Edward Lowassa aumbuka Arumeru Mashariki

Edward Lowassa aumbuka Arumeru Mashariki

hahahaha.. kwa kweli nimeamini na sasa namkubali lowassa fuluu. yaani akiwekwa tu, lazima ukute page 5-10. kweli jamaa ni tishio kubwa sana, sio bure huyo rais/mwenyekiti wa chama anakosa usingizi akimfikiria lowassa. humu ndani nimeshaona watu wengi sana wanamkubali, nilitegemea leo mngechambua hotuba ya jana ya rais. lakini naona mmeanza unafiki wa msg zimekutwa. izo message ziko wapi. kama kweli wangeanika, ni fikra za mtu tu.hamna jipya

mi nilitegemea nitakuta labda hoja ya mgombea wa chadema arumeru, au jinsi mbowe alivyokusanya hela kumfanikisha ashinde.

ivi kweli kwa mtu kama lowassa ataweza kukaa na kuchat aagize watu wakachukue hela. lazima anawatendaji wengi tu wa kufanya ivyo. acheni zengwe

Uzinifu huanzia ufichoni siku zinavyosonga mbele hudhani ni halali yao! Huja kujua sio halali yao watakapokutwa sebuleni na mama mwenye nyumba!
 
Hizi ni kamba wazazi mtu mzima el huwa anatwanga siyo mtu wa sms mlio arusha wekeni issue sawa tujue kama jao wazazi wako lupango
 
Lowassa mpaka leo hajui mbinu za kupanga madili? He should ve called using private number in secured line. Ye si mtu mkubwa banaa! Inakuwaje anacheza kitoto?
 
Kweli Jakaya kaamua kula hiki kichwa jumla.
Lowassa anatakiwa kutafutwa popote alipo na yeye awekwe ndani
OTIS

Anambana kila kona. Mara rushwa, mara nataka raisi kijana. . .haya tusubiri
 
Takukuru Leo wameamua kumgeuka Edward Lowasa na vibaraka wake katika marudiano ya uchaguzi wa Arumeru. Katika sakata Hilo katibu wa UVCCM wilaya ya Monduli ndugu Ezekiel Mollel ametupwa rumande Mara baada ya kukamatwa na simu yake ilipo pekuliwa na kukutwa na mesej alizokuwa Akiwasiliana na Lowasa kuhusu kuchukua hela kwa askofu na mathius manga kwa Lengo la kwenda kuwahonga wajumbe wa arumeru Mashariki.

Katibu huyo amekiri kupewa maelekezo hayo na Lowasa na kuomba asamehewe kwa kuwa Lowasa ni kiongozi mkubwa yeye asingeweza Kuwa na ujasiri wa kumkatalia. Hadi wakati huu Ezekiel Mollel na Askofu wapo rumande.

Pia katika tukio lingine Fred Lowasa amethibitika kumhonga ticket ya ndege Elirehema kaaya ili amsaidie Sioi aweze kushinda. Kwenye simu ya elirehema Kaaya zimekutwa mesej Kuwa nakulipia ndege pamoja na kukupa lile fungu la kuwapelekea wajumbe. Kwa ushahidi huu hadi sasa elirehema Kaaya yupo rumande.

Wakati wowote mambo haya yatapelekea wahusika kupelekwa mahakamani.

Wana Arumeru mashariki wafanye uchaguzi kwa amani na utulivu na tena wasiwe na hofu yoyote.

Hii habari inaoneka umeitoa kwenye gazeti pendwa la udaku KIU.
Hivi Edward Lowassa anaweza kuangaika kuandika sms? Hahahahaha Chadema bana!
 
Rafiki zangu wa karibu sana Mheshimiwa Pasco & Matola,

Niliwaambia Lowassa alishapotezwa siku nyingi wakanibishia sijui mpaka leo na baada ya kusoma kisa hiki bado wana amini Lowassa is next President ?.

Kitendo cha Lowassa kumuumbua Mwenyekiti wake ndani ya kikao cha Halmashauri kuu ya taifa kwamba alijua kila kitu katika ule mradi tata wa RICHMOND & DOWANS na kwamba alipelekewa jina la Rostam Aziz na kulikubali wakati mwenyekiti alishajitetea hamjui mmliki wa RICHMOND & DOWANS alikuwa akitengeneza jeneza lake kwa mikono yake mwenyewe.Lowassa alikwenda mbali sana alipohakikisha mazungumzo yake yanawafikia wahariri wa magazeti kupitia simu za kiganjani ndani ya kikao cha Halmashauri kuu !.

Mkuu Ngongo, kiukweli Takukuru wanajifurahisha tuu!, hakuna kesi yoyote serious ya rushwa!. Kama uchaguzi uliopita Takukuru waliwakamata watu na rushwa red handed na hakuna kesi yoyote, ndio itakuwa sms za rushwa!.

Machalii wa Arusha wanapenda kash kash za Godbless Lema type. Kushikiliwa polisi kwa wana AR ni ushujaa hivyo sasa kitendo cha kuwashikilia mahabusu hao wafuasi wa Sioi, hivyo ndio kampeni funga kazi kwa Sioi, amemaliza kila kitu!.

Kabla ya purukushani hii, CCM wangeweza kumtosa Sioi, lakini hii promo ya Takukuru sasa ndio imemrudisha Sioi at the top, hivyo sasa Arumeru ngoma bado ni mbichi, Sioi ndiye mgombea wa CCM and to my honest opinion, Arumeru is done, tuanze kupima upepo wa nguvu ya EL kuelekea 2015!.
 
Takukuru Leo wameamua kumgeuka Edward Lowasa na vibaraka wake katika marudiano ya uchaguzi wa Arumeru. Katika sakata Hilo katibu wa UVCCM wilaya ya Monduli ndugu Ezekiel Mollel ametupwa rumande Mara baada ya kukamatwa na simu yake ilipo pekuliwa na kukutwa na mesej alizokuwa Akiwasiliana na Lowasa kuhusu kuchukua hela kwa askofu na mathius manga kwa Lengo la kwenda kuwahonga wajumbe wa arumeru Mashariki.

Katibu huyo amekiri kupewa maelekezo hayo na Lowasa na kuomba asamehewe kwa kuwa Lowasa ni kiongozi mkubwa yeye asingeweza Kuwa na ujasiri wa kumkatalia. Hadi wakati huu Ezekiel Mollel na Askofu wapo rumande.

Pia katika tukio lingine Fred Lowasa amethibitika kumhonga ticket ya ndege Elirehema kaaya ili amsaidie Sioi aweze kushinda. Kwenye simu ya elirehema Kaaya zimekutwa mesej Kuwa nakulipia ndege pamoja na kukupa lile fungu la kuwapelekea wajumbe. Kwa ushahidi huu hadi sasa elirehema Kaaya yupo rumande.

Wakati wowote mambo haya yatapelekea wahusika kupelekwa mahakamani.

Wana Arumeru mashariki wafanye uchaguzi kwa amani na utulivu na tena wasiwe na hofu yoyote.

Nduguyetu joseph Peter, inaonekana wewe umebobea upotoshaji na umebobea Kabisa. Mimi naomba ni toe facts Kama zilivyo na nipo tayari kuwa challenged na mtu yoyote. Kwa sasa hivi nipo nje ya ukumbi wa mkutano wa kupigia kura na wajumbe wameshaingia wote wakiwa wamependeza na mashati yao ya kijani na njano na nimefurahia Sana kumuona kamanda wangu Elirehema Kaaya akiingia ukumbini kwa nyuso ya furaha kabisa hata baada ya kupigwa msukomsuko na maafisa wa takukuru.

1. Elirehema Kaaya alikwenda Dsm kushirki vikao vya secretariat na kamati kuu akiongozana na ndugu Kisali sarakikya ambaye name anapigiwa kura leo, walikaa wote Dsm na baada ya kikao wakafanya safari ya kurudi wote arusha. Ni mjumbe halali wa mkutano wa leo na Jana wakati amekamatwa alikuwa amekaa kwenye grocery na wapiganaji wake wakibadilishana mawazo, hakukuwa na mambo yoyote ya pesa. Elirehema anajimudu kiuchumi na ninategemea ana uwezo Kabisa aw kulipia nauli zake, lakini Kama kuna wa kumtuhumu kumsaidia usafiri labda iwe sarakikya, lakini bado siamini hivyo.

2. Ezekiel Mollel ni katibu wa vijana wa uvccm monduli na ni mkazi na mwenyeji wa wilaya ya arumeru, uvccm mkoa kwa kupitia katibu wake wa mkoa Mpokwa wanashiriki marudio haya ya kura Kama jumuiya zingine zote za mkoa kwaajili ya maandalizi ya uchaguzi mkuu tar 1 april. Huyu alishikwa akiwa peke yake anapanda pikipiki na inasemekana maafisa walikuwa na kijani anaitwa ammo akiwaonyesha watu wa kukamata, kwenye kundi hilo hilo walikuwepo makatibu wa wilaya zote za mkoa na katibu mwenyewe wa mkoa, napa unaona u-monduli ulitumika ili kwa Mara nyingine tena tuliingize jina la lowassa kwenye midahalo ya CCM. Mawasiliano yake na simu siwezi kuwa na uhakika, ila ukiniambia alikuwa anawasiliana na lowassa, hiyo ni PUMBA.

Tukirudi kwenye mchakato wenyewe wa kura za leo, inasikitisha na inatia aibu kubwa sana, ningekuwa mimi ndiyo Huyo kijana anaitwa sioi ningejitoa. Jana Mkuu Wa wilaya aliwaita madiwani wote wa arumeru mashariki na kuwaambia msimamo wa serikali ni ssarakikya, na ikatokea vurugu kubwa na polisi wakaweka madiwani wengine chini ya ulinzi. Tujiulize kwanza kwanini huu uchaguzi unarudiwa Leo? Hamna Majibu ya kuridhisha, na ukijiuliza tena ni watu gain walipinga matokeo ya sioi kwenye vikao? Unapata majibu ni wateule wote wa serikali na chama, sishangai kusikia haya ya takukuru leo ila inasikitisha Sana. Demokrasia ya Kweli iko wapi? Ningefikiri kazi ingekuwa kusimamia uchaguzi wa kweli na haki, na wananchi wapate fursa ya kuamua wawakilishi wao.

Namalizia,baada ya kamati kuu kuamua uchaguzi kurudiwa, wazee wawili wa kamati kuu walimfuata Sioi kumshauri ajitoe kwasababu sababu za yeye kukatwa jina hata Kama akishindwa zimeshaandaliwa na Sioi akawajibu kwamba sivyo ambavyo nimelelewa na wazazi wangu, nilifanya sala Kuomba baraka za marehemu baba, ningependa huko aliko alone kijana wake sikumuangusha na nilismamia ninachokiamini mpaka mwisho whether win or lose.

Tusubiri tuone cinema hivi inaishia wapi.
 
bye bye lowasa,
mzimu wa mwakyembe umeanza kazi
akingali hai bado.
 
Hawa magamba kwa strategy za kizamani kweli hawajambo... Yani sasa wanataka kuwaaminisha wananchi kwamba wapo vitani na rushwa ni adui yao, lakini ukweli ni kwamba nani kati yao anayeweza kumnyooshea mwenziwe kidole? kinachoendelea hapo ni mbinu tu ya kuwakoga wabongo na hasa wana Arumeru Mashariki ili waonekane wanatuletea mtu safi.

Wana Arumeru Mashariki zindukeni achaneni na sarakasi za magamba kamataneni na wanamageuzi ili mkombolewe kifikra na kiuongozi.
 
Takukuru Leo wameamua kumgeuka Edward Lowasa na vibaraka wake katika marudiano ya uchaguzi wa Arumeru. Katika sakata Hilo katibu wa UVCCM wilaya ya Monduli ndugu Ezekiel Mollel ametupwa rumande Mara baada ya kukamatwa na simu yake ilipo pekuliwa na kukutwa na mesej alizokuwa Akiwasiliana na Lowasa kuhusu kuchukua hela kwa askofu na mathius manga kwa Lengo la kwenda kuwahonga wajumbe wa arumeru Mashariki.

Katibu huyo amekiri kupewa maelekezo hayo na Lowasa na kuomba asamehewe kwa kuwa Lowasa ni kiongozi mkubwa yeye asingeweza Kuwa na ujasiri wa kumkatalia. Hadi wakati huu Ezekiel Mollel na Askofu wapo rumande.

Pia katika tukio lingine Fred Lowasa amethibitika kumhonga ticket ya ndege Elirehema kaaya ili amsaidie Sioi aweze kushinda. Kwenye simu ya elirehema Kaaya zimekutwa mesej Kuwa nakulipia ndege pamoja na kukupa lile fungu la kuwapelekea wajumbe. Kwa ushahidi huu hadi sasa elirehema Kaaya yupo rumande.

Wakati wowote mambo haya yatapelekea wahusika kupelekwa mahakamani.

Wana Arumeru mashariki wafanye uchaguzi kwa amani na utulivu na tena wasiwe na hofu yoyote.




Haya bwana kwa mara nyingine tunaletewa maigizo and then we succumb in the fictious drama na kuachana na mambo nyeti. TAKUKURU have for so many days been toothless bull dogs that cannor bark. Sasa kwa kuwakamata hao watu waliotajwa tena kwa kutumia txts za simu ndio kutufanya sisi tuwapongeze? Hapana nafikiri TAKUKURU wana wajibu mkubwa kuweka efforts za kuwakamata wala rushwa kubwa kubwa ambao vitendo vyao vimeliangamiza taifa hili katika lindi la umaskini. Hatujawasikia wakitumia nguvu hiyo kukamata waliokwapua pesa toka BOT maarufu kama EPA, hajakamata list of shame ambayo haijawahi kukanushwa, watuhumiwa wa MEREMETA, Richmond, waliotorosha wanyama wetu kwenda Qartar watuhumiwa wa Kiwira na wote waliosainisha mikataba tata ya madini na kutuacha kama taifa kuambulia asilimia 3 kama mrahaba na mengine mengi yanayofanana na hayo. Sasa wanatumia reveneu za serikali zitokanazo na wananchi kukimbizana na wanaotoa pesa ya soda. Shame on you TAKUKURU. Maofsa wanaokimbiza na vijitu vidogovidogo kwa gharama kubwa ingefaa washtakiwe wao. ANy effort should pay off itself for public benefit.

Halafu wanasiasa waangalie na wajue kuwa kumchafua EL sio kwamba ndio mtasafishika. La hasha. Watanzania wa leo sio wa jana. Hivi sasa awareness yetu ni kubwa. Makosa ya EL hayawezi kuwasafisha kwa madudu yaliyoelezwa hapo juu. It's a matter of time. Saa ya ukombozi yaja na nyie mtajibu ya kwenu. EL anafanyiwa character assassination na kama mnafikiri anayo makosa mbona hamjampeleka mahakamani? Uko si ndio haki inapopatikana? Enough is enough with EL tunataka kujua walioifilisi na ambao wanaendelea kuifilisi watakamatwa lini?
 
Mimi nina maoni tofauti hii yote ni danganya toto ya takukuru ili muamini kweli wamefanya kwa nia njema kumbe kuna zaidi ya hayo. wanatumia tu hii iwe sababu kwamba wanakamata rushwa kumbe mpango mzima wa kugawa pesa unakuja baadaye. Nimeamini hivyo kutokana na CCM walivyo na njia nyingi za kutudanganya na wanajua kabisa watanzania huwa hatufikirii zaidi ya tukio. Ni maoni yangu tu
 
mzee issue hapa tunataka utuoneshe zilipo nguvu za lowassa hutuonyesha unatapa tapa tu mara utupeleke ukada mara uturudishe kwenye remote ya batteries mpya,tuonyeshe nguvu za lowassa alizobaki nazo,mimi kukurahisishia ntataja alizokuwa nazo ambazo sasa hana tena..

-alikua waziri wetu mkuu kwa miaka isiyozidi mitatu,sasa sio waziri mkuu tena wala hayuko kwenye cabinet
-alikua mjumbe wa kamati kuu sasa hayuko tena huko
-alifight sana kurudi kwenye baraza la mawaziri hakuweza kurudi
-yeye kupitia kwa wapambe wake kina bashe waliapa kwamba ubunge wa igunga unaenda upinzani wakashindwa vibaya sana
-alipenda sana suala la kujivua gamba lizimwe na nec lisiende kamati kuu akashindwa licha ya kulilia sana aonewe huruma na mwenyekiti eti kwa kuwa na yeye mwenyekiti aliwahi kuonewa huruma na mkapa haikumsaidia sana
-aliomba nape aadhibiwe kwa kumpulizia vuvuzela ambalo hapendi kulisikia masikioni hakuna aliyemsikiliza
-kwenye nec ya juzi aliwatumia wapambe wake kingunge na peter serukambaa wapinge mabadiliko ya katiba yatakayomchinja yeye kwenye uchaguzi ujao wa ccm lakini wajumbe wa nec ileile ambayo huwa tunaambiwa ana nguvu wakasema hapana mzee tunamuunga mkono mwenyekiti akiimarishe chama,akashindwa tena kwa mar nyingine ndani ya nec yake
-Na sasa kuna hili mkwewe kugombea ubunge arumeru ndio watu wake wamekamatwa na jina lake kwa mara ya kwanza limetajwa na vyombo vya usalama...
KK

Naona humjui Lowassa na RA kwenye nchi hii.
 
Anambana kila kona. Mara rushwa, mara nataka raisi kijana. . .haya tusubiri

Sasa makucha yameanza kunjuliwa.
Upenyo kama huu sio wa kuuachia ili apotezwe kabisa.
OTIS
 
KGBtz,
Aliyenisikitisha mimi ni Nape. Alitutangazia maamuzi ya ajabu ya kikao cha CC ya CCM huku akijua fika kuwa kanuni hiyo imekiukwa mara nyingi tu kwenye teuzi za ndani ya CCM. CCM haohao kwa kutumia wingi wa WABUNGE wao walikiondoa kipengele kinachofanana na kanuni hii ya mgombea kufikisha zaidi ya nusu ya kura ili atangazwe mshindi kwenye uchaguzi wa Rais wa JMT.
 
Wajameni tuwe wakweli toka ndani ya nafsi zetu, kama issue ni rushwa, kwa CCM, its order of the day!. CCM kwa upande wa rushwa imeoza juu mpaka chini na ndani mpaka kwenye kiini, hivyo hayo yanayoendelea ni harufu tuu ya uvundo wa rushwa, rushwa yenyewe halisi, CCM ndio nyumbani kwake!.

Naendelea kusimama na EL ateuliwe kuwa mgombea wa CCM, rais atoke Kaskazini tupate ukombozi wa kweli wa Mtanzania!.

Mnaoamini kila supporter wa EL amelipwa, naomba niwasemee kabisa ili msijisumbue kusema, "mimi nimelipwa" na kwa vile takukuru pia wanashinda himu, njooni pia mnikamate tena sio na sms, but hard cash, lots of them!.

Invisible, Takukuru wakiniulizia, just disclose info and expose it!
 
Kadri siku zinavyo sogea ndivyo CCM inazidi kuwa chama kichovu zaidi. Hizi sarakasi tutazishuhudia vizuri kampeni zitakapoanza. Niko na wasiwasi vituo hewa tayari vimeisha tayarishwa ili CCM ishinde.
 
Back
Top Bottom