KK,
Kura za maoni AruMeru Mashariki kwa wagombea wa CCM zinarudiwa kwa nini? Sababu alooitoa Nape sio. Vinginevyo watu kama Kigwangala waliteuliwaje kugombea na CCM hiyohiyo na kanuni hiyo ikiwepo!
mzee issue hapa tunataka utuoneshe zilipo nguvu za lowassa hutuonyesha unatapa tapa tu mara utupeleke ukada mara uturudishe kwenye remote ya batteries mpya,tuonyeshe nguvu za lowassa alizobaki nazo,mimi kukurahisishia ntataja alizokuwa nazo ambazo sasa hana tena..
-alikua waziri wetu mkuu kwa miaka isiyozidi mitatu,sasa sio waziri mkuu tena wala hayuko kwenye cabinet
-alikua mjumbe wa kamati kuu sasa hayuko tena huko
-alifight sana kurudi kwenye baraza la mawaziri hakuweza kurudi
-yeye kupitia kwa wapambe wake kina bashe waliapa kwamba ubunge wa igunga unaenda upinzani wakashindwa vibaya sana
-alipenda sana suala la kujivua gamba lizimwe na nec lisiende kamati kuu akashindwa licha ya kulilia sana aonewe huruma na mwenyekiti eti kwa kuwa na yeye mwenyekiti aliwahi kuonewa huruma na mkapa haikumsaidia sana
-aliomba nape aadhibiwe kwa kumpulizia vuvuzela ambalo hapendi kulisikia masikioni hakuna aliyemsikiliza
-kwenye nec ya juzi aliwatumia wapambe wake kingunge na peter serukambaa wapinge mabadiliko ya katiba yatakayomchinja yeye kwenye uchaguzi ujao wa ccm lakini wajumbe wa nec ileile ambayo huwa tunaambiwa ana nguvu wakasema hapana mzee tunamuunga mkono mwenyekiti akiimarishe chama,akashindwa tena kwa mar nyingine ndani ya nec yake
-Na sasa kuna hili mkwewe kugombea ubunge arumeru ndio watu wake wamekamatwa na jina lake kwa mara ya kwanza limetajwa na vyombo vya usalama...