Edward Lowassa aumbuka Arumeru Mashariki

Takukuru Leo wameamua kumgeuka Edward Lowasa na vibaraka wake katika marudiano ya uchaguzi wa Arumeru. Katika sakata Hilo katibu wa UVCCM wilaya ya Monduli ndugu Ezekiel Mollel ametupwa rumande Mara baada ya kukamatwa na simu yake ilipo pekuliwa na kukutwa na mesej alizokuwa Akiwasiliana na Lowasa kuhusu kuchukua hela kwa askofu na mathius manga kwa Lengo la kwenda kuwahonga wajumbe wa arumeru Mashariki.

Katibu huyo amekiri kupewa maelekezo hayo na Lowasa na kuomba asamehewe kwa kuwa Lowasa ni kiongozi mkubwa yeye asingeweza Kuwa na ujasiri wa kumkatalia. Hadi wakati huu Ezekiel Mollel na Askofu wapo rumande.

Pia katika tukio lingine Fred Lowasa amethibitika kumhonga ticket ya ndege Elirehema kaaya ili amsaidie Sioi aweze kushinda. Kwenye simu ya elirehema Kaaya zimekutwa mesej Kuwa nakulipia ndege pamoja na kukupa lile fungu la kuwapelekea wajumbe. Kwa ushahidi huu hadi sasa elirehema Kaaya yupo rumande.

Wakati wowote mambo haya yatapelekea wahusika kupelekwa mahakamani.

Wana Arumeru mashariki wafanye uchaguzi kwa amani na utulivu na tena wasiwe na hofu yoyote.
Kumbeeeeeeeeeeeee!!! huyu bwana anazungikia makanisa kwa kisingizio cha harambeee za ujenzi wa kanisa kumbe anaacha pesa kwa ajili ya rushwa sasa TAKUKURU mpo wapi kamata maaskofu wote mapadre wachungaji na wafuasi popote alipopita huyu bwana sweka ndani kwa mahojiano zaidi. Huu ni upuuzi uliokithiri.
 
Takukuru Leo wameamua kumgeuka Edward Lowasa na vibaraka wake katika marudiano ya uchaguzi wa Arumeru. Katika sakata Hilo katibu wa UVCCM wilaya ya Monduli ndugu Ezekiel Mollel ametupwa rumande Mara baada ya kukamatwa na simu yake ilipo pekuliwa na kukutwa na mesej alizokuwa Akiwasiliana na Lowasa kuhusu kuchukua hela kwa askofu na mathius manga kwa Lengo la kwenda kuwahonga wajumbe wa arumeru Mashariki.

Katibu huyo amekiri kupewa maelekezo hayo na Lowasa na kuomba asamehewe kwa kuwa Lowasa ni kiongozi mkubwa yeye asingeweza Kuwa na ujasiri wa kumkatalia. Hadi wakati huu Ezekiel Mollel na Askofu wapo rumande.

Pia katika tukio lingine Fred Lowasa amethibitika kumhonga ticket ya ndege Elirehema kaaya ili amsaidie Sioi aweze kushinda. Kwenye simu ya elirehema Kaaya zimekutwa mesej Kuwa nakulipia ndege pamoja na kukupa lile fungu la kuwapelekea wajumbe. Kwa ushahidi huu hadi sasa elirehema Kaaya yupo rumande.

Wakati wowote mambo haya yatapelekea wahusika kupelekwa mahakamani.

Wana Arumeru mashariki wafanye uchaguzi kwa amani na utulivu na tena wasiwe na hofu yoyote.



Ni hakika Lowassa kaumbuka yeye na mwanawe!!! Itabidi Takukuru iwaunganishe kwenye kesi ya hao waliokamatwa!! Na Sioi aenguliwe kwa kutumia rushwa!!
 
Sawa una sababu zako japokuwa sio uchungu kwa maslahi ya Taifa. Mimi naamini kabisa I can make a Change, wewe mnazi unatazama mpira tu na kushangilia mradi Arsenal wafungwe na ManU..

Nadhani huo mtazamo wako kwangu lakini ipo siku utanielewa.
 
Kwanza mi naombea EL ndio angewekwa lupango. Ila hapo waliowekwa lupango ni watu tofauti..
Sioi na EL wapo wanatanua mtaani, hata hawajahojiwa.


Itabidi Lowassa akirudi toka Ujerumani akamatwe nae aingie Lupango kwa kutoa rushwa akiwa nje ya nchi badala ya kusguhulikia ugojwa unaomsumbua hata kuamua kwenda kutibiwa kimya kimya!!!
 
Kumbeeeeeeeeeeeee!!! huyu bwana anazungikia makanisa kwa kisingizio cha harambeee za ujenzi wa kanisa kumbe anaacha pesa kwa ajili ya rushwa sasa TAKUKURU mpo wapi kamata maaskofu wote mapadre wachungaji na wafuasi popote alipopita huyu bwana sweka ndani kwa mahojiano zaidi. Huu ni upuuzi uliokithiri.
Na wewe acha kupayuka hovyo, sio ukisikia Rais basi ndio ujue ni JK, hata TFF wana Rais wao, hapa Askofu anayeongelewa ni yule Mfanyabiashara ya Tanzanite Mollel na diwani wa Mbuguni.
 
Watu wamechoka hata rushwa yenewe haina dhamani tena hela imeshuka dhamani. Time to give up magamba.
Mpaka 2015 Lowasa atabaki na hela tena kweli? na hizi hela anachota wapi?
Kama aliiba haziishi?

Hili nalo ni swali na linahitaji majibu!
 
Siyoi tayari keshashinda hivyo ktkt vikumbo vya ndani ya ccm EL kanyanyua ndoo japokuwa bado kuthibitishwa na nec.Tunasubiri kuona ladha ya siasa pale EL,Chatanda na Nape watakaposhirikiana jukwaani!
 
Kumbeeeeeeeeeeeee!!! huyu bwana anazungikia makanisa kwa kisingizio cha harambeee za ujenzi wa kanisa kumbe anaacha pesa kwa ajili ya rushwa sasa TAKUKURU mpo wapi kamata maaskofu wote mapadre wachungaji na wafuasi popote alipopita huyu bwana sweka ndani kwa mahojiano zaidi. Huu ni upuuzi uliokithiri.

siyo Askofu wa kanisani mkuu. Ni jina tu la jamaa mmoja maarufu aliwahi pata mijihela mingi ya madini akapanda ghorofani na kurushia watu mijihela kwa watu walio chini.
 
Kumbeeeeeeeeeeeee!!! huyu bwana anazungikia makanisa kwa kisingizio cha harambeee za ujenzi wa kanisa kumbe anaacha pesa kwa ajili ya rushwa sasa TAKUKURU mpo wapi kamata maaskofu wote mapadre wachungaji na wafuasi popote alipopita huyu bwana sweka ndani kwa mahojiano zaidi. Huu ni upuuzi uliokithiri.

Na wewe acha kupayuka hovyo, sio ukisikia Rais basi ndio ujue ni JK, hata TFF wana Rais wao, hapa Askofu anayeongelewa ni yule Mfanyabiashara ya Tanzanite Mollel na diwani wa Mbuguni.

Sasa Matola na wewe unaongelea nini, mie nadhani huyu anamsema EL, labda muulize muelewane maana mmmmhhh. Mbona unapenda kuanzisha sentensi zako na maneno fulani always?
 
Bado Jacob Zuma mpaka kufa kwangu ndio atakuwa Mwalimu wangu wa siasa hizi za majitaka za kiafrika, Lowasa nina kila sababu ya kuamini ndio Jacob Zuma wa Bongo, kinachowatofautisha tu ni kwamba huku kwetu Lowasa wanamuogopa kumpeleka Mahakamani maana wataumbuka wao kama Costa Mahalu anavyowaumbuwa sasa hivi.


Mahalu alidai kuwa katika mazungumzo hayo, Kikwete alimuuliza mama huyo, “Hivi ni kwanini kunakuwa na mikataba miwili? na mama huyo alimjibu kuwa hiyo ni kawaida kwa Italia ukitaka kununua jengo kwa bei nafuu.

Profesa Mahalu aliendelea kudai kuwa baada ya kupewa jibu hilo, Kikwete hakuzungumza tena zaidi ya kucheka na kwamba mwenye jengo alimkumbusha kuhusu malipo ya awali ya Dola za Marekani milioni moja ambapo aliafiki na kuahidi kuwa zingelipwa kabla ya mwisho wa mwaka.

Mzee acha kutapa tapa tuko kwenye vitendo vinavyoashiria rushwa ambavyo vimenaswa na taasisi yetu ya kupambana na rushwa tanzania,taasisi ambayo lowassa akiwa nguvu iliwahi kujaribu kumsafisha alipopata ile "ajali" yake ya kisiasa na ni taasisi hiyo hiyo ndio imewadaka watu ambao baada ya mahojiano jina la lowassa limejitokeza kuwa maarufu miongoni mwa waliohojiwa...

Kuhusu kumfanisha jz na lowassa naona unachanganya mambo,lowassa tunaweza kumfananisha na julius malema ambae juzi kamati kuu cc ya ANC Imemvua uanachama;

Kwa nini lowassa wanafanana kimtindo na Malema?

Ni hivi,Julius Malema na genge lake ndio waliofanikisha JZ kuwa pale alipo,yani rais wa nchi na mwenyekiti/rais wa ANC,kutokana na hilo Malema licha ya umri wake mdogo aliogopwa na kila mtu ndani ya ANC na serikali,Malema akavimba kichwa akajiona mkubwa kuliko chama,mkubwa kuliko rais.Kila mtu ndani ya chama akamlaumu sana JZ kwa kumuendekeza malema.

Baada malema kuhisi zuma anamuogopa akaanza kutishia eti kumng'oa uenyekiti ANC,akaanza kubishana nae na kumkosoa hadharani,zuma akaona huu sasa upuuzi akaamua kupambana nae ka tika mpambano uliomalizika juzi kwa malema kufukuzwa uanachama na cc ya nec.

Nikirudi kwa lowassa huyu na genge lake ndio inasemakena wamemfikisha jk hapo alipo,lakini baadae lowassa akataka awe mkubwa kuliko rais awe mkubwa kuliko mwenyekiti wa chama,yakampata yaliyompata kwanza akaondoka serikalini bila kupenda,baada ya hapo lowassa akataka kuitikisa serikali,akataka kukitikisa chama jk akalaumiwa na kila m2 ndani ya chama kwa kumuendekeza lowassa ikasemekana eti mwenyekiti anamuogopa yeye na genge lake.Lowasa kichwa kikavimba akaanza kufikiria kumuondoa mwenyekiti madarakani kama malema alivyojaribu kufikiria kwa zuma,mwenyekiti akaona huu u.p.u.u.z.i. huyu mtu nambeba kwa mbeleko ya chuma ananiona mimi m.ji.n.g.a. sio???akaanzisha msamiati kwa kujivua gamba...kwanza yakafanyika mabadiliko makubwa kwenye sekretariet yalimzoa mzee makamba na timu yake wakaingia kina nape,kama hiyo haitoshi Lowassa akangolewa cc na sasa saula lake la kuvuliwa gamba liko ndani ya cc ambamo yeye hayumo,ikumbukwe ni cc ya ANC ndiyo iliyomvua gamba Juliua Malema mtu amabae ndio anafanana fanana na lowassa katika style yao ya kufanya siasa.

J e cc itamfanya nini lowasa??tusubiri tuone wakati huo huo lowassa anatakiwa kupima kati ya ubunge na u nec kipi kinamfaa ili aachia kimojawapo....
 
Nadhani huo mtazamo wako kwangu lakini ipo siku utanielewa.
Mkuu nayajua mengi yaliyozungumzwa kuhusu Chadema na najua hata habari za kina JK kutaka kuhamia Chadema na kilichofuatia lakini ndio siasa. Elewa tu kwamba mimi mutoto wa mujini nayajua mengi sana isipokuwa siwezi kuwa mnafiki hilo pekee ndilo lililonishinda na kwa siasa za Bongo mtu kama mimi sifai wala sitaki.. Isipokuwa nina hakika naweza kabisa kutoa mchango mkubwa kwa jamii ya Kitanzania kupitia Chadema kwa sababu ni wasikivu kuliko vyama vingine na wepesi kujivua gamba lakini sii CCM wala CUF hawa wanauhalisia wa magamba ya Udini, Ufisadi na Umimi.
 
hapa patamu kama ni kweli waliotoa fedha na wao wawekwenda ndani na TAKUKURU ndipo tutaona haki inatendeka
 
Haukujibu swali langu KK! Haya unayoyaeleza hapa hayajampunguzia nguvu Lowasa. Na mengine yamemfanya kuwa na nguvu zaidi. Narudia swali langu: Kwa nini kura za maoni CCM kule AruMeru zinarudiwa?

kwa hiyo hiyo ndio nguvu pekee ya lowassa aliyonayo au?hivi ni mara ya kwanza kwa uchaguzi wa ndani ya ccm kurudiwa au matokeo ya mteule kutenguliwa?vipi issue ya bashe wa lowassa na kigwangala napo palikua na guvu za lowassa au?
 
Mzee acha kutapa tapa tuko kwenye vitendo vinavyoashiria rushwa ambavyo vimenaswa na taasisi yetu ya kupambana na rushwa tanzania,taasisi ambayo lowassa akiwa nguvu iliwahi kujaribu kumsafisha alipopata ile "ajali" yake ya kisiasa na ni taasisi hiyo hiyo ndio imewadaka watu ambao baada ya mahojiano jina la lowassa limejitokeza kuwa maarufu miongoni mwa waliohojiwa...

Kuhusu kumfanisha jz na lowassa naona unachanganya mambo,lowassa tunaweza kumfananisha na julius malema ambae juzi kamati kuu cc ya ANC Imemvua uanachama;

Kwa nini lowassa wanafanana kimtindo na Malema?

Ni hivi,Julius Malema na genge lake ndio waliofanikisha JZ kuwa pale alipo,yani rais wa nchi na mwenyekiti/rais wa ANC,kutokana na hilo Malema licha ya umri wake mdogo aliogopwa na kila mtu ndani ya ANC na serikali,Malema akavimba kichwa akajiona mkubwa kuliko chama,mkubwa kuliko rais.Kila mtu ndani ya chama akamlaumu sana JZ kwa kumuendekeza malema.

Baada malema kuhisi zuma anamuogopa akaanza kutishia eti kumng'oa uenyekiti ANC,akaanza kubishana nae na kumkosoa hadharani,zuma akaona huu sasa upuuzi akaamua kupambana nae ka tika mpambano uliomalizika juzi kwa malema kufukuzwa uanachama na cc ya nec.

Nikirudi kwa lowassa huyu na genge lake ndio inasemakena wamemfikisha jk hapo alipo,lakini baadae lowassa akataka awe mkubwa kuliko rais awe mkubwa kuliko mwenyekiti wa chama,yakampata yaliyompata kwanza akaondoka serikalini bila kupenda,baada ya hapo lowassa akataka kuitikisa serikali,akataka kukitikisa chama jk akalaumiwa na kila m2 ndani ya chama kwa kumuendekeza lowassa ikasemekana eti mwenyekiti anamuogopa yeye na genge lake.Lowasa kichwa kikavimba akaanza kufikiria kumuondoa mwenyekiti madarakani kama malema alivyojaribu kufikiria kwa zuma,mwenyekiti akaona huu u.p.u.u.z.i. huyu mtu nambeba kwa mbeleko ya chuma ananiona mimi m.ji.n.g.a. sio???akaanzisha msamiati kwa kujivua gamba...kwanza yakafanyika mabadiliko makubwa kwenye sekretariet yalimzoa mzee makamba na timu yake wakaingia kina nape,kama hiyo haitoshi Lowassa akangolewa cc na sasa saula lake la kuvuliwa gamba liko ndani ya cc ambamo yeye hayumo,ikumbukwe ni cc ya ANC ndiyo iliyomvua gamba Juliua Malema mtu amabae ndio anafanana fanana na lowassa katika style yao ya kufanya siasa.

J e cc itamfanya nini lowasa??tusubiri tuone wakati huo huo lowassa anatakiwa kupima kati ya ubunge na u nec kipi kinamfaa ili aachia kimojawapo....

Maandishi kibao pumba tupu!!
 
Sasa Matola na wewe unaongelea nini, mie nadhani huyu anamsema EL, labda muulize muelewane maana mmmmhhh. Mbona unapenda kuanzisha sentensi zako na maneno fulani always?
Wewe ndio hujui hata ulichokiandika, nakushauri next time jipe muda wa kusoma kwanza kabla ya kucomment, nilichomjibu mimi huyo ni kwamba yeye anasema Lowasa amewapa pesa maaskofu wa kanisa wakati ukweli ni kwamba Askofu aliekamatwa sio Askofu wa kanisa bali hiyo ni Nick name yake tu. ni nini usichoelewa hapa!!??
 
Askofu anayezungumziwa ni mmasai mmoja semi illetarate ambaye alilala maskini na kuamka tajiri pale alipopata jiwe la Tanzanite la thamani ya mabillioni wakati hakuwa hata na laki mfukoni,kuanzia hapo alianza viroja vingi ,alinunua hotel isyo na parking pale Arusha kama sikosei inaitwa Parson,pia alikuwa supporter mkubwa wa Lyatonga wakati anagombea uraisi kitu kilichomkosanisha na TRA na nusura wamfilisi na tokea hapo alipotea kabisa na ndio sasa anaanza kusikika tena.

anachafua vyeo vya wenzake nilishaamini ni askofu wa kanisa.
 
Mkuu nayajua mengi yaliyozungumzwa kuhusu Chadema na najua hata habari za kina JK kutaka kuhamia Chadema na kilichofuatia lakini ndio siasa. Elewa tu kwamba mimi mutoto wa mujini nayajua mengi sana isipokuwa siwezi kuwa mnafiki hilo pekee ndilo lililonishinda na kwa siasa za Bongo mtu kama mimi sifai wala sitaki.. Isipokuwa nina hakika naweza kabisa kutoa mchango mkubwa kwa jamii ya Kitanzania kupitia Chadema kwa sababu ni wasikivu kuliko vyama vingine na wepesi kujivua gamba lakini sii CCM wala CUF hawa wanauhalisia wa magamba ya Udini, Ufisadi na Umimi.

Mkuu Mkandara,
Nimecheka sana na hii post yako ya mutoto wa mujini.

Basi tumekutana sote matoto ya mujini..naheshimu misimamo yako na vitu vingi tunakubaliana tuombe uzima tutakumbushana huko mbeleni.

Tupo pamoja sana mkuu wangu lakini kumbuka kwenda kuwasalimia ukara( Nansio).
 
Mkuu Mkandara,
Nimecheka sana na hii post yako ya mutoto wa mujini.

Basi tumekutana sote matoto ya mujini..naheshimu misimamo yako na vitu vingi tunakubaliana tuombe uzima tutakumbushana huko mbeleni.

Tupo pamoja sana mkuu wangu lakini kumbuka kwenda kuwasalimia ukara( Nansio).
Dar Ukara na Nansio ni sawa na kusema Unguja na Pemba...lakini yote powa! nitakuja kabla ya mwaka huu kwisha acha Ukara nategemea kwenda Kisolya, Kitengule, Kibara, Namibu, Kagunguli, Buramba hadi Majita yaani safari ni ndefu...
 
Back
Top Bottom