Vituko vya Maisha ya Boarding, Tukumbushane Tuliosoma Huko

BUSARA ZANGU

JF-Expert Member
May 5, 2013
779
1,267
Asalam Aleikhum

Katika Maisha ambayo siwezi kuyasahau ni maisha ya Boarding. Maisha ya Boarding noma aliimba Jay Mo, moja kati ya wasanii waasisi wa Bongo Flavor.

Maisha ya Boarding ni moja kati ya maisha matamu lakini pia yenye changamoto nyingi. Kuna matukio na vimbwanga ambavyo vinatia chachandu katika Maisha ya Boarding.

Kuanzia kuingia shule ukiwa form 1 ni burudani tosha. Kwanza tuliitwa majina mengi sana, nyoka, Salamanda, njuka, soksi ya mlinzi n.k

Tulipigishwa simu chooni, tulichapwa mikanda usiku hasa tulipowasnitch watesaji kwa walimu. Aisee tuliooingia form 2 tukawa eti ma MP, na sisi ndio wababe dhidi ya Form 1...hataree.

Maisha ya Boarding bhana, tulikula ada, home walipojua ikawa msala wengine ilibidi kipindi cha kuchukua cheti tutafute hela kwa udi na uvumba ili tukakomboe ada tuliyokula.

Nakumbuka kipindi tunajiandaa kwenda shule baada ya likizo tulikuwa tunanunua mafuta ya kupikia na dagaa na viungo, tunachemsha huo mchanganyiko na tukifika shule duh.. hatari, kijiko kimoja cha mafuta kwa bakuli moja la maharage, waombaji sasa, weeeeengi, nyama ilikuwa mpaka ng'ombe wa shule augue.

Siku ya wali wengine ndio tulikuwa tunaoga hasa wale Tuliosoma maeneo yenye baridi. Kuna wakati tulikula ugali na sukari, sukari ni mboga wakuu sio mnashanga tena tamu kweli. Tukiandikiana barua na masela wetu wa shule nyingine, lazima ndani ya bahasha tuambatanishe punje mbili tatu za wali, watajuaje huwa tunakula wali.

Ukipoteza sahani usiwaze, kwa wali au uji utatumia ndoo unayoogea, kwa ugali utabeba mkononi na maharage utaweka kwenye kikombe chako cha uji.

Kuna wakati tulikuwa tunaenda jikoni kuiba upper layer au top layer pale msosi unapokaribia kuiva. Upper layer ni yale mafuta yanayoelea juu ya maharage, ukichanganya na maharage utamu wake sio wa nchi hii.

Kuoga haikuwa lazima. Boarding wengi ndipo walioojifunza kupiga Punyeto, a.k.a Puli. Nakumbuka kuna siku washikaji waliifanya mashindano nani atatoa wazungu haraka na mshindi alipatikana.

Kwa wapenda soka kulikuwa hamna namna unaweza kukosa Mechi za UEFA au za ligi za usiku. Kutoroka lazima, tukirudi tuna fegi mfukoni tukifika Shuleni tunampa mlinzi inakuwa sio kesi. Ikiwa zamu ya mlinzi mnoko tunatumia mbinu za kijasusi kuingia na kutoka eneo la shule.

Maisha ya boarding tulilima, tulifyeka, tulicheza. Kulikuwa na wasongo na wanafeli, halafu kulikuwa na wasongo na wanafaulu. Kubaki bwenini wakati wenzako wapo class ilikuwa kawaida sana, ila ukikutwa na bwana Pepsi shauri yako, yaani ni msala. Ila sisi wazoefu hatukukamatwa.

Muda wa prep a.k.a prepo hatukwenda class, tulisubiri usiku wa manane mtu atuamshe ndio tukasome hii ilikuwa sana sana wakati wa mitihani, tuliita msuli pepa.

Dah siku ya kuondoka school baada ya mitihani ya kitaifa kuisha ilikuwa very sad day. Wa mbeya walikwenda, wa Dar walikwenda, wa Morogoro walikwenda, wa Dodoma, wa Arusha. Kweli boarding school inakutanisha watu kutoka kila kona ya nchi.

I bet waliosoma day schools hawakupata hii informal education katika shule walizosoma.

Waliosoma maisha boarding tiririka your experience.
 
Nilikutana na mchizi wangu baraka anapenda kuangalia video si mchezo, ikawa ni kutoroka kila night hakuna cha prepo wala nini tunazama kibanda umiza.

Cheki movie mpaka ngoma 6 inawekwa pilau aseeh, siku moja ma njagu wakatuotea kibanda umiza tunacheki pilau wakatudaka watu kama 8.

Hapo tukilala kituoni ni msala skuli, kufukuzwa nje nje ilibidi tuwaambie ukweli sie wanafunzi tuwape mkwanja fulani watuachie wakakubali ikawa pona pona yetu.

Matukio ni mengi sana, niliweka wali kwenye tranka mjinga fulani akalitingisha juu chini chini juu daaa! nguo zilitapakaa wali si kidogo
 
Kipindi nasoma Tanga pale Muheza kuna jamaa alikua na kawaida ya kubakisha maharage yake ili akitoka prepo aje kula na alikua mnoko balaa wenzie wakimuomba tule wote anawakatalia....

Sasa bana siku hiyo kuna dogo mmoja aliamua kumfanyizia na ili aweze kutoa aibu ya alichotaka kufanya akaenda kula sana ganja ili apate choo kama mwenyewe alivyosema na kweli alifanikiwa kupata choo sie tupo prepo yeye kaenda bwenini kachukua ile sahani ya dogo yenye maharage akaitia chini ya uvungu wa matako yake akaachia kinyesi cha maana tu...

Kurudi prepo wote tupo bwenini dogo kapanga vitu vyake fresh katulia anavuta sahani yake kula maharage lahaula lakwata anakutana na mzigo wa mavi........itaendelea mechoka kuandika
 
kipindi nasoma Tanga pale muheza kuna jamaa alikua na kawaida ya kubakisha maharage yake ili akitoka prepo aje kula na alikua mnoko balaa wenzie wakimuomba tule wote anawakatalia....
sasa bana siku iyo kuna dogo mmoja aliamua kumfanyizia na ili aweze kutoa aibu ya alichotaka kufanya akaenda kula sana ganja ili apate choo kama mwenyewe alivyosema na kweli alifanikiwa kupata choo sie tupo prepo yeye kaenda bwenini kachukua ile sahani ya dogo yenye maharage akaitia chini ya uvungu wa matako yake akaachia kinyesi cha maana tu.....
kurudi prepo wote tupo bwenini dogo kapanga vitu vyake fresh katulia anavuta sahani yake kula maharage lahaula lakwata anakutana na mzigo wa mavi........itaendelea mechoka kuandika
endelea mkuu
 
Nilikutana na mchizi wangu baraka anapenda kuangalia video si mchezo, ikawa ni kutoroka kila night hakuna cha prepo wala nini tunazama kibanda umiza.

cheki movie mpaka ngoma 6 inawekwa pilau aseeh, siku moja ma njagu wakatuotea kibanda umiza tunacheki pilau wakatudaka watu kama 8.

hapo tukilala kituoni ni msala skuli, kufukuzwa nje nje ilibidi tuwaambie ukweli sie wanafunzi tuwape mkwanja flani watuachie wakakubali ikawa pona pona yetu.

Matukio ni mengi sana, niliweka wali kwenye tranka mjinga flani akalitingisha juu chini chini juu daaa! nguo zilitapakaa wali si kidogo
Mkuu hiyo ilikuwepo sana, kuna mchizi walimtingishia locker a.k.a kabati
 
Kupiga simu chooni, kuvuta mjani, kugonja walimu wa kikeni waliokuwa wakija field, kuuza biskuti, kuvunja makontena ya vilaza, watu tulikuwa na funguo zaidi ya 500 hizi ni za kupampu makufuli, wakati tuko shule, tunamiliki shamba bondeni, la nyanya na miwa, kupiga walimu wanoko mida ya prep, kutoroka usiku tunaenda mlima zinaa, kulala ktk mabweni ya wasichana na wasichana kujichanganya ktk mabweni ya masela, kuingia class na vi-bom, kupiga simu chooni, disko vumbi, kuwekeana mafuta ya taa ktk chakula, kuchambia godoro, kulamba sahani baada ya kula, kupiga passpot size,

Njuka mnyonge alibanduliwa au kunyonya rungu, kufunga mawe ktk mataulo kisha taa inazimwa dakika tano, muda wa kufunzana adabu, hii kila siku saa tano usiku, kupakana losheni, au kuvunjiwa yai ukilala kisha wanasingiziwa vibwengo, kuuza magodoro ya walioingia darasani wiki dume, godoro linabadilishwa na sahani ya wali maharage, mchaka mchaka saa kumi za usiku kisha mnafuata maji ya kuoga chini ya mlima..na mwisho tukachoma shule moto kisa hawakutupikia wali wiki mbili mfululizo

Nilikuwa waziri wa chakula, kampani yangu walijaziwa kuliko maadui zetu, sisi chakula tulikuwa tukiweka katika ndoo ya lita 20 watu watano, tulikuwa wanafunzi 1200 lakini nyama inapikwa kilo kumi na tano tuu, hapo waziri wa msosi nachoma kilo moja na ikiiva najaza kisado, wengine wanakunywa supu...tulibadilishana wali kwa penzi....pamoja na yote, darasani tulikuwa vizuri... mvua ikinyesha wote tulitoka nje uchi tukioga...kutokana na utukutu niliokuwa nao, pesa ya matumizi nilipewa buku na panadol tu, lakini nikirudi rikizo nilikuwa na zaidi ya laki tatu...
 
Kufuta stamp kwa sponji iliyolowanishwa kwenye maji yenye sabuni.Ule mchanganyiko wa vitunguu,dagaa na mafuta uliokaangwa na pilipili umenikumbusha mbali, prepo mwisho saa nne usiku, ila nakumbuka wakati wa national exams tulikuwa tunakesha kwenye store moja, Maisha ya boarding kwa kweli ila ilikuwa hapana aisee. Sitaki wanangu wayaishi. Ninatamani siku moja nikatembelee na wanangu shule nilizosoma na niwaonyeshe shamba, viwanja vyenye nyasi tulivyofeka. Maana wao shuleni kwao hizo kazi zinafanywa na wafanyakazi.
 
Back
Top Bottom