EAC Chief warns Tanzania on regional Integration

EAC Chief warns Tanzania on regional Integration

Alichosema Dr Sezibera ni kwamba:



Tukianza na suala la liberalization of current account - makubaliano ni kwamba barriers & restrictions zote on the movement, sale, investment & payments of capital inatakiwa viondolewe; Vile vile kuna makubaliano ‘to remove all discrimination based on the nationality or on the place of residence of the persons or on the place where the capital is invested.' Ni kweli kwamba wenzetu Kenya, Uganda na Rwanda wameshafungulia haya, imebakia Tanzania na Burundi; Lakini pamoja na hayo, makubaliano ilikuwa kwamba Tanzania na Burundi wawe wametekeleza haya katika kipindi cha 2010 – 2015, kwahiyo tusubri tuone nini kitajiri ndani ya miaka miwili ijayo;

Tukija kwenye suala la work permit fees – makubaliano ni kwamba workers kutoka any partner state waruhusiwe kutafuta kazi katika nchi yoyote mwanachama wa EAC; Free movement of labour ni kwenye professions Fulani Fulani, sio professions zote, na professions hizi zipo listed wazi;

That said and done, lazima tuambiane ukweli kwamba pamoja na kwamba Tanzania ilikuwa mstari wa mbele baada ya uhuru kutafuta regional integration, katika kipindi cha hivi karibuni, tumejionyesha kuwa "shy partners'; kwa kweli hatujiamini, hivyo kufanya tusiwe na imani sana na EAC; Kuna vituko kadhaa tumevifanya in the past two years kuashiria kwamba hatuna genuine commitment – mfano kufunga mpaka wetu na Kenya Taveta (2012), kuzuia kuvusha mazao/nafaka kwenda nchi jirani(2011), kupingana na political federation and mutual defense pact (2011), na mahakama kuu Tanzania kuikingia kifua kampuni ya kitanzania (blueline) iliyofisadi;

Mbali ya haya, pengine hali yetu ya kusua sua pia inachangiwa Zaidi na hoja ifuatayo aliyotoa Waziri Mwakyembe mwaka jana wakati wa uchaguzi wa wabunge wa Tanzania to the EAC (Dodoma) ambapo alisema:



Maswali yanayofuatia ni je, ipi ni tafsiri sahihi kati ya hizi:


  • Kusua sua kwetu kunatokana na ukweli kwamba suala la EAC integration tulikuwa tunaliendesha kisiasa Zaidi na sasa uchumi unapoanza kupewa prominence na kuanza kupambanishwa na wenzetu (hasa Kenya), tunagundua jinsi gani hatujajiandaa – both on the micro/household level, na pia macro – level, structure of the economy and how it affects the balance of trade kati yetu na wakenya?
  • Ni woga wetu to share rasilimali na ardhi ambazo ni nyingi sana kuliko wenzetu?
  • Ni ignorance juu ya compromise zinazokuja na regional integration?

Pengine kuna justification katika suala la ardhi, kwani makala moja inatusema kwamba:



Tanzania accounts for about 52% of East Africa's total land area, na ingawa we have the largest population in the region, bado there is is significant land available. Suala hili is both a THREAT and an OPPORTUNITY kwetu sisi katika muktadha wa EAC, na ukweli utaendelea kubakia hivyo;

Mwisho ni suala la passport – uraia – hapa pia tuna sua sua linapokuja suala la common passport tofauti na wenzetu; Katika hili, given given ukweli kwamba almost 33% ya population ya EAC region ipo Tanzania, tunahitaji kuwa waangalifu sana hasa ikizingatiwa kwamba wenzetu wanasukumwa Zaidi na population pressure & shortage of land kuliko chochote – kwa mfano population density Tanzania ipo chini sana ikilinganishwa na Burundi, Rwanda, Kenya na Uganda; we have 47 people per square Kms, the lowest in the regions, huku Uganda na Kenya wakiwa juu Zaidi, na Rwanda na Burundu wakiongoza, 430 & 301, respectively;

Inawezekana sijapanga hoja katika mtiririko mzuri, lakini mniwie radhi, ilikuwa ni suala la haraka haraka tu katika kuchangia hoja; Nitarudi kwa hoja Zaidi……


nakala JokaKuu, Nguruvi3

Mkuu@Machambuzi, wakati naendelea kulipitia kwa ufasaha bandiko lako nimeona hayo masuala niliyoweka red, ambayo nilikuwa na mawazo kama yako ya kuona ni uwoga wa Tanzania. Hata hivyo, nimefanyia utafiti zaidi na kubaini ukweli kadhaa.
1.Mutual Difense Pact: Katika suala hili, Tanzania ilipingana na kifungu kilichokuwa kikisema kwamba iwapo nchi moja ya Afrika Mashariki itaingia kwenye vita na nchi nyingine iliyo nje ya Afrika Mashariki, Nchi zote za Afrika Mashariki zishirikiane na kuchangia nguvu ili kumpiga adui wa mshirika wetu. (Kama mfano wa NATO Pact vile. Utafiti wangu umebaini mambo yafuatayo ambayo nahisi Tanzania ilikuwa right kufanya hivyo (not sure kama ndizo hoja walizotumia hizi ni hoja zangu za kitafiti)

a) Nchi nyingi za Afrika Mashariki yaani Rwanda, Uganda na Kenya haziko kwenye mahusiano mazuri na majirani zao na pia ni 'nchi chokozi kiasili" hivyo kitendo cha kuwa na "alliance" ya namna hii, ni kuongeza kujiamini kwa nchi hizo kuingia kwenye vita wakiamini kwamba nchi nyingine wanachama zita-bear cost ya vita hivyo. Hivyo uwezekano wa Tanzania kuingizwa kwenye vita isiyowahusu ulikuwa ni mkubwa sana iwapo wataridhia/wangeridhia kwa muktadha huu.

b) Tanzani ina mipaka na nchi nyingi ikiwa pamoja na DRC ambayo iko kwenye majaribu ya muda mrefu na Rwanda. Kusani kwa makubaliano haya maana yake ingetokea/ikitokea Rwanda kuingia kwenye vita na Congo DR, automatically, Tanzania ingebidi ishiriki kwenye vita ikipigana upande wa Rwanda na kumpiga Congo DRC, pamoja na kuharibu mahusiano ya kibiashara na Zaire, hii kitu ingetutia matatani kule SADC ambapo nchi kama Congo ni mwana SADC

3. Alliances za kijeshi chini ya muundo wa kikanda zina kawaida ya kusababisha kuenea kwa vita kwa eneo kubwa kama historia inavyotueleza kwenye WWI na WWII. EAC ikiwa na Alliance ya kupigana vita, na ile Jumuiya ya Afrika ya Kati (ikitokea) kuwa na alliance ya kivita, maana yake vita (let say) baina ya Rwanda na Congo ingesababisha vita ya nchi zaidi ya nchi kumi. Ukichukua model hii katika multiplier effect yake, utaona kwamba Bara lote la Afrika linaweza kuingia kwenye vita, just iliyosababishwa na migogoro ya nchi mbili tu. Kwa mfano, kwasasa huenda Tanzania ilipaswa kuwa na vikosi vyake Somalia-sipati picha kungetokea nini.

2. Kuhusu Shirikisho la Kisiasa, ni uroho wa hizo nchi tatu kwa sababu wao wanaamni kwamba, njia rahisi ya kuunda shirikisho ni kuanza na shirikisho lenyewe kisha shirikisho litumike ku-enforce Customs Union, Common Market na Monetary Union; kitu ambacho ni kinyume na Mkataba na pia ni kinyume cha Kanuni zinazotawala Jumuiya za Kiuchumi za Kikanda ambazo sababu zao kubwa ni Biashara wala si utawala na ndio maana zinasajiliwa WTO si Baraza la Usalama la UN.

Nina hakika, hata nawe ukifuatilia haya uta-withdrawa na hizi propaganda kwamba Tanzania ni "sleeping elephant" au "stumbling bloc" katika Jumuiya.
cc Nguruvi3, joka Kuu
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Mchambuzi,
Huu ni mwendelezo wa bandiko na. 161....Je Wewe binafsi pamoja na Nguruvi3, mnadhani hii model ya kuanza na Shirikisho na kisha shirikisho litumike kuimarisha Soko la Pamoja(niliyoielezea katika bandiko na 161 itaweza ku-function vizuri katika mazingira haya ya kinafiki ya ki-EAC? Ni kweli movement ya kibiashara itastawi vema kupitia model hii kuliko CU-PF?

Na ikumbukwe kwamba hili wazo la kuanza na Shirikisho limekuja baada ya kushindwa kwa wazo la kutaka kubadili Mkataba ili maamuzi yawe yanafanywa kwa kura badala ya consensus, vilevile ni wazo lililokuja baada ya kushindwa wazo la kubadili Mkataba ili eac iwe "community based organization badala ya Intergovernmental organization; kwamba nchi wanachama zitoe full authority (zipoteze authority) kwa Sekretarierti kufanya kila kitu na nchi wanachama ziridhie tu kama ilivyo EU ya sasa (ingawa "variable geometry wangetaka iendelee kuwepo)
.
 
Ruzibiza,

..mkataba wa EAC unaeleza kwamba masuala ya ARDHI na free movement yataamuliwa kulingana na sheria za nchi wanachama.

..Tanzania haijakiuka mkataba wa EAC kwa kuendelea kusisitiza kwamba ardhi yake siyo suala la EAC. Dr.Sezibera anaelewa hilo lakini ameamua kupotosha hao waandishi wa habari.

..Kwa mwana EAC anayehitaji ardhi hapa Tanzania anapaswa kuwasilisha maombi kwa kuzingatia sheria zetu za uwekezaji. Mahali pazuri pa kuanzia ni Tanzania Investment Center[TIC].

..Kwa upande wangu naamini utaratibu huo ni mzuri. Tunachohitaji huku Tanzania ni wawekezaji wakubwa-wakubwa na siyo wakulima wachumia tumbo, au wafugaji wanaohama-hama.

..Kama kuna wa-Tz mafisadi ambao wanahodhi ardhi kubwa bila kuitumia basi hayo ni mapungufu ktk utekelezaji wa sheria zetu za ardhi. U do not solve that problem kwa kufungua milango kwa squatters toka Kenya, Rwanda, au Burundi.


wapi mtoa mada kasema Dr. Sezibera anataka ardhi unajua idad ya protocol za eac?mbona unakomaa na hilo la ardhi?hilo linaeleweka...what doest it mean by common market?kama tz ilijua haijawa tayari nani aliwalazimisha kuingia eac?who negotiated hiyo mikataba?kwanini katka implementation ionekane nongwa?eac agreement inawapa watu uhuru wa kutosha na ndo maana sioni sababu ya tz kusononeka inapotengwa katika baadhi ya mambo....tz haiwezi pace ya eac so uamzi wa kujitoa utawafaa coz hata watakapo baki hawana uwezo wa kuigeuza jumuiya fursa.....badala yake wanaiona tishio.....faida ya eac haiwezi onekana hadi pale watakapopatikana watu wenye uwezo wa kugeuza kinachoonekana tatizo into fursa...

Tanzania haikuomba kuingia eac bali ilianzisha eac, walioomba kuingia ni rwanda na burundi. Tanzania ilipoanzisha eac ilisema tunaenda kwa stages mtoto anazaliwa, ana tambaa, anajifunza kusimama, anatembea na kuanza kukimbia kisha anajitegemea. Yani ya kwamba, Tanzania ilipoanzisha inataka soko la pamoja lifanye kazi, mambo ya mapato yafanye kazi, mambo yasingo currency yafanye kazi, na baadae kuya evaluate kama yana tija kwa mda fulani kisha kama kuna tija basi political federation.

Tatizo linakuja kwa wale walioomba kuingia kama Rwanda, wame adopt mtoto ambaye anajisimamia, yani kwa kuingia eac, hawajui mtoto alizaliwa vipi, na anatambaa je na kujifunza kukimbia, wao kwa vile wame adopt mtoto wanafikiri mtoto huzaliwa akiwa anakimbia.
 
Tanzania ni muhimu kuliko EAC
1. No to land purchase
2. No to common tourist visa
3. No to free work permit
ukiangalia wanachokitaka ni ivyo vitatu ambavyo kwa TZ sie tutakua tuna loose hatuna cha kugain ktk ivyo vitatu kutoka kwa hawa wenzetu so tuachane nao kabisa tujiunge na tuimaishe sadc kwani hakuna m south africa atayekuja apa aanze kulia lia akiomba auziwe ardhi au atake kuja kufanya kazi bure!!! wanataka lile jeshi la wasio na ajira kule kenya lije hapa!! big Nooooooooooooooooooooo!!!!!
 
Heshima sana wanajamvi,

Dr Sezibera ni nani ?.

Dr Sezibera ni Mnyarwanda (Mtutsi) na ni daktari wa binadamu aliyosomea chuo kikuu cha Makerere Uganda na baadae akachukua shahada ya uzamili (Master of Arts) chuo kikuu cha Georgetown Marekani.

Amewahi kufanyakazi ya udaktari Mbuyu Hosipital na Mbale Hospital zote za nchini Uganda kabla hajajiunga na kikundi cha kigaidi RPF akihudumu kama daktari wa jeshi kwa muda mrefu hadi akafikia ngazi ya Major.Mwaka 1994 Dr Sezibera aliteuliwa kama daktari wa Rais Kagame kabla hajateuliwa nafasi ya ubalozi na baadae waziri wa afya.

Dr Sezibera ni mwanajeshi mtiifu wa kundi la RPF ambao ajenda yao kubwa ni kuhakikisha kabila la watutsi linatawala Rwanda na Uganda na hatimaye waitawale EA yote.Dr Sezibera ni kikaragosi cha Dictator Kagame yuko Arusha kukamilisha kazi haramu ya kuhalalisha utawala wa kitutsi EA baada ya kufanikiwa kukandamiza kabila la wahutu walio wengi Rwanda.

nilifikiri huyu ps wa eac ni daktari wa fani kama uchumi anayeweza kuipeleka eac na wanainchi wake kwenye ukuransa mpya kumbe cv yake ni rebel doctor au war lord, yaani ea nzima kulikuwa hakuna mtu mwenye cv nzuri zaidi!!!!
 
Kubali ukweli huna uzalendo na nchi yako. Mtanzania halisi yuko tayari kwa gharama zote kuilinda, kuitetea, na kuiheshimu nchi yake na siyo kutaka kugawa raslimali zetu kisa Jumuia. Wewe unajua kabisa wenzetu wanagombania ardhi yetu, wanagombania ajira, wanagombania uchumi wetu. EU Uingereza imekubali yote lakini si fedha wala kuingiliana hivyo hivyo na ndiyo maana si membe wa Schengen na amebaki na Pound yake

Kama wewe ni incompetent kwenye labor market shauri yako, hatuwezi kusubiri hadi wewe ujitambue ndio tuungane wakati umekumbatia ujinga. Kama woga ndio kuheshimu nchi yako ni bora nionekane siheshimu. Serikali ya awamu ya tatu chini ya Mkapa ilikuwa na ujasiri wa kujadiliana na kutekeleza makubaliano, nyie akina Mwanaasha hamueleweki mnataka nini kwenye jumuia, ni bora kujitoa ijulikane moja kuliko kuwa mguu nje mguu ndani. Ni bora kuwa moto au kuwa baridi kuliko kuwaVUGUVUGU
 
kiingereza ndiyo degree ya kuelewa au?
Akisha kijua atakuwa muelewa au?

ndo maana nikaweka " / " ukizingatia thread ipo kwa kiingereza nilitaka kuestablish kati ya lugha na uelewa jamaa anaweza nini vzuri maana alichojibu ni tofauti kabis na kilichoandikwa
 
nilifikiri huyu ps wa eac ni daktari wa fani kama uchumi anayeweza kuipeleka eac na wanainchi wake kwenye ukuransa mpya kumbe cv yake ni rebel doctor au war lord, yaani ea nzima kulikuwa hakuna mtu mwenye cv nzuri zaidi!!!!
Unaijua Georgetown? au unafikiri ni vyuo vyako vya kata ulivyosoma na wapumbavu wenzako.
 
if your wife is a fool, then you know how to deal with fools then you are a MEGA SUPER FOOL

it doesnt matter who i may be...it is only a "MEGA SUPER fool" who believes that a doctor needs to be extremely ill to treat a patient...
 
UK inatekeleza makubaliano yote ya EU isipokuwa la common currency. Usiwe mwepesi wa kupindisha ukweli.

Sidhani kwamba ukweli umepindishwa hapa. kwanza, sio kweli kwamba UK inatekeleza yote isipokuwa common currency. Baadhi ya mambo ambayo UK ime-opt out (mkataba wa EU unaruhusu nchi ku-opt out) ni pamoja na schengen agreement (immigration entry visa); police and justice (along with Denmark); charter of fundamental rights (pamoja na Poland) nd Commom Security and defence (pampja na Ireland).
 
Kuna mambo ambayo yanapaswa kuangaliwa kwa kina katika hili. Ukweli unabakia kwamba:
1. Integration hailazimishwi. Aidha umo au haumo (kwa faida yako). kama unaona huwezi kasi basi achia ngazi.
2. Hawa majirani walikuwapo, wapo na wataendelea kuwepo. Lililopo ni kuamua kushughulika na swala hili sasa au kusuburi.... japo halitaondoka hili? LIPO na LITAENDELEA KUWEPO!
3. Faida za economic integration hazikaniki. Jinsi gani utatetea maslahi yako ndani ya jumuiya ni swala la ufahamu na kujiandaa for what is an eventuality.
 
Waganda wana msemo mmoja unaitwa SERWAJJA KWOTA,hiki ni kisa cha mtu mmoja aliyekuwa amekoka moto wake nyumbani kwake,pamoja nakupika chakula chake nje kulikuwa na mvua kali inanyesha ikiambata na baridi kali,kwa hiyo moto ulikuwa ukimsaidia kuondoa baridi aliyokuwa nayo.
Ghafra akatokea mtu nje aliyekuwa amelowa chapachapa nakuomba asogee akapashe mwili moto cha ajabu baada yakukubaliwa akajitanua na kumkinga mwenyeji wake, kwa EAC Tanzaia ma SERWAJJA KWOTA itawaona wengi.
Ikumbukwe Tanzania ina uzoefu wa muungano kuliko hizi nchi zote wanachama wa EAC na naona tahadhari zao zina mantiki na kama tuna maana ya kuwa na muungano wa kudumu hatuna budi kwenda taratibu tunakimbilia nini ni lazima ufanyike upembuzi yakinifu na kila mwanachama ajirizishe kwa maslahi ya wananchi wake hakuna sababu ya kukurupuka.
Kama kuna hali yakuburuzana hata kabla safari haijakolea ni bora tukabaki bila ushirika huo maanake huko mbele ya safari mambo hayaelekei mazuri.
 
Mkuu JokaKuu
Dr sezibera amekwenda kuongea mambo ya EAC katika mkutano binafsi Kenya ili kutoa nafasi ya vyombo vya habari kueleza nafasi ya nchi yake na Kenya dhidi ya Tanzania.Kama mtendaji mkuu wa EAC alipaswa kutoa kauli siku yoyote na si kwenye mikutano binafsi.

Dr Sezibera ameshindwa kuongelea mwendo wa EAC na matatizo yanayojitokeza. Kwanza lazima afahamu makubaliano ya soko la pamoja yalikuwa na hatua zinazopaswa kufuatwa.
Suala la ardhi ambalo limemuudhi kama Mnyarwanda na kibaraka wa Kenya, hayamo katika makubaliano ya EAC

Ilikubaliwa kuwa kila nchi iwe na utaratibu wake wa ardhi, hakuna mambo ya faster ameshindwa kuona facts.
Sezibera anaongoza na fikra za Kagame. Makatibu wengine walikuwa wanadiplomasia na jumuiya ilikwenda mbele.
Tangu Sezibera apewe ukanda EAC imezidi kuwa hovyo kwasababu ya kuongozwa na PK na kuwa kibaraka wa Kenya.

Kibaraka SEzibera aelewe Tanzania ndiyo nchi pekee iliyokuwa mstari wa mbele kuanzisha EA Federation na EAC iliyokufa na ya sasa. Tuna uzoefu wa kufanya mambo na tuna uzoefu wa matatizo yaliyotokea 1977.Rwanda alikotoka hawana uzoefu wa ''muungano'' hata wa Watusi na Wahutu, hawezi kufundisha asicho na ujuzi nacho.

Kuhusu ushindani, inategemea mtu anatafsiri gani ya ushindani i.
Ukabila kama wa Waluo na Wakaikuyu ni competetion. Wahutu na Watusi ni competition pia.Museveni na Koni ni competition.
Kwahiyo Tanzania inaweza kuogopa ushindani huo na sijui kama ni kosa.

Marekani taifa kubwa linalaumiwa katika NAFTA katika mambo ya ajira na uwekezaji.
Marekani inalinda masilahi yake kwa vile ndani ya NAFTA itapoteza zaidi kuliko kupata.
Nchi nyingine wanataka milango ifunguliwe ili waifadike. Vipi Tanzania ionekane inafanya makosa kuchukua hadhari.

Kwa wale waliokuwa hawapo au wadogo,miaka 25 hakuna ambaye angesema Tanzania inaweza kuwa second economy na tishio kwa first economy EAC. Leo hali ni tofauti sana.
Muhimu si kukimbia bali kukimbia kwa tahadhari hasa kuangalia interest za wenzetu ni nini.

Nakubaliana na JokaKuu kwamba mapungufu yaliyopo yafanyiwe kazi lakini siyo sababu kwanini Tanzania inachukua hadhari.

Fikiria kuwa EAC ya mataifa matatu wakikaa pamoja hawaongelei ardhi, Tanzania ikiwemo suala la ardhi linachukua nafasi.
Kwanza lilipokataliwa wakaja na njia ya vitambulisho ambayo ni mlango wa uani.
Kenya na Uganda walikaribia kupigana kwasababu ya KM 1, leo wapo mbele kusema tunaogopa ushindani.Upi huo? Je kugombania migingo ya KM1 siyo ushindani?

Hizi ni mbinu za kufunika hoja yao kubwa ya ardhi hakuna jingine.
Kama Tanzania ingekuwa inaogopa EAC Kenya isingekuwa mwekezaji namba 2 Tanzania.
Milango itafunguliwa kwa taratibu na sheria, siyo kutanguliza watu 20,000 halafu iletwe hoja ya soko la pamoja n.k.

argument yako ni kama ya mtu yeyote failure,unachoongea ni kwa kutanguliza feelings zako mbele tu...Dr. hajasema chochote kuhusu ardhi ila kila kinachoongelewa hapa ni ardhi ili kupumbaza watu na ku-inculcate chuki kati ya watu...mfano u can't be fair ku-blame rwanda kwa tuhuma zilizofanywa na katibu mkuu wa eac eti kwa kuwa yeye ni mnyarwanda...mambo kama haya nayaona kila mara tu hata hum jamii..pale unapokuwa na mtizamo tofauti katika baadhi ya mambo unaishia kuitwa kibaraka wa kagame...ninachotaka kujua in the first place ni watz tunashindania nini na wanyarwanda/wakenya?mbona kama tunachuki za wake wenza?Rwanda/kenya are member like any other members,isitoshe nchi zote members ni nchi huru kila nchi inamaamuzi on its own for its own intrests....tz haijakubaliana juu ya ardhi na hakuna anyebisha juu yahilo...ndo maana nasema watz hatupo tayari kwa muungano na ndo maana kila kinachofanyika tunaona kama tunataka kuibiwa,flani atafaidika zaidi n.k.....na ni kwasababu ya uoga wetu hadi suala la vitambulisho tunaita ni mlango wa nyuma....usumbufu tunaoupata upande wa migration watz ni mkubwa tukiwa tunavuka kuelekea nchi zingine za jumuiya, imagine utaulizwa maswali weee....wakati upande mwingine ni kutereza tu hii inamaanisha nini?hata kama nje kunafursa viongozi wetu hawatutengenezei mazingira ya kunufaika nazo...wengi mnazungumza kwa hisia tu bila ya kujiuliza pamoja na raslimali zetu kwanini tusifanye kenya,uganda,rwanda na burundi soko la bidhaa zetu?badala yake tunakaa kulalama land land wakati sisi tumegeuzwa soko la east africa....kenya is the 2nd big investor in tz....badala ya kutumia muda mwingi kujiuliza raslimali tunazojivunia zinatusaidiaje kubenefit muungano..tunakaa kusema muungano umelenga kukwapua raslimali zetu...yes inawezekana....tumefanya nini zaidi ya kulalamika hovyo?sijaona juhudi za maksudi mfano tz imeruhusu from 2010-2015 kuwa hawa watu wataingia na kufanya kazi i.e Professionals and Technicians and Associate Professionals....nchi yetu inakabiliwa na uhaba wa waalimu,na ni kwa exchange programs na kuruhusu walimu kutoka nchi wanachama(hasa wale wenye mifumo mizuri ya elimu zaidi yetu kama Kenya,Uganda) ili tuweze kupata ushindani katika soko la ajira matokeo yake working permit kwa mwalim wa english medium kutoka ndani ya eac ni kama "USD 3200" kwa mwaka,tunadhamilia kuondoa ujinga na kupata ushindani katika jumuiya?na zaidi ya hayo walimu kibao wamepeperushwa na kimbunga....for real are we serious?
u have some weak argument eg. umeongelea migingo.... kama issue ya nyasa itasettle itafanya malawi na tz zisiwe SADC?migogoro huwa ipo na humalizwa,na in fact that is one of the benefits of any integration be it EAC,SADC,EU,NAFTA, mention it!
 
Tanzania ni muhimu kuliko EAC
1. No to land purchase
2. No to common tourist visa
3. No to free work permit
ukiangalia wanachokitaka ni ivyo vitatu ambavyo kwa TZ sie tutakua tuna loose hatuna cha kugain ktk ivyo vitatu kutoka kwa hawa wenzetu so tuachane nao kabisa tujiunge na tuimaishe sadc kwani hakuna m south africa atayekuja apa aanze kulia lia akiomba auziwe ardhi au atake kuja kufanya kazi bure!!! wanataka lile jeshi la wasio na ajira kule kenya lije hapa!! big Nooooooooooooooooooooo!!!!!

tutakaa hivi hadi lini?jeshi la wasiyo na ajira tz ni kubwa pia sana tu...makaburu walojazana migodini hadi kwa kazi za kawaida sana ni wa wapi?hatutaweza kushindana kama tutajifungia ndani doing nothing...WTO is on our neck ina adjust mambo kila kukicha, WB vile vile na IMF vile vile,ipo siku utakumbuka muda ambao tungeutumia kujifunza na kushidana na wenzetu,tuliutumia kujifungia ndani ya bongo na kupiga domo ardhi ardhi..nk ruhusu watu waje turuhusu twende nje japo si kiholela tujifunze wanafanyaje ndo akili itafunguka...nimechoka na nyimbo zile zile za raslimali,ardhi n.k huku sina hata mia mfukoni
 
nimechoka na nyimbo zile zile za raslimali,ardhi n.k huku sina hata mia mfukoni
,Na hiyo mia utaipataje kwa uakika under EAC?

Kwanza hao wenzetu wanaonyesha ubabaifu wao wazi vile ambavyo wanaweza fanya wenyewe na vyenye maslahi kwa Mkenya wanaenda na go ahead ya Waganda na Wanyarandwa hila yakija kwenye mambo ambayo hili maslahi yawe mazuri kwao ndio Tanzania inagwaya.

Mbona kwenye maslahi kama ya kwenye ka reli kao uchwara hawajasubiri na wala kulalamika hila kwenye maslahi yetu ndio sisi tunawachelewesha, kama wangekua na nia ya wote wangelazimisha makubaliano kabla kuwahi kilicho kwenye maslahi yao, nyie ngojeeni wewe, Koba na ma traitors wenzako hiko siku tutawatia ababu kwa unafiki wenu.
 
Kama wewe ni incompetent kwenye labor market shauri yako, hatuwezi kusubiri hadi wewe ujitambue ndio tuungane wakati umekumbatia ujinga. Kama woga ndio kuheshimu nchi yako ni bora nionekane siheshimu. Serikali ya awamu ya tatu chini ya Mkapa ilikuwa na ujasiri wa kujadiliana na kutekeleza makubaliano, nyie akina Mwanaasha hamueleweki mnataka nini kwenye jumuia, ni bora kujitoa ijulikane moja kuliko kuwa mguu nje mguu ndani. Ni bora kuwa moto au kuwa baridi kuliko kuwaVUGUVUGU
Ima hujielewi au huelewi au vyote
 
Unaijua Georgetown? au unafikiri ni vyuo vyako vya kata ulivyosoma na wapumbavu wenzako.

Huu ndio unaitwa upofu wa fikra, kwani mtu akisoma Georgetown University ndiye anakuwa perfect kila kitu? Umesahau kuwa Chenge amesoma Harvard? AU Membe aliyesoma John Hopkins, je Georgetown na Harvard kipi kiko juu? na je huyo Graduate wa Harvard anaifanyia nini Tanzania kwa sasa? Comment ya emike still valid, kwamba yeye alikuwa akidhanni udaktari wa Sezibera ni wa PhD tena labda ya Uchumi au related discipline, kumbe si hivyo, hizi habari za Georgetown hazina maana yoyote kwani kusoma kwake Georgetown hakumuondolei uhalisia wake kwamba yeye ni "rebel doctor"
 
Last edited by a moderator:
argument yako ni kama ya mtu yeyote failure,unachoongea ni kwa kutanguliza feelings zako mbele tu...Dr. hajasema chochote kuhusu ardhi ila kila kinachoongelewa hapa ni ardhi ili kupumbaza watu na ku-inculcate chuki kati ya watu...mfano u can't be fair ku-blame rwanda kwa tuhuma zilizofanywa na katibu mkuu wa eac eti kwa kuwa yeye ni mnyarwanda...mambo kama haya nayaona kila mara tu hata hum jamii..pale unapokuwa na mtizamo tofauti katika baadhi ya mambo unaishia kuitwa kibaraka wa kagame...ninachotaka kujua in the first place ni watz tunashindania nini na wanyarwanda/wakenya?mbona kama tunachuki za wake wenza?Rwanda/kenya are member like any other members,isitoshe nchi zote members ni nchi huru kila nchi inamaamuzi on its own for its own intrests....tz haijakubaliana juu ya ardhi na hakuna anyebisha juu yahilo...ndo maana nasema watz hatupo tayari kwa muungano na ndo maana kila kinachofanyika tunaona kama tunataka kuibiwa,flani atafaidika zaidi n.k.....na ni kwasababu ya uoga wetu hadi suala la vitambulisho tunaita ni mlango wa nyuma....usumbufu tunaoupata upande wa migration watz ni mkubwa tukiwa tunavuka kuelekea nchi zingine za jumuiya, imagine utaulizwa maswali weee....wakati upande mwingine ni kutereza tu hii inamaanisha nini?hata kama nje kunafursa viongozi wetu hawatutengenezei mazingira ya kunufaika nazo...wengi mnazungumza kwa hisia tu bila ya kujiuliza pamoja na raslimali zetu kwanini tusifanye kenya,uganda,rwanda na burundi soko la bidhaa zetu?badala yake tunakaa kulalama land land wakati sisi tumegeuzwa soko la east africa....kenya is the 2nd big investor in tz....badala ya kutumia muda mwingi kujiuliza raslimali tunazojivunia zinatusaidiaje kubenefit muungano..tunakaa kusema muungano umelenga kukwapua raslimali zetu...yes inawezekana....tumefanya nini zaidi ya kulalamika hovyo?sijaona juhudi za maksudi mfano tz imeruhusu from 2010-2015 kuwa hawa watu wataingia na kufanya kazi i.e Professionals and Technicians and Associate Professionals....nchi yetu inakabiliwa na uhaba wa waalimu,na ni kwa exchange programs na kuruhusu walimu kutoka nchi wanachama(hasa wale wenye mifumo mizuri ya elimu zaidi yetu kama Kenya,Uganda) ili tuweze kupata ushindani katika soko la ajira matokeo yake working permit kwa mwalim wa english medium kutoka ndani ya eac ni kama "USD 3200" kwa mwaka,tunadhamilia kuondoa ujinga na kupata ushindani katika jumuiya?na zaidi ya hayo walimu kibao wamepeperushwa na kimbunga....for real are we serious?
u have some weak argument eg. umeongelea migingo.... kama issue ya nyasa itasettle itafanya malawi na tz zisiwe SADC?migogoro huwa ipo na humalizwa,na in fact that is one of the benefits of any integration be it EAC,SADC,EU,NAFTA, mention it!

Kwanza nina masikitiko makubwa sana kwa Idara ya Uhamiaji, RITA ikiwa wewe uitwaye Ruzibiza una-hold tittle ya uraia wa Tanzania. Pia masikitiko yangu yawafikie Kikosi cha Operesheni Kimbunga kama hawajaweza kukufikia na kukurudisha kwenu.

Pili, usitumie Jukwaa hili la JF kuandika chuki, uzandiki na uongo ili kuchafua mamlaka zetu. Ni wapi Mtanzania anapokwenda nchi nyingine za eac anaulizwa "mswali wee" na immigration wa Tanzania na haulizwi maswali hayo kutoka kwa immigration wa Kenya? Kama wewe ni mnyarwanda lazima tukuulize maswali unapotaka kuingia kama fomu yako haina maelezo yanayotosheleza yanayoendana na Mkataba wa Soko la Pamoja.

Tatu, unasema kwa kujua au kuhisia kwamba mfumo wa elimu wa Kenya na Uganda ni mzuri kuliko wa Tanzania? Huoni kama umejichanganya hapa? Mfumo wa Uganda kiasi unafana na wa Tanzania kwamba wana kidato cha sita ule wa Kenya unaishia kidato cha nne kabla ya kuingia chuoni, nini kusudia lako hapa. By the way, Tanzania iko katika "traffic light system" kwa masuala yote na sasa hivi taa inayowaka ni yellow, kwa hiyo wewe na mabwana zako kaeni tayari kuipokea red light itakayowafanya muwe kimya (sidhani kama utakuwa umeelewa hapa). Ungelikuwepo miaka ya tisini, ungejua idadi kubwa ya watanzania waliokuwa wakivuka kwenda Kenya na Ugnada kufuata the so called "international english medium schools", lakini leo hii watanzania wana "International English Medium Schools za kufa mtu; watanzania wanaovuka kwenda Uganda ni wale walifeli Tanzania na wanaenda kufanya-repeatition huko na kuafulu ili wajiunge na vyuo vya huko. Je unajua record ya wahitimu wa vyuo vikuu 10 years back kwa Tanzania ilikuwaje ukilinganisha na nchi za Kenya na Uganda, na sasa hivi hali ikoje? Huu ni mfano mchache wa "yellow light" inayowashwa na Tanzania. Kwa kifupi Tanzania hatuna tatizo kubwa na "mfumo mbaya wa elimu" labda ungelisema usimamizi mbaya wa elimu kidogo ungelieleweka.
 
Last edited by a moderator:
eu mbona hawakuibagua united kingdom?
tanzania knows its identity and position in east africa and it cant bow at elusive demands from its neighbours . This orientation is looked upon very cautiously . Sezibera is a rwandese personnell in east africa trying to propagate the long standing ideology of the bahima empire in east africa. We are not ready. Tumemsikia waziri wa africa mashariki mh. Samuel sita kwahiyo hatuwezi kumpuuza hata kidogo. Huo uhuni unaofanywa na secreatariet inayoongozwa na sezibera hauwezi kuachwa hivihivi na watanzania kamwe hatuko tayari kuingia east africa KICHWAKICHWA bila kujielewa, kamwe haitatokea potezea muendeleee ninyi wenyewe wahuni
 
Back
Top Bottom