Edward Lowassa aumbuka Arumeru Mashariki

Edward Lowassa aumbuka Arumeru Mashariki

Safari hii hakuna pa kupumulia!!!

Waulize wanaomjua JK, akikubadilikia kakubadilikia,
kama (JK) angekuwa bado upande wa EL hayo hote yasingetokea lakini sasa wapo tofauti kabisa
na hii vita inapoelekea EL atachemsha kabisa na hata huo uraisi hataweza kuusimamia akiwa ndani ya CCM hii ya JK-Mukama
 
Mkuu Mkandara,
Naona tupo kwenye chumba cha mtihani, mie nipo upande wa yoyote anayepambana Chadema huo ndio msimamo wangu.
Sawa una sababu zako japokuwa sio uchungu kwa maslahi ya Taifa. Mimi naamini kabisa I can make a Change, wewe mnazi unatazama mpira tu na kushangilia mradi Arsenal wafungwe na ManU..
 
Iliyoumbuka ni CCM wala si Lowassa.

Aliyeumbuka hapo si CCM ni watu waliokamatwa na tuhuma hizo ujue chama cha CCM kwa taratibu zake na kanuni zake ndani ya katiba yake hakuna sehemu inayomruhusu mtu kufanya vitendo kama hivyo vya rushwa na vingine viovu na ndiyo maana mtu akienda kinyume anachukuliwa atua kwa mujibu wa katiba nakuomba uovu huo usiuhusishe na chama ata kdg chama kiko vizuri maswala ya mtu binafsi yasihusishwe na chama,Kidumu Chama Cha Mapinduzi CCM!
 
Mkuu Mkandara,
Naona tupo kwenye chumba cha mtihani, mie nipo upande wa yoyote anayepambana na Chadema huo ndio msimamo wangu.

Vipi mbinu iliyotumika Igunga na Uzini kuwagawa watu kwa misingi ya udini itatumika Arumeru?
 
Aliyeumbuka hapo si CCM ni watu waliokamatwa na tuhuma hizo ujue chama cha CCM kwa taratibu zake na kanuni zake ndani ya katiba yake hakuna sehemu inayomruhusu mtu kufanya vitendo kama hivyo vya rushwa na vingine viovu na ndiyo maana mtu akienda kinyume anachukuliwa atua kwa mujibu wa katiba nakuomba uovu huo usiuhusishe na chama ata kdg chama kiko vizuri maswala ya mtu binafsi yasihusishwe na chama,Kidumu Chama Cha Mapinduzi CCM!
Kama hivi ndivyo imekuwaje mgombea sioi kashinda? waliompa ushindi huo ni CHAMA au pia ni watu! yaani Sioi atakuwa mwakilishi independent!
 
Waulize wanaomjua JK, akikubadilikia kakubadilikia,
kama (JK) angekuwa bado upande wa EL hayo hote yasingetokea lakini sasa wapo tofauti kabisa
na hii vita inapoelekea EL atachemsha kabisa na hata huo uraisi hataweza kuusimamia akiwa ndani ya CCM hii ya JK-Mukama

Unayajua matokeo yaliyotangazwa hivi punde? Au unajifurahisha tu,EL ni kiboko ya CC-CCM
 
Waulize wanaomjua JK, akikubadilikia kakubadilikia,
kama (JK) angekuwa bado upande wa EL hayo hote yasingetokea lakini sasa wapo tofauti kabisa
na hii vita inapoelekea EL atachemsha kabisa na hata huo uraisi hataweza kuusimamia akiwa ndani ya CCM hii ya JK-Mukama
Wewe kweli kituko, Lowasa leo ndio kidume na kama CCM sababu zao zilikuwa ni asilimia 50 plus, basi hichi kidume kimehakikisha kijana wake anatwanga kwa zaidi ya 70% JK &CO, chali.
 
Vipi mbinu iliyotumika Igunga na Uzini kuwagawa watu kwa misingi ya udini itatumika Arumeru?
Uzini nani alotumia mbinu za Udini? kama Chadema wangetumia mbinu ya Udini wangeweza kupata hata hizo kura 200. Usiwafanye watu wa Uzini wajinga kiasi hicho kama alivyosema huyo Jussa mwafrika wa kiapo cha uraia. CCM wameshinda Uzini kwa sababu waliweza kushinda hata uchaguzi wa 2010 kwa asilimia kubwa sana. Kwa CDM, kampeni za week moja au mbili hata siku moja haziwezi kuleta ushindi hata kama wangempeleka nani. Igunga kilichofanyika ni Kukipaka Chadema maana wakazi wengi wa mjini Igunga ni Waislaam na propaganda za CCM kuhusu Udini zilianza hata kabla Rostam hajajiuzuru.

Chadema isingeweza kushinda Igunga na haitaweza shinda sehemu zozote zenye Waislaam kwa sababu tumeshindwa kujihusisha na tuhuma mlowajaza watu Ujinga. Udini upo kila sehemu, hata Chadema lakini ni vichwani mwa watu sio chama wala siasa za Chadema. CCM wanazitumia waziwazi.. Lowassa kisha kamata Masheikh ubwaba (Bakwata) wote sasa hivi anaingia makanisani - mchezo umekwisha.
 
Haya ni maneno ya Nape facebook akimpiga vijembe Sioi Sumari kambla ya Matokea haya kupatikana.

[h=6]Nape Nnauye
[/h][h=6]Matumizi ya pesa kutafuta uongozi- RUSHWA, ni uthibitisho wa kutotosha kwa mgombea kwa nafasi aiombayo hivyo kulazimika kuziba na rushawa![/h]
y-2LR9eyI1L.gif
Share · 12 hours ago via mobile ·


Sasa swali linakuja je Nape na CCM yake wako tayari kumnadi kwa Wananchi mgombea mtoa Rushwa!!??
 
Leo asubuhi ktk hii thread kulikua na watoto/vijana wa Nape wakimponda sana Lowassa,sasa siwaoni tena humu! Tutarajie kampeni moja ngumu sana kwa pande zote mbili CDM na CCM. Muhimu ziwe kampeni za kistaarabu.
 
Dah afu watu wanabisha EL sio bao la mkaburu...
Mi nauwakika huyu jamaa mkifwatilia family tree yake lazma kuna bibi au babu alicheza faulo kwa mzungu...uzawa ukaendelea weeee ndo sampuli za lowassa zika evolve..
Uyu jamaa amefeli ule utanzania walau masalia ya utu wa kizalendo...a.k.a mkaburu uyu kiumbe...:hana huruma kabsAa
 
kama huna ushahidi kaa kimya. usituletee ushabiki wako.
 
Wewe kweli kituko, Lowasa leo ndio kidume na kama CCM sababu zao zilikuwa ni asilimia 50 plus, basi hichi kidume kimehakikisha kijana wake anatwanga kwa zaidi ya 70% JK &CO, chali.

Mkuu Matola nakuheshimu sana na pia huwa naheshimu sana michango yako,
lakini kwa leo umenikatisha tamaa kabisa, Mimi sikuongelea habari za uchaguzi uliokuwa unaendelea mimi nimejadili hoja iliyowekwa mezani kwa jina la Lowassa kuhusishwa na mambo ya rushwa , sasa hapo hiyo hoja ya matokeo ya uchaguzi inauhusiano gani na hoja yangu?
 
Takukuru Leo wameamua kumgeuka Edward Lowasa na vibaraka wake katika marudiano ya uchaguzi wa Arumeru. Katika sakata Hilo katibu wa UVCCM wilaya ya Monduli ndugu Ezekiel Mollel ametupwa rumande Mara baada ya kukamatwa na simu yake ilipo pekuliwa na kukutwa na mesej alizokuwa Akiwasiliana na Lowasa kuhusu kuchukua hela kwa askofu na mathius manga kwa Lengo la kwenda kuwahonga wajumbe wa arumeru Mashariki.

Katibu huyo amekiri kupewa maelekezo hayo na Lowasa na kuomba asamehewe kwa kuwa Lowasa ni kiongozi mkubwa yeye asingeweza Kuwa na ujasiri wa kumkatalia. Hadi wakati huu Ezekiel Mollel na Askofu wapo rumande.

Pia katika tukio lingine Fred Lowasa amethibitika kumhonga ticket ya ndege Elirehema kaaya ili amsaidie Sioi aweze kushinda. Kwenye simu ya elirehema Kaaya zimekutwa mesej Kuwa nakulipia ndege pamoja na kukupa lile fungu la kuwapelekea wajumbe. Kwa ushahidi huu hadi sasa elirehema Kaaya yupo rumande.

Wakati wowote mambo haya yatapelekea wahusika kupelekwa mahakamani.

Wana Arumeru mashariki wafanye uchaguzi kwa amani na utulivu na tena wasiwe na hofu yoyote.


Wadau, tuache mzaha! Tulidhani kuwa E L ndiye ameumbuka kwa kurushwa lupango akisubiri kesho apelekwe mahakamani kwa pilato kusulubiwa, kumbe ni wasugua-lami, akina Kaaya!
Si mnakumbuka mbaya wa Lema, Batilda na Wajumbe wake walidakwa kavu-kavu ktk Ukumbi fulani wa vinywaji, nadhani mitaa ya kwa-Mromboo au Sombetini kama sijakosea, wakati wa kampeni za Uchanguzi wa 2010 wakigawana fedha za kuwafisadi wananchi, je Balilda alisulubiwa popote? Na je Mama Sitta naye si alikamatwa ready-handed na minoti kibao pamoja na wajumbe wa kampeni zake 2010, je walifikishwa mahakama ya wapi?
Wadau, tukumbushane...Mahakama zetu za sasa sio kwa ajili yao wala-nchi wanaofisadi, bali ni kwa ajili ya wasugua-lami! Hadi tuibadili nchi hii ndio mahakama zitakuwa kwa ajili ya akina EL, na wafisadi-nchi wengine!
Pamoja daima, tutashinda taaaaratiib...!
 
Thread zingine bwana. Inawezekana jamaa amekaa chini, ametengeneza story na kuipost. Jamaa tunajimwaga na data kumbe ni suala la kutunga tu. Anyway, labda hiyo ndiyo raha ya jf.
 
Mkuu Matola nakuheshimu sana na pia huwa naheshimu sana michango yako,
lakini kwa leo umenikatisha tamaa kabisa, Mimi sikuongelea habari za uchaguzi uliokuwa unaendelea mimi nimejadili hoja iliyowekwa mezani kwa jina la Lowassa kuhusishwa na mambo ya rushwa , sasa hapo hiyo hoja ya matokeo ya uchaguzi inauhusiano gani na hoja yangu?
Mkuu wangu kama ulishindwa kunielewa basi haukuwa na nia ya kunielewa, Lengo la hii thread ya leo ilikuwa ni kumdhihaki Lowasa kuhusiana na uchaguzi wa leo, sasa kijana wa Lowasa ndiye alieshinda ni kwa nini matokeo ya uchaguzi huo yasihusishwe na thread hii!!?? labda ningekuomba uisome upya hii thread then hakuna utakachokishangaa.
 
Kwanza mi naombea EL ndio angewekwa lupango. Ila hapo waliowekwa lupango ni watu tofauti..
Sioi na EL wapo wanatanua mtaani, hata hawajahojiwa.

Neno hilo/hukumu yao kifo.
 
Back
Top Bottom