Epukeni bidhaa za Game Mlimani City!

Epukeni bidhaa za Game Mlimani City!

Miaka mitano iliyopita mke wangu alinunua fridge kwa shillingi laki tisa huko kwenye maduka ambayo hayatoi guarantee na iliharibika ndani ya miezi sita. Tukanunua frdige nyingine pale Game, double door, na bado inafanya kazi mpaka leo hii na haijatuletea matatizo yoyote.

Binafsi sipendi kununua kitu cha gharama ambacho hakina guarantee. Kwa hiyo huwa siingii huko mitaani kama Kariakoo kununua vifaa vya electronic, umeme, au mashine nyingine kama vitu hivyo naweza kuvipata kwenye maduka yanayotoa guarantee.

Kuhusu vyakula mara nyingi napenda vilivyo fresh na sipendi kabisa vyakula vya kwenye makopo.
 
Miaka mitano iliyopita mke wangu alinunua fridge kwa shillingi laki tisa huko kwenye maduka ambayo hayatoi guarantee na iliharibika ndani ya miezi sita. Tukanunua frdige nyingine pale Game, double door, na bado inafanya kazi mpaka leo hii na haijatuletea matatizo yoyote.

Binafsi sipendi kununua kitu cha gharama ambacho hakina guarantee. Kwa hiyo huwa siingii huko mitaani kama Kariakoo kununua vifaa vya electronic, umeme, au mashine nyingine kama vitu hivyo naweza kuvipata kwenye maduka yanayotoa guarantee.

Kuhusu vyakula mara nyingi napenda vilivyo fresh na sipendi kabisa vyakula vya kwenye makopo.

Kwahiyo unashauri tuendelee kutumia bidhaa zao hazina matatizo kabisa.
 
Taarifa hizi tulishawatumia TBS na TFDA wafuatilie kwa ukaribu kwani wafanyakazi wa Game wenyewe walituhabarisha juu ya hili. Kama wanataka facts tunaweza kuziweka hapa pindi zikihitajika!

Not only Game, hata Shoprite nao walewale.
Hadi leo vitu vibovu bado vinaingizwa nchini na hao Game na Shoprite. Nitavipiga picha na kuvionyesha hapa jamvini Bw Invisible
 
Kwahiyo unashauri tuendelee kutumia bidhaa zao hazina matatizo kabisa.

Kwa kweli sipendi kuwapigia debe Game au Shoprite. Lakini kwangu miye kifaa kisichokuwa na guarantee sipendi kukinunua na kile ambacho kimetumika sikikinunui (mtumba) kabisa.
 
Dah, 4yrs later bado kuna tatizo hili?
IMG_1665.JPG

Hii Leximark printer, ilikufa mara tu baada ya kuprint copies chache, nilinunua pale Mlimani City ,Game Supermarket.
 
IMG_1666.JPG
Hizi rechargeable spot lights, ya kwanza ilikufa baada ya kucharge mara mbili.
Nikifikiri nilifanya kosa nikaenda nunua ya pili, nayo ikafa baada ya kucharge mara moja!
 
IMG_1395.JPG
Viti hivi vya kurelax nje ya nyumba yako ni of very poor quality na si kwa ajili ya outdoor use.
Kwanza, fabric material iliyotumika kutengeneza hiyo cloth SIYO canvas, material hiyo ukiiona utafikiri canvas lakini ni synthetic material-poor quality.
Material hii ikikaa nje ikapigwa weather(siyo juani wala kwenye mvua), ina dis intergrate kama picha invyoonyesha.
Pili joints zake zinaachia hivyo ukiwa na mgeni kibonge anaweza kupiga tiki taka hadi chini kwa makalio!!
 
...Asante Mkuu LGwakisa kwa kuweka ushahidi huu. Tufanyeje sasa Wakuu??
 
Ndugu yangu alinunua washing mashine game,mpaka kesho ni pambo tu nyumbani kwake.
 
Vyakula kwa sana ndivyo tatizo katika maduka haya. Baada ya kuarifiwa juu ya hili tulijaribu kuziarifu mamlaka husika zifuatilie, nadhani walipuuza. Impact yake ni watanzania kuugua magonjwa yasiyoeleweka!

Huwa hawapuuzi, wanaenda kupitia mlango wa nyuma, wanapa hizo taarifa na kuwatisha, jamaa wanawakatia chochote mambo yanaisha. ukifuatilia utaambiwa kuna maofisa wanaenda pale kuchukua mshahara kila mwisho wa mwezi... mlichofanya ni kuwapa dili!!
 
Wakuu,

Bidhaa famba hazikosekani mahali popote duniani ila kama kuna sheria zimewekwa pia bidhaa hizi haziwezi kuwekwa madukani kama GAME na Shoprite tena ndani ya shopping centre kama Mlimani City.

Bidhaa mbovu zimekuwa zikiingizwa Tanzania miaka nenda rudi na si TBS wala Polisi wamechukua hatua mabli ya kufahamu au kuelewa kuhus jambo hilo.

Kwa wale wanaoishi Ulaya duka la GAME ambalo sasa limeuzwa, lilikuwa likichukua bidhaa umeme kama game consoles na game cards ambazo watumiaji walikuwa hawazihitaji na wakawa wakizifanyia usafi au reconditioning. Kwahio hata kama bei ya Nintendo DS ambayo imefanyiwa reconditioning ni paundi 120 au Euro 90 lakini inakuwa ikilingana na bei ya Nintendo DS mpya ya paundi 199.

Kwahio wateja wa "interactive games" wengi wenye kipato kidogo walikuwa wakikimbilia maduka ya GAME na walikuwa wakimudu bei zake.

Sasa retailers wa Tanzania kwakuwa wana uchu wa kupata faida kwa uharaka ndio wanakwenda Taiwan na China ambako ni rahisi kwenda na kuokota bidhaa hizo ambazo nyingi hutupwa sehemu maalum badala ya kufanya biashara na suppliers ambao watakuwa wakiwatoza mamilioni ya dollars ili kuweza kufikisha bidhaa hizo nchini Tanzania.

Kuna mambo mengi tu ya kuzingatia kama ushuru wa kuingiza bidhaa hizo zifikapo bandarini, kodi ya VAT, kodi ya pango pale Mlimani City, mishahara kwa watumishi wao na kamisheni kwa maofisa wa TBS kila mwezi.

Sasa katika nchi yenye mfumo mzuri wa kodi wenye kujali maslahi ya taifa na wananchi wake ambapo wafanyabiashara wanafuata misingi ya biashara zao kwa kujali wateja, basi haiwezekani kuweka bidahaa mbovu madukani tena Mlimani City. Pia kama kweli TBS wanafuatilia kila bidhaa inayoingia Tanzania basi tusingekuwa na bidhaa mbovu madukani.

Tatizo ni kwamba kila mahala Tanzania kunanuka UFISADI na watu wenye biashara nje kama watu wa PC world, makampuni mengine makubwa ambao wanaweza kuleta bidhaa za uhakika, mpya na zenye guarantee hata ya miaka mitatu lakini wanasema "no".
 
Invisible, Hivi kwanini kama kuna matatizo pasifungwe tu kwa muda maka hapo watakopokamilisha uchunguzi?mie huwa nashangaa sana nchi yangu inavyoendeshwa. Mataka kakosea ,kwanini asifukuzwe kwanza!Shame
Kufungwa au kufukuzwa ni suala lisilowezekana mkuu especially katika nchi inayoongozwa na serikalii ambayo yenyewe pia ni mbovu, ubovu wa aina yoyote ile wahusika wanaotakiwa kuchukua maamuzi hayo huona ni sahihi na hakuna tatizo. The whole country is rotten!!
 
Duka lenyewe laitwa GAME, so si kuna kupata na kupoteza game bwaaana, shauri yenu.
 
mi nilinunua feni,ilikaa only 6months nikatupa,nimehamia kariakoo mchina kanirahisishia life,tv elfu tisini lol
 
polen wafiwa
maana na mimi ni mfiwa mmoja wapo wa mali za game watoto wanachezea tu
 
Wakuu,hii issue ya ufeki bado ipo pale game?,maana niko mbioni kwenda kujinyakulia ka home theatre kangu pale(naogopa ule mpango wa ebay nisijeibiwa nako).
 
Back
Top Bottom