Enzi ulipokuwa boarding

Enzi ulipokuwa boarding

Nili kamatwa na second master katikati ya shamba la mahindi nmekoka moto nachoma mahindi. but nliyamaliza. ilikua 1997 form two.
 
Nakumbuka ilikua form3 mida ya prepo mimi nilikua naenda kama nimelazimishwa tu, ilikua kuanzia saa moja jioni mpaka saa tatu na nusu usiku, basi kila siku nilikua nabeba kidaftari changu kimoja kidogo kimeandikwa page moja tu, nyingine zimechorwa mapicha, sasa kumbe kuna ticha mnoko alikua ananifuatilia, kila siku ikifika mida ya saa tatu ni lazima aje mpaka nilipokaa kidume aangalie ninachosoma, basi ikawa mi nikifika navua shati nafungua kidaftari changu nakua bize na mapicha, nikimuona tu nafunua fasta ile page yangu halafu nakua bize balaa mpaka aondoke.
Kumbe kila siku akipita anaona page ni hiyo hiyo siku akanitolea uvivu.
alichukua kile kidaftar ghafla kisha akaanza kusema.
Naona mwenzetu hubadiliki, wewe kila siku unasoma hapa hapa inaelekea umepaelewa sana, sasa nakuuliza maswali kutokana na hapa, basi akaniuliza maswali halafu sikupata hata moja wakati kila siku ananikuta nasoma page hiyo hiyo, si ndio akaamua kufunua page inayofuata, ilikua ni noma, kesho yake parade nikatangazwa mpaka nikawa maarufu.
 
Daaa loleza galz balaaa yan hasa kun shmu inaitw golgota ww ukiitw apo ni balaaaaa
 
Hivi kwanini viranja wa misosi na wanafunzi wanaogawa gawa misosi jikoni huwa hawafanyi vizuri ?

Hii ishu nimeiona kama miaka mitatu hivi niliyokaa shule ya bweni!
 
nilikamatwa na headmaster nimeruka ukuta saa sita ya usiku,nilichezea majifi hadi nikaona mawenge maana headmaster ni mbeba nondo
 
hahaha bro umenikumbusha mbali.. dah!! boys kulikuwa na vituko

Hii mi nimeifanya sana tu pale MAVI. Daktari aliniandikia kuwa na vidonda vya tumbo. So tangu form two hadi six nakulaga special diet ya shangazi!
 
Daa me nakumbuka pale Malangali sec-Iringa huko kuna choo unapoingia lazima uvue nguo zote ili usitoke na harufu iliyobaki kwny nguo.Shkamoo choo cha DAY.
MALANGALI SEC 2010,4m 6
 
kuna jamaa ile form 5 ameripoti, yeye o'level alisoma day so akapewa deka la juu,siku ya kwanza tu aliporomoka to juu hadi chini,haaaaah haaaaaah haaaaaah
 
Ebana nakumbuka Umbwe kulikuwa na baridi sana sAsa dogo mmoja ametoka Dar Akawa kila muda anaenda kuoga...basi nomaa alapata pneumonia
 
Hivi kwanini viranja wa misosi na wanafunzi wanaogawa gawa misosi jikoni huwa hawafanyi vizuri ?

Hii ishu nimeiona kama miaka mitatu hivi niliyokaa shule ya bweni!

hilo ulosema ni kweli mwenyewe hilo jambo nimeliona sana yaani aliyefaulu kapata IV 27
 
hilo ulosema ni kweli mwenyewe hilo jambo nimeliona sana yaani aliyefaulu kapata IV 27

mi nimeona sifuri za 20 na 21 nyingi tu kwa viranja wa jikoni na wapakuaji wa misosi!
sijui hawa jamaa wanaathiriwa sana na ule moshi ama kila wakati wanawaza tu kula top layer? lol..
 
mi nimeona sifuri za 20 na 21 nyingi tu kwa viranja wa jikoni na wapakuaji wa misosi!
sijui hawa jamaa wanaathiriwa sana na ule moshi ama kila wakati wanawaza tu kula top layer? lol..

hahahaaaa haka ka msemo ka top layer kumbe tumekatumia wengi duuu kuna master food mmoja alikuja kimbaumbau hatar baada ya kupigwa menu alinawiri shavu dodo kifriji kwa mbaaali kikaanza
 
Mimi sintasahau mwenzetu mmoja alidata tu kuwa form five Same Sec. Nakumbuka alitoweka katika mazingira tatanishi na ilibidi tuanze msako wa kumtafuta kuanzia saa mbili usiku mpaka saa kumi alfajiri bila mafanikio!! Baadae kama baada ya mwezi hivi mwili wake ulipatikana milimani mifupa mitupu na inasemekana alishambuliwa na fisi!! Waliosaidia upatikanaji wake ni vijana waliokuwa wanachunga mbuzi kwenye mlima koko. Waliopitia Same miaka ya tisini mwishoni wataikumbuka hii. . RIP Nathaniel.
 
Mi nilikuwa nashangaa sana,Tanga tech siku ya vyoo vya shimo kuzibuliwa,yanatolewa mawe,magunzi,sahani,vijiko,vikombe n.k,sasa sijui watu wanakula msosi na kunywa chai chooni au hivi ndo vifaa alternative vya kutawadhia,na cha ajabu zaidi ukutani kuna maandishi,herufi zimeundwa vizuri sana kwa kinyesi!
Hahahah unakumbuka KIMUKI?
 
Yaani kama umepita shule moja inaitwa KIBiTi, utakuwa na kila 7bu ya kusimulia, maana kwa vituko vya uchawi usiseme, na mateso kwa form nyoya usiseme, nakumbuka 4m 1 yetu kuna watu walilazimishwa kuwa chua(pu.ny.eto) form 4! Noma sana!
 
Nilikua na mtindo wa kwenda kuwachungulia wanafunzi wa kike waendapo chooni, nyuma ya choo chao kulikuwa na vichaka ila kidume nilipenya mpaka kwenye ukuta kisha nikatoboa tundu zuuuriii kwa ajili ya chabo ya jicho moja(usiku walikua wanaogopa kuingia vyooni kabisa kwa hiyo wakawa wanamaliza mambo yao ule usawa wa tundu) baada ya mchezo kunoga ikawa hata prep usiku siingii, mi nikifika darasani naweka daftari langu kisha huyoooo naruka ukuta kisha vichakani kwenye video ya bure, Za mwizi arobaini bwana, siku ikafika nipo mimi na washkaji zangu wawili tunaangalia (kila mtu na tundu lake hapo) Kumbe second master kashajificha karibu kabisa na mgongo wangu na boonge la fimbo mbichi, yaani ile utamu wa video unaanza kunoga nilistukia bonge la kitu kizito kinatua mgongoni, kwa kasi ya umeme nikageuka naona mtu nae ghafla akanirukia kwa lengo la kunikamata(wenzangu hapo wameshakimbia) nilimpiga push moja ya ajabu akaanguka kwenye vichaka halafu nikakimbia kisha nikaenda darasani.
Baada ya kama dk10 hivi nimetulia na daftari langu huku nasikilizia maumivu kwa mbaali second akaingia darasani akiwa ameongozana na waalimu wengine watatu, wakapita moja kwa moja mpaka nyuma ya darasa(kumbe wanaangalia alama ya fimbo mgongoni sababu jamaa alinichapa kwa fimbo mbichi). Mimi hapo nimetulia nasikilizia kama sio mim, mara nikasikia " yule pale" . Yaani kipigo nilichopata kuanzia mle darasani ni historia mpaka kwa wajukuu wangu, ila mwisho kabisa nilikataa kuhusika wakaishia kuni suspend kwa muda wa wiki mbili tu.
 
Back
Top Bottom