Dunia ijadili chanzo cha ugaidi sio matokeo yake

Dunia ijadili chanzo cha ugaidi sio matokeo yake

Amani ya kulazimisha huzaa ugaidi. Tanzania tujihadhari.

Li-avatar lako linatisha:

God__TheFather.jpg
 
Mmhhh mie sisemi maana walinisemea wasambaa (mruka gemo aweea kigha)ila niseme marekani kigha chake kilikua kidogo na matunda yake kujifanya anaweZa ni haya yatokeayo sie kama kopo la taka kila kitu tunapokea poleni wakenya lakini choo mlichoingia hakiwafai mtacheka tu
 
Rais JK amesema kakasirishwa sana na kitendo cha Al Shabaab kuua watu huko Kenya,nafikiri ni wakati muafaka wa kupeleka kikosi maalum cha JWTZ huko Somalia kumaliza wahuni wa Al Shabaab,hatuko salama kama Kenya si salama
 
Watu wetu wengi wasio na hatia wanapoteza maisha na viungo vyao kutokana na ugaidi, hii inauma, lakini inauma zaidi kuona dunia iko kimya kujadili chanzo halisi cha ugaidi duniani, badala yake tunalia na matokeo ya ugaidi tu. Hii ni ngoma ya 'do me do you', kama Marekani yenye nguvu ilishindwa vibaya huko Somalia enzi zile, je, Kenya? al-shababu na 'magaidi' watasambaratisha maisha yetu na chumi zetu tusipokuwa waangalifu na ugaidi. Tunacheza ngoma tusizozijua vema. kenya ondoka Kenya, vinginevyo uchumi wako utasambaratika kabisa kama Uchumi wa marekani unavyoyumba sasa kwa kuwasaka magaidi duniani.

Kwanini chanzo cha ugaidi hakisemwi huko the Huge?

Je kama chanzo ni tofauti za kiimani utaweza kutoa solution? Je kama ni dini fulani inafundisha watu wake ugaidi na kuchukia wakristo utaweza kubadili wanachoamini?
 
hakuna vita ya jihad ya kupigana na mkristo/ kafiri. kuna vita inayopiganwa dhidi ya wenye kudhulumu haki za waislamu hiyo ndiyo inyoitwa jihad. kule Uganda kuna Kony anayepigana vita dhidi ya serikali ya Uganda ili iendeshwe kwa amri kumi za Mungu,wanaua,wanabaka,wanateka watoto kuwaingiza jeshini je hawa ni waislamu. mkumbuke tu "bila haki hakuna amani" nawauliza nyie makanjanja Mbowe na Mbatia juzi wamesema "DAMU ITAMWAGIKA KIKWETE AKITIA SAINI JE HAWA NI WAISLAMU?" mnaimbishwa tuuu

......Dogo, umekurupuka kujibu. Hakuna sehemu nilipotaja Jihad, Uislam wala Vyama vya siasa. Nilitaja sababu za Ugaidi kama mleta uzi alivyokuwa akihitaji au sababu hizo zipo 'direct related' na hiyo dini uliohitaja?. Cha msingi ni kwamba ujumbe umekuingia vyema.
 
Mkuu nikuengezee ubeti katika shairi...Watu wa Horn of Africa ni waVisasi visasi walienda Uganda wakalipua kwa sababu ya AU pcs forces only, mbona hawarudi? Awali walitoa ONYO kwa jirani zao zikapuuzwa !!

Mbona unaji-quote na kujijibu mwenyewe khaa..
 
life is Short nimetoa sababu ns sijahalalisha uonevu huo wa waislam kama upo, Ugaidi ulikuwepo toka enzi lakini ugaidi wa leo asilimia kubwa ni madai ya uislam kuonewa, na rudia tena zaidi ya asilimia 90 ya vitendo vya kigaidi dunia vinafanywa na waislam,
Ngoshanyi sijazungumzia jihad hapa nimezungumzia sababu kuu ya ugaidi dunia ni uislam kudai unaonewa, akina cony na wengine wasio waislam pia wapo lakini asilimia kubwa ya vitendo vya ugaidi vinafanywa kwa kivuli cha uislam
Mpendwa PSS za Asubuhi, Tuliza hasira Uislam utaacha matumizi ya Nguvu !! Lakini Waisiliamu wataendelea saka haki zao !! Waisiliamu wataendelea kudai haki za popote walipo. Nafikiri umeelewa!!
Pamoja kujenga Taifa.
 
Mbona unaji-quote na kujijibu mwenyewe khaa..
Ninajaribu kumfahamisha Mh.mmoja humu yakuwa hawa jamaa wa Horn of Afrika huwaga na nature ya visasi haya mambo hayatakwisha na ni ya milele.... Ona walivyojikusanya kutoka pembe zote duniani kuja kuitikia wito wa wandugu zao..!
Yaani vijana wengi wamacha masomo shule maisha bora huko Majuu, wameweza kuja kupambana na kifo!! Very Sad kuingilia maisha ya watu.
 
umenena vyema, naongezea sio imani tu, ugaidi ni zao la dhulma na uonevu.
Hebu jiulize, mtu akiwauwa wazazi wako, kakufanya mkimbizi ndani ya nchi yako, kabomo nyumba, shule ulokuwa unasoma, kawajeruhi nduguzo kawaacha vilema.
Maisha yako yote kayavuruga, je utaona manufaa ya kuendelea kuwa hapa duniani?
Utasita kumfanya lolote upatapo nafasi?

kula 100%
 
Rais JK amesema kakasirishwa sana na kitendo cha Al Shabaab kuua watu huko Kenya,nafikiri ni wakati muafaka wa kupeleka kikosi maalum cha JWTZ huko Somalia kumaliza wahuni wa Al Shabaab,hatuko salama kama Kenya si salama

weeee! msituletee majanga, marekani wenyewe wamewashindwa itakuwa TZ, alshabab sio M23
 
Nami naheshimu sana rai za wengine.
Tumeshahu matukio ya kuteka watalii yalivoathiri sekta ya utalii Kenya? Kenya ingakaa mbali kwa mtazamo upi? Kwamba iwaache tu waendelee na shughuli zao hata kama ina athiri uchumi wao. Haki ya kujilinda inakuwa wapi?

Na sisi tuliwafundisha Polisi wa Somalia kwa nia njema tu. Tukiruhusu Alshabaab watishe basi hakuna aliye salama.
Nakumbusha kuwa majangili nao walikuwa wanatishia kama Alshabaab.
Kwa jinsi Somalia ilivyo haya majina ya Alshabaab kuwa vijana ni ulaghai tu. Viongozi wao ni wazee wengine miaka 50 na 60. Kuna kijana wa umri huo.

Hoja yangu ni kuwa watu wasishabikie matukio ya maafa kama haya. Hili ni tatizo lipo ukumbini kwetu.
Watu wasitafute sababu za kuwapa Alshabaa sababu kwa kusema tujadili uhalifu.
Ugaidi ni uovu tu bila kujali kafanya nani.

Kuna vitu vya kujadili lakini hawa Alshabaab wanaopita mitaani na 'plaizi' na kung'oa meno watu wenye meno ya dhahabu kwa kisingizio cha dini, kugawana mitaa ili kuchukua kodi na hata kuteka meli maana watekaji ni vijana (Alshabaab) leo tujiulize kwanini wanfanya hayo! serious! Tujadili chanzo cha watu walioshindwa kuelewana wakiwa na kila sababu za kuwaunganisha kijamii.
Real! Tujadili hadi upumbavu ili tupate jibu la matokeo! real!

Leo tukimbie na kukubaliana na vitisho vyao badala ya kufikiria kupambana nao.
Kukimbia ni kuwapa ushindi na hawataachi hapo watadai zaidi kwasababu wanajua tunawaogopa.
Nashukuru ubarikiwe Mkuu, Maelezo muwafaka na Sahihi Muhimu zaidi wahusika walishughulikie ipasavyo. Time will Tell.
Good Luck
 
MMM, labda nifunguke kuwa kinachofanyika hapa ni spinning za kutaka kuhalalisha tukio la Nairobi na kukwepa ukweli kuhusu tukio.
Inatafutwa njia ya kuingiza mataifa ya magharibi ili ujengeke uhalali wa uovu.

Watu wanashindwa kujiuliza ni vipi Wasomali ambao kijamii ni jamii iliyo na ufungamano washindwe kuishi kwa amani miaka 20? asilimia 99.9 ni waislam na lugha moja, hawana kabila wana koo na tamaduni zao ni sawa.
Hili ni nyongeza ya swali mleta mada atusaidie ili kutoa mwelekeo wa majadiliano.

Watu wanasahau kuwa Kenya ilishambuliwa katika sekta za utalii na Alshabaab licha ya manshambulizi mengine yaliyotangulia kule Mombasa. Leo equation imegeuzwa wanaambiwa Kenya wanaonekana wabaya

Watetezi wa Alshabaab wana hoja moja inayowasumbua.
Wao wanadhani Alshabaab inapigana vita ya dini dhidi ya watu wa imani nyingine.
Kwasababu au kutoelewa facts na kuzikwepa zingine kwa spinning mara nyingi hujikuta wakiwa mahali pabaya zaidi.

Hakuna dini katika hizi tuzijuazo inayohubiri mauaji na ukatili. Hakuna! kama ipo nitajiwe moja.
Alshabaab wanatafuta sympathy ya kidini na bahati mbaya wasiojua dini wamewaunga mkono na kujikuta wanapaka dini matope. Huu ndio ukweli hata kama utauma. Huwezi kutetea Alshabaab kwa dini na dini ikabaki katika hadhi na heshima yake(Nina maana kufungamanisha dini na Alshabab ni kuichafua dini ambayo haisemi lolote kuhusu Alshabab)

Alshabaab wanasema jino la dhahabu ni haram kidini. Wanapita waking'oa kwa plaizi halafu wanauza meno hayo!!
Alshabaab wanasema ni harama kuangalia soka, wakati huo huo wanaangalia TV kusikia Marekani wanasema nini.
Wanasema ni haramu kutumia vifaa vya magharibi, wanatoa Tanganzo hilo wapo juu ya gari lililotengenezwa magharibi.
Alshabaab wanasema ni haram kutumia msaada wa FAO, wanakusanya magunia ya misaada wanakwenda kuuza nchi nyingine.
Wamefikia mahali wanazuia watu wasitumie mbolea, watumie kilimo cha zamani, njaa ikiuma wanawakimbia watu kwasababu wao wana pesa haram na uwezo wa kujikomboa.

Sasa anapotokea mtu na kudhani tunapaswa kujadili hawa wapuuzi ili tujue chanzo cha hasira zao inasikitisha.
Katika hayo hapo juu kipi unaweza kukiweka mezani ukasema kina mashiko.

Alshabaab si watetezi wa dini. Ni wahuni na wapuuzi wachache, kuwaunga mkono ni upuuzi kuliko upuuzi wao.
Hawana sababu ya kuulizwa wana chuki gani kwasababu hawana hata moja bali wamejaa ujinga na upumbavu.

Nashawishika kuamini unachokisema, lakini napata shida sana kwa sababu zifuatazo,
1.Kwanini hawa washukiwa wa ugaidi wanaoonekana kuwa mobilised sehemu mbali mbali duniani?
2.Kuwepo kwa taarifu toka kwa wachache waliosalimika ndani ya Mall kuwa waliachiwa baada ya kugundulika kuwa ni waislamu?
Pamoja na kuwa unajaribu kuondoa dhana ya udini lakini bado mzunguko unarudi palepale.
 
Usiongozwe na hamaki, soma nilichoandika vizuri.
Sijakutisha bali ilitokea. Nimeweka mfano wa majangili waliokuwa wanauaa Arusha watu na wanyama pori.
Sekta ya utalii nchini iliingia doa kama ilivyokuwa ya Kenya.
Hatuongei kwa nadharia, tuna mifano na huo ni mmoja wapo.

Ukishakubali kuwa alshabaab wana haki ya kuteka meli, wana haki ya kuteka watalii utakataa vipi siku watakapodai haki yao ya kumiliki tembo Arusha? Umeelewa dhana nzima?


Ukishakubali kuwa Alshabaab wana haki ya kutungua ndege Mombasa, utawanyima vipi haki yao ya kutungua ndege JNIA?
Huu ni uovu usiohitaji certificate au diploma kuulani. Ni vitendo vya uhayawani kwanini tuvipe promotion?
Wameingia mall na kuua hadi watoto, bado tunadhani upo umuhimu wa kuwasikiliza.
Miaka 20 hawajaweza kusikilizana wao wenyewe kwa wenyewe wakiwa na kila sababu za kijamii kuwa taifa moja, vipi unadhani wataweza kuisikiliza dunia?

Nguruvi3
With all of my due respect,nashukuru kwa kunialika nije hapa kuzunumza nawe,naam nimekuja tuzungumze kwa hoja na kindugu,


Kwanza kabisa naomba nitamke sipo hapa kuwatetea alshabaab wala sipo hapa kuwaunga mkono serikali ya kenya,
Pia katika kusherehesha hoja yako,either unipe uthibitisho ya kwamba hao wanaohusika na utekaji nyara wa meli,uharamia na mapigano ya wenyewe kwa wenyewe ni Alshabaab,naomba kama uthibitisho unao,uweeke hapa na kama hauna basi nami nachelea kusema kwamba unazungumzia watu wawili tofauti,
Ni kweli wapo wasomali wanaopigana wenywe kwa wenywe kwa vita vya kikabila hadi kufikia hatua ya kuwa wakimbiz na ni kweli wakati mwingine kenya imekuwa inawapokea,

Wasomali ni wasomali,wapo waumin wa dini mbali mbali,ikiwemo christians,muslims na kadhalika,

Hoja kuu ya alshabaab katika miaka hii ya enzi zao za kuchomoza kwao ni kutaka ufreee katika ardhi yao kuish kwa namna ambayo wao wanaona ni bora kuishi nayo,na kutokuingiliwa kwa jumuiya ya mataifa kwa interest zingine ambazo si kweli kwamba ni kwa minajili ya kwenda kurudisha aman,mi na wewe tutakubaliana kabisa kabisa kwamba America hawez kutia mguu sehem yyte bila ya kuwa na maslahi yake kwa namna moja ama nyingine,hilo liko wazi.


Mimi naungana na mtoa mada ya kwamba hapa tusidiscuss outcomes,tuangalie nini ni chanzo cha hayo yote yanayotokea hadi kufikia umwagaji damu na uvunjifu wa aman na mauji ya watu wasio na hatia,

Umeona hapo juu ni kwa jins gani baadhi ya watu walipokuja kuushutumu uislam moja kwa moja ya kwamba waliofanya ivyo wamechochewa na uislam pamoja na mafundisho ya iman yao,kitu ambacho si cha kweli,


Sote tunajua alqaeda ni nani,na nani kaianzisha na ni vipi uhusiano ulikuwapo baina ya osama na marekani kabla ya kuhitilafiana.

Sote tunafaham nani ni TALIBAN,ALIKUWA ANAFANYA NIN AFGHANSTAN hadi marekani kawavamia na kuwaita magaid ili hali kwa sasa amerudi nyuma na kumwambia ahmed karzai akae azungumze nao,tunashuhudia kila leo viongoz wakuu wa taliban waliokashikwa kwa hila,marekan anashinikiza waachiwe huru ili waje kukaa kwenye meza ya mazungumzo,wanahitaji mazungumzo gani na magaidi??nadhan ukweli uko wazi na unafahamika.


Hiyo ya kusema Alshabaab kutungua ndege mombasa ushasema ni tetes na sio kweli,na hilo la kusema la uharamia na utekaji nyara pia sio kweli,wao wako na mission maalum na wako wazi especially pale yanapofanyika mashambuliz moja kwa moja huwa wanakuja kutoa tamko ya kwamba wao wamehusika,

Kwa mantik hiyo basi,mimi naweza kusema kwamba propagnda ziangaliwe vizuri na iman ziangaliwe kwa umakini,na pale tunapoamua kukemea umwagaji wa damu tukemee kote kote bila ya kuangalia wapi unafanyika uovu huo,

Alshaabab wanasema kwamba wao wana vita na kenya kwa kuwa kenya kapeleka majesh yake katika ardhi ile,na ile ni ardhi yao,we unasema kwamba kenya imekwenda kule kwa kuwa alshabaab walikuwa wanatishia usalama na biashara ya utalii ukanda wao,uthibitsho uko wapi ya kwamba wanaofanya ivo ni wao??wapo wasomali wengi ambao kwa namna moja ama nyingine hujihusisha na uharamia na vita vya kikabila,lakini kwakuwa anaefahamika kwa ukanda huo ni alshabaab basi propaganda zinajengwa kuonesha wao ni wahalifu,sawa,kwa namna yyte ile iwavyo tuzungumze nin chanzo cha hayo yote,


Hoja ni kwamba mauaji mengi yanafanyika huko somalia,kina mama na watoto wanauwawa na serikali za ushirika na kenya yakiwemo majesh yao,lakini huwez kuiskia BBC & CNN wakilielza hilo,ila sasa kwakua pale WASTEGATE waliouwa ni wengi wakiwemo na wazungu na raia wa nchi mbali mbali wao lazima walipoti,

Nadhani umeiona ile list ya wale vijana waliofanya shambuliola utekaji kuwa ni vijana kutoka mataifa mbali mbali ikiwemo kenya,uingereza,marekani na kadhalika,umejiuliza ni kwa nini??

Tusipokuwa makin media zinaweza kutufanya tuwachukie wasiostahili kuchukiwa na kuwapenda wanaostahili kuchukiwa,

Ghadaff(marehemu) pamoja na maovu yake yote,tuseme kipi kimewapa uhalali wazungu kuvamia nchi ile na kuharibu hali ya hewa katika ardhi ile??watoto,wanawake na watu wasio na hatia wameuwawa kwa sababu zisizo za msingi,mbona hatuoni jumuiya ya kimataifa ikipiga kelelekuhusu suala lile hadi mauaji yalipotokea??


Au ndio kusema kwa kuwa thaman ya uhai wa wanadamu wale haulandan na thaman ya mafuta waliyokawa wanayahitaji??

Au kwa kuwa wanaoish kule asilimia kubwa ni watu wa iman flan ambayo inasemekana wamezoea sana vurugu vurugu??

TUNAPOJADILI MAMBO YANAYOUMIZA KAMA HAYA,TUEPUKA KUJADILI KUHUSU OUTCOMES,TUJADILI SANA CHANZO CHA HAYO YOTE.
 
Last edited by a moderator:
Watu wetu wengi wasio na hatia wanapoteza maisha na viungo vyao kutokana na ugaidi, hii inauma, lakini inauma zaidi kuona dunia iko kimya kujadili chanzo halisi cha ugaidi duniani, badala yake tunalia na matokeo ya ugaidi tu. Hii ni ngoma ya 'do me do you', kama Marekani yenye nguvu ilishindwa vibaya huko Somalia enzi zile, je, Kenya? al-shababu na 'magaidi' watasambaratisha maisha yetu na chumi zetu tusipokuwa waangalifu na ugaidi. Tunacheza ngoma tusizozijua vema. kenya ondoka Kenya, vinginevyo uchumi wako utasambaratika kabisa kama Uchumi wa marekani unavyoyumba sasa kwa kuwasaka magaidi duniani.

Kwanini chanzo cha ugaidi hakisemwi huko the Huge?


chanzo ni waisilam wanataka watu wote wawe waisilamu, na serikali zote duniani ziwe za utawala wa kiisilamu! na sharia zitumike sio common laws. mkuu hicho kitu hakiwezekani na ndo kama umefuatilia issue ya kenya target ya kwanza ilikuwa migahawa inayomilikiwa na waisraeli na mashuhuda wamesema militants walikuwa wanasema walio waisilam simameni na ondokeni!!
 
Chanzo kikuu cha ugaidi ni dini ya Uislam kudai inaonewa na kuhujumiwa duniani kote.........period
Asilimia zaidi ya 90 ya vitendo vya kigaidi duniani vinafanywa na waislam


First of all,you have to define terrorism properly,


What is terrorism???Who is a terrorist??

What is islam??Who is Muslim??What does islam say concerning terrorism??


You have to define it properly,


Who started the first world war??muslims??

Who started the second world war??muslims??

Who killed about 20 milions of Aborigines in Australia?muslims??

Who sent the nuclear bombs of hiroshima and nagasaki??muslims??

Killed more than 100 millions of indians in north america?muslims??

Who killed more than 50 millions of indians in south america?muslims??

Who took more than 180 millions of african people as slaves and 88% of them died and were thrown in Atlantic ocean?muslims??

Who is fighiting the war with the lord resistance army in uganda??muslims??

NO,NOT MUSLIMS...!!

So,you have to define terrorism properly,

If a non muslim does something bad,it is crime,but if a muslim commits the same is a terrorist...
 
.. kiongozi wao ALLI MOHAMED RAGE akiongea na waandishi wa habari huku anakunywa kahawa.
**JAMANI HAPO KWENYE RED HUYU JAMAA NI UKOO MMOJA NA ISMAIL ADEN RAGE?**

Kwa vile Somalia wanatambuana kwa koo, nakubaliana na swali lako elekezi, yaani ni 100% bila chenga. Siku Tanzania tukiingia kwenye mchafuko ndo tutajua nani mtanzania, nani mkimbizi na nani mhamiaji haramu!
 
First of all,you have to define terrorism properly,


What is terrorism???Who is a terrorist??

What is islam??Who is Muslim??What does islam say concerning terrorism??


You have to define it properly,


Who started the first world war??muslims??

Who started the second world war??muslims??

Who killed about 20 milions of Aborigines in Australia?muslims??

Who sent the nuclear bombs of hiroshima and nagasaki??muslims??

Killed more than 100 millions of indians in north america?muslims??

Who killed more than 50 millions of indians in south america?muslims??

Who took more than 180 millions of african people as slaves and 88% of them died and were thrown in Atlantic ocean?muslims??

Who is fighiting the war with the lord resistance army in uganda??muslims??

NO,NOT MUSLIMS...!!

So,you have to define terrorism properly,

If a non muslim does something bad,it is crime,but if a muslim commits the same is a terrorist...

Haya ndo tunaita MAJANGA! Uelewa wa namna hii ni HATARI kwa usalama wa Dunia. Kama watu wanashindwa kutofautisha aina za MAJANGA kwa sifa zake na vyavzo vyake basi na wao ni MAJANGA! Hii ni kwa sababu ya kuwa na undugu na mapepo!
 
Mpendwa PSS za Asubuhi, Tuliza hasira Uislam utaacha matumizi ya Nguvu !! Lakini Waisiliamu wataendelea saka haki zao !! Waisiliamu wataendelea kudai haki za popote walipo. Nafikiri umeelewa!!
Pamoja kujenga Taifa.

Huko Iraqi, Afganistani na Pakistani zote ni nchi za kiislamu, lakini inakuwaje wanalipuana misikitini kila kukicha, wanadai haki kwa nani? Mwl. JKN alipata kusema "...ukimbagua mwenzako,... dhambi ya ubaguzi haita kuacha, itakutafuna tu...!" He was VERY CORRECT-RIP Mwl. JKN.
 
na zile risasi sheikh Aboud Rogo na wale waislam 7 waliokuwa wakitoka msikitini walivyo uawa labda ndio muendelezowake .


Tena huyo Sheikh Rogo walimchelewesha,ni kama yule wa kwetu ambaye anapreach hatred kwenye Utube,kuua mapadre au maaskofu.
Nawasifu Jews huwa,wana get rid hawa vilaza mapema sana.
 
Back
Top Bottom