white wizard
JF-Expert Member
- May 18, 2011
- 8,314
- 13,277
Sio kweli kuwa wanaodai katiba mpya ni wanaharakati tu, kwani sioni kama nao ni wanufaika wakubwa, bali ni mwananchi wa kawaida kabisa!!na wanachi mbona walishatoa maoni yao kupitia tume ya warioba?ili kilichotokea kila mtu anajua nani ni mchawi (CCM), chama tawala ndio kizingiti kikubwa , kwani hawako tayari kuona madaraka ya RAIS, yanapunguzwa!!na kuwe na tume huru ya uchaguzi, matokeo ya rais yahojiwe mahakamani, teuzi za upendeleo zisiwepo, mbunge aweze kuwajibishwa na wapiga kura wake?!!kweli kwa haya machache tu ccm watakuwa tayari kuyaona yanafanyika?HAKUNA ANAYE PINGA KATIBA MPYA, ISIPOKUWA KWANZA WANAODAI KATIBA MPYA NI WANAHARAKATI WENYE VYAMA VYAO NA MATAKWA YA VYAMA VYAO. KWAHIYO MPAKA SASA WANASIASA KUDAI KATIBA NIKUTAFUTA KATIBA ITAKAYOJAA MLENGO NA MATAKWA YA WANASIASA KWA MASILAHI YA VYAMA VYAO. OMBILANGU NI KWAMBA, WANASIASA WOTE WA VYAMA VYA SIASA WAKAE PEMBENI KABISA KWAKUWA TAYALI WAMESHA NAJISI ZOEZI ZIMA. KWA HALI ILIVYO MPAKA SASA IKITOKEA MCHAKATO UKAWA RASMI KATIBA HAITATOKA TENA ZAIDI KAMA HATUTAKUWA MAKINI TUTAISHIA KWENYE MACHFUKO MAKUBWA. WANASIASA WA VYAMA VINGI HAWAWEZI LETA KATIBA KWAKUWA WANAMLENGO TOFAUTI.
Hivi leo tuseme ile katiba ya warioba ipitishwe kama ilivyo nani atakuwa mhanga mkubwa??kweli kuna mwananchi ambaye hataki kuona hayo?mtu unawekwa mahabusu miaka, huku DPP, anasema kirahisi tu ushahidi bado haujakamilika!!Kwa Afrika kumwambia kiongozi aliyeko madarakani akubali katiba kutoka kwa wananchi anaona ni sawa na kumshika MAKALIO!!
Hata hao upinzani wakiingia madarakani hiyo katiba wanayoipigania wataona tena ni kero kwao, hao ndio wanasiasa, lakini kama taifa likiamua katiba haitaweza kuchezewa chezewa tu.