paulinho, andre gomez, paco alcacer, alex vidal.
kwa maoni yangu ili msimu ujao barcelona iwe ni timu ya ushindani zaidi kwenye ligi ya mabingwa basi wachezaji wanne hawa wanapaswa watafutiwe mbadala. ukiwaangalia real madrid japokuwa msimu huu hawajafanya vizuri kwenye ligi kuu utagundua wana substitution nzuri zaidi kuliko barcelona kwenye eneo la mbele.
barcelona si timu ya kusajiili wachezaji wa kufanyia majaribio.
uwepo wa
sergio roberto ni zawadi kutoka mbinguni kwa klabu ya barcelona kwa sababu anaweza kucheza nafasi ya alex vidal, andre gomez, paulinho na hata nafasi ya paco alcacer.
kama klabu itawauza wachezaji hawa wanne na baadae kusajili wachezaji watatu watakaoleta ushindani wa kugombea nafasi basi upo uwezekano wa kurudisha heshima ya msimu wa 2008.
umefika wakati wa barelona kupunguza watumishi hewa.
tusisahau pia andres iniesta anatazamiwa kuondoka mwishoni mwa msimu na pia performance ya osmane dembele haina tofauti na homa ya vipindi msimu huu.