EAC Chief warns Tanzania on regional Integration

EAC Chief warns Tanzania on regional Integration

Tutauza wapi bidhaa??
Kama hawezi fikiria kwamba soko la bidhaa za tz sio lazima ziwe nchi za EAC pekee...basi wewe bado unafikiri ndani ya box na utuondolee utumbo wako hapa

Kwa taarifa yako wewe uliye ndani ya box ni kuwa uwezo wetu sisi wa uzalishaji kwa teknolojia duni sehemu nzuri kuuza ni nchi ambazo hazijaendelea sana kama Kenya, Uganda, Rwanda, Congo na nyinginezo za jirani. Kutengeneza bidhaa Tanzania ikaingia kwenye soko la Marekani si kazi ndogo. Tunatakiwa kujikita kwenye soko la nchi za hapa hapa jirani. Nchi yetu iko strategic kutumia soko la afrika mashariki na kati na Kenya ndio nchi yenye fursa nyingi.

Tatizo walimu wenu walikuwa wanawafundisha kujibu mitihani tu, hamuendi kujisomea pembeni na sasa dunia ina integrate nyie mmekuwa waoga kwa kuwa hamuwezi kushindana na watu wengine kwenye interview. Bakieni na uoga wenu, mbakie na umaskini wenu
 
Lazima tukubali kuwa intergration ya EAC imeingia doa siku Rwanda ilipoingia EAC, Rwanda wanakuwa na sinister move in conjunction na waganda, muda wote manashiriki kudistabilize Eastern Congo, na sasa wamemuingiza Rais asiye na ujuzi Kenyatta. Tanzania lazima tupige vita hii kwa nguvu zote, hatuwezi kuwa na mpaka mrefu na Congo ambayo haiko stable kama nchi. Kama EAC haiwezi kuona hivyo (kumbuka Balozi Sezibera ni mnyarwanda), basi heri ife tuu. Usalama wa nchi yetu ni paramount kuliko EAC intergration. I hope President Kenyatta amejifunza after the Wesgate Mall issue, (you need a stable naighbour, to have a stable society) , hawa mashetani wawili lazima wapigwe vita kwa nguvu zote, kwanza hawana democratic societies, mliwaruhusu vipi kushirikiana na sisi, wao waunge ushirikiano wao, kagame, museveni, al -bashir na al shabaab, wote hawana tofauti
 
Ni kweli bongo kuna ambayo wanaleta uzito, kama mtatazama Doing Business Roadmap - Trading Across Boarders kuna ambayo wala hayahitaji msuli kutekeleza lakini wabongo wanambwela bila sababu za msingi. Kwa mfano kuondoa barriers barabarani yaani ndio kwanza walizoondoa wanazirudisha tena kwa mfano VISIGA wamerudisha tena, Hivi barriers za polisi zinaongeza tija gani na kama sio vituo vya kupokea rushwa. One stop boarder post na urasimu usio wa maana wa kutoa mizigo bandarini. Mizani isiyokuwa na ufanisi zaidi ya kuumiza wafanya biashara na wasafirishaji kutokana na kukaa katika misururu mirefu na duplication kupima katika kila mzani. Mfano gari linauzwa USD 2000 CIF lakini kulitoa itagharimu USD 4000 tena kwa mbinde. Utamaduni wa mteja bongo kuwa ---- tu na viongozi ndio wafalme. Mkiambiwa mnaanza kutengeneza zengwe la kumtoa mtu ili muendelee kusifiwa.

Kuruhusu pasi za kusafiria kunapunguza nini? kama mkiruhusu wageni kuja kwa utaratibu mzuri kuna ubaya gani? Ardhi ndio wabongo wanatumia kama kigezo cha kusuasua lakini kuna mgeni gani kataka kununua ardhi na mbona wenyewe mnauza kiboya zaidi. Lazima tukubali viongozi wetu wazito katika kufanya maamuzi na hawana business mindset na warasimu wa kutupwa. Kama hakuna dili kwao wanambwela sana lakini kama wanavuta mpunga fasta.
 
Sikubaliani hata kidogo na ugawaji wa ardhi yetu.Hapa tulipo tuna matatizo lundo ya kuletewa the so called wawekezaji ambao wamefanya watanzania wakawauda kunyang'anywa ardhi na kupewa wageni.Hebu fikiria Wakenya,Warundi,wanyarwanda,waganda waje waingie waanze kupewa ardhi hivi mwananchi wa kawaida ataweza kumudu?Tusikimbilie kwenye moto,mpaka sasa sijaona umuhimu wa hiyo EAC.Hapa tulipo ajira za vijana ni mshikemshike na kwa sasa waajiri wengi wanaajiri wageni na kuwaacha wazawa kwa kigezo cha Lugha.Kwa sasa bado watanzania hawako tayari tunakokimbilia kuna nini?Tuna tatizo la Muungano bado haujatatuliwa tunataka kuingia kwenye maafa mengine?Hakuna jipya EAC zaidi ya ARDHI.Watanzania tuseme HAPANA kwenye masuala ya ardhi yetu.Pamoja na kuwa na ombwe la uongozi lakini bado raslimali ardhi isiwe ndani ya EAC.

Nadhani wakati umefika kwa waziri Sitta kuanza kutoa elimu kwa watanzania kuhusu Jumuia ya Afrika mashariki, naona wengi hamuelewi hii kitu ni nini?? Sasa Mnyarwanda atapewaje Ardhi ya Tanzania?? Ebu jaribu wewe nenda kijiji cha Budalabujinga halafu kawaambie WAKUPE ARDHI kama inawezekana. There is nothing like kugawana ardhi kwenye muungano wa afrika mashariki. Mmekuwa waoga mno kwa kuwa hamjishugulishi hata kujua tunaungana kwenye nini. Tatizo kubwa lililotufikisha hapa ni mfumo wetu wa kielimu, tunajiona wanyonge kwenye kila kitu. Sisi wengine tunasema waache hao wana afrika mashariki waje, tutawaonesha kuwa Tanzania is the next Super Power in East Africa, we will take the battle to their markets and they will eat, drink, wear and sleep everything from Tanzania while we get rich
 
.....ni Dr. Richard Sezibera ni Katibu mkuu wa EAC,Tanzania haiwezi kumtimua Dr kwa kuwa yupo kisheria na si mwajiriwa wa serikali ya TZ....
......ana uwezo wa kutuhumu na hata kushitaki mahamani nchi yoyote mwanajumuiya wa EAC pale anapoona haifuati utaratibu
.......Dr sezibera siyo Rwanda...sijajua umetumia nini (kichwa/tumbo)kufikiria na kuandika..."hivi kweli Dr.Seziraba/Rwanda inaweza kuituhumu Tanzania "
.......rwanda wameingiaje katika hizi tuhuma anazotoa katibu mkuu? Chuki zako zinazosababishwa na uelewa mdogo/uvimba macho sidhani kama zinakufanyia haki hata wewe mwenyew maana zinakufanya uonekane mp..umb...avu mbele za watu. mfano Rwanda imeingiaje katika hili?

Ukirusha jiwe, ukasikia Mbwa anabweka, ujue limempata
 
We kweli punguani. Kwani wewe unavojiona una ubavu gani kutuzidi sisi watz tunaopinga EAC? hebu hamia basi huko Rwanda au Kenya ukafaidike na hiyo EAC ndani ya EAC, halafu uje utuletee ripoti.

Mlikimbia shule sasa mnakosa mbinu za kuyashinda mazingira yenu. Sasa mimi mbongo halisi, nchi yangu ina kila kitu, kuanzia madini, mbuga za wanyama za hali ya juu, mlima mrefu kuliko yote afrika, uwanda mpana zaidi wa bandari, kuna maziwa makubwa kabisa afrika, kuna BEACH za kufa mtu,,,, halafu wewe kula kulala unaniambia nihamie Rwanda ambako hawana chochote badala ya kunihamasisha kupiga kazi kwa bidii kuhakikisha kuwa natumia rasilimali za nchi yangu kuhakikisha kuwa hao majirani wanakunywa, kula, kuvaa na kulala kwenye bidhaa za Tanzania. Kweli ujinga uko kwa mtoto mdogo, lakini kiboko kitauondoa. Hii nchi ilipofikia inahitaji viboko tu ndio itaendelea. Lazy but knows it all attitude inaua hii nchi, tupambane, Marekani iko pale ilipo kwa sababu ya kupambana, sio kucheka cheka kama Kikwete
 
Kuna sehemu yoyote kwenye hiyo article umesikia nchi ya rwanda ikisema hayo? Huyu ameongea kama katibu mkuu wa EAC. Na Tanzania ilimpigia kura. Kwa hiyo usitoe povu hapa. Ongea point..

jamani huu sio muungano, tayari watu wanaopinga mawazo ya Tanzania, either waganda au wanyarwanda, hawa wanadhani sisi wajinga bado hatuoni, this people will never, ever intergrate, ni wabinafsi wa kutupa, i will rather live with an apartheid dutchman from south africa, kuliko hawa wanaojiona wako superior, naomba, president kabila naye aje ku recruit askari tanzania , tupambane na hawa ebony racists
 
Hawa watu Rwanda na Kenya wanachotaka ni ardhi na kinachowafanya watake ardhi ni watawala wao kutaka kupunguza pressure ya ndani kwa kuwasukumia raia wao nje ya nchi zao.
Kenya wana ardhi tatizo ni kwamba imeshikwa na watawala wachache sasa ili kupunguza pressure ya ndani kutoka kwa wananchi watakaouliza au kutaka kuleta mabadiliko ya sera ya umiliki wa ardhi, inabidi watawala watafute mahali pa kuwapunguzia ili ndani kuwe salama, same to Rwanda ila wao ardhi hawana na pa kukimbilia ni Tanzania.

Why only Tanzania ??
kuna nchi kama Congo DRC, Uganda, Somalia Sudan, S
Sudan kote huko hawataki kwenda wanalia na TZ utadhani ni kwao.
Tanzania ni nchi nzuri kuliko nchi zao na hao majirani wanaowazunguka ndiyo maana wanalia na hapa TZ.

Rwanda Kenya na wengineo pigeni kelele weee mkimaliza mnakutana na bango kubwa, HAKUNA ARDHI TZ.

Juzi tu Rwanda imeingizwa kwenye EAC, sasa hivi ni fujo EAC haieleweki huyo Kagame asiyekuwa na adabu ya kuishi na watu ndani ya nchi yake ndiyo huyo amekuja kuleta hiyo tabia yake ya kishenzi ya kubagua nchi na nchi, hana ustaarabu hata kidogo. Wakae na hiyo EAC yao waliyojiundia, TZ haipo EAC.
 
UK inatekeleza makubaliano yote ya EU isipokuwa la common currency. Usiwe mwepesi wa kupindisha ukweli.

Shirikisho la majambazi halina nafasi Tanzania.

Tanzania inataka shirikisho la mioyo ya watu. Watawala wetu hadi sasa mmefanya vyema kusikiliza na kuzitambua hisia za Watanzania. Chochote nje ya matakwa ya moyoni ya wananchi wa Tanzania HAKIKUBALIKI.

Kama kuna manufaa yo yote si waendelee na shirikisho lao bila Tanzania
 
September 23
21:002013


THE EAST AFRICAN COMMUNITY ( EAC) HAS RAISED CONCERNS OVER TANZANIA’S COMMITMENT TO THE REGIONAL INTEGRATION PROCESS.



EAC Secretary General Dr Richard Sezibera hit out at those dilly-dallying over integration process, saying they were missing the point.

Dr Sezibera said Tanzania has faltered on a number of key issues agreed upon by EAC regional States including the liberation of its current accounts and waiving of work permit fees.

“We don’t have compelling powers over those countries which seem not to be co-operating with the process of regional integration but the EAC treaty provides for the Secretary-General to take a country that is lagging behind to court. But this is a long process,” Sezibera told reporters in Nairobi yesterday.

Long-term goal

“Those still putting barriers to trade and integration are missing the point. We need to integrate much faster,” he added.

Sezibera noted that some people were interested in the benefits of regional integration yet they were not ready to participate in achieving its long-term goal.
“I’m concerned that at the individual and regional level, many actors are interested in plucking the fruits of regional integration rather than growing the tree,” he said, adding that the fundamental aim is to have East Africa’s prosperity by integrating. Sezibera was speaking on the sidelines of the Second Annual Banking and Research conference organised by the Kenya Bankers Association in Nairobi yesterday.

Tanzania’s commitment to regional integration has been under sharp focus since Kenya, Uganda andTanzania agreed to revive the defunct EAC in 1997. Tanzania has been viewed as a reluctant party to the integration process.

It has on several occasions asked for more time to open up its economy to East African counterparts. It is also understood that Tanzania negotiated as a member of the Southern African Development Community, but transferred its allegiance to the EAC after pressure from European Union.
Early this month, Presidents Uhuru, Yoweri Museveni of Uganda and Paul Kagame of Rwanda met in Mombasa to discuss cross-border infrastructure projects without Tanzania’s input.Similarly, Tanzania and Burundi were conspicuously absent at an earlier meeting in June 2013 by the three presidents; Museveni, Kenyatta and Kagame in Entebbe which was dubbed as EAC’s first infrastructure summit.Tanzania’s objections to both land purchases and a common EAC passport in 2009 also raised fears over its government’s commitment to the regional integration efforts.

By JAMES ANYANZWA, The Standard

Go to hell, we will never ever compromise over our land and the common passport! Lets EAC collapse once again! We opt to SADC rather than to join these "MANYANG'AU's"

Who is Sezibera anyway? What about Rwanda a very shallow and small country like Kaloleni ward in ARS!! Who gave them mandates to finger point on us? Stupid sana...shame on you! Seriously we warn Sezibera that if the government of Tz won't take an urgent action over this guy, then we will deal with him for the interest of our nation (he is our enemy)..tuko nae mara nyingi Mount meru, New Arusha hotel, Kibo Palace na Naura spring! Now its time, time has come indeed! Imekula kwake!
 
Nadhani wakati umefika kwa waziri Sitta kuanza kutoa elimu kwa watanzania kuhusu Jumuia ya Afrika mashariki, naona wengi hamuelewi hii kitu ni nini?? Sasa Mnyarwanda atapewaje Ardhi ya Tanzania?? Ebu jaribu wewe nenda kijiji cha Budalabujinga halafu kawaambie WAKUPE ARDHI kama inawezekana. There is nothing like kugawana ardhi kwenye muungano wa afrika mashariki. Mmekuwa waoga mno kwa kuwa hamjishugulishi hata kujua tunaungana kwenye nini. Tatizo kubwa lililotufikisha hapa ni mfumo wetu wa kielimu, tunajiona wanyonge kwenye kila kitu. Sisi wengine tunasema waache hao wana afrika mashariki waje, tutawaonesha kuwa Tanzania is the next Super Power in East Africa, we will take the battle to their markets and they will eat, drink, wear and sleep everything from Tanzania while we get rich

Si mlisema soon, Somalia ita join political federation la Kenya,Uganda na Rwanda. Vipi integration na somalia imefikia wapi msije waacha nyuma wasomali maana wana elimu nzuri na mnaweza kuuza bidhaa kirahisi zaidi na kununua ardhi kule kirahisi.
 
..Tanzania inasubiri nini kumtimua Dr.Seziraba?

..hivi kweli Dr.Seziraba/Rwanda inaweza kuituhumu Tanzania kwamba ktk EAC tunachuma tusichopanda?

..kwani Rwanda wana mchango gani ktk EAC mpaka wawe na kiburi na dharau kiasi hiki kwa Tanzania?
Inanikumbusha hadithi na msafiri na ngamia wake.
Kwa wale ambao hawaifahamu ni kwamba msafiri akiwa na ngamia jangwani walikumbana na 'sand storm' bwana msafiri kwa kuona hali mbaya akasitisha safari na kusimamisha hema ili ajisitiri. Kwa vile hali ilikuwa mbaya hapo nje akamkaribisha ngamia ndani kwa kurushu kichwa cha mnyama huyo kupenyezwa ndani lakini ngamia akaona hajastirika vizuri akawa anapiga kelele na bw msafiri kwa kumuonea huruma akamruhusu aingize sehemu ya mwili wake ndani[kwa vile hema lilikuwa linatosha kwa mtu mmoja tu] lakini alichokifanya yule ngamia ni kumpiga teke na kumtoa nje mfadhili wake naye akahodhi hemia.
 
Si mlisema soon, Somalia ita join political federation la Kenya,Uganda na Rwanda. Vipi integration na somalia imefikia wapi msije waacha nyuma wasomali maana wana elimu nzuri na mnaweza kuuza bidhaa kirahisi zaidi na kununua ardhi kule kirahisi.
Mkuu umeweka kimpumu asubuhi yote hii? Tunaongelea Jumuia ya Afrika mashariki wewe unaleta habari za Somalia, wapi na wapi. Au ndio product za shule za kata...
 
Kwani hapo alikuwa anazungumza kama Mnyarwanda?

Ndio,tena kabisa alikua akitoa hisia za nchi yake na hizo nchi tatu zilizojitenga! Wala huhitaji kuwa na certificate kujua huyu mtu alikua anasema nn na kwa faida ya nani! Au ww ni mnyarwanda nini, kama ndio Habari ndio hiyo kama ni chungu tema!!
 
Wewe hapo ulipo Una ardhi wapi, hauna hata robo eka na huenda unaishi kwenye Mbavu za Mbwa Tandale kwa Tumbo lakini unajifanya msemaji wa ardhi za wengine. Hapo ndio ujinga Wako ulipokufikisha. To be the best you have to beat the best, nyie majinga mnaogopa tusipambane na wana afrika mashariki wenzetu. Mimi mwerevu naangalia solo la Kenya, Soko la Uganda na Rwanda huku Tanzania ndio nchi yenye rasilimali zaidi, tutauza wapi bidhaa zetu? Fikiria nje ya box wewe Kula kulala


Ninakereka sana ninapokutana na Watz wa aina yako ambao ama kwa makusudi au kutokuelewa wanaitikia vibwagizo vinavyoimbwa na watu wa nchi nyingine za EAC eti sisi tunaogopa ushindani. Ushindani upi? Mbona tumefungua masoko sio kwa EAC tu bali dunia nzima na kila siku tunakaribisha uwekezaji

Sisi hatuna tatizo na EAC ila tunachotaka ni kuwa wakati sisi tuna ardhi na raslimali kibao hawa wenzetu wana nini cha kuchangia? Nasema ni uwendawazimu kung'ang'ania kushikirikiana na mtu ambaye hana kitu na anakutegemea wewe kumaliza matatizo yake. In short, ktk dunia ya leo unaanza na NIPE ndio inafuatia NIKUPE na sio NIKUPE tu sikuzote bila kujua na wewe ni lini UTANIPA
 
UK inatekeleza makubaliano yote ya EU isipokuwa la common currency. Usiwe mwepesi wa kupindisha ukweli.

Wewe ndio unaongea mambo kwa kupindisha ( yasiyo kweli ) UK wana mambo mengi wasiyofuata kutoka EU hata visa kwa EU wenzao kuna masharti ya zaida tena magumu tu, ukazi wana masharti ya ziada pia kaka ku ripoti police kila baada ya muda furani, misaada Kama benefit etc etc wana masharti mengi ya ziadi kwa EU wenzao sasa UK ipi una zungumzia
 
Ninakereka sana ninapokutana na Watz wa aina yako ambao ama kwa makusudi au kutokuelewa wanaitikia vibwagizo vinavyoimbwa na watu wa nchi nyingine za EAC eti sisi tunaogopa ushindani. Ushindani upi? Mbona tumefungua masoko sio kwa EAC tu bali dunia nzima na kila siku tunakaribisha uwekezaji

Sisi hatuna tatizo na EAC ila tunachotaka ni kuwa wakati sisi tuna ardhi na raslimali kibao hawa wenzetu wana nini cha kuchangia? Nasema ni uwendawazimu kung'ang'ania kushikirikiana na mtu ambaye hana kitu na anakutegemea wewe kumaliza matatizo yake. In short, ktk dunia ya leo unaanza na NIPE ndio inafuatia NIKUPE na sio NIKUPE tu sikuzote bila kujua na wewe ni lini UTANIPA

Kwa mtazamo wako ni kuwa jumuia ya afrika mashariki ni kuchangiana ardhi kama mchango wa harusi au?? Unaposema SISI tuna ardhi unamaanisha nini?? Ina maana hujui kuwa azimio la Zanzibar lilifuta azimio la Arusha na hivyo siasa ya ujamaa na kujitegemea imeishakufa. Hii ardhi tuliyonayo ndio tunayotaka kuitumia kuzalisha na kuuza kwenye hizo nchi ambazo hazina ardhi. Ujima bado umewajaa watanzania, hamjui kwa nini mnahitaji shirikisho na kwa nini hamhitaji.

Mtazamo wangu mimi ni kuwa sisi watanzania tutapata FURSA na kunufaika zaidi kwa kuwa ''SISI TUNA ARDHI'' wao hawana. Tutaitumia hiyo ardhi kuzalisha na kuwauzia majirani zetu, sio tu wa afrika mashariki bali kokote duniani.
 
Back
Top Bottom