Eti hatujui... kipimo gani kinatumika?


Hii nayo ni issue nyingine Nat,

Hivi mtu unatengenishaje matamanio yako ya uroda na mahaba ya kweli???

Mie huwa naamini kuwa bila kumsifia sifia mwanamke hupati kitu ng'o!!! Labda kama hiyo inaapply kwetu wa mwaka 1947 tu!
 
Kama mtu hauko romantic, na unajijua kweli hauko romantic, usijidanganye kuwa uko romantic, jifunze juwa romantic, hata kwenye internent, unakuta mwanaume mwingine anajisifu kuwa romantic wakati anatumia kugha ya matusi, kumtukana Mpenzi wake kila mara na hata kumpiga wanapokuwa ndani pamoja, huyo ana maana kweli, hata asafiri mwaka mzima huna mpango naye, sana sana atakukuta umeshakuwa na mwingine.
 
Mtu anaweza akawa ni very good romantically kwenye mapenzi hata kama ndio uhusiano wake wa kwanza wa kimapenzi, na mwingine akawa hajaweza bado kuwa good romantically hata kama uhusiano wa kimapenzi aliopo muda huo ni wa tatu kwake, utakuwa very good romantically kama, moyo wako na hisia zako zote ziko kwa kiasi kikubwa kwa yule uliyenaye kwenye huo uhusiano wa kimapenzi, utapenda kumfanyia yale hata wewe ungependa kufanyiwa, utamjali, utampenda, utamthamini, utamuhurumia, utamuweka moyoni mwako na kumheshimu, sio kumpiga na kumtukana.
 

....owkey,.....kwahiyo tafsiri yako romance ni hisia?...


Hahahahahahh umemaliza shemeji yangu. Lizzy haitaji presha hapa. Ghobyala mayo ghobyala ghawiza, alikwing'ombe ghobyala ghawizaa eh.
Nahene lolo, bhebhe ang'u

...dahhh, mwanajamiione hapa naona kama unanisengenya vile? aahhh....
 

...i second with with you... kwani kwa tafsiri yangu, being romantic ni vile ninavyomjali mwenzangu/mwenzangu anavyonijali ....

...ni pale ninapofikia level ambayo njaa yake, shida zake, raha zake, wasiwasi wake, matarajio yake, machungu yake, wasiwasiwasi na mengineyo mengi niwezavyo kuyachukulia kama sehemu ya maisha yangu...(empathy!)...
---'spiritual' level ya mapenzi---
 

....owkey,.....kwahiyo tafsiri yako romance ni hisia?...



Hapana, ni mazingira yanayojengwa/tengenezwa ili kuamsha/kukoleza hisia za mapenzi kwa mwenza (nisome tena mkuu Moskwito).

Pia kwangu mimi romance ni kitu ambacho unique kwa kila binadamu, romance yako wewe inaweza isiwe romance kwangu mimi na vice versa.
Mfano: Hiyo MJ1 kuongea kilugha inaweza ikawa romantic kwako mkuu Mbu lakini iskuwe romantic kwa PAW.
 

Mkuu moskwito, hapo buluu japo ni tafsiri yako binafsi lakini naomba niulize kidogo!

Hivi haujawahi kuwaona binadamu ambao they find it so romantic when their partners are careless and kinda animal behaved? , umewahi kuyaona maisha ya wale street rock and rollers?
 
Kwani hailiki/hailambiki????

Siku hizi nasikia hata vibabu vimeshazoea....Wewe umechelewa wapi au bado una hang-over ya mwaka 1947???

come on DC acha hizo bana,usiniharibie breakfast yangu ya supu ya miguu ya kuku,mwenzio najichana hapa keko toroli.
 
...hehehehe....e bana umemaliza kila kitu...ATM, kuchunwa, buzi.....
ngoja wenyewe waje kupinga hapa.

wakati huo huo na mimi na swali kwa wanaume wenzangu;
kuwa romantic maana yake nini?

1. ?
2. ?
3. ?

Mbu,asikudanganye mtu hapa,pesa sabuni ya roho bana!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
mmmmmmhhhhhhhh!!!!
 
come on DC acha hizo bana,usiniharibie breakfast yangu ya supu ya miguu ya kuku,mwenzio najichana hapa keko toroli.

Kama kweli umefikia hapo, na katika dunia hii ya vichaa wa dot.com na wale misukule wa 1947 wanaohangaika kuwaiga, basi huna chako...Nakushaur ujiunge na convient uwe towashi tu!!!

Huo ndio wosia wa Babu DC!!
 

Kwa hivi vingezo vyako, ambavyo tayari vimekatiwa rufaa na klorokwini, hebu basi malizia swali letu la msingi...Wanaume na wavulana wa Tz (ukiwemo na wewe), tunavyo hivyo au ndo tumebakiwa kuwa washika pembe ili majirani zetu (hapa namaani Wakongo na wengineo) waje kukamua???!!!
 

Do they call them romantics? The way I see those street rock and rollers dont want to hear that word around them. lol

I guess they will define it as down to earth, spiritually connected, punk love......

The word romantic has roots on certain things which goes more with the classic culture than pop culture ......

or is it just me ??
 


Gaijin, nimekusoma sana mwalimu wangu......

Lakini tukumbuke kuwa vionjo vya weupe vitaendelea kuwa vya weupe,

na vya weusi vitaendelea kubaki hivyo..

Neno kujali kwenye mapenzi hasa kwa maisha ya kiafrika....limejikita zidi katika majukumu,

na wala sio hiyo romance sijui romantic love.........

Mwanamke wa kiafrika, kwa walio wengi anaweza kudefine kuwa unampenda,

kama utajali mahitaji yake ya kimaisha...................na wala sidhani hapa makissing, mahugging ndo yana nafasi kwa sana,

hebu jaribu kupiga hayo makissing, mahugging, sijui kununuliana vito vya samani pasipo kutimiza yale mahitaji yake ya kimsingi.....

nadhani utakuwaumepotea.................

Mwanamke wa kiafrika anaweza kuonyesha na kutambua kuwa unamjali kutokana na mambo mengi tu yanayohusiana na mahitaji yake ya kmsingi...

mfano, kujali ndugu zake, kujali familia yako, watoto katika ujumla wa maisha hayo.......

Haya mambo ya kissing, sijui mahuggung na mengine ya dizaini hiyo mengi ni vionjo vya wazungu, ingawa si mbaya kuyaonyesha lakini,

hayana uzito ule unaosimuliwa hasa katika context ya kiafrika........

Nawasilisha.KARIBUNI KAHAWA JAMANI.....
 
Kama kweli umefikia hapo, na katika dunia hii ya vichaa wa dot.com na wale misukule wa 1947 wanaohangaika kuwaiga, basi huna chako...Nakushaur ujiunge na convient uwe towashi tu!!!

Huo ndio wosia wa Babu DC!!

Mkuu DC wala usikonde, kina mama Kayai kibao mjini ambao nao mambo ya dot.com hawataki kuyasikia pia,ni kwenda nao sambamba tu.
 

Mwalimu ,
Muhimu sio wao kuita romantic au la, nadhani muhimu ni kuwa je ni actions gani wanatumia kama vigezo vya mazingira ya kufall/kunogesha mapenzi kwao ?

Hawa jamaa The crazier u behave, the more attractive and sexier u become.
heheheeh, Hata sex yao ni balaa tupu, unaweza ukalembewa bonge la kibao katikati ya mchezo shavu likavimba ,ukazani umekosea stepu kumbe ndo romance zenyewe. Khaaa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…