Epukeni bidhaa za Game Mlimani City!

Epukeni bidhaa za Game Mlimani City!

I wish hii forum ingekuwa na like button, we get 2 knw many thnz that the gvt have kept quite abt them,.! Alafu miji2 mingine inackia raha gani kununua shati la 100,000 kama s.africa ni sh.10000, huo c ufahari bt ulimbukeni ona sasa mnaibiwa! Alowaambia kuvaa nguo za bei ndo kila k2 ni nani wakat unakaa kwny nyumba icyoeleweka!! Being of quality is how u design urself hata kwa nguo za 15000 n ur respect towards everyone n not spending money kwenye nguo za ndani za elfu 40000!
 
Game wako makini hawawezi kuuza bidhaa mbovu kama kariakoo hizi ni fitna za Quality centre maduka yanadorora wanatafuta wateja kwa nguvu wenye hela kutoka pande za sinza,mwenge,masaki,mlalakuwa,obey,knyama,mbezi,kimara maana kule ni full TMK!!!
 
Mamlaka husika zinatakiwa kuchukua hatua juu za bidhaa mbovu/feki zinazoingizwa sokoni bila kujali zinatoka ndani au nje ya nchi. Mojawapo ya bidhaa zinazoingiwa nchini zilizo chini ya kiwango ni helmet za waendesha pikipiki.
 
Nilinunua ka'home theatre (LG)' kangu pale kama mwaka mmoja na kitu uliopita lakini hivi sasa kanachanganyiwa....in short ni mbovu. (unlucky me, the so called warrantee has already expired)

2011 nilinunua heavy duty whilrlpool washing machine costing about 1.6m . Nina kamradi kangu ka pagu na paguzi. Nikafikiri nimejikomboa. Ukifua mara moja tu, lazima usuburi at least two to three hours uwezi kufua tena. heavy duty ya namna gani hii. Kwa hiyo hela unatakiwa hii washing machine ifue angalau loads tanu au sita kwa siku. Kwa hiyo nimeliwa. wala sina muda wa kulalamikia Milimani city maana hawana any solutions.
 
Game wako makini hawawezi kuuza bidhaa mbovu kama kariakoo hizi ni fitna za Quality centre maduka yanadorora wanatafuta wateja kwa nguvu wenye hela kutoka pande za sinza,mwenge,masaki,mlalakuwa,obey,knyama,mbezi,kimara maana kule ni full TMK!!!

kwel hizi fitina tu
 
Game wako makini hawawezi kuuza bidhaa mbovu kama kariakoo hizi ni fitna za Quality centre maduka yanadorora wanatafuta wateja kwa nguvu wenye hela kutoka pande za sinza,mwenge,masaki,mlalakuwa,obey,knyama,mbezi,kimara maana kule ni full TMK!!!

Fitina gani unazozungumzia..sidhani ka unajua Quality Center imefunguliwa lini na hii thread imeanzishwa lini!
 
Game wako makini hawawezi kuuza bidhaa mbovu kama kariakoo hizi ni fitna za Quality centre maduka yanadorora wanatafuta wateja kwa nguvu wenye hela kutoka pande za sinza,mwenge,masaki,mlalakuwa,obey,knyama,mbezi,kimara maana kule ni full TMK!!!

Uwezo wako wa ku'analyze ni mdogo sana. Nyie ndo mnafeli mitihani kwa kutosoma instructions. Thread ilipostiwa tarehe 24th
December 2008! Haya Quality Centre ilikuwepo enzi hizo? Natamani ungekuwa karibu nikupige masingi!!
 
Kuna mfumo niliuona South Africa kwenye Super market zao. Huwa wanagawa kwa masikini bidhaa zinazokaribia kuexpire ili kupunguza gharama ya kuziharibu, lakini kwa hapa Tanzania bado sijauona na sijaona bidhaa zikiharibiwa kwa sababu zimexpire! Hii ina maana gani?

Hapa kwetu bidhaa zote huwa zinaisha on time (haziharibiki) au ndio haya mambo ya re-packaging kama alivyobainisha mleta maada? Mimi ndio maana sipendi vyakula vya viwandani, kwani ni kujitafutia cancer tu
 
Game wako makini hawawezi kuuza bidhaa mbovu kama kariakoo hizi ni fitna za Quality centre maduka yanadorora wanatafuta wateja kwa nguvu wenye hela kutoka pande za sinza,mwenge,masaki,mlalakuwa,obey,knyama,mbezi,kimara maana kule ni full TMK!!!

kwel hizi fitina tu

Hivi nyie wawili huwa hamuangalii tarehe ya threads?
Mada hii ni ya mwaka 2008, ilhali quality centre imefunguliwa mwaka jana tu, sasa suala la kuvunjiana biashara linatoka wapi hapo? Huu ndio ukweli, wabadili mwenendo wao, otherwise tutawasusa.
 
ndio maana napita kung'aa macho na kujua bei...nanunua maji ya uhai nasepa..
 
wafanyabiashara ni watu wa kwanza kuingia motoni

hii ni business forum usitutukane kwa kujumlisha kila kitu kumbuka hata hesabu za kutoa.

cha mhimu ni kuboresha bidhaa zinaendane na mahitaji yawatumiaji.
 
nakubaliana na wewe kwenye yote uliyoandika, isipokuwa ubora wa bidhaa kuwa za Game zina nafuu kwani zinatoka SA.

Issue ya ubora wa bidhaa nafikiri ni tatizo linaloanzia kwetu, yaani TBS na TDFA. Sina uhakika kama tuna viwango kwa bidhaa zote zinazoingizwa nchini, na hata kama tuna viwango, je kuna uthibiti wa kutosha. Ulaya na hata SA wanapata vitu vya kutoka China/Thailand, lakini kwa vile wana viwango basi ubora wa bidhaa zao siku zote unakidhi viwango.

Kuna wakati mimi nilinunua bidhaa fulani ya umeme hapo Game, kufika nyumbani ndiyo nikaona kuwa sehemu ya kuchomeka kwenye soketi si wa viwango vya kwetu. Nilipiga simu TBS kuuliza inakuwaje duka kubwa kama Game linauza vifaa ambayo si vya viwango vya kwetu, majibu niliyoyapata huko siwezi kuandika hapa, kwani yanaonyesha ni kwa kiwango gani hakuna umakini.

Nini tufanye? Kwavile TBS, TDFA, FCC zinaonyesha kushindwa kufanya kazi yao sawasawa, basi nguvu ya umma itumike kuwalazimisha kutenda kazi yao. Kwa wenzetu wanaojua kuhusu mapungufu yaliyopo kwenye bidha mbalimbali zinazoingizwa kwenye soko wasikae na taarifa hizo badala yake wajitahidi kuwafikishia watu wengi kadiri inavyowezekana. JF, nakala kwenye magazeti, nk kuwataarifu waTZ.
Mkuu Mzawa Halisi, pole kwa tatizo la ile mi plug mikubwa ya South, siku hizi wanauza na adapter zake kwa size ya socket zetu na pale pale the game, kuna vijana hiyo ndio ajira yao kufanya conversion kwa kulikata hilo li plug la South na kukuwekea ya kwetu.

Hata hivyo tatizo la plug ni issue ya compatibility and not quality, its the same kwa bidhaa zote za US na Taiwan zilizotengenezwa kwa matumizi ya soko lao la ndani, zote zinatumia umeme wa 110 wakati sisi umeme wetu ni 240, this has nothing to do with quality au Video Format ya US ni NTSC, UK na Anglophone yote ni PAL na French na Francophone ni Secam!.

Hizo bidhaa za South ni za quality ya ukweli kuliko mazaga zaga ya Mchina ila pia nakiri kuna Mchina wa ukweli na Mchina fake!.
 
Na ya ma apple ambayo mama watoto anayapenda sana ya pale Shoprite nayo Fake?

Jamani mimi nilinunua hair dryer ya wife toka mwaka 2008 hapo Shoprite hadi hivi sasa anaitumia toka alipokuwa gf hadi sasa ni wife. Na mwaka huo huo nilinunua DVD player LG pale The Game hadi sasa inadunda. Inamaanisha kuna baadhi fake baadhi vya ukweli au wafanyakazi wenyewe wanabadilisha wanachukua original wanaenda kuuza wanaweka za kichina? au wameanza siku hizi huu mchezo?
 
TV stations badala ya kurecycle mavipindi wangeweza kutoa documentary inayohusu bidha feki na athari zake na ku-expose yale maduka notorious kwa hizi bidha. Feki na substandard!!

Mbona TBS huwa wanajitahidi sana kuelimisha umma kupitia TV na maonesho kama sabasaba
 
si wamegundua serikali ni legelege! we unafikuri serikali ingekuwa makini na imara, hawa wawekezaji wangefanya huu upuuzi, afu wamegundua na style mpya skuizi ya kuwapa tuzo viongozi. ili hili swala lishughulikiwe haina haja ya kupoteza muda na serikali, bali sisi wanunuzi ni kuhamasishana kutokwenda kununua bidhaa zao! na wenyewe watakaa sawa, tukiwaangalia tbs tutakufa vibudu, mana wao kilasiku wanatoa vibali tu sijui vya nini
 
Back
Top Bottom