EAC Chief warns Tanzania on regional Integration

EAC Chief warns Tanzania on regional Integration

Mkuu JokaKuu
Dr sezibera amekwenda kuongea mambo ya EAC katika mkutano binafsi Kenya ili kutoa nafasi ya vyombo vya habari kueleza nafasi ya nchi yake na Kenya dhidi ya Tanzania.Kama mtendaji mkuu wa EAC alipaswa kutoa kauli siku yoyote na si kwenye mikutano binafsi.

Dr Sezibera ameshindwa kuongelea mwendo wa EAC na matatizo yanayojitokeza. Kwanza lazima afahamu makubaliano ya soko la pamoja yalikuwa na hatua zinazopaswa kufuatwa.
Suala la ardhi ambalo limemuudhi kama Mnyarwanda na kibaraka wa Kenya, hayamo katika makubaliano ya EAC

Ilikubaliwa kuwa kila nchi iwe na utaratibu wake wa ardhi, hakuna mambo ya faster ameshindwa kuona facts.
Sezibera anaongoza na fikra za Kagame. Makatibu wengine walikuwa wanadiplomasia na jumuiya ilikwenda mbele.
Tangu Sezibera apewe ukanda EAC imezidi kuwa hovyo kwasababu ya kuongozwa na PK na kuwa kibaraka wa Kenya.

Kibaraka SEzibera aelewe Tanzania ndiyo nchi pekee iliyokuwa mstari wa mbele kuanzisha EA Federation na EAC iliyokufa na ya sasa. Tuna uzoefu wa kufanya mambo na tuna uzoefu wa matatizo yaliyotokea 1977.Rwanda alikotoka hawana uzoefu wa ''muungano'' hata wa Watusi na Wahutu, hawezi kufundisha asicho na ujuzi nacho.

Kuhusu ushindani, inategemea mtu anatafsiri gani ya ushindani i.
Ukabila kama wa Waluo na Wakaikuyu ni competetion. Wahutu na Watusi ni competition pia.Museveni na Koni ni competition.
Kwahiyo Tanzania inaweza kuogopa ushindani huo na sijui kama ni kosa.

Marekani taifa kubwa linalaumiwa katika NAFTA katika mambo ya ajira na uwekezaji.
Marekani inalinda masilahi yake kwa vile ndani ya NAFTA itapoteza zaidi kuliko kupata.
Nchi nyingine wanataka milango ifunguliwe ili waifadike. Vipi Tanzania ionekane inafanya makosa kuchukua hadhari.

Kwa wale waliokuwa hawapo au wadogo,miaka 25 hakuna ambaye angesema Tanzania inaweza kuwa second economy na tishio kwa first economy EAC. Leo hali ni tofauti sana.
Muhimu si kukimbia bali kukimbia kwa tahadhari hasa kuangalia interest za wenzetu ni nini.

Nakubaliana na JokaKuu kwamba mapungufu yaliyopo yafanyiwe kazi lakini siyo sababu kwanini Tanzania inachukua hadhari.

Fikiria kuwa EAC ya mataifa matatu wakikaa pamoja hawaongelei ardhi, Tanzania ikiwemo suala la ardhi linachukua nafasi.
Kwanza lilipokataliwa wakaja na njia ya vitambulisho ambayo ni mlango wa uani.
Kenya na Uganda walikaribia kupigana kwasababu ya KM 1, leo wapo mbele kusema tunaogopa ushindani.Upi huo? Je kugombania migingo ya KM1 siyo ushindani?

Hizi ni mbinu za kufunika hoja yao kubwa ya ardhi hakuna jingine.
Kama Tanzania ingekuwa inaogopa EAC Kenya isingekuwa mwekezaji namba 2 Tanzania.
Milango itafunguliwa kwa taratibu na sheria, siyo kutanguliza watu 20,000 halafu iletwe hoja ya soko la pamoja n.k.
 
Last edited by a moderator:
..Tanzania pia si tumetekeleza yote isipokuwa ardhi?

Nakubaliana na hoja mia kwa mia ndio maana juzi tume tekeleza operesheni kibunga kwa mafanikio makubwa. Kwa unafiki hatujambo.

Operesheni Kimbunga ni operesheni ya kuwatimua wahamiaji HARAMU waliokuwa wakiishi Tanzania kinyume cha sheria, sasa kama kwa kufanya hivi unamaanisha ni unafikia na kukiuka makubaliano ya EAC, tunaomba tutajie ni makubaliano yepi na yameandikwa wapi yanayoruhusu nchi za EAC kuishi na wahamiaji HARAMU?
 
Ruzibiza,

..mkataba wa EAC unaeleza kwamba masuala ya ARDHI na free movement yataamuliwa kulingana na sheria za nchi wanachama.

..Tanzania haijakiuka mkataba wa EAC kwa kuendelea kusisitiza kwamba ardhi yake siyo suala la EAC. Dr.Sezibera anaelewa hilo lakini ameamua kupotosha hao waandishi wa habari.

..Kwa mwana EAC anayehitaji ardhi hapa Tanzania anapaswa kuwasilisha maombi kwa kuzingatia sheria zetu za uwekezaji. Mahali pazuri pa kuanzia ni Tanzania Investment Center[TIC].

..Kwa upande wangu naamini utaratibu huo ni mzuri. Tunachohitaji huku Tanzania ni wawekezaji wakubwa-wakubwa na siyo wakulima wachumia tumbo, au wafugaji wanaohama-hama.

..Kama kuna wa-Tz mafisadi ambao wanahodhi ardhi kubwa bila kuitumia basi hayo ni mapungufu ktk utekelezaji wa sheria zetu za ardhi. U do not solve that problem kwa kufungua milango kwa squatters toka Kenya, Rwanda, au Burundi.


wapi mtoa mada kasema Dr. Sezibera anataka ardhi unajua idad ya protocol za eac?mbona unakomaa na hilo la ardhi?hilo linaeleweka...what doest it mean by common market?kama tz ilijua haijawa tayari nani aliwalazimisha kuingia eac?who negotiated hiyo mikataba?kwanini katka implementation ionekane nongwa?eac agreement inawapa watu uhuru wa kutosha na ndo maana sioni sababu ya tz kusononeka inapotengwa katika baadhi ya mambo....tz haiwezi pace ya eac so uamzi wa kujitoa utawafaa coz hata watakapo baki hawana uwezo wa kuigeuza jumuiya fursa.....badala yake wanaiona tishio.....faida ya eac haiwezi onekana hadi pale watakapopatikana watu wenye uwezo wa kugeuza kinachoonekana tatizo into fursa...
 
Acha kwasemea watz, wakati ww si miongoni mwao...,sema straight tujue ww ni wa wapi. Lkn ukijichanganya tunashindwa kuelewa aidha ni mtz unatetea ujinga wa wanyarwanda na Mseng...ebera wao au mnyarwanda.

......failures wote huwa kama wewe...badala ya kuconcentrate kwenye argument zangu unaanza kutafuta uraia wangu...mwenye akili hupingana na hoja na si mtoa hoja....ukweli hauna uraia
 
Salaam sana mkuu, baada ya salaam ningependa kujua ni kwa nini michango yako mingi humu jamvini inatawaliwa mara nyingi na lugha za jazba na mara chachae matusi. Cha msingi ni kukubali kutofautiana kwa kutumia nguvu ya hoja na wala isiwe hoja ya nguvu. Ushauri wangu ''just try to control your emotions and feelings and that will justify how civilised, cultured and refined you are''.

"my wife is a fool, so i know how to deal with fools"....did i make my point clear?
 
Salute mkuu. Umeongea vizuri!

Mkuu JokaKuu
Dr sezibera amekwenda kuongea mambo ya EAC katika mkutano binafsi Kenya ili kutoa nafasi ya vyombo vya habari kueleza nafasi ya nchi yake na Kenya dhidi ya Tanzania.Kama mtendaji mkuu wa EAC alipaswa kutoa kauli siku yoyote na si kwenye mikutano binafsi.

Dr Sezibera ameshindwa kuongelea mwendo wa EAC na matatizo yanayojitokeza. Kwanza lazima afahamu makubaliano ya soko la pamoja yalikuwa na hatua zinazopaswa kufuatwa.
Suala la ardhi ambalo limemuudhi kama Mnyarwanda na kibaraka wa Kenya, hayamo katika makubaliano ya EAC

Ilikubaliwa kuwa kila nchi iwe na utaratibu wake wa ardhi, hakuna mambo ya faster ameshindwa kuona facts.
Sezibera anaongoza na fikra za Kagame. Makatibu wengine walikuwa wanadiplomasia na jumuiya ilikwenda mbele.
Tangu Sezibera apewe ukanda EAC imezidi kuwa hovyo kwasababu ya kuongozwa na PK na kuwa kibaraka wa Kenya.

Kibaraka SEzibera aelewe Tanzania ndiyo nchi pekee iliyokuwa mstari wa mbele kuanzisha EA Federation na EAC iliyokufa na ya sasa. Tuna uzoefu wa kufanya mambo na tuna uzoefu wa matatizo yaliyotokea 1977.Rwanda alikotoka hawana uzoefu wa ''muungano'' hata wa Watusi na Wahutu, hawezi kufundisha asicho na ujuzi nacho.

Kuhusu ushindani, inategemea mtu anatafsiri gani ya ushindani i.
Ukabila kama wa Waluo na Wakaikuyu ni competetion. Wahutu na Watusi ni competition pia.Museveni na Koni ni competition.
Kwahiyo Tanzania inaweza kuogopa ushindani huo na sijui kama ni kosa.

Marekani taifa kubwa linalaumiwa katika NAFTA katika mambo ya ajira na uwekezaji.
Marekani inalinda masilahi yake kwa vile ndani ya NAFTA itapoteza zaidi kuliko kupata.
Nchi nyingine wanataka milango ifunguliwe ili waifadike. Vipi Tanzania ionekane inafanya makosa kuchukua hadhari.

Kwa wale waliokuwa hawapo au wadogo,miaka 25 hakuna ambaye angesema Tanzania inaweza kuwa second economy na tishio kwa first economy EAC. Leo hali ni tofauti sana.
Muhimu si kukimbia bali kukimbia kwa tahadhari hasa kuangalia interest za wenzetu ni nini.

Nakubaliana na JokaKuu kwamba mapungufu yaliyopo yafanyiwe kazi lakini siyo sababu kwanini Tanzania inachukua hadhari.

Fikiria kuwa EAC ya mataifa matatu wakikaa pamoja hawaongelei ardhi, Tanzania ikiwemo suala la ardhi linachukua nafasi.
Kwanza lilipokataliwa wakaja na njia ya vitambulisho ambayo ni mlango wa uani.
Kenya na Uganda walikaribia kupigana kwasababu ya KM 1, leo wapo mbele kusema tunaogopa ushindani.Upi huo? Je kugombania migingo ya KM1 siyo ushindani?

Hizi ni mbinu za kufunika hoja yao kubwa ya ardhi hakuna jingine.
Kama Tanzania ingekuwa inaogopa EAC Kenya isingekuwa mwekezaji namba 2 Tanzania.
Milango itafunguliwa kwa taratibu na sheria, siyo kutanguliza watu 20,000 halafu iletwe hoja ya soko la pamoja n.k.
 
Last edited by a moderator:
Heshima sana wanajamvi,

Dr Sezibera ni nani ?.

Dr Sezibera ni Mnyarwanda (Mtutsi) na ni daktari wa binadamu aliyosomea chuo kikuu cha Makerere Uganda na baadae akachukua shahada ya uzamili (Master of Arts) chuo kikuu cha Georgetown Marekani.

Amewahi kufanyakazi ya udaktari Mbuyu Hosipital na Mbale Hospital zote za nchini Uganda kabla hajajiunga na kikundi cha kigaidi RPF akihudumu kama daktari wa jeshi kwa muda mrefu hadi akafikia ngazi ya Major.Mwaka 1994 Dr Sezibera aliteuliwa kama daktari wa Rais Kagame kabla hajateuliwa nafasi ya ubalozi na baadae waziri wa afya.

Dr Sezibera ni mwanajeshi mtiifu wa (kundi la RPF ambao ajenda yao kubwa ni kuhakikisha kabila la watutsi linatawala Rwanda na Uganda na hatimaye waitawale EA yote.Dr Sezibera ni kikaragosi cha Dictator Kagame yuko Arusha kukamilisha kazi haramu ya kuhalalisha utawala wa kitutsi EA baada ya kufanikiwa kukandamiza kabila la wahutu walio wengi Rwanda.

ningekutukana kama hii post ingekuja miaka 14 iliyopita,ila kwa sasa sina cha kufanya zaidi ya ku- scroll down!
have a nice weekend though
 
....
......ana uwezo wa kutuhumu na hata kushitaki mahamani nchi yoyote mwanajumuiya wa EAC pale anapoona haifuati utaratibu
.......
Ni kifungu gani hicho kinachompa mamlaka Katibu Mkuu kwenda kwenye media au forums au makongamano na kutuhumu? By the way, Seziraba wako amevunja mkataba wa Jumuiya kwa kukubali/kupewa "majukumu" kutoka kwa baadhi ya Nchi wanachama (refer Tripartite KKK) bila kupitia kwenye Baraza la Mawaziri la Jumuiya (Refer. Article 72 (2) of EAC Treaty). Katibu Mkuu anaweza kuishtaki kuipeleka nchi mwanachama mahakamni sawa, ikiwa ni hatua ya tatu kabala ya kufanya hivyo, lakini wapi alipopewa uwezo wa kwenda kuituhumu nchi kwenye makongamano? Acheni ujinga wenu, Tanzania anafanya yaliyopo kwenye mkataba nyie mnataka mfanye mnaopigiana simu, Jumuiya haiwezi kuongozwa kwa kupigiana simu. period
 
Commitment ya Tanzania ni kwa watu wa Tanzania na sio kwa EAC.

EAC is just a social community, haipaswi kutuumiza kichwa...
 
jina lako tu limekaa kinyarwanda najua wewe na sezbera wote ni watumwa wa kagame na tanzania tulikosea sana kuruhusu nchi kama rwanda ambazo bado zipo vitan rejea m23 ni kikosi cha kagame cha kuwaua wakongo ili apanue nchi ndogo ya rwanda na kuipata kivu ya kusini na kaskazini hima empire,,,mwambie kagame tunajua bila tanzania hakuna east afrca community so hamuwez kutulazmisha ndoa isiyo na maslahi kwetu wote kenya,rwanda, na uganda hamna ardhi na resource sasa mtagawana nini tanzania si shamba la bibi

umekosea tena sana nitake radhi!
 
Wee kichefuchefu sisi Watanzania tulikuwepo EAC kabla ya Rwanda na Burundi. Kulikuwa shwari; mbona mnaleta hoja ya vioja wakati nyinyi wachache mnataka EAC kwa nguvu.

Kwa kweli watawala wa sasa wa Tanzania wasipoangali hili suala litachukua maisha ya mtu. Walionywa hawkusikia, sasa wanatendwa wamenyamaza. Tanzania was there before EAC. It decided postpone its independence to accommodate the community. Sasa wanaharamu, wauaji wabaguzi wa kikabila wako madarakani wanataka kumuamrisha kila mtu. Ujinga na upuuzi huu uishie huko huko.

NI WAKATI MUAFAKA KUWAACHIA EAC YAO. Waondoke wakatengeneze jumuiya yao.

mimi siyo kichefu chefu labda we utakuwa mjamzito....nitake radhi mimi na nani unatutuhumu?
 
Mkuu mngejiuliza nyie kwanza mbona hamna MELI wala TRAIN?. Halafu unauliza ndege kwa mwenzio! Ha ha ha!

Sina ugomvi na watanzania. Nampasha huyu f.a.l.a ambae hajui akiongeacho anabwabwaja tu. Na kutokuwa na ndege sio tusi bali ni ukweli halisi. Hivi nikuulize kwa nini na utajiri wenu wote huo mnaojivunia hamna ndege? Naomba unijibu.
 
Alichosema Dr Sezibera ni kwamba:

Tanzania has faltered on a number of key issues agreed upon by EAC regional States including the liberation of its current accounts and waiving of work permit fees.

Tukianza na suala la liberalization of current account - makubaliano ni kwamba barriers & restrictions zote on the movement, sale, investment & payments of capital inatakiwa viondolewe; Vile vile kuna makubaliano ‘to remove all discrimination based on the nationality or on the place of residence of the persons or on the place where the capital is invested.’ Ni kweli kwamba wenzetu Kenya, Uganda na Rwanda wameshafungulia haya, imebakia Tanzania na Burundi; Lakini pamoja na hayo, makubaliano ilikuwa kwamba Tanzania na Burundi wawe wametekeleza haya katika kipindi cha 2010 – 2015, kwahiyo tusubri tuone nini kitajiri ndani ya miaka miwili ijayo;

Tukija kwenye suala la work permit fees – makubaliano ni kwamba workers kutoka any partner state waruhusiwe kutafuta kazi katika nchi yoyote mwanachama wa EAC; Free movement of labour ni kwenye professions Fulani Fulani, sio professions zote, na professions hizi zipo listed wazi;

That said and done, lazima tuambiane ukweli kwamba pamoja na kwamba Tanzania ilikuwa mstari wa mbele baada ya uhuru kutafuta regional integration, katika kipindi cha hivi karibuni, tumejionyesha kuwa “shy partners’; kwa kweli hatujiamini, hivyo kufanya tusiwe na imani sana na EAC; Kuna vituko kadhaa tumevifanya in the past two years kuashiria kwamba hatuna genuine commitment – mfano kufunga mpaka wetu na Kenya Taveta (2012), kuzuia kuvusha mazao/nafaka kwenda nchi jirani(2011), kupingana na political federation and mutual defense pact (2011), na mahakama kuu Tanzania kuikingia kifua kampuni ya kitanzania (blueline) iliyofisadi na kukaribia kuifilisi east african development bank (EADB);;

Mbali ya haya, pengine hali yetu ya kusua sua pia inachangiwa Zaidi na hoja ifuatayo aliyotoa Waziri Mwakyembe mwaka jana wakati wa uchaguzi wa wabunge wa Tanzania to the EAC (Dodoma) ambapo alisema:

We should not hide from the fact that Tanzania’s status in EAC has taken a hit in recent years because we have been sending incompetent people to represent us,” says Dr. Harrison Mwakyembe

Maswali yanayofuatia ni je, ipi ni tafsiri sahihi kati ya hizi:


  • Kusua sua kwetu kunatokana na ukweli kwamba suala la EAC integration tulikuwa tunaliendesha kisiasa Zaidi na sasa uchumi unapoanza kupewa prominence na kuanza kupambanishwa na wenzetu (hasa Kenya), tunagundua jinsi gani hatujajiandaa – both on the micro/household level, na pia macro – level, structure of the economy and how it affects the balance of trade kati yetu na wakenya?
  • Ni woga wetu to share rasilimali na ardhi ambazo ni nyingi sana kuliko wenzetu?
  • Ni ignorance juu ya compromise zinazokuja na regional integration?

Pengine kuna justification katika suala la ardhi, kwani makala moja inatusema kwamba:

Tanzania’s objections to both land purchases… also raised fears over its government’s commitment to the regional integration efforts.

Tanzania accounts for about 52% of East Africa’s total land area, na ingawa we have the largest population in the region, bado there is is significant land available. Suala hili is both a THREAT and an OPPORTUNITY kwetu sisi katika muktadha wa EAC, na ukweli utaendelea kubakia hivyo;

Mwisho ni suala la passport – uraia – hapa pia tuna sua sua linapokuja suala la common passport tofauti na wenzetu; Katika hili, given given ukweli kwamba almost 33% ya population ya EAC region ipo Tanzania, tunahitaji kuwa waangalifu sana hasa ikizingatiwa kwamba wenzetu wanasukumwa Zaidi na population pressure & shortage of land kuliko chochote – kwa mfano population density Tanzania ipo chini sana ikilinganishwa na Burundi, Rwanda, Kenya na Uganda; we have 47 people per square Kms, the lowest in the regions, huku Uganda na Kenya wakiwa juu Zaidi, na Rwanda na Burundu wakiongoza, 430 & 301, respectively;

Inawezekana sijapanga hoja katika mtiririko mzuri, lakini mniwie radhi, ilikuwa ni suala la haraka haraka tu katika kuchangia hoja; Nitarudi kwa hoja Zaidi……


nakala JokaKuu, Nguruvi3
 
Last edited by a moderator:
Ruzibiza,


wapi mtoa mada kasema Dr. Sezibera anataka ardhi unajua idad ya protocol za eac?mbona unakomaa na hilo la ardhi?hilo linaeleweka...what doest it mean by common market?kama tz ilijua haijawa tayari nani aliwalazimisha kuingia eac?who negotiated hiyo mikataba?kwanini katka implementation ionekane nongwa?eac agreement inawapa watu uhuru wa kutosha na ndo maana sioni sababu ya tz kusononeka inapotengwa katika baadhi ya mambo....tz haiwezi pace ya eac so uamzi wa kujitoa utawafaa coz hata watakapo baki hawana uwezo wa kuigeuza jumuiya fursa.....badala yake wanaiona tishio.....faida ya eac haiwezi onekana hadi pale watakapopatikana watu wenye uwezo wa kugeuza kinachoonekana tatizo into fursa...

Tatizo lenu ndilo hilo, mnajifanya ni wajuaji kumbe hamjui lolote. Ni kujua kwenu huko ndiko kunakoyumbisha Jumuiya.

Haya tutajie hizo idadi za protocol za eac unazozijua.

Unatuuliza maana ya Common Market? Common Market imewekwa kwenye Mkataba tokea 1999, wewe Rwanda umeingia kwenye Jumuiya 2007, hivi wewe uwe unajua zaidi Common Market kuliko sisi tulioiweka? Ni nani aliyekwambia Common Market means Single Market?

Sawa, Tanzania ni signatory wa Common Market, ni wapi au kifungu gani kutoka kwenye Common Market ambacho Tanzania haijatekeleza na nyie rwanda mmetekeleza? Sidhani kama umeisoma au unaijua hiyo protocol, kama ungeisoma na kuielewa ungejua kwamba Tanzania ndiye anayeiokoa eac.

Tanzania haitojitoa eac kwa ajili yako wewe, kama itajitoa ni kwasababu nyingine kabisa na wala haina wazo hilo.

Kwanza ujue ya kwamba Sezibera wako amekiuka Mkataba wa Jumuiya hivyo tukiamua tunampiga na chini kwasababu EAC haiendeshwi kwa kura,bali by consensus, so hata wazo la nchi moja linatosha kujengea hoja.

Kwenye mambo ya EAC wewe bora ukae kimya, kwasababu hujajadili hivyo huwezi kujua kifungu kadhaa Tanzania, Kenya na Uganda walibishana vipi kabla ya kufikia kukubaliana na kuandika, hilo ni jambo muhimu sana kwenye ustawi wa RTAs.
 
Huyu Seziraba mbona anafanana sana na mkuu wetu flani wa Makamanda!? Hebu jaribuni kumuangalia kwa umakini paji lake la uso na hasa macho yake, then conect dots. Isije ikawa ndo chimbuko kuu la kiburi cha mh. PK.... anyway just hisia tu wakuu, ila jamaa nimekuwa na mashaka nae toka akiwa Manyota wa Jiwe la Kujenga Tafuo.
 
Wewe hapo ulipo Una ardhi wapi, hauna hata robo eka na huenda unaishi kwenye Mbavu za Mbwa Tandale kwa Tumbo lakini unajifanya msemaji wa ardhi za wengine. Hapo ndio ujinga Wako ulipokufikisha. To be the best you have to beat the best, nyie majinga mnaogopa tusipambane na wana afrika mashariki wenzetu. Mimi mwerevu naangalia solo la Kenya, Soko la Uganda na Rwanda huku Tanzania ndio nchi yenye rasilimali zaidi, tutauza wapi bidhaa zetu? Fikiria nje ya box wewe Kula kulala

Well said brother, but punguzeni matusi.. we need integration but on fair grounds. i think tungeanza na biashara kwanza.. then taratibu kwenye mambo mengine
 
Back
Top Bottom