Naomba uulize haya maswali yafuatayo:
Nape
1. CCM tuluyoijua sisi toka inaanzishwa 1977, ilikuwa na sera ya ujamaa na kujitegemea (na hili halikuwa na ubishi wa aina yoyote). Kutokana na mabadiliko yaliyojitokeza toka mwanzoni mwa mika ya 1990, sera ya CCM (kinadharia na vitendo, theoretically and practically) ni ipi?
2. Alama za bendera ya CCM zililenga kuonesha wigo wa wanachama na wamiliki wa chama (wakulima na wafanyakazi. Je, Nape anaamini bado hao ndio wamiliki wa chama?
3. Ndugu Nape, siku zote muungwana uhukumiwa kwa maneno anayaoyasema (especially anapotoa ahadi) na huokolewa na matendo yake...Kwa ahadi zako kuhusu kauli mbiu ya kujivua gamba, Nape haoni kwamba umeshapoteza uhalali wa kuendelea kuwa Katibu mwenezi wa chama? Do you think you still have any piece of moral authority to sit on this Nobel post?
Ruge
Kila chombo cha habari hutakiwa kutangaza ama kwa kutoa maelezo rasmi au kwa mfumo wa uendeshaji wake mrengo ambao kinauunga mkono (ama ni partial au impartial) katika kushirikiana na serikali iliko madarakani pamoja na chama tawala. Je anaweza kutueleza kama Clouds ina mrengo (wa kisiasa) ambao kinauunga mkono? Na je, Clouds ina sera gani katika kuhudumia vyama vya siasa? Inaweza kuacha milango wazi kwa chama chochote iwe ni CCM, CHADEMA, TLP, NCCR-MAGEUZI au CUF? Kama jibu ni hapana, kwa nini? Kama jibu ni ndiyo, je Clouds haijawahi kutoa habari kwa ushabiki wa wazi kwa chama chochote cha siasa nchini?
Natanguliza shukrani!