E Fm mbona mnakomalia suala la Bashite hivyo?

E Fm mbona mnakomalia suala la Bashite hivyo?

98292a191b674b9b9414c0486eec0ca9.jpg
 
Alitoa awamu ya kwanza
Akatoa awamu ya pili na mimi nimo
Akatoa ya tatu

Mimi nimetoa awamu ya kwanza tuu kaanza kuhaha.............. ninamazaga zaga mengi kuhusu huyu Daudi Albert Bashite
(in Gwajima's voice)
Duh
 
MAONI YA MHARIRI gazeti la Mwananchi: Ni muhimu Makonda amalize utata huu

Wakati Rais John Magufuli alipoteua wakurugenzi wa majiji, manispaa na halmashauri kuliibuka maneno mengi, hasa mitandaoni kuwa mmoja wa watu walioteuliwa hana elimu ya kutosha kustahimili kazi hiyo.

Maneno hayo yalifikia hatua ya watu kusema kuwa mtu huyo amesomea masuala ya hoteli. Ilikuwa bahati kwamba walioteuliwa wakati huo walitakiwa wahakikiwe elimu yao kabla ya kuapishwa.

Kabla ya kula kiapo cha maadili ya uongozi, Rais Magufuli alizungumzia suala hilo na baadaye kumtaka mtu aliyetuhumiwa kuwa hana elimu ya kutosha, aonyeshe hadharani cheti chake na alifanya hivyo...
Bashite je
 
kumjadiri=kumjadili huko shule ulienda kusomea ujinga au na wewe ni zile type za kina bashite?????, atoe vyeti mengine yafuatwe kama ni jela miaka saba au faini au vyote kwa pamoja.
Vyeti vyeti tuu
 
mkuu ujuwe kuna watu wamepoteza kazi kwa kosa kama la Bashite hivyo familia yao inahangaika. Kwa nini Bashite naye asifukuzwe?
 
dawa pekee ajitoe ufahamu aelezee elimu yake japo ni jambo gumu kama kuchambia upupu !
Mwaka Jana aliita watu,vilaza,vichaa,hawajielewi na kumbe yy ndo kichaa
 
Naunga mkono hoja,jamani itoshe sasa hii ni too much! Tukilala Makonda tukiamka Bashite wengine mpaka tunaota tupo koromije! Loh! Emu kuweni na huruma hata kiduchu.
"hawa ndio vichaa tunaowatafuta..hebu tooka hapa"

Mkuu unaikumbuka hiyo kauli dhidi ya yule mwanamama? Huku TV zikiwa mubashara?

Unajua ni kiasi gani yule mama alivyoumia kudhalilishwa vile na kijana mdogo aliyeshindwa kufanya mambo yake kwa busara?

Kwanini aonewe huruma na wakati uwezo wa kujitokeza na kuwafunga watu midomo anao? Si hajaghushi vyeti?
 
Back
Top Bottom