Mkuu The Big, kwanza nikuhakikishie kuwa tunazungumza kiungwana, kiraia na kindugu kama Watanzania kama ulivyosema hata kama tutakuwa na mitazamo tofauti, ndio tija ya mjadala.
Pili, hao vijana unaosema wametoka mataifa mbali mbali ni Wasomali waliopewa ukimbizi na nchi hizo.
Mwaka huu mwezi wa 3 Marekani imechukua wakimbizi wa Somnalia 240 kwa gharama zao, kuwapa hifadhi na haki ya ukaazi moja kwa moja.Ndivyo ilivyo kwa Sweden, Norway n.k. Ni mradi endelevu kwa miaka mingi
Hakuna nchi yoyote ya kiarabu ikiwemo Saudi Arabia iliyofikiri kuwachukua hata kama wanatenganishwa na km 80 za maji ya bahari ya sham. Huu ni ukweli mchungu lakini ndio ukweli wenyewe. Hakuna aliyewaona kama wanadamu, jirani au waislam. Hakuna!
Hivyo vijana hao wamepata hati za kusafiri kama raia wa nchi husika lakini haiondoi ukweli kuwa ni wasomali. Hakuna suala la kutoka mataifa mbali mbali, ni wasomali waliotokea mataifa mbali mbali na kutumia fursa walizopewa kwa njia chafu na ovu. Walikuwa na option ya kubaki Mogadishuwakakataa sasa tunawaona ''mashujaa''! jamani!
Tatu, Watalii walitekwa na Alshaabaab wakitaka wapewe pesa ili wawaachie. Sijui unataka ushahidi gani zaidi ya huo.Ndege ya Mombasa ilinusurika kutunguliwa, Alshabaab walidai kuhusika kisa ni ndege ya Israel.
Nne, Mharamia ni vijana ambao kwa jina lao halisi ni Alshabaab. Hata kama si wao bado suala linabaki ni wasomali.Kwenye maeneo ya mapambano ya makabila yapo mengine salama kama Baidoa, Putland, na kidogo Hergesa. Sehemu kubwa ya vurugu za Mogadishu ni Alshabaab.
Nne, hakuna anayewakataza wasiishi kama wanavyotaka. Kinachokataliwa ni wao kutaka kuingilia mambo ya nchi nyingine. Haiwezekani waishi Isleigh Kenya, wafanye vurugu Kenya eti waachwe kwasababu wanataka nchi yao.
Wameachiwa nchi yao miaka 20,sasa inatawaliwa kwa kata hata kabla ya majeshi hayajaingia.
Hawa si watu wanaosimamia masilahi ya Somalia ni makundi yenye interest zao. Huwezi kuamini kuwa wanaoendesha shughuli ni matajiri wakubwa na hawataki amani kwasababu kupitia vurugu wao wanafaidika.
Tano, kuhusu kulaumiwa na kuhusishwa kwa dini hapa lazima Waislam wajilaumu wenyewe.
Sikubaliani na dhana ya kutuhumu dini na wanaofanya hivyo mara nyingi uwezo wao wa kufikiri ni mdogo sana.
Nasema waislam lazima wajilaumu kwasababu wamekuwa wanakwepa ukweli kwasababu rahisi.
Kuuhusisha uislama ili kukidhi haja za magaidi ni jambo la kawaida kwa magaidi.
Bahati mbaya waislam wanaingia katika mtego kwa kutokuwa tayari kukemea maovu kwavile tu wameonewa huruma na waovu na waovu wana majina yanayofanana nao na wanatumia maandiko vibaya, who cares! muhimu wanajua aya hata kama wana 'misuse au abuse'' maandiko matakatifu. Utasikia ni wenzetu, ni ndgu zetu! n.k.
Alshabaab wameua sana, wanafanya hivyo kwa mgongo wa dini na waislam wanaonekana kama wameridhika.
Ni ukweli lazima usemwe. Hakuna anayesema maovu wanayofanya kwa kutumia dini, kila mmoja yupo bize kuwatetea kwasababu wana majina tu yanayoonyesha imani fulani.
Nimetoa mifano ya uhalifu wa Alshabaab, hutasikia hata siku moja waislam wakilaani kinyume chake utawasikia wakitetea kwa njia za ajabu na kusikitisha. Hapa jamvini ni mfano mzuri, hakuna anayekataa niliyoorodhesha kama uhalifu wa Alshabaab, zinatafutwa njia za kutetea uhalifu huo.
Hili si kwa Alshabaab ni sehemu kubwa ya EAC na pengine dunia.Ni kosa kubwa kwasababu waislam wanaingizwa katika mitego isiyohusisna na dini na wanaingia bila sababu kwa kutojua au hofu isiyo na mantiki.
Mathalan, znz, aliwahi kutoa maneno Sophia Kawawa.
Hayakuwa mazuri asilani lakini yalizua tafrani sana.
Leo watu wanaumizwa kwa Tindikali umememshikia nani akialaani,sababu ni tofauti ya Iman kitu ambacho hakipo katika uislam. Watu wanakubali uhalifu kwa kuhusisha na dini hata kama wanajua si sahihi, kinyume chake wanahamaki na kurukia mambo yasiyo na mantiki.
Ukiuliza unaambiwa kuna aya so and so ambayo haina uhusiano na upuuzi au uovu bali kujenga tu mazingira ya kutetea uovu kwa kutumia dini. Matumizi haya mabaya ndiyo mtego ambao watu wameingia na kuingiza dini bila sababu za maana. Tukumbuke kuna watu wanaoamini dini na kuna dini, hivi ni vitu viwili tofauti kabisa
Ustadh alisema Qisas kimerhusiwa, ''tafuta…kata kichwa kwa siri''.
Leo watu wanamwagiwa tindikali hilo linaonekana sawa na watu wamekaa kimya.
Wakati huo huo watu wameandamana kwasababu mkuu wa Wilaya mwenye jina la Amina kavuliwa hijabu hata kama hakuwa mwislam.
Hoja yangu ni kuwa magaidi na waouvu wengine wanatumia dini ''kuwateka '' waislam kisaikolojia wakijua huo ndio mtego unaonasa kwa urahisi.
Waislam wanatetea uhalifu kwa kutumia dini bila kujua kufanya hivyo ni kutoitendea haki dini.
Inakuwa rahisi dini kuhusishwa kwasababu ya matumizi mabaya yasiliyolingana na maandiko au mfunzo.
The Big, nimalizie kwa swali moja, hivi inakuwaje Somalia yenye 99.9 Waislam washindwe kutumia imani yao kuwaleta pamoja na watumie imani hiyo hiyo kulaani kinachotokea kwingine.
Kwanini waislam wadhani kuna uhalifu uliofanyika Libya kwa akina mama na watoto wasifikirie miaka 20 ya uhalifu kama huo Somalia?
Naomba unipe shule na elimu kidogo.
Hivi kusema hili jambo ni baya na ovu kunamuondoa mtu katika imani au kunamwimarisha?
Hivi mtu ana qualify vipi kiiimani, anaposimamia haki na ukweli au anapotumia imani kuficha haki na ukweli?
Sub'hana ALLAH..
Mkuu
Nguruvi3 umekuja na hoja maridhawa sana,
Na mara nyingi huwa naburudika sana kujadiliana na wewe kwani huwa naenjoy hasa pale napokusoma kwa undan hisia zako,kama vile nakuona vile,insha allah na tuendelee...
Nakujibu swali lako linalosema ya kwanba
1.
INAKUAJE SOMALIA YENYE WAISLAM 99.9% WASHINDWE KUTUMIA DINI YAO KUWALETA PAMOJA BALI WANATUMIA IMANI YAO KULAANI KILICHOTOKEA SEHEMU ZINGINE??
JIBU;
Somalia ya kusema kwamba wako 99.9% muslims washindwe kuungana unaweza ukawa una hoja kubwa katika hilo jambo mimi naomba nilizungumze kwa muktadha wa kipekee kidogo,
Ukiona watu wa iman moja na asili moja,wanashindwa kuelewana na kuungana lazima ujiulize swali la uhalisia sana,ya kwamba kuna nini kinawapelekea kuwa ivo??
Nin chanzo cha migogoro yao??iman yao au nin haswa??
Uislam kama uislam ni mfumo wa maisha unaohubiri amani na upendo,
Uislam ni mfumo unaojipambanua katika nyanja mbali mbali ikiwemo za kifamilia mfano ndoa,mirathi,n,k
Kibiashara,kibenk,kiulinzi,na kadhalika,kwa ufupi ni mfumo ulioweka namna ya kuendea kila kitu kinachomgusa mwana damu na maisha yake,na yule ambae anausoma na kuufuata kikamilifu huwez kumskia anaangukia kwenye hali ya mtafaruku na vurugu kwa namna moja ama nyingine,
Uislam pia haujampa muislam unyonge wa kutokujitetea pale anapoona anadhulumiwa na kuhatarishiwa maisha yake bila makosa ya aina yoyote,umemruhusu mwanadam kujilinda na kujitetea uhai wake pale anapohis unachukuliwa bila kudhuru nafsi za watu wasio husika na wasio na makosa,
Pia uislam unaruhusu kisas kuwa ni haki lakini kwa kuangalia mipaka yake,na inaruhusu pia kusamehe ni bora zaid kwani mungu ndie mwenye hekima zaid(SAMAHANI KWA KUKUHUBIRIA DINI KIDUCHU)
Kwaiyo sasa,hoja ya kusema kwanin wasomali 99.9% ni waislam wanashindwa kutumia iman yao kuwaunganisha,mimi nakujibu kwamba kipo kitu kinawapelekea kuwa ivo,either kutofuata mafundisho na kuusoma uislam unataka nini,ama kugawanywa na kutawaliwa na watu wa nje wenye interest na ardhi yao kama kulivofanywa miaka 20 iliyopita,
Pia nguruvi3 al akhiy,unakosea sana unaposema ya kwamba Marekani kaondoka pale sasa yapata miaka 20..!!,suala si kuondoka,suala ni kwamba kaacha nin baada ya kuondoka,na alipakuta vipi wakati anaenda au palikuwa vipi kabla hajaenda,NAONA HAPO UMEFANYA TENA KOSA LA KUDISCUSS OUTCOMES...!!
WAISLAM KUFIKIRIA UHALIFU UNAOFANYWA NCHI MFANO WA LIBYA NA KUTOFIKIRIA ULE ULIOFANYWA SOMALIA MIAKA 20 ILIYOPITA SIO HOJA SANA NGURUVI3,
Hoja hapo ni kwamba nin chanzo cha uhalifu huo??ni uislam au watu husika??
Kimfano kama wasomali wanapigana vita vya koo kwa koo,ni kusema kwamba uislm ndio umewaamrisha ivo au ubinadam wao??waislam si wasomali peke yao dunian,na haukuanza huko somalia,kwaiyo waangaliwe kwa muktadha huo.
Concerning non violence,its a crime kuwaambia watu wasichukue tahadhari kwa pale wanapoona wanakuwa victims of constant brutal attacks kutoka kwa jamii ya watu wengine,,
Hilo la Tindikali zanzibar na sehemu zingine,mfano umefanya case study yako hapa TANZANIA,MIMI KAMA MUISLAM NAWEZA KULIPANGUA KUWA ATAFUTWE MCHAWI katika HILO,na mchawi uislam,
Kwan zanzibar kumekuwa na makanisa na ukristo kwa miaka mingi sana,na waislam na wakristo wamekuwa wanaish kwa aman kwa miaka mingi sana,haya mbona tunakuja kuyaskia leo?yametoka wapi??
Ni uislam umebadilika kimafunzo au kuna jambo lipo nyuma ya camera??
Uislam ni ule ule,haujabadilika tokea zama hizo,hauna versions,haya yametokea wapi??
Needless to say,sio tuh wakristo wamekutwa na dhahama hiyo,hata masheikh wameshawahi mwagiwa tindikali,lakin hakuna alieamua kunyooshea kidole iman ya mtu mwingine kwa kuwa tunajua fika iman zetu hazifundishi ivo,sasa kwanin mchawi asitafutwe tuishie kunyoosheana vidole??
Ndio kwa maana siku zote mimi nasema kwamba tusome iman zetu,tuyafanyie kazi mafundisho yetu,na tujifunze kuvumiliana katika jamii yetu,
PIA KABLA YA KUTAFUTA SULUHU YA MAMBO TUSIKIMBILIE KUANGALIA TU OUTCOMES,BALI TUANGALIE PIA NIN CHANZO??
TAREJEA BAADENI UKINIHITAJI,SHUKRANI.