Dunia ijadili chanzo cha ugaidi sio matokeo yake

Dunia ijadili chanzo cha ugaidi sio matokeo yake

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
17,182
Reaction score
16,866
Watu wetu wengi wasio na hatia wanapoteza maisha na viungo vyao kutokana na ugaidi, hii inauma, lakini inauma zaidi kuona dunia iko kimya kujadili chanzo halisi cha ugaidi duniani, badala yake tunalia na matokeo ya ugaidi tu. Hii ni ngoma ya 'do me do you', kama Marekani yenye nguvu ilishindwa vibaya huko Somalia enzi zile, je, Kenya? al-shababu na 'magaidi' watasambaratisha maisha yetu na chumi zetu tusipokuwa waangalifu na ugaidi. Tunacheza ngoma tusizozijua vema. kenya ondoka Kenya, vinginevyo uchumi wako utasambaratika kabisa kama Uchumi wa marekani unavyoyumba sasa kwa kuwasaka magaidi duniani.

Kwanini chanzo cha ugaidi hakisemwi huko the Huge?
 
Chanzo ni kutoheshimu imani za wengine. Haswa hawa jamaa zetu wa . . . . . . .
 
Watu wetu wengi wasio na hatia wanapoteza maisha na viungo vyao kutokana na ugaidi, hii inauma, lakini inauma zaidi kuona dunia iko kimya kujadili chanzo halisi cha ugaidi duniani, badala yake tunalia na matokeo ya ugaidi tu. Hii ni ngoma ya 'do me do you', kama Marekani yenye nguvu ilishindwa vibaya huko Somalia enzi zile, je, Kenya? al-shababu na 'magaidi' watasambaratisha maisha yetu na chumi zetu tusipokuwa waangalifu na ugaidi. Tunacheza ngoma tusizozijua vema. kenya ondoka Kenya, vinginevyo uchumi wako utasambaratika kabisa kama Uchumi wa marekani unavyoyumba sasa kwa kuwasaka magaidi duniani.

Kwanini chanzo cha ugaidi hakisemwi huko the Huge?


well said
 
Kenya alichokipanda ndicho anachovuna sasa asitegemee atabaki salama , nahiyo tone lamaji ndani ya bahari
 
Chanzo cha ugaidi duniani ni Marekani kwani Kiongozi Mkuu wa Ugaidi OSAMA BIN LADEN alipewa mafunzo maalum Marekani na wakamtumia katika mambo yao mengi waliposhindwana wakageukana akawa adui. na kwa uhalisia na matukio ya mwanzo kabisa yalianzia kwa hawa waarabu against Marekani na Islael Why?
 
Kenya alichokipanda ndicho anachovuna sasa asitegemee atabaki salama , nahiyo tone lamaji ndani ya bahari

Wewe utakuwa umelaaniwa, hivi unachoshabikia hapa ni nini? kumbuka hao watekaji nao hata kama wapo hai hadi sasa lakini ni maiti zilizosimama kwani hawatapona kamwe na nashangaa sana kwa hawa watu kukubali kutumika kipumbavu kiasi hiki huku ukijua kabisa kufanya operation kama hiyo ni kujiingiza katika hukumu ya kifo huko kiongozi wao ALLI MOHAMED RAGE akiongea na waandishi wa habari huku anakunywa kahawa. na wewe kwa akili zako ukitumwa kama hao wenzako unaweza kujitolea kufanya upumbavu kama huo.

**JAMANI HAPO KWENYE RED HUYU JAMAA NI UKOO MMOJA NA ISMAIL ADEN RAGE?**
 
Pia hizi imani tuwe macho nazo kwa umakini sana,tujaribu kuwa tunafikiria kidogo kwa kutumia bongo zetu,haiwezekani mtu eti uamini kuwa kuua mtu asiye wa Imani yako utakwenda peponi,tena wengi wao wanaouwawa hata hawana hatia,sasa watu kama hawa unawaua kwa kutegemea kuwa utakwenda peponi kweli??,imani gani jamani hizi,kuna walakini mkubwa sana juu ya imani za aina hii,viongozi wa Dini zetu wana jukumu kubwa sana la kuwafundisha waumini wao juu ya kuishi vizuri na wasio wa Imani yao kwa kuwa haiwezekani mkafanana kwa kila kitu,kuvumiliana ni jambo la msingi sana kama kweli utaiheshimu pumzi aliyopewa huyo asiye wa imani yako na MUNGU aliyewaumba nyote ila mkatofautiana imani tu
 
Chanzo ni kutoheshimu imani za wengine. Haswa hawa jamaa zetu wa . . . . . . .

umenena vyema, naongezea sio imani tu, ugaidi ni zao la dhulma na uonevu.
Hebu jiulize, mtu akiwauwa wazazi wako, kakufanya mkimbizi ndani ya nchi yako, kabomo nyumba, shule ulokuwa unasoma, kawajeruhi nduguzo kawaacha vilema.
Maisha yako yote kayavuruga, je utaona manufaa ya kuendelea kuwa hapa duniani?
Utasita kumfanya lolote upatapo nafasi?
 
Chanzo ni kutoheshimu imani za wengine. Haswa hawa jamaa zetu wa . . . . . . .

umenena vyema, naongezea sio imani tu, ugaidi ni zao la dhulma na uonevu.
Hebu jiulize, mtu akiwauwa wazazi wako, kakufanya mkimbizi ndani ya nchi yako, kabomo nyumba, shule ulokuwa unasoma, kawajeruhi nduguzo kawaacha vilema.
Maisha yako yote kayavuruga, je utaona manufaa ya kuendelea kuwa hapa duniani?
Utasita kumfanya lolote upatapo nafasi?
Ndivyo ugaidi unavyotengenezwa duniani kote.
 
kama dunia itakua inafuatilia matokeo tuu tutegemee maafa zaid
 
Wewe utakuwa umelaaniwa, hivi unachoshabikia hapa ni nini? kumbuka hao watekaji nao hata kama wapo hai hadi sasa lakini ni maiti zilizosimama kwani hawatapona kamwe na nashangaa sana kwa hawa watu kukubali kutumika kipumbavu kiasi hiki huku ukijua kabisa kufanya operation kama hiyo ni kujiingiza katika hukumu ya kifo huko kiongozi wao ALLI MOHAMED RAGE akiongea na waandishi wa habari huku anakunywa kahawa. na wewe kwa akili zako ukitumwa kama hao wenzako unaweza kujitolea kufanya upumbavu kama huo.

**JAMANI HAPO KWENYE RED HUYU JAMAA NI UKOO MMOJA NA ISMAIL ADEN RAGE?**
kwaiyo rage ni......
 
ugaidi ni fikra potofu ambayo wajanja huwaubiri vijana na kuwapa mafunzo ya kiiman na wao kwa kuwa wamekulia katika iman hiyo ubadilika kitabia kufuatana na mwenye mafunzo kumteka akili na kifkra; hata hivyo wanaojitoa muhanga wengi ni umri ndogo hawana familia hawategemewi hivyo huona sana tu kufa si hasara kwao. Angalia kwa makini hawa wamerekani wanavyopenda uhai kwa sababu wanamaisha mazuri, nchi zenye kukumbatia ugaidi ni maskini sana au zinatafuta haki sana
 
Wale mapadri waliopigwa risasi pale Zenj na kumwagiwa tindikali ni copycat ya itikadi hii
 
Chanzo cha ugaidi duniani ni Marekani kwani Kiongozi Mkuu wa Ugaidi OSAMA BIN LADEN alipewa mafunzo maalum Marekani na wakamtumia katika mambo yao mengi waliposhindwana wakageukana akawa adui. na kwa uhalisia na matukio ya mwanzo kabisa yalianzia kwa hawa waarabu against Marekani na Islael Why?

Osama ni nadharia iliyotengenezwa na Mmarekani kuteleza hujuma zake dhidi ya uislamu.
 
Chanzo cha ugaidi duniani ni Marekani kwani Kiongozi Mkuu wa Ugaidi OSAMA BIN LADEN alipewa mafunzo maalum Marekani na wakamtumia katika mambo yao mengi waliposhindwana wakageukana akawa adui. na kwa uhalisia na matukio ya mwanzo kabisa yalianzia kwa hawa waarabu against Marekani na Islael Why?

Hilo lipo wazi,SAVIMBI,GARANG na hata kwenye list ya hawa vijana wengi wametoka marekani!!!chanzo cha ugaidi duniani ni United States of America
 
Back
Top Bottom