Enzi ulipokuwa boarding

Enzi ulipokuwa boarding

Nakumbuka siku moja nikiwa o-level form 1 kibaha sec,si unajua ule utaratibu wa misosi,watu kadhaa mnaunda kikosi,maybe watu 13 mnakuwa na dishi lenu moja la ugali/wali na moja la mboga.

Ugumu ulikuwa unatokea ikifika zamu yako, unafuata msosi jikoni,unagawa kwa wenzio na kuosha madishi na kuyarudisha jikoni.siku moja jamaa alipojua ni zamu yake akaamua kutokuja kabisa.

Tulikuwa form one 5,form two 4 na form four 2.Form four mmoja akashauri form one(nyoya,salamanda,nyoka) mmoja ajitolee lakini tuligoma wote. Wale form iv walijitolea ku-save msosi,ila walichofanya sitasahau.

Waligawana msosi wao wawili wakatosheka, baada ya hapo walimwaga wali wote uliobaki chini na mchuzi wakaugeuza maji ya kunawa,kiufupi tulipigwa dash.

Dah!vp wewe ulipokuwa form one,tupe kisanga kilichokukuta!

Imenichekesha sana, kiufupi, nimesoma shule ya kata, boarding nimeenda advance tena mtata kidogo, so sina kigumu cha kusimulia,
Shule yetu haikuwa na tabu sana hata Rejao anajua
 
Last edited by a moderator:
dah ucpime, TARIME SEC kulikua na dogo mchawi toka ukerewe, siku moja mpirani c akakwatuana na mshikaji pande la mtu mkurya, huwezi amini alimtupia mwenzie radi, Mungu mkubwa mshkaji akapona!

Tarime sec kulikua na secondmaster huyo anaitwa mwl gamba duh noumer tupu
 
dah ucpime, TARIME SEC kulikua na dogo mchawi toka ukerewe, siku moja mpirani c akakwatuana na mshikaji pande la mtu mkurya, huwezi amini alimtupia mwenzie radi, Mungu mkubwa mshkaji akapona!

Tarime sec kulikua na secondmaster huyo anaitwa mwl gamba duh noumer tupu
 
basi bana tarime sec,ilikua mwisho wa kusoma ni saa 4 na taa zinazimwa,mara kadhaa walinzi wanapita bwenini kukagua kama watu wamelala,sasa mlinzi mmoja alikuaga na mbwa,na anaingia nao hadi bwenini,mabweni yetu yalikua marefu yenye cubes yaani you can walk straight mwanzo mwisho,sasa siku moja mlinzi kaingia na mbwa wake yeye katatngulia mbele mbwa wako nyuma, jamaa moja la kikurya likaamka kwa kunyatia na mpini,likapiga mbwa mpini mmoja tu mbwa akalia mara1 tu na ku rip hapo hapo,yaan tulicheka ile mby, ingawa wanafunzi walikua wamefunga wamelala ila kipigo cha mbwa watu wote hawana mbavu
 
Mpande Namkubali sana!! Mwingine ni Mboya a.k.a Commando. Je wewe ulikuwa enzi zipi? Malale,Kimario,Malissa au Kisuu?Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums
Enzi za Malissa, sitasahau siku tumefanya uchaguzi afu Mpande akatukanwa kwenye vikaratasi vya kura.
 
ili kuwa mwaka gani ?
Nafikiri ilikuwa 2001 au 2002, mpande kasimama kwenye ukuta wa mesi ya Karume muda wa rolcall akaanza kuyasoma. Mpande unat...wa, Mpande unaf..., Mpande una.... . Wazenji wanamuomba asiendelee kusema ye anakazana tu niacheeni niseme. Dah enzi zile nourma sana
 
Nafikiri ilikuwa 2001 au 2002, mpande kasimama kwenye ukuta wa mesi ya Karume muda wa rolcall akaanza kuyasoma. Mpande unat...wa, Mpande unaf..., Mpande una.... . Wazenji wanamuomba asiendelee kusema ye anakazana tu niacheeni niseme. Dah enzi zile nourma sana

Duh noma kweli Isee!!
Mie nilichukua Gamba 2001 sikuiona hiyo kadhia nadhani itakuwa ni 2002 ya kina Uniform Gear na Amir Maftah.
pamoja na Mikwara yake Mpande namkubali mia mia maana alikuwa akitukinga kwa baadhi ya soo zisipande juu.
 
Yah ukweli mpande alisaidia kupunguza suspension nyingi kwa kumaliza case mwenyewe na ofisi ya vijana. Ila muda mwingine alikuwa msumbufu sana.
 
Mi bodingi nilikua napiga sana puli nikienda kuchunga ng'ombe polini
😡😡😡😡😡
 
Duh, basi mi nakumbuka tukiwa Old Moshi sec...
kwanza ni bifu tulilokkua nalo na Moshi tech...yani kuna siku tulitembea mpaka huko Moshi tech..kuanzisha vita tu!
Ila nakumbuka zaidi nilipoingia form one nikaitwa na majamaa (na walikuwa wakurya.. kutokana na lafudhi zao-afu nikakumbuka stori nlizokua nasikia kuhusu wakurya ati wakija kusoma sekondari ni wababa kabisa na wao vita ni jambo la kawaida kwao)
basi wakaniita nje ya bweni pale Hanang...wakanipa kiatu kinachonuka uvundo..wakasema nipige simu nyumbani nimwambie baba pesa zimeisha...kwa hiyo nikajifanya ninaongea na baba yangu. Basi nikatunga stori nilipokata simu nikawaambia amesema, atanitumia baada ya muda. Hivyo wakajifanya wana huruma sana...wakanipa shilingi mia, wakasema dogo kajinunulie maandazi na soda ila kabla hujanunua uje na maziwa na mkate mkubwa...duh! nilitoka jasho....
ilibidi niingie bwenini nichukue pesa zangu nikawanunulie...!!!!
tangu siku hiyo...mimi na njia ya hanang siendi...
sanasana nilikua natembea na wale majamaa vipofu, ukiwa nao hawakusumbui...hicho ndo kilichonisave....GUD OL' DAYZ....Auld Lang Syne...

Dah nimefurahi sana kuona nawe mkuu Mentor ni alumn wa Old Moshi...Old is Gold, Mawenzi, Hanang, Meru, Shengena and Kibo Forever!!!!!
 
Last edited by a moderator:
Nakumbuka Umbwe Sec siku ya kwanza kufika tu, walituita "njuka" jamaa mmoja alinifata nikiwa juu ya kitanda pale dom 4, akaniambia kuwa "oya dogo unanilipa hela yangu lini" nikamuambia ipi, akanijibu , si ya hizi ndala ulizovaa? au ni zako? kuanzia leo hizo ndala ni zangu na nimekuuzia tayari na unipe hela yangu haraka, kwanza nipe sabuni na taulo nikaoge (huku akinivua zile ndala mpya za Umoja - 1997) akazichukua na kutokomea nisikokujua, ila brother mmoja akaniambia kuwa usijali nitakuonesha anapolala utaenda kuzichukua, duh kaka mbona niliona shule chungu.....

Nimesoma Umbwe pia
 
Kuna jamaa alikuwa anaweza kubeba madishi mawili kwa pamoja, moja mkono wa kulia na lingine mkono wa kushoto. Jina lake Lobilo. Mwalimu mmoja alikuwa anafanana naye, hivyo akabatizwa hilo jina la Lobilo. Miaka mingi baddaya akabakia na hilo jina, analichukia, lakini bado wanamwita Lobilo. Akajaribu kila kitu, akalia parade ground, bado haikusaidia, amabakia Lobilo.

Bila shaka umesoma umbwe
 
enzi hzo ndan ya ikizu.kipindi cha kiangaz maji yalikuwa ya shida sana.ikawa tunaoga mtoni,kwa kuwa hatukuwa na taulo tunatembea naked kuelekea skonga ili mkaukie njian mvae nguo hii ndiyo ilikuwa tabia.day moja tukiwa kama ppipo kumi na tana tuko naked tume tumejipanga njiani tumetoka kuoga na kufua mton kama kawa tukakutana na akinamama nao wanaelekea mtoni wako na watoto wao wa kike na kiume,hakuna aliyepisha njia walivyoona tuko naked halafu hatupishi njia wakakimbia.

Ulikuwa unaishi flamingo simba au twiga
 
kwa waliosoma mawenzi sec ilikuwa tunapata luch shule ila wavulana waliokuwa bweni walikuwa wanamind hivyo walikuwa wanaenda kunachukua madishi hata ya madarasa matano wanaenda kuyaficha wanakula badae ila walikuwa wakikamatwa wanaletwa assembly cha kushangaza kila dishi walikuwa wanakula watu wawili .
Halafu kulikuwa na wengine wanaenda jikoni wanachota krimu wa juu kwenye sufuria ya maharage
Kwa kweli thoz dayz a nice 2 remember

Dah! Cream ya maharage ilikua tamu sana, nakumbuka nilishawahi kumwagia maji ya moto mpishi aliponibamba nimezamia jikoni kupitia dirishani na vibakuli vyangu viwili kwa ajili ya cream ya kwenda kuuza.
 
Hahaha hii thread imenichekesha mnoo

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom