Mwembebasha
JF-Expert Member
- Dec 27, 2013
- 1,424
- 406
Yaani nimejaribu kuvuta picha ya hili tukio nimecheka mpaka mbavu zinauma!!!Nakumbuka kuna mlinzi aliwahi ona bundi akajua simba basi akaja kutangaza kua kuna simba alikua ni mmasai .Mimi nilikua napenda kutoroka kwenda kijijini na washkaji siku moja niliwauliza wana zengo kua huku kuna simba wakasema ni bundi wakubwa tu.Basi ulipita kama mwezi siku moja nilikua natoka prepo ile mida ya saa za wasongo kama saa nane usiku hivi nilikua nakimbia kwa korido kuna jamaa akatokea mbele yangu alikua anaenda kunawa uso ili akasome akaniuliza unakimbia nini?Nikajibu simba!Aisee yule jamaa alitupa maji na kukimbilia domitory na kuanza kulia simbaaaaaaa!Shule nzima ilikimbizana yule mlinzi ndio usiseme!Basi madom yetu yalikua na kenchi yaani watu walininginia kama popo ili simba aiwangate!Kuja kuja kama wameuzwa walikua wame umia vibaya aisee members wa mkandawile mpo hapa???