The big, Tatizo la Somalia linakuwa unique kutokana na ukweli kuwa sababu zenye kuleta mifarakano hazipo na hilo lingewasaidia kupambana na majaribu mengine .
Kilichomuondoa Siade Barre si Marekani, ni watu wa koo yake mwenyewe kutokana na mgawanyo wa madaraka.
Endapo zipo sababu za nje, hizo ni ndogo kulinganisha na zile za ndani za kina Farah Aideed n.k.
Kinachoendelea Somalia ni makundi ya Wasomali kutumia vita kupata mafao. Matajiri wakubwa wa Somalia walioko USA, UK, Canada, Norway na Sweden ndio wafadhili wakubwa wa vita.
Kutotawalika kwa Somalia ni mafao kwa baadhi ya watu.
Kudhani kuwa Somalia inanyemelewa ardhi yake na Marekani si kweli.
Kugawanyika kwa Wasomali hakutokani na kushambuliwa kwasababu ya imani yao au kabila zao.
Ukweli ni kuwa katika darsa uliyotoa kuhusu Uislam, Wasomali hawana la kujivunia isipokuwa mambo mawili.Moja ni hilo la kutumia fursa ya kutoonewa kuhalalisha uhalifu na pili, kutumia Kisasi kuhalalisha uhalifu.
Ile maana nzima uliyonena ya 'mfumo mzima wa maisha' haiwagusi wasomali.
Makundi kama Alshabaab ni matokeo ya kuuchukua Uislam na kuutengeneza katika njia zao ili zikidhi matakwao yao kinyume na Uislam wenyewe.
Hivi unazuiaje mtu asitumie Mbolea ukiwa na kipaza sauti kimeandikwa made in UK, tena juu ya Toyota na AK47 kutoka Russia. Hapo kuna uislam wa aina yoyote kama si upotoshaji.
Wapi na lini Uislam umezuia matumizi ya Mbolea.
Endapo dhana ya kujitetea pale unapoonewa ingekuwa inatekelezwa, uonevu na mauji yangeshasita Somalia.
Kwanini wananchi wasijitetee dhidi ya wahuni wachache wanaovuruga Somalia.
Kwanini kujitetea kuje kwa kubomoa mall za nchi nyingine. Kujitetea gani huku kusikojali maisha ya akina mama na watoto wa Mogadishu
Hata kisasi unachosema kimeruhusiwa, hivi kuua vijana waliofuzu mafunzo ya udaktari, au kunyang'anya watu mali zao kama mifugo ni kisasi cha nani dhidi ya nani. Kwamba Alshabaa wamepewa haki hiyo kuliko wasomali wengine?
Hili la kutumia hoja za kisasi na kujitetea ndilo linaitafuna znz pia.
Hakuna mabadiliko ya Uislam bali yapo mabadiliko ya mafunzo ya Uislam znz.
Huko ndiko kunapelekea chuki zinazoonekana za kipuuzi. Tindikali kwa sheikh ilisemwa ni kupambana na dhalimu! sijui nani amepewa vigezo vya usafi na udhalimu.
Baada ya kupambana na udhalimu na kuachiwa, wakaingia 'wanazuoni' na kuhubiri kisasi.
Wakapandikiza chuki dhidi ya watu halafu wakatoa hukumu kuwa ni muafaka '' ukionewa na askari' bila kujali chanzo cha tatizo wewe tafuta' .... mkate kichwa kwa siri''.
Sasa hivi wantekeleza mafunzo waliyopata kwa kumwaga tindikali watu walioambiwa ndio wawe target.
Bado tunatafuta sababu za ujinga kama huo tukijua ni wajinga waliofanya. Hivi kuna cha kujali kuhusu ugaidi znz?
Mafunzo ya ajabu namna hiyo hayawezi kuleta muafaka katika jamii. Tatizo la znz si Uislam ni kundi la wahuni lililoteka ajenda ya Uislam na kujifanya ni waislam zaidi kwasababu za kisiasa na kijamii.
Kwabahati mbaya sana kama ilivyokawaida ya waislam, kwao ni muhimu kutetea jina hata kama liafanya uovu.
Ukiangalia misimamo ya Alshabaab na Uamsho hakuna tofauti. Wote wamefanikiwa kutanguliza ngao ya Uislam huku nyuma wakifanya uasi na maovu makubwa. Uislam hausemi kuhusu mwanadamu kumdhuru mwanadamu mwingine. Wewe umesema ni amani na upendo, sasa kuna amani gani na upendo gani kwa Uamsho na Alshabaab.
Ni kwa msingi huo waislam wanakuwa 'victims of circumstance' kwasababu, kwanza hawasimami katika Uislam wenyewe na message yake. Wanasimama katika majina na kusomewa mambo na baadhi ya watu.
Pili, wanashindwa kusimama na kusema this is right, this is wrong kwasababu wameshafungwa kiakili kuwa ukisema hili ni kosa unakuwa msaliti.
Tatu, wengi wanakuwa washabiki badala ya kuwa waumini. Kuvuliwa hijabu Amina asiyelazimika kuivaa kwasababu si mwislam hakuwezi kuzua hisia kuliko Padre aliyepigwa risasa na kufa, na wengine kujeruhiwa au sheikh alkiyemwagiwa tindikali.
Hakuna rationale ya kuangalia kipi kinasimama katika dini na kipi ni 'fanaticism'.
Message wanayopata watu wengine ni kuwa mambo hayo maovu yanaungwa mkono na waislam.
Kwavile yamekuwa yanajirudia sana sasa inaonekana kama sehemu ya Imani.
Kosa si la anayeoona bali ni la wale wanaofanya ionekane.
Unajua Nguruvi3,
We una akili na busara nyingi sana,
Namimi siku zote huwa napenda sana kufanya mijdala ya kuwekana sawa na watu sampuli yako,kwa kuwa naamin huwa najifunza mengi sana,
Tufanye CASE STUDY KENYA KWA TUKIO LA WASTEGATE MALL,
WAKENYA kama wakenya,kwa UTAIFA wao wamejua tatizo ni nin..
Wamejua tatizo si uislam wala si waislam,
Wamejua kwanin Alshabaab kavamia nchi yao,na wamejua wao kama TAIFA Kwa pamoja wachukue jukumu gani kuliendea hilo,
NDIO KWA MAANA UKAONA PALE MASHIEKH,MAASKOFU NA MAPADRI WALISIMAMA KWA PAMOJA KWENYE PRESS na kulaani bila kuwekeana duku duku ndan ya mioyo yao na nafsi zao ya kwamba lile lililofanyika ni tukio la kulaaniwa na dini zote kwa ujumla zinakemea mambo yale,
Hata Sheikh wa kenya na viongoz wengine wamelisema pale,tena wakasema kabisa kutoka kwenye mafundisho linazungumzwaje lile,
Sikuona hata mkenya mmoja kuanza kuwaanyooshea vidole watu wa iman zingine kwa namna yyte ile,na ule ndio UTAIFA NA ULE NDIO UELEWA WA MAMBO.
Uislam umesimama katika nguzo zake kuu,na miongon mwa kitu kikubwa ambacho kimepewa msisitizo katika uislam ni elimu,
Japo najua kuna watu wengi wako Brainwashed ya kwamba waislam ni watu wenye kuikimbilia elimu na kuconcentrate katika mambo yahusuyo dunia ya baadae baada ya kufa,hilo si kweli nawewe nguruvi3 najua si miongon mwao.
Kuna Jamaa mmoja anaitwa 'ALKHAWARIZM'
GOOGLE na utafute habari zake,huyo ni miongon mwa Great Mathematicians kuwahi kutokea na ndie mgunduzi wa hesabu za ''LOGARITHM'' HIZI tunazozitumia kwa manufaa mbali mbali hadi leo,
Bila hesabu za LOGARITHM hizi LAPTOP tunazotumia leo ingekuwa historia katika matumiz yake,the MAN WAS A MUSLIM,
ANAEJITAMBUA NA NI MFANO WA WENGI KATIKA ULIMWENGU HUU WALIOPITA.,huyo nimekupa kama mfano tuh,
Sasa naona kuna watu wanazungumza kuhusu waislam na uislam kupuuza elimu au kutia huruma kwa namna moja ama nyingine jambo ambalo si la kweli.
Aya ya kwanza kabisa kushushiwa mtume Mohammad{may peace be upon him} aliambiwa asome,asome kwa jina la mola wake aliemuumba,aliemuumba mwanadam kwa tone ya manii,asome kwani mola wake ni mkarim.ni mola yule aliemjuza mwanadam kwa msaada wa kalam,aliemjuza mwanadam mambo ambayo alikuwa hayafaham,
Na katika muktadha huo hakuambiwa achague elimu za kusoma,ameamrishwa muislam kusoma elimu zote zenye manufaa ya kumfanya aish vema hapa dunian na kumfanya amjue mola wake vema,
So,tunapokuja kuzungumzia mambo ambayo yanaleta mushkil kwenye jamii na kuyatazama katika picha ya dini ni lazima tuangalie hasa je vifungu vya dini vinasemaje?ni watu wanavitumia vibaya,au kuna propaganda mbovu katika hilo?hapo tutapata picha,
Mfano,hii ishu ya Alshabaab,
Wao wamesema wazi,kwamba wameenda kufanya vurugu kenya kwa kuwa kenya kapeleka majesh yake somalia,
Nguruvi3 nakuuliza,Alshabaab kaenda kenya kwa hoja ya kwenda kuupigania Uislam?
Nilikua nasikiliza na kutazama Aljazeera wakati wana muhoji kiongoz wa Alshabaab,alisema waz waz kwamba wako vitan na kenya kwa kuwa kenya kapeleka majesh yake katika ardhi ya somali,na ili suluhu ije basi kenya sharti iyatoe majesh yake somalia,
Je,walisema wana kwenda kenya kupigania uislam ili wakifa wapate MAKIBIRA SABA??NAONA KUNA WATU WANAKUJA NA KEJELI KEJELI KAMA HIZO,SASA KWANIN WAIVUSHE HOJA KUIPELEKA HUKO?
UMEKUJA TENA NA HOJA YA ZANZIBAR NA TINDIKALI,NIMEKUULIZA HUJAONA HATA MASHEIKH WALIODHURIWA NA HALI HIYO HAPA TZ?UMESKIA WAISLAM WAKINYOOSHE WATU WA IMAN ZINGINE?
Au ndio vile waislam wamevuka mipaka mpaka sasa wanajifanyia wenyewe kwa wenyewe?
Nashukuru hapo uliposema ya kwamba kuna watu wanaotoa mafundisho ya chuki na kuegemea katika uislam,hilo nakubali kabisa,
Lakin sasa swali ni kwamba kwanin haya yanatokea leo?
Zaman kwa nin hayakuwapo?tumeshajaribu kuchunguza chanzo ni nin?
Na tunakichukulia hatua zipi??
Uislam umekuwapo tokea zaman sana,
Kipindi cha Mtume kulikuwa na watu ambao si waislam,na hadi anakufa alikuwa anaish na watu ambao si waislam katika jamii yake kwa aman na upendo na hakuwalazimisha kuingia kwenye uislam,kwamba wakikataa wanauliwa,hilo si kweli kama wengine wanavoshadadia,
Mtume aliish na kulelewa na ndug yake,Baba yake Mlezi,hakuwa muislam,na hadi mtume anakufa yule mlez wake hakuwahi kuwa muislam hadi wote wanaondoka ulimwengun,ila waliish kwa aman na upendo,na huo ndio msingi katika uislam
ipo aya katika uislam inasema ''HAKUNA KULAZIMISHANA KATIKA DINI''.HAKUNA KULAZIMISHA MTU AAMIN IMAN FLAN,KILA MTU AWE HURU KUIFUATA IMAN YAKE ANAYOIPENDA''
Kinachofanyika katika uislam ni kuwahubiria dini watu wengine wasio waamin katika uislam kwa hekima na busara,wakikubali ni jambo la heri,wasipoafiki kila mmoja ana maisha yake,na ni marufuku kumlazimisha mtu katika hilo,
Nimeongea mengi sana,ila kikubwa ni kuwekana sawa Nguruvi3.