.

Sikubali kwa sababu bwana Balali anahusika kwenye tuhuma nyingi tu juu ya uhujumu uchumi wa nchi, kuzingatia taarifa ambazo bado zinaandaliwa na wataalam wa "auditing".
 
Not at all!

I certainly believe the letter is genuine and come from reputable source.

My suspicions really, rely on the message in the letter as it is very brief so I haven't got a clue about it -infact I don't understand it.

Mr Balali has not answered many questions about mismanagement of our public money through BOT. Surely, one has to come forward and clarify the letter and when are gonna get the answers?

However I appreciate your concern about the authenticity and intentions of my reply.
 
Kithuku, you have a point there.
Hiyo barua imechapwa katika stationary yenye heading ya BOT. Ukifikiria pia kuwa Balali wakati akienda Boston kwa 'check-up' hakujua kuwa itabidi ajiuzulu katika mazingira haya, hivyo si rahisi kuwa alienda na stationary za BOT.

Kwa hiyo mtazamo mzuri ni kuwa hiyo barua ilitayarishwa na kuchapwa Dar halafu akapelekewa huko Boston na kuambiwa ai-sign, mtu akaondoka nayo au ikatumwa kurudi Bongo. Kwa kufanya hivyo inaongeza pia uwezekano wa ku-leak, which is what happened.

Visitors and corresponding dates agree with your theory; plus the Ernst and Young report findings, of which we're not privy to, but the powers that be know its contents.
 
Wanajambo ni kweli kwamba Waziri wa Fedha Mama Zakhia Meghji amewaambia waandishi wa Habari kuwa "Hana Habari za kujiuzulu kwa Dr.Balali".Mama Meghji ameendelea kusema kuwa,ilipaswa apate barua hiyo rasmi Ofisini kwake (Hazina),lakini kwa mshangao mkubwa amesoma habari hizo ktk magazeti.Kwenye Taarifa ya Habari ya ITV leo Ijumaa saa mbili ya usiku wameonyesha "Kauli hiyo ya Mama Meghji".

Sasa Wakuu ingekuwa vyema tukapata uhakika wa habari hii ya kujiuzulu kwa Gavana,na kama kuna Uhakika wa habari hii Tuchukue jukumu la Kumtaarifu Mama Meghji.Jinsi habari hii ilivyo hapa, ninaamini kuwa ni ya kweli,lakini sijui kwa nini Serikali wanaikanusha.Haya Mazingaombwe ya Serikali ya Kikwete ni Makubwa.
 
Tatizo ni kuwa barua hii ilikuwa imetumwa Ikulu; sasa mjanja mmoja akaamua kuilikisha kwa waandishi kabla haijafika Ikulu/haijatangazwa rasmi. Na binafsi kitu kimoja kinachoweza kutokea na msishangae ni kuwa Rais akiamua kukataa kujiuzulu kwa Balali kuwakomoa wale waliolikisha barua hii. Hata hivyo kuna jambo jingine hapa kuhusu mama Meghji, Balali hayuko chini ya Meghji (at least not directly) ndiyo maana barua imeelekezwa kwa Rais na ni jukumu la Ikulu kuvitangazia vyombo vyake kuwa Balali amejiuzulu.
 
Barua yenyewe jamani hata Heading hakuna. Husitake kutuzuga wee Balali (Balaa hili) kuwa huwezi kurudi kazini kwa sababu umefanyiwa Major Surgery. Tunajua sababu inayokufanya husirudi kazini na huenda Tanzania. Ulitakiwa uondoke muda mrefu sana katika hiyo nafasi ila tu ni mambo yenu ya kufichana fichana na kulindana. Vasco da Gama aliona noma kukuchomoa kwenye kiti chako, sasa hivi unajifanya oh Major surgery. Lakini imekuwa nafuu kujichomoa maana ungechomolewa kwa nguvu ya wananchi.
 
Tatizo ni kuwa barua hii ilikuwa imetumwa Ikulu; sasa mjanja mmoja akaamua kuilikisha kwa waandishi kabla haijafika Ikulu/haijatangazwa rasmi. Na binafsi kitu kimoja kinachoweza kutokea na msishangae ni kuwa Rais akiamua kukataa kujiuzulu kwa Balali kuwakomoa wale waliolikisha barua hii. Hata hivyo kuna jambo jingine hapa kuhusu mama Meghji, Balali hayuko chini ya Meghji (at least not directly) ndiyo maana barua imeelekezwa kwa Rais na ni jukumu la Ikulu kuvitangazia vyombo vyake kuwa Balali amejiuzulu.

Patamu hapo...
 
Back
Top Bottom