FMES: Tuwakumbuke Wanamichezo Africa!

Pepe+Kalle,+front.jpg



- Jamani hivi kweli ninahitaji kusema zaidi, maana hapa kila kitu kinajisema chenyewe, Kabasele ya Mpanya Pepe Kalle RIP, chini kuna Emoro Attatche, kati kati ni kipenzi cha Marehemu Pepe aliyekua Atalaku wake na sasa ana bendi yake mwenyewe.

- Pepe Kalle marehemu, alikuwa mwanamuziki kutoka Zaire aliyefahamika sana hapa kwetu na aliwahi kutembelea sana Tanzania, yeye siku zote ndiye aliyekwua inspiration ya Jabali la Muziki yaani Marijani Rajab, kama unaukumbuka wimbo wa "Salama" basi utamuona Pepe Kalle kabisa katika kile kibao, ambaye mpaka kufa kwake alikuwa akioendesha bendi maarufu huko Zaire kwa jina la "Empire Bakuba", Mungu amuweke pahali pema peponi.

333.jpg



Respect.


FMEs!
 
Nashukuru sama Field marshall hasa hasa kwa wasifu wa Patrick Balisidya. Nillikuwa napenda sana jinsi muziki wake ulivyokuwa na asili ya Kitanzania, hakuwa naiga mziki wa Zaire kama baadhi ya wanamuziki wa kitanzania wa miaka ya 70. Siku hizi hatuna hayo utafikiri hatuna utamaduni wetu, hakuna mtu mwenye guts za kuanzisha kitu original ( Naelewa naelewa kuwa labda ukianzisha mziki kwa ajili ya art hutapata pesa lakini wakati mwingine ni vizuri kujitoa mhanga)
Wimbo mwingine mzuri wa Balisidya ni ule aliomtungia dada yake siku ya harusi. ( kuoana ni jambo lasifa nafikiri ulikuwa ukianza hivyo)

Lunalo,
Huyo dada yake na yeye ni siku nyingi ni Marehemu. Wakati akikaa Korogwe, ilikuwa nikienda kwake basi anatuwekea album za "kaka yake". Ila nilikuwa sijawahi kumuona hadi tulipohamia wote Dar na tulipoenda kwake ndiyo akatuambia huyu ndiyo Patrick. Siku hizo dada mtu anafahamika zaidi kwa jina May Materu hadi alipotunga kitabu na kujiandika "Ndyanao Balisdya".

Kuhusu Patrick kuiga miziki ya watu wengine hili hadi leo linanipa shida. Labda mkuu FMes anisaidie hapa. Kuna wimbo aliimba "tufurahi jama, tufurahi weekend ehh". Huu wimbo umefanana sana yaani kasoro maneno tu na lugha na wimbo wa Caiphus Semenya & Letta Mbulu uitwao everybody sing along. Huu unaweza kuusikiliza hapa: [ame]http://www.amazon.fr/Thalassa-collection-Afrique-Sud-Cap/dp/B00005UV78[/ame]

Sema ni kipande cha 30 seconds tu ila utausikia. Album hii ya mama Mbulu na mumewe ni ya mwaka 1980 http://www.discogs.com/Letta-Mbulu-Sound-Of-A-Rainbow/release/1527293


Kuna wimbo ambao nimegundua juzijuzi kuwa Marijan Shaaban alichukua beats zake ni huu hapa chini. Huu unafanana sana na wimbo wa Mayasa unavyoanza.
[ame]http://www.youtube.com/watch?v=MSrklNeDwNM[/ame]

Ngoja chini na mie nichangie mwanamziki mmoja: hmmm!!!
 
Nadhani wazazi wangu wangekuwa wanaingia hapa wangesema tumewasahau George Mkabya na Jean mwenda Bosko. Oh Tusimsahau Issa Matona naye.

watu wa liokuwa vijana miaka ya kati kati, sabini kulikuwa na mwanamuziki Silimu Ali naye alizuzua vijana enzi za bugi.

Tusiwasahau

Prince Nico Mbarga, The Soki Brothers, Mopero and nyboma among many
 
Lunalo,
Huyo dada yake na yeye ni siku nyingi ni Marehemu. Wakati akikaa Korogwe, ilikuwa nikienda kwake basi anatuwekea album za "kaka yake". Ila nilikuwa sijawahi kumuona hadi tulipohamia wote Dar na tulipoenda kwake ndiyo akatuambia huyu ndiyo Patrick. Siku hizo dada mtu anafahamika zaidi kwa jina May Materu hadi alipotunga kitabu na kujiandika "Ndanao Balisdya".




Nashukuru kwa hilo, ndiyo namfahamu nilikuwa mlimani wakati akifundisha na niliwafahamu baadhi ya rafiki zake ( ambao nadhani unawafahamu waalimu mashuhuri wa kiswahili na theatre Arts pale milmani) siko comfortable kutaja majina yao na hata jina la marehemu dada ya Patrick. Ilijulikana kama angekufa kwa hiyo hao marafiki walikuwa wana huzuni sana siku za mwisho. Alikuwa jasiri sana, alipotoka matibau aliweza sikumoja kushiriki katika moja ya maonyesho ya Paukwa group ( akiwa mmoja wa P.wanasanaa walioonyesha siku hiyo, nadhani mchezo ulikuwa Lina Ubani by P. Mlama)
 
- Wakuu vipi huku? Ni vyema sometimes tukawakumbuka wanamuziki wetu Africa, unajua majuzi nilienda huko Ma-Broadway kuona ile paly maarufu sana sasa hivi ya Fela, ambayo iko sponsored na PDidy akishirkiana na Jay-Z, what a play ndio nikaona kuwakumbuka wanamuziki wetu ni halali
sana.

- Tuanze na Mbaaraka Mwinshehe, hapa chini.



Respect.

FMEs!


Asante sana mkuu. sijui kama kuna mwenye picha za vigogo wa taarabu kama Issa Matona, na Ali Tajuruna.
 
Nashukuru kwa hilo, ndiyo namfahamu nilikuwa mlimani wakati akifundisha na niliwafahamu baadhi ya rafiki zake ( ambao nadhani unawafahamu waalimu mashuhuri wa kiswahili na theatre Arts pale milmani) siko comfortable kutaja majina yao na hata jina la marehemu dada ya Patrick. Ilijulikana kama angekufa kwa hiyo hao marafiki walikuwa wana huzuni sana siku za mwisho. Alikuwa jasiri sana, alipotoka matibau aliweza sikumoja kushiriki katika moja ya maonyesho ya Paukwa group ( akiwa mmoja wa P.wanasanaa walioonyesha siku hiyo, nadhani mchezo ulikuwa Lina Ubani by P. Mlama)

Huyu mama walikuwa marafiki sana na dada yangu miaka hiyoo. Infact alikuwa kama dada yake/mtani wake kwani wakati marehemu sister akianza kazi Roleza, huyu mama alikuwa hapo tayari. Ila tulipohamia Dar, nilikaa mwaka mmoja na nikarudishwa kijijini huko Sikonge. Kutoka hapo sikufanikiwa kumuona tena. Mikiki ya maisha ilifanya wakapoteana hadi alipokuja kupata PhD na akawa amerudi Tanzania akiwa tayari mgonjwa. Alianza kutafuta contact za rafiki zake wote. Basi wakawa wakiona tena karibu kila siku.

Hivyo, hao walimu wa UDSM kusema ukweli wengi siwafahamu na kwa sababu sikusomea hapo, na sikusoma masomo ya ARTS, siwafahamu. Hiki kitabu chake na cha huyo Mlama kama sikosei tulitumia kwenye Kiswahili mtiani wa form 4. Ilikuwa ni hadithi ya kijana wa Kigogo aitwaye Chonya of Chilonwa.

Turudi kwenye wanamuziki:

Lovi Longomba ni mwanamuziki wa Kikongo ambaye baba yake pia alikuwa mwana muziki kwenye kundi la Franco and TP OK Jazz. Lovi alikuja kuishi Tanzania na baadaye akahamia Kenya na mwisho akarudi tena Tanzania hadi alipokuja kupata ajali na kufariki. Watoto wake ni hawa wanajiita LONGOMBAS na mdogo wake ni Awilo Longomba.

Huyu jamaa alitesa sana wakati wa bendi ya Shika Shika na baadaye kuwa SUPER MAZEMBE. Super Mazembe nilifanikiwa kuja kuwaona walipokuja Dodoma miaka ya 80 mwanzoni. Ilikuwa furaha kusikiliza wimbo wa Kasongo, Nanga, Nabimakate na nyingine nyingi.

lla hawa jamaa nao naona walikuwa waki-copy. Ila copy yao kwa kweli imeniuwa maana walienda wakawacopy THE BEETLES. Hebu sikilizeni wimbo huu...................

[ame]http://www.youtube.com/watch?v=pzAsLAfqmVk[/ame]

url
 
Mkuu nazidi kukurudishia heshima. Unazidi kupanua wigo wa nini tunatakiwa kukiona ili tuweze kuijenga identity yetu. Ni mmoja ya watu ambao michango yao naipa heshima kubwa sana humu JF. Mungu akubariki!
 
Lunalo,
Huyo dada yake na yeye ni siku nyingi ni Marehemu. Wakati akikaa Korogwe, ilikuwa nikienda kwake basi anatuwekea album za "kaka yake". Ila nilikuwa sijawahi kumuona hadi tulipohamia wote Dar na tulipoenda kwake ndiyo akatuambia huyu ndiyo Patrick. Siku hizo dada mtu anafahamika zaidi kwa jina May Materu hadi alipotunga kitabu na kujiandika "Ndyanao Balisdya".

Kuhusu Patrick kuiga miziki ya watu wengine hili hadi leo linanipa shida. Labda mkuu FMes anisaidie hapa. Kuna wimbo aliimba "tufurahi jama, tufurahi weekend ehh". Huu wimbo umefanana sana yaani kasoro maneno tu na lugha na wimbo wa Caiphus Semenya & Letta Mbulu uitwao everybody sing along. Huu unaweza kuusikiliza hapa: http://www.amazon.fr/Thalassa-collection-Afrique-Sud-Cap/dp/B00005UV78

Sema ni kipande cha 30 seconds tu ila utausikia. Album hii ya mama Mbulu na mumewe ni ya mwaka 1980 http://www.discogs.com/Letta-Mbulu-Sound-Of-A-Rainbow/release/1527293


Kuna wimbo ambao nimegundua juzijuzi kuwa Marijan Shaaban alichukua beats zake ni huu hapa chini. Huu unafanana sana na wimbo wa Mayasa unavyoanza.
http://www.youtube.com/watch?v=MSrklNeDwNM

Ngoja chini na mie nichangie mwanamziki mmoja: hmmm!!!

- Patric na kundi lake la muziki walianza kama Marijan Rajab, yaani wasomi kwa hiyo uwezo wao wa kuona mbali ulikuwa umepanuka kidogo, mara kwa mara Patric alikua akiiga style za Jive za wazulu hasa baada ya mama wa ki-Zulu Ninie, kujiunga nao yaani Afro 70, kwa mfano wimbo wake wa "Kwaheri ndugu Samora", ambao uliwika sana enzi hizo.

- Baadaye akaja Lwambo Makiadi, sasa Patric tena akabadili mipigo yake na kuanza kupiga solo kama Lwambo, hasa katika wimbo wake wa "Mapinduzi ya Africa" ambao ndio uliompa tiketi ya kutuwakilisha Tanzania, kule Lagos kwenye maonyesho ya mtu mweusi. Akiwa Lagos bendi iliyotia fora sana ilikuwa ni ya Osibisa Group, toka UK aliyokua comprised na wa-Ghana, kina Ted-Oseyi na McAcktonto, Patric was impressed na ile beat yao ndipo sasa akaubadili kabisaa muziki wake na kuwa Afro Beat, mpaka alipofariki bado alikuwa akipiga muziki huo wa kimajuu.

- Patric was a big talent na tatizo lake ni moja tu nalo alishindwa kuki-transfrom kipaji chake na kuweka legacy imara kuliko iliyopo, he made a lot of money lakini hakuwa mtunzaji mzuri na haku-invest kabisaa as the results hakuacha chochote worthy kwa familia yake, that is sad truth, lakini bado muziki wake upo na mdogo wake Freedom anajaribu sana kupanda juu lakini bado sana.

Respect.


FMEs!
 
Msondo Ngoma Band

SANY5713.jpg


MIAKA 48 KATIKA MUZIKI - MAALIM MUHIDIN GURUMO KUACHA MUZIKI

1.jpg


Akizungumza katika kipindi cha bambataa leo alhamis maalim huhidini gurumo, amekiri kuwa yuko mbioni kuacha muziki kwa kuwa umri sasa umeenda sana na anafikiria kufanya mengine katika familia yake ila yoyote atakae kuwa tayari kutaka ushauri kuhusu uimbaji atakuwa tayari kumsaidia kimawazo ikumbukwe kuwa gurumo alianza muziki mwaka 1961, na kupitia bendi tofauti tofauti.

naweza kusema kweli ni nguli wa muziki nchini,au kwa lugha ya wenzetu wanasema legendery.
Mzee Gurumo amekaaa kwenye sanaa hii akiwa na miaka ishirini na moja tu,sasa piga hesabu leo hii ana miaka mingapi?na bado anadunda kwenye fani..... amepita pia katika bendi tofauti nyingi tu ikiwemo ya msondongoma ambayo amedumu kwa miaka takriban 29 swali linabaki kuwa atakapo jiuzulu na kwenda kupumzika bendi ya msondo itakuwaje kwakuwa yeye ndie kiongozi aliedumu na bendi hiyo kwa muda mrefu unadhani ndio kufa kwa bendi au?

Respect.


FMEs!
 
FMES...hii thread muhimu sana ..itafanya vijana wajuwe kuwa sisi ndio tuliokula raha....

mimi naomba kuwashirikisha KINGI [king] ENOCK...huyu alikuwa mwalimu maarufu wa muziki aliyeifanya sikinde ipige muziki ulioenda shule..yeye mwenyewe akipiga SAX....

Enzi hizo sikinde wanalo basi lao.....kila weekend jioni lilikuwa likisomba mashabiki na kuwapeleka kula raha DDC MLIMANI PARK...[Ndio oposite na mlimani park mall ya sasa]...

Hapo wale wa msondo ....walikuwa hawahitaji usafiri ..wao hata kwa mguu walitembea toka pande zote za jiji kwenda pale AMANA kucheza msondo ngoma...

Wale wapenzi wa OSS[ochestra safari sound]...walikuwa wakichukuliwa na usafiri mjini hadi KIMARA....wanakula raha hadi asubuhi...wana masantula,...kumbukeni mzee kisima pia alijaribu kuwa na timu ya mpira wa kulipwa sambamba na SUPERSTAR ..timu iliitwa SAFARI CONTRACTORS......kisima bado mkewe anamiliki safari jewellers...lakini alivuma sana sana!!

Pale urafiki watu wa viwandani walikuwa wanakula raha URAFIKI HALL na URAFIKI JAZZ ya kina hamza kalala...wakati mwingine wana BAYANKATA .- uda JAZZ pia walipiga pale...

Ukienda ukanda wa kurasini walikuwa wanakula raha na BIASHARA JAZZ....

acha bendi za majeshi kama wana mkote ngoma,MAGEREZA JAZZ,POLISI JAZZ....MWENGE JAZZ wana PASELEPA!!

uKIENDA ukanda wa kinondoni unakula raha na MARQUIZ DU ZAIRE...PALE FM STUDIO..ENZI HIZO TUNAPAITA LANGATA....UKIJA Sinza unakula raha na SUPER MATIMILA.....Au badaye LEGHO STARS....

mwananyamala mnakula raha na wanaPAMBAMOTO...vijana jazz....ukija ukanda wa kati unakutana na WATUNJATANJATA....WASHIRIKIKA TANZANIA STARS....

piA KULIKUWA NA BENDI KAMA BIMA LEE..wana motisha..,super rainbow[eddy sheggy], SAMBULUMAA BAND..... ETC....ILIKUWA SAFI KWANI HATUKUWA KABISA NA USHABIKI NA BAND ZA NJE AU MIZIKI YA NJE,,..KWA KIASI CHA SASA!!

VIKUNDI VYA UTAMADUNI PIA HAVIKUKOSA WAPENI....DDC KIBISA NGOMA TROUPE...NA MUUNGANO!!...TULIKUWA TUKIPATA RATIBA YA BURUDANI KWENYE GAZETI LA UHURU....PAMOJA NA RATIBA YA MOVIES...

KAMA KUNA MTU ANA COPY YA MZALENDO AU UHURU SEHEMU YA BURUDANI NAOMBA ABANDIKE HAPA TUKUMBUKE!!
 
FMES...hii thread muhimu sana ..itafanya vijana wajuwe kuwa sisi ndio tuliokula raha....

mimi naomba kuwashirikisha KINGI [king] ENOCK...huyu alikuwa mwalimu maarufu wa muziki aliyeifanya sikinde ipige muziki ulioenda shule..yeye mwenyewe akipiga SAX....

Enzi hizo sikinde wanalo basi lao.....kila weekend jioni lilikuwa likisomba mashabiki na kuwapeleka kula raha DDC MLIMANI PARK...[Ndio oposite na mlimani park mall ya sasa]...

Michael Enock "Teacher": Sikinde Ngoma Ya Ukae!


Mlimani.gif



Like just about everybody, I love the Tanzanian band DDC Mlimani Park Orchestra, led by Michael Enoch (above). We were very fortunate indeed when a wonderful "Best of" compilation of their hits was released some time ago (Sikinde [Africassette AC9402] in the U.S.). I believe it may still be in print. One CD, however, just isn't enough to embrace all of the "best" of this prolific congregation. Fortunately, I have in my posession the two-volume Best of DDC Mlimani Park Orchestra issued in Kenya and produced by our friend Doug Paterson of the East African Music Page.

So, here are five tunes from those LPs. "Mume Wangu Jerry" and "M. V. Mapenzi 1" are from Best of DDC Mlimani Park Orchestra Vol. 1 (Ahadi AHDLP 6002, 1986). The other songs are from Best of DDC Mlimani Park Orchestra Vol. 2 (Ahadi AHDLP 6006, 198.

DDC Mlimani Park Orchestra - Mume Wangu Jerry

DDC Mlimani Park Orchestra - M. V. Mapenzi 1

DDC Mlimani Park Orchestra - Matatizo ya Uke Wenza

DDC Mlimani Park Orchestra - Majirani Huzima Radio

DDC Mlimani Park Orchestra - Naheshimu Ndoa


Respect.

FMEs!
 
Discography of MLIMANI PARK ORCHESTRA

<hr>
Mlimani Park OrcestraÊ(also known as DDC Mlimani Park Orchestra, after its sponsor the Dar es Salaam Development Corporation), led by Michael Enoch, above, has been a fixture on the Tanzanian music scene since 1978. The great majority of the listings in this discography were kindly provided by Doug Paterson, producer of The Best of DDC Mlimani Park Orchestra Vols. 1 & 2, among other recordings. For more information on East African music, go to his East African Music Page .

-- John Beadle


<hr>
1979?

Various Artists
Hit Parade Number 1 (LP; Polydor [Nairobi] POLP 516)
[A] Sikujua Utabadilika (Simba Wanyika) / Sina Makosa (Les Wanyika)
Sauda Unatia Aibu (DDC Mlimani Park Orchestra) / Charo Ni Wasi (Maroon Commandos)

1982
DDC Mlimani Park Orchestra
Taxi Driver (LP; Polydor [Nairobi] POLP 523)
[A] ?
?

1982
DDC Mlimani Park Orchestra
Dunia Kuna Mambo (LP; Polydor [Nairobi] POLP 530)
[A] Asie Sikia la Wazazi /ÊLinda Rafiki Yangu / Fikirini Nisamehe
Ubaya / Penzi la Mwisho / Duniani Kuna Mambo

1983
DDC Mlimani Park Orchestra
Pesa Pt. 1 / Pesa Pt. 2 (7" 45; Ahadi [Nairobi] AHD 01)

1983
DDC Mlimani Park Orchestra
Matatizo ya Nyumbani Pt. 1 / Matatizo ya Nyumbani Pt. 2 (7" 45; Ahadi [Nairobi] AHD 02)

1983
Various Artists
African Gold Vol. 1 (LP; Makumbusho AGLP 001)
[A] Kifo cha Mbaraka Mwinshehe (Orchestra Magola International) / Ubaya (DDC Mlimani Park Orchestra)
Mama Ester (Orchestra Simba Wanyika) / Stellah Mwenye Fikara Nzuri (Orchestra Vijana Jazz)

1985
Various Artists
Swahili Hits (Cassette; Ahadi [Nairobi] AHD (MC) 001)
[A] Tabu (Juwata Jazz Band) / Ubaya wa Jirani (Dar International Orchestra) / Moyo Wangu (Bimalee)
Pesa (DDC Mlimani Park Orchestra) / Dunia Msongamano (Orchestra Safari Sound) / Mama Njiti (Vijana Jazz Orchestra)

1985
DDC Mlimani Park Orchestra
Matatizo ya Nyumbani (Cassette; Ahadi [Nairobi] AHD (MC) 002)
[A] Diana / Pesa No. 2 / Pole Mkuu Mwenzangu
Pesa / Matatizo ya Nyumbani / Hiba

1985
Various Artists
Swahili Hits Vol. 2 (Cassette; Ahadi [Nairobi] AHD (MC) 004)
[A] Wastara (International Safari Sound) / Karubandika (Orchestra Maquis Original) / Makulata (Bimalee Orchestra)
MV Mapenzi (DDC Mlimani Park Orchestra) / Mtoto Nampenda (Juwata Jazz Band) / Dunia Uwanja Wafujo (Dar International Orchestra)

1985
DDC Mlimani Park Orchestra
MV Mapenzi (Sauda) Pt. 1 / MV Mapenzi (Sauda) Pt. 2 (7" 45; Ahadi [Nairobi] AHD 06)

?
DDC Mlimani Park Orchestra
Siwalaumu Wakwe Pt. 1 / Siwalaumu Wakwe Pt. 2 (7" 45; CBS [Nairobi] CBS (K) 7024)

?
DDC Mlimani Park Orchestra
Kiu ya Jibu Pt. 1 / Kiu ya Jibu Pt. 2 (7"45; CBS [Nairobi] CBS (K) 7025)

1985
DDC Mlimani Park Orchestra
Hiba Pt. 1 / Hiba Pt. 2 (7" 45; Ahadi [Nairobi] AHD 07)

1986
DDC Mlimani Park Orchestra
The Best of DDC Mlimani Park Orchestra (LP; Ahadi [Nairobi] AHDLP 6002)
[A] Neema / MV Mapenzi No. 2 / Mume Wangu Jerry
Clara / Usitumie Pesa Kama Fimbo / MV Mapenzi No. 1

1988
Various Artists
Tanzania Hit Parade '88 (LP; Ahadi [Nairobi] AHDLP 6005)
[A] Mundinde (Vijana Jazz Orchestra) / Clara (Maquis Original) / Marashi ya Pemba (International Orchestra Safari Sound [Duku Duku])
Christina Moshi (International Orchestra Safari Sound [Ndekule]) / Chaurembo (Vijana Jazz Orchestra) / Hasira (DDC Mlimani Park Orchestra)

1988
DDC Mlimani Park Orchestra
The Best of DDC Mlimani Park Orchestra Vol. 2 (LP; Ahadi [Nairobi] AHDLP 6006)
[A] Mtoto Akililia Wembe / Matatizo ya Uke Wenza / Conjesta
Majirani Huzima Radio / Naheshimu Ndoa / Epuka Jambo Lisilokuhusu

1988 DDC Mlimani Park Orchestra
Maisha Ni Kuona Mbele (LP; Polydor [Nairobi] POLP 579)
[A] Maisha Ni Kuona Mbele / Nani Aliyemdanganya Mpenzi Wangu
Mpende Mwenzio / Kisonoko

1989
DDC Mlimani Park Orchestra
Dua la Kuku (LP; Polydor [Nairobi] POLP 589)
[A] Dua la Kuku / Nakubali Nimekosa
Heko Rais Moi / Ukombozi wa Africa

1990
Various Artists
Tanzania Dance Bands Vol. 1: Sikinde (CD; Monsun [Hamburg] MSCD 9.00902) (CD; Africassette [Detroit, USA] AC9402 [1994, as "Sikinde"])
Neema / Mnanionyesha Njia ya Kwetu / Tucheze Sikinde / Ubaya / Mtoto Akililia Wembe / Tangazia Mataifa Yote / Fikirini Nisamehe / Nalala kwa Taabu / Usitumie Pesa Kama Fimbo

?
Various Artists
Swahili Hits Vol. 3
(Cassette; Ahadi [Nairobi] AHD (MC) 008) [A] Kifo (Super Matimila Orchestra) / Clara (Orchestra Maquis Original) / Christina Moshi (International Orchestra Safari Sound)
Majirani Huzima Radio (DDC Mlimani Park Orchestra) / Solemba (Juwata Jazz Band) / Mary Maria (Vijana Jazz)

Early 1990s?
Various Artists
Tanzania Hit Parade Vol. 2 Cassette; Ahadi [Nairobi] AHD (MC) 013)
[A] Mtumishi Nyumbani (Kurugenzi Jazz Band) / Husia Mwanadamu (Mlimani Park Orchestra) / Asha Mwana Seif (Juwata Jazz Band)
Jirani (African Roots) / Saleh (Orchestra Maquis Original) / Mwisho wa Mwezi ( Vijana Jazz Band)

?
DDC Mlimani Park Orchestra
Tunazikumbuka Vol. 1 (Cassette; Ahadi [Nairobi] AHD (MC) 015)
[A] Barua Kutoka kwa Mama / Celina / Mwenyekiti Mwalimu Nyerere
Maua Ni Nyumbani / Weekend / Kassim

?
DDC Mlimani Park Orchestra
Utafiti wa Mpenzi (Cassette; Ahadi [Nairobi] AHD (MC) 6014)
[A] Utafiti wa Mapenzi / Husia za Mwanadamu / Maisha Ni Kuona Mbele
Ukombozi wa Afrika / Tusameheane Wanadamu / Visa vya Wenya Nyumba

?
DDC Mlimani Park Orchestra
Tunazikumbuka Vol. 3 (Cassette; Ahadi [Nairobi] AHD (MC) 017)
[A] Kassim Amefilisika / Ugomvi Kila Siku Sipendelei / Hadija
Tuwe na Nidhamu / Talaka ya Hasira / Fitina za Watu

?
DDC Mlimani Park Orchestra
Tunazikumbuka Vol. 4
(Cassette; Ahadi [Nairobi] AHD (MC) 018)
[A] Nawashukuru Wazizi / Gama Unisamehe / Pongezi Wanakisomo
Tucheze Sikinde / Duniani Kuna Mambo / Taxi Driver / Ubaya

?
DDC Mlimani Park Orchestra
Sitokubali Kuwa Mtumwa (Cassette; Ahadi [Nairobi] AHD (MC) 6024)
[A] Sitokubali Kuwa Mtumwa / Ukali wa Nyuki / Safia
Naomi / Epuka Jambo Lisilokuhusu No. 2 / Naomba Tuaminiane

?
DDC Mlimani Park Orchestra
MV Mapenzi (Cassette; Ahadi [Nairobi] MSKCAS 501)
[A] MV Mapenzi / Christina Bundara / Hasira
Clara / Mume Wangu Jerry / Munanionyesha Njia ya Kwetu

?
DDC Mlimani Park Orchestra
MV Mapenzi No. 2 (Cassette; Ahadi [Nairobi] MSKCAS 504)
[A] MV Mapenzi No. 2 / Naijibu Telegram / Zuwena
Neema / Siwalaumu Wakwe / Naheshimu Ndoa

?
DDC Mlimani Park Orchestra
Majirani Huzima Radio (Cassette; Ahadi [Nairobi] MSKCAS 506)
[A] Majirani Huzima Radio / Matatizo ya Uke Wenza / Kiu ya Jibu
Barua Kutoka kwa Mama / Ndoa ya Lazima / Dawa ya Pendo

?
DDC Mlimani Park Orchestra
Mtoto Akililia Wembe (Cassette; Ahadi [Nairobi] MSKCAS 510)
[A] Mtoto Akililia Wembe / Dada Bishada / Conjesta
Shahada ya Uvumilivu / Wema Waleta Kilio / Epuka Jambo Lisilokuhusu

?
DDC Mlimani Park Orchestra
Golden Hits 80s (Cassette; Ahadi [Nairobi] MSKCAS 511)
[A] Pata Potea / Talaka Rejea / Wivu / Aza
Shemeji Issa / Penzi la Mwisho / Edita / Visa Vimenichosha

1994
DDC Mlimani Park Orchestra
Maisha na Mapambano (Cassette; label unknown RC 312)
[A] ?
?

1994
Mlimani Park Orchestra
Sungi (CD; Popular African Music [Frankfurt] PAM 403)
Uzuri Wa Mtu / M.V. Mapenzi / Hiba / Sungi / Naukata Ndima / Duniani Kuna Mambo / Hapendeki / Penzi La Fukara / Nzimu

1995
Various Artists
Muziki wa Dansi: Afropop Hits from Tanzania (CD; Africassette [Detroit, MI, USA] AC 9403)
Ngalula (Orchestra Maquis Original) / Tupa Tupa (Juwata Jazz) / Chatu Mkali (International Orchestra Safari Sound) / Mpenzi Luta (Orchestra Maquis Original) / Msafiri Kakiri (Juwata Jazz) / Edita (Mlimanii Park Orchestra) / Makumbeli (Orchestra Maquis Original) / Somboko Ama (International Orchestra Safari Sound) / Usia Kwa Watoto (Juwata Jazz)

?
DDC Mlimani Park Orchestra
Nelson Mandela (Cassette; Ahadi [Nairobi] MSKCAS 512)
[A] Nelson Mandela / Tumetoka Mbali / Utamaduni
Kauli Yako Nimeisikia / Maneno Maneno ya Nini / Kupenda Sio Ndoto

1996
DDC Mlimani Park Orchestra
Ndomo Huponza Kichwa (Cassette; FM Productions no reference number)
[A] Esta / Kitendawili / Hasidi / Dawa ya Dini / Esta (Remix)
Mdomo Huponza Kichwa / Maluma / Uchungu wa Mwana / Mdomo Huponza Kichwa


Respect.

FMEs!
 
Mlimani Park Orchestra: Wana Sikinde Ngoma Ya Ukae.

sikindebc1.jpg



Bila hiana wala ubishi, DDC Mlimani Park(Wana-Sikinde Ngoma ya Ukae) ni mojawapo ya bendi zilizowahi kutamba na kujizolea sifa kemkem nchini Tanzania. Pichani ni kikosi kizito cha Wana-Sikinde. By Fresh Jumbe



WALIOSIMAMA NYUMA TOKA KUSHOTO:Habibu Abbas Mgalusi “Jeff” (Drums), anayefuatia ni Shaaban Lendi (saxphone), Hamisi Milambo (Trumpet), Nyuma ya Hamisi Milambo ni Kalamazoo (Saxphone), Huruka Uvuruge (Rhythm guitar), Machaku Salum (Trumpet), Kassim Rashid “Kizunga” (Lead guitar), Charles Ngosha (Bass) na Ali Jamwaka au Ali “Tumba” (Congers).


WALIOCHUCHUMAA MBELE TOKA KUSHOTO:Wa kwanza simjui, wa pili ni Juma Shabani (Drums) (Huyu nilikuwanae Dar International, Anaefuata mwenye kofia ni Tino Masinge (Muimbaji) nae pia nilikuwa nae Dar International na nimeimba nae karibu nyimbo zote kule Super Bomboka, alijiunga na Sikinde baada ya mimi kutoka.



Anaemfuatia Tino kwa nyuma kidogo simjui, anaefuatia mwenye viatu vyeupe ni Husein Jumbe (Muimbaji), nyuma ya husein Jumbe aliyeshikwa bega na Dede simjui, halafu Shaaban Dede (aliyegeuka nyuma na kumshika mwenzie bega (Muimbaji), baada ya Dede kwa mbele kidogo ni Adam Bakari “Sauti ya zege” (Muimbaji), Nyuma kidogo ya Adam ni Hassan Kunyata (Muimbaji), Baada ya Kunyata ni Joseph Bernard (Saxphone) na wa mwisho kabisa mwenye kipara simjui.


Respect.


FMEs!
 
Orchestra Super Mazembe, Kaivaska

2751804607_89475b66b0.jpg


Orchestra Super Mazembe reissue the passport to fun with each spin of Kaivaska, their 1982 album released in the U.K. by Virgin Records. The nine songs comprising Kaivaska are of consistent quality, energizing and vibrant. Collectively, they commemorate an African dance band at the top of its form connecting with the recording studio. Which hardly ever happens.

A friend (of Danish decent, so she really meant it) once described Orchestra Super Mazembe as "the happiest band in the word." Its membership might argue otherwise, as they weathered much of the grief routinely visited upon working musicians in Africa. Orchestra Super Mazembe — the latter portion of its name an homage to earth-moving equipment — relocated to Eastern Africa, specifically Nairobi, to establish itself at a remove from the highly competitive scene in its native Zaîre. Earlier on, the band had its instruments repossessed by its first patron immediately prior to crossing the Zambian border; fortunately, the club owner in Zambia owned gear they could use. Subsequent morbidity and mortality influenced Super Mazembe's shifting membership. By the mid-'80s, the group was effectively out of the running.

Factoring in these career speedbumps, my friend's words hold true. There probably isn't music much happier sounding than that played by Orchestra Super Mazembe. As one might expect of Congolese natives, Super Mazembe dealt in Congolese rumba (or [ame="http://en.wikipedia.org/wiki/Soukous"]soukous[/ame]), the Latinate sound that still remains the Congo Republic's great contribution to music, one that could be described as salsa with the hysteria filtered out. Super Mazembe augmented their rumba template with elements of the local music in their adopted home, Kenyan [ame="http://en.wikipedia.org/wiki/Benga"]benga.[/ame] They weren't the first or the last band to do so, but may have been the best at it. Ultimately, theirs was indisputably an African music, with contours somewhat more linear than its Afro-Cuban antecedents, yet every bit as sensual.

Those readers interested in the greater history of Orchestra Super Mazembe should investigate Giants Of East Africa, a career-spanning overview of the band's music from the mid-'70s through the subsequent decade, as issued on a compact disc a few years ago by the Earthworks label. Trevor Herman's liner notes for this collection are the defining historical account this splendid band deserves. Even as he recounts their success on the hotel and agricultural fair circuit — really — Herman observes that Super Mazembe's timing for success outside of East Africa could have been better. The band peaked in the era of Kaivaska's release, then disintegrated shortly thereafter, a few years in advance of the coming world music boomlet.


2752638534_cdfb5ed2e4.jpg
 
Super Mazembe

emalp0560.jpg




Orchestra Super Mazembe was a popular band based in [ame="http://en.wikipedia.org/wiki/Kenya"]Kenya[/ame][ame="http://en.wikipedia.org/wiki/Soukous"]Soukous[/ame]) music. The band had roots in Super Vox, a band formed in 1967 in [ame="http://en.wikipedia.org/wiki/Democratic_Republic_of_the_Congo"]Congo[/ame] playing Lingala (then Zaire) and led by Mutonkole Longwa Didos. The band moved to Nairobi in 1974 and changed its name to Orchestra Super Mazembe.

Their biggest hit was "Shauri Yako", a cover song originally performed by Nguashi Ntimbo & Festival Du Zaire. Other popular songs included "Samba", "Bwana Nipe Pesa" and "Kassongo". The group was disbanded in 1985. Super Mazembe is considered as one of the golden era of Kenyan [ame="http://en.wikipedia.org/wiki/Lingala_music"]Lingala music[/ame] acts alongside [ame="http://en.wikipedia.org/wiki/Les_Mangelepa"]Les Mangelepa[/ame], Baba Gaston and [ame="http://en.wikipedia.org/wiki/Samba_Mapangala"]Samba Mapangala[/ame] <sup id="cite_ref-0" class="reference">[1]</sup>.

Like many East African and Congolese groups, Super Mazembe experienced constant line-up changes. Some of its members were:
<!-- start content -->
  • Mutonkole Longwa Didos (vocals)
  • Lovy Longomba (vocals) - Left the band in 1981 and formed groups "Super Lovy" and later "Bana Likasi". He died in 1996. Lovy is son of [ame="http://en.wikipedia.org/wiki/Vicky_Longomba"]Vicky Longomba[/ame] and brother of [ame="http://en.wikipedia.org/wiki/Awilo_Longomba"]Awilo Longomba[/ame], both famous Congolese musicians. Lovy's sons Christian and Lovi have formed [ame="http://en.wikipedia.org/wiki/Longombas"]Longombas[/ame], today a popular hip hop group in Kenya.
  • Kassongo Wa Kanema (vocals) -Left the band in early 80'a and joined [ame="http://en.wikipedia.org/wiki/Orchestra_Virunga"]Orchestra Virunga[/ame].
  • Loboko Bua Mangala (guitar)
  • Kilambe Katele Aley (vocals)
  • Bukasa wa Bukasa "Bukalos" (lead guitar) -Died 1989
  • Kayembe Miketo (guitar) -Died 1991
  • Mwanza wa Mwanza Mulunguluke (bass guitar)
  • Komba Kassongo Songoley (guitar) -Died 1990
  • Kitenge Ngoi wa Kitombole (drums)
  • Musa Olokwiso Mangala
  • Atia Jo (Frederick Mulunguluke Mwanza) (bass guitar) -Died 2006<sup id="cite_ref-1" class="reference">[2]</sup>

Orchestra_Super_Mazembe.jpg

Respect.

FMEs!
 
Thursday, 12 August, 2004, Tanzania mourns beloved musician

<!-- S BO --> <!-- S IBYL --> By Vicky Ntetema

BBC correspondent in Dar es Salaam
<!-- E IBYL --> <!-- S IIMA -->
_39939140_albumcover203ok.jpg
<!-- E IIMA -->


The funeral of one of Tanzania's most loved musicians, Patrick Balisidya, has taken place in Dar es Salaam.
Hundreds of fans turned out on Tuesday to mourn the co-founder of the Afro 70 band, popular in East Africa in the 1970s.His music fused traditional beats of percussion instruments such as marimba and drums with modern music, guitars, saxophones and trumpets.
Described by many as a down-to-earth man, Balisidya's lyrics often carried educative messages.

The wedding song


He used his music to publicise campaigns such as trachoma and HIV/Aids. Balisidya's father, Mzee Yohana Balisidya, said that his songs carried good instructions for everyone.
<!-- S IBOX -->
" Patrick Balisidya was a very good man... he was like a brother to me " Joyce Chambai Patrick Balisidya's neighbour


<!-- E IBOX --> "He was my first born, one of the beloved sons in my family... I was very impressed and very pleased to hear his songs... some of the songs are still as good as they were," Mzee Balisidya said. Produced in the 1970s, Harusi - meaning wedding - is one of Balisidya's most popular songs.
Nowadays there is almost no wedding reception in Tanzania that does not play the song. The lyrics tell new partners in marriage to be humble and generous in their new home, to respect their parents and to teach their children manners.

'Unique sounds'


Balisidya's neighbour since 1975, Mrs Joyce Chambai, said he used to like to play music in front of his house and taught many people how to play his instruments.
"Patrick Balisidya was a very good man, a very good neighbour, more than a neighbour, he was like a brother to me."
<!-- S IIMA -->
_39939544_formerbandmembers.jpg
<!-- E IIMA --> His younger brother Freedom was a member of Afro 70 founded in the 1970s.

"Patrick taught me music... he composed and produced unique sounds which distinguish him from other artists. We have lost a huge talent which cannot be replaced," he said.


Afro 70 disbanded after a terrible traffic accident in 1975 when all their instruments were destroyed. The band never recovered from the loss, and Balisidya continued a solo career in Sweden. Original members of the band are thinking of reforming to honour Patrick Balisidya's memory.
Your memories and tributes to Patrick Balisidya:

<hr> Patrick Balisidya was a very humble man, friendly and down to earth kind of guy. I had the privileged of working with him in 2000 at the Don Bosco Studio. He helped produce a song I recorded with my cousin. I saw him perform once at the Mnazi Mmoja grounds, Dar Es Salaam, Tanzania, his showmanship on stage was truly amazing; he was in sync with the audience. He really knew how to move a crowd and he was loved for that. Although it was the year 2000, his dress code still reflected the 70's style he sort of wanted to make a fashion statement. Furthermore, he is one of the few Tanzanian artists to bring our music to an international audience. My condolence goes to his family. He will be missed and may his soul rest in perfect peace.
Balozi Dola, New York, USA




I remember Afro 70 band and the late Patrick Balisidya during the 1970s. My brother was in the band too, I saw him today on TV at the funeral. Their songs were just good. May God rest his soul in eternal peace.
Murad Vellani, Zanzibar, Tanzania



Patrick Balisidya's death came as a shock to me. As a young child in the 1970's in Dar-es-Salaam, the radio was my best friend. Balisidya's sweet lyrics and flowing melody captured the memories of all newly weds in the coastal shores. But most importantly, his talent rewarded Tanzania with its own soundtrack. Angels are singing a sweeter melody tonight in heaven. May God bless Patrick Balisidya.
Emanuel Nkulila, Los Angeles, California, USA



I was in secondary school in the 1970s and I used to enjoy listening to the slow lyrics of Patrick Balisidya. I loved his song, "Nikitisama Dirishani oo, naona ni mvua yanyesha oo". That song was our class master's favourite and I used to go near his house to listen to the music that used to flare through his living room window, over the weekend. Patrick Balisidya will be missed by Kiswahili speaking fans all over east, central and south Africa. May the almighty, God, rest his soul in eternal peace. I will miss him.


Daudi Elijah Osoro, Raleigh, North Carolina, USA
Patrick B was a great musician and my family and I knew him since the 1970s. He came to perform on my sister's wedding in 1975. He sang Harusi. He will never be forgotten and the last time I saw him was about three months ago 2004 , when he came back from Sweden he visited our studios of Clouds FM in Dar. May his soul rest in eternal peace.


Mpr'ss Gypsy Vancy, Dar es Salaam , Tanzania
I happened to hear about Patrick Balisidya from my Mama. She is known as Mama Africa a producer / presenter of Radio Clouds FM here in Dar es Salaam. I saw photographs of the late Patrick in my grandma's family albums from 1975 when he came to perform with Afro 70 at my aunt's wedding. My family and I will always treasure what memories we have of him. He was a great musician and will be missed by many and my family is one of those who will miss him dearly. May his soul rest in eternal peace.

Precious G Huggins, Dar es Salaam, Tanzania.


Patrick was great from secondary school in Dodoma through to Dar technical college and to a musician with sense and direction. It is a Kongwa Music Spirit that is regrettably fading.
Albert, Kongwa



One of the most talented young musicians in his time, who tried to carve Tanzanian music into its own blend - against and amidst the powerful Western and Congolese music. I remember him when he was at the then Technical College Dar, how he teamed up with the late Emmanuel Joseph to play with Dar Jazz B... May his soul rest in peace!!

John W.Nyoka, Windhoek, Namibia


As a music-loving young man growing up in Kenya's Rift Valley, I remember Patrick Balisidya and the Afro 70s. Perhaps the most memorable song was "Dirishani". It was a block-buster, especially on the then Voice of Kenya (VOK). May he rest in peace.
James Sang, Washington DC, USA



Patrick Balisidya was a very humble man, friendly and down to earth kind of guy. I had the privileged of working with him in 2000 at the Don Bosco Studio. He helped produce a song I recorded with my cousin. I saw him perform once at the Mnazi Mmoja grounds, Dar Es Salaam, Tanzania, his showmanship on stage was truly amazing; he was in sync with the audience. He really knew how to move a crowd and he was loved for that. Although it was the year 2000 he dress code still reflected the 70s style he sort of wanted to make a fashion statement. Furthermore, he is one of the few Tanzanian artists to bring our music to an international audience. My condolence goes to his family. He will be missed and may his soul rest in perfect peace.
Balozi Dola, New York, USA

<!-- E BO -->
 
Lunalo,
Huyo dada yake na yeye ni siku nyingi ni Marehemu. Wakati akikaa Korogwe, ilikuwa nikienda kwake basi anatuwekea album za "kaka yake". Ila nilikuwa sijawahi kumuona hadi tulipohamia wote Dar na tulipoenda kwake ndiyo akatuambia huyu ndiyo Patrick. Siku hizo dada mtu anafahamika zaidi kwa jina May Materu hadi alipotunga kitabu na kujiandika "Ndyanao Balisdya".

Kuhusu Patrick kuiga miziki ya watu wengine hili hadi leo linanipa shida. Labda mkuu FMes anisaidie hapa. Kuna wimbo aliimba "tufurahi jama, tufurahi weekend ehh". Huu wimbo umefanana sana yaani kasoro maneno tu na lugha na wimbo wa Caiphus Semenya & Letta Mbulu uitwao everybody sing along. Huu unaweza kuusikiliza hapa: http://www.amazon.fr/Thalassa-collection-Afrique-Sud-Cap/dp/B00005UV78

Sema ni kipande cha 30 seconds tu ila utausikia. Album hii ya mama Mbulu na mumewe ni ya mwaka 1980 http://www.discogs.com/Letta-Mbulu-Sound-Of-A-Rainbow/release/1527293


Kuna wimbo ambao nimegundua juzijuzi kuwa Marijan Shaaban alichukua beats zake ni huu hapa chini. Huu unafanana sana na wimbo wa Mayasa unavyoanza.
http://www.youtube.com/watch?v=MSrklNeDwNM

Ngoja chini na mie nichangie mwanamziki mmoja: hmmm!!!

Ndugu yangu Sikonge,

Kwa nini unadhani kuwa wanamuziki wetu ndio walioiga tu badala ya kufikiria kuwa huenda muziki wao uliigwa na wanamuziki wa nje. Wimbo wa Balisdya wa tufurahi na weekend ulitungwa mwaka 1970 wakati wimbo huu wa Letta Mbulu uliimbwa mwaka 1980, miaka mitatu baada ya Afro 70 kufa. Huoni kuwa kama kuna uigaji basi utakuwa ulifanywa na huyu Mbulu?

Vile vile wimbo wa Mayasa ulipigwa kati ya mwaka 1979 mwishoni na mwaka 1980 mwanzoni, lakini wimbo huu wa wa Byron umepigwa mwaka 1984. Siyo tu kuwa nyimbo hizi mbili hazifanani kabisa kwa vile Byron kama walivyokuwa wanamuziki wote wa visiwa vya Trinidad na Tobago, kama Lord Kitchener na Arrow, alikuwa akiimba katika mtindo wa Soca yenye matarumbeta ya nguvu sana wakati Mayasa umeimbwa katika Afro rumba yenye magitaa ya umeme mengi sana. Utakuwa humtendi haki Jabari la mziki ukisema kuwa alikopi wimbo huo.


BTW: Kuhusu Dr. Balisidya, aliweka tendo la kishujaa sana kwa kutetea Ph.D thesis yake huku akiwa mahututi kitandani akiwa anahesbau siku zake za kuishi. Hakutaka kufa bila kukamilisha Ph.D yake hiyo.
 
Ndugu yangu Sikonge,

Kwa nini unadhani kuwa wanamuziki wetu ndio walioiga tu badala ya kufikiria kuwa huenda muziki wao uliigwa na wanamuziki wa nje. Wimbo wa Balisdya wa tufurahi na weekend ulitungwa mwaka 1970 wakati wimbo huu wa Letta Mbulu uliimbwa mwaka 1980, miaka mitatu baada ya Afro 70 kufa. Huoni kuwa kama kuna uigaji basi utakuwa ulifanywa na huyu Mbulu?

Vile vile wimbo wa Mayasa ulipigwa kati ya mwaka 1979 mwishoni na mwaka 1980 mwanzoni, lakini wimbo huu wa wa Byron umepigwa mwaka 1984. Siyo tu kuwa nyimbo hizi mbili hazifanani kabisa kwa vile Byron kama walivyokuwa wanamuziki wote wa visiwa vya Trinidad na Tobago, kama Lord Kitchener na Arrow, alikuwa akiimba katika mtindo wa Soca yenye matarumbeta ya nguvu sana wakati Mayasa umeimbwa katika Afro rumba yenye magitaa ya umeme mengi sana. Utakuwa humtendi haki Jabario lka mziki ukiseama kuwa alikopi wimbo huo.

Kichuguu,

Ndiyo maana nikauliza kwa sababu moja kubwa sana. Nilikuwa sifahamu/sikumbuki ni mwaka gani hizo nyimbo zimepigwa. Inawezekana kabisa jamaa wakawa wameiga wao kama walichukua baada ya miziki ya Tanzania au hata wote wakawa waliiga kutoka kibendi fulani kidogo sana.

Ule wimbo wa Mayasa vs Byron nilisema ni kile KIPANDE CHA MWANZO tu kama 20 seconds za mwanzo. Kule mbele hazifanani kabisa kabisa.

Wimbo ambao hadi leo nina uhakika Koffi Olomide ali-copy ni huu aliimba Max Bushoke sina uhakika na bendi gani ila anaimba "Kiu ya jibu mamaa, ndiyo inisumbuaayo. Natafuta jibu litakalonirushia? furaha, nimechoka kulala macho na kuota ndoto za alinacha...." Huu pekee nina uhakika kuwa ulipigwa kwanza Tanzania na baadaye Koffi akaja akapiga.

[ame]http://www.youtube.com/watch?v=jfoxX7jZwtc&feature=related[/ame]

(Anzia 0:20. Beats zake ni sawa kabisa na huo wa Chidumule. Labda ni bahati mbaya).

Kwa Koffi Olomide, hii album yenye wimbo huu (Noblesse Oblige) kwangu inbaki milele kuwa THE BEST OF KOFFI OLOMIDE. Ila kila album kulikuwa na wimbo wa kukata na shoka. Kama Civilise, Coucou, Loi, etc////
 
Vijana Jazz Band




Nilitaka Iwe Siri: Vijana Jazz Band.
<noscript>
61nxVFPDlBL._SS500_.jpg

</noscript> <script language="Javascript"> var imageViewerTagDiv = '
61nxVFPDlBL._SS500_.jpg

'; document.write(imageViewerTagDiv); </script>
61nxVFPDlBL._SS500_.jpg





- Hii ni bendi ya Vijana Jazz, iliyokuwa bendi ya umoja wa vijana wa Tanu na baadaye CCM, ilianzishwa na Mzee John Ondolo, baadaye ikaja kuwika sana na kiongozi wake Hemedi Maneti "Chiriku", pamoja na mpiga solo wake maarufu sana Hamza Kalala "Komandoo".

- Vijana Jazz waliwahi kupiga vibao maarufu sana enzi hizo kama "Kuruka Ukuta", "Zuhura", "Salima", "Chiku", "Operation Maduka" na zinginezo kama "Amba Baharia". Mungu amuweke pahali pema peponi marehemu Maneti.

Respect.


FMEs!
 
Kichuguu,

Ndiyo maana nikauliza kwa sababu moja kubwa sana. Nilikuwa sifahamu/sikumbuki ni mwaka gani hizo nyimbo zimepigwa. Inawezekana kabisa jamaa wakawa wameiga wao kama walichukua baada ya miziki ya Tanzania au hata wote wakawa waliiga kutoka kibendi fulani kidogo sana.

Ule wimbo wa Mayasa vs Byron nilisema ni kile KIPANDE CHA MWANZO tu kama 20 seconds za mwanzo. Kule mbele hazifanani kabisa kabisa.

Wimbo ambao hadi leo nina uhakika Koffi Olomide ali-copy ni huu aliimba Max Bushoke sina uhakika na bendi gani ila anaimba "Kiu ya jibu mamaa, ndiyo inisumbuaayo. Natafuta jibu litakalonirushia? furaha, nimechoka kulala macho na kuota ndoto za alinacha...." Huu pekee nina uhakika kuwa ulipigwa kwanza Tanzania na baadaye Koffi akaja akapiga.

http://www.youtube.com/watch?v=jfoxX7jZwtc&feature=related

(Anzia 0:20. Beats zake ni sawa kabisa na huo wa Chidumule. Labda ni bahati mbaya).

Kwa Koffi Olomide, hii album yenye wimbo huu (Noblesse Oblige) kwangu inbaki milele kuwa THE BEST OF KOFFI OLOMIDE. Ila kila album kulikuwa na wimbo wa kukata na shoka. Kama Civilise, Coucou, Loi, etc////

Sikatai kuwa watanzania hawakukopi nyimbo nchi za nje, kuna nyimbo nyingi za nje zilikopiwa na wanamuziki wa kitanzania lakini vile vile kuna nyimbo nyingi za Watanzania zilikopiwa nchi za nje.

Napenda kukumbusha wimbo uliotungwa na kupigwa na watoto wa nyumbani pale mtaa wa rufita wakiitwa, Wazee wa Kazi au ukipenda Segere Matata. Walitoa vibao vingi sana miaka ya sabini lakini mmoja uliovuma sana ni ule wa Asha namba mbili ambao ulikopiwa na wanamuziki wengi wa Zaire wakati huo sina hata haja kukutajia majina yao nadhani utakubaliana nami.

Kuna Wimbo wa "Unapenda dezo dezo" ulitungwa na kuimbwa na Ndala Kasheba miaka ya themanini lakini wimbo huu ukaja kufyatuliwa na kurekodiwa na Tshala Mwana.

Hata hivyo tunafahamu kuwa Kilwa jazz waliiga wimbo wa Mokolo Nakokufa wa Rocherau na kuupiga kwa jina la "Napenda nipate lau Nafasi" ambao ulisifika sana hadi miaka ya tisini bado Shikamoo Jazz walikuwa wakiupiga. Mbaraka mwinshehe naye alichukua nyimbo kadhaa kutoka nje kwa mfano kuna wimbo fulani, ingawa sikumbuki jina lake sasa hivi, aliuiga kutoka Beetles.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom