Eti hatujui... kipimo gani kinatumika?


Kuna kitabu kimoja nilisoma mwandishi Mzungu anasema

"Waafrika ni masikini mno, na kwa nadharia ya Kimagharibi umasikini ule lazima ukufanye unhappy, lakini kwa vile Waafrika hawana/hawajui zaidi ya kile wanakuwa maskini na happy vya kutosha pengine zaidi ya hata Mzungu tajiri kiasi"

So falsafa hiyo inaweza kuwa inahusika. Kwa wale walotizama Egoli sana na kuishi ughaibuni hata wakifundwa vipi unakuta system ishachakachuliwa. LOL ....Lakini wa enzi hizo, vitu simple anafurahia vya kutosha, hamna kukwazana na mwenza wake kwa vitu viso msingi
 
lol.....Dah!
 
Ahsante sana Mwalimu wangu,

Siwezi kuacha kuwa na wasi wasi ndugu.. Unajua, enzi zetu wanawake walifundwa na kufundishwa kusema maneno mawili makubwa kwa mume wake ..."NDIYO" na "AHSANTE"!!!

la hasha mkuu, sikubaliani nawewe kwanini ujitie wahka bure....maswali yako yalikuwa hivi;

1. Ni kweli wanaume wa Kitanzania hawajui mahaba??

2. Kama hawajui, ni kosa lao peke yao au na wenzi wao (wanawake)???

3. Na vigezo gani vinatumiwa ku-judge kama mtu anajua mahaba au la?

...iwapo wewe na bi mkubwa baada ya miaka yote hii mnakenua na kuridhiana 'hivyo mlivyo' kama ulivyotanabahisha hapa;

Sasa inawezekana mama DC bado anaaply hayo mafunzo na mimi nakenua mijino kwamba ninaweza kumbe patupu!!!

Hata hivyo huwa anafurahia migunia yangu ya mikaa na kuku wa Boss,... ingawa maji simsaidii kubeba!!

...sioni sababu ya nini blog ya bwana macha ikuingizie mdudu kwenye kokwa la embe...
maisha ni vile wewe mwenyewe unavyoyachukulia na kukubaliana nayo,...who are we to judge you ati
huna mahaba kwa mkeo?
...lol!
 
@Shantel,
halaf kuna mod tunataftana ubaya kweli hapa, yaani daily nikiquote post za Shantel ananibania lakini ole wake nisimjue.

bek to ze topik: sasa wewe unafagilia zile za mauwa au gunia la mkaa na kuku?
 
Mie mwenzenu nimejifunza mengi ila haya ndiyo makubwa,

Mahaba ndiyo kwa kizungu yanaitwa romance hata kama Gai hataki kusikia hivyo. Na haya mahaba hayawezi kuwa generalized...Njiwa wa Muhogo Mchungu anaweza kuzua hisia za mahaba sawa sawa au zaidi ya chorcolates and mabusu ya wazungu!! Kwa ufupi tu, dume la ng'ombe wa kimasai ni ng'ombe dume sawa na dume la friesian ingawa wanatofautiana kwa attributes nyingi sana!

Pili, hakuna mahaba kama mwisho wake hautakuwa kwenye ngono...Ndo maana hakuna mahaba kati ya baba na binti yake au kijana na mama yake mzazia....Exceptions hapa ni kwa wanyama kama mbuzi na ng'ombe. (Hii naongeza mwenyewe....Kwa vile kila mtu anajua kufanya ngono, basi atakuwa na vichembe chembe vyake vya mahaba kwa mwenzi wake)!!

Tatu, mahaba ni kwa watu wawili tu.. mbinu zao haziwezi kutumiwa na watu wengine hata kama mmoja wao ndiye anayehamia kwa mtu mwingine. Hii inanikumbusha mambo nilisoma mahali kwamba, "sex is an art learned over time and used by a couple, it cannot be transferred to another pair". Hapa tunahimizwa tukwepane na mambo ya kuiga iga vya watu...!! Kwa ufupi hakuna package ya mahaba ambayo ni universal!!

Kabla sijasahau...Kuna waliosema kuwa hakuna dominance kwenye mambo ya mahaba...Kwa hiyo hata mahaba yetu ya kule kijijini yako juu tu ingawa vijana wa dot com wanayumbishwa na luninga!

Naishia hapa kwa sasa...Nitarudi baadaye kumalizia!

Mwenye cha kuongeza alete hapa....PM Not allowed!!!!
 
@Shantel,
halaf kuna mod tunataftana ubaya kweli hapa, yaani daily nikiquote post za Shantel ananibania lakini ole wake nisimjue.

bek to ze topik: sasa wewe unafagilia zile za mauwa au gunia la mkaa na kuku?
Gunia la mkaa na kuku mwenzangu, maua ya nini mie, hata sijui maana yake,sie tushazoea zawadi unaletewa blue lady na wewe unapeleka ayu sasa hii ya maua haijakaa vizuri
 
hahaaaaaaaaaaaaa lol nimependa hapo nilipobold.....................

 
Nilibahatika kuuona huu mjadala kupitia wanabidii.........it was hot. Watu wanajibu hoja kwa references jamani ah. kuna points zilizungumziwa kule nikabaki kumwomba mwenzi wangu abakie wa kibantu kama alivyo.


ahaaa.....:whistle:
 
Gunia la mkaa na kuku mwenzangu, maua ya nini mie, hata sijui maana yake,sie tushazoea zawadi unaletewa blue lady na wewe unapeleka ayu sasa hii ya maua haijakaa vizuri

Mhhhh...Kama hawa wakubwa wa JF wangekuwa wanaruhusu ningeomba siku moja tu-break codes ili tuondokane na haya majina ya key boards,

Inawezekana wewe ndiye mama DC na mimi napata taabu hapa kwamba huenda unanichora wakati eti mahaba siyajui!!

Week ijayo naenda field, haki ya nani nitaongeza gunia jingine la mkaa. Pia nitaleta na bata dume!!
 
hahaaaaaaaaaaaaa lol nimependa hapo nilipobold.....................

Kumbe na wewe Chauro ni mchokozi???

Tueleze basi uko upande gani? Wa magunia ya mikaa au maua maua na mabusu mabusu!!
 
Gunia la mkaa na kuku mwenzangu, maua ya nini mie, hata sijui maana yake,sie tushazoea zawadi unaletewa blue lady na wewe unapeleka ayu sasa hii ya maua haijakaa vizuri
Thats my gal! hii kuiga iga inatukosti sana aisee! kuna familia niliwahi kuishuhudia , kijana alinikabili kuniambia kwamba waifu wake amemtaka wabane matumizi mpaka ya msosi na huduma za watoto ili wapate Plasma TV, na ahadi ya waifu kwa hazbendi ilikuwa ni kwamba hapo ndio ataamini kuwa mume wake anampenda! alitaka ushauri but sikumshauri kwavile nilijua effect ya ushauri wangu ingeharibu romance za watu.
 
Haha labda ndio mie wallah, maana naona mambo mengi uloyasema yanaendana na style yangu lol
 
Haha labda ndio mie wallah, maana naona mambo mengi uloyasema yanaendana na style yangu lol

Uwiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii,

Haiwezekani Shantel.........Usitake nivunje hii PC.....Halafu fisadi wangu keshajiuzulu...Nitapata wapi nyingine??
 
Dah hii kali pamoja na kuolewa bado nikiwa dot com hii hapana ...............plsma tv inaongezaje mahaba au mie mshamba



 
Freddy Macha mbona kazua balaa!

DC hamkani....atangaza bata dume


Wewe teacher wewe....Complements ni dawa ya magonjwa kibao...Huna haja ya kwenda kwa Ndodi au kutafuta dawa za ajabu ajabu!!

Complements za Mama DC (au Shantel) baada ya kukupokea bata dume ni dawa ya kutosha...Tena inaweza kuzidi hata valium!!
 
Dah hii kali pamoja na kuolewa bado nikiwa dot com hii hapana ...............plsma tv inaongezaje mahaba au mie mshamba
Hii ni mada nyengine, samtaimu waswahili wana hii competition ya romance na mahaba, kaenda kwa jirani kaona hiki na yeye unamkuta anakomaa afanyiwe anasahau kuwa mwenza wake ni muuza karanga.
 
Hii ni mada nyengine, samtaimu waswahili wana hii competition ya romance na mahaba, kaenda kwa jirani kaona hiki na yeye unamkuta anakomaa afanyiwe anasahau kuwa mwenza wake ni muuza karanga.

Hii mada sasa inaenda wapi?

Hayo ni mahaba yake au kayakopa kwa majirani!!
 
Uwiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii,

Haiwezekani Shantel.........Usitake nivunje hii PC.....Halafu fisadi wangu keshajiuzulu...Nitapata wapi nyingine??
Usivunje bana, si ndio vizuri kukujua au vipi bana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…