Freightliner
JF-Expert Member
- Aug 22, 2013
- 720
- 528
Dr wilbroad peter slaa
Wakati gazeti la Nipashe likianzisha kura ya maoni miongoni mwa wana-CCM wanaotajwa kuwania kuteuliwa na CCM kuwakilisha chama hicho katika uchaguzi mkuu ujao kwa lengo la kugombea nafasi ya uraisi kupitia chama hicho na huku bwana Lowassa akiongoza kwa kura,nafikiri ni busara na sisi kupitia mtando huu wa JF kumpambanisha bwana Lowassa na Dr. Slaa katika kinyang'aricho hicho cha uraisi kwa mwaka 2015.
Tupige kura kwa kuandika jina tu la mgombea unaedhani atafaa kuwa raisi endapo itatokea hao wawili wanateuliwa kuviwakilisha vyama vyao katika uchaguzi mkuu ujao.
NB😛iga kura bila kuendesha campaign yoyote.
------------------------------------------------------------------
*Kwa maoni zaidi ya washiriki wa JamiiForums kupitia ukurasa wa Facebook - Dr. Wilbrod Slaa Vs Edward Lowassa (JamiiForums facebook page)
CHAMVIGA, kwani taabu nini? Si upige tu kura kwamba wote hawafai? Mnavyohatamia kujibu posts kinazi, mtu atadhani mko wengi...haya sasa, onesheni kwa vitendo. Piga kura! Safari hii mods wamefanya jema kweli, hakuna kutumia IDs zaidi ya moja, ukishapiga kwa ID moja hupigi tena labda uwe na IP address, server au VPS nyingi tu...safari hii imekula kwenu.Hao wote ni wadini/wakatoriki hawapaswi kuongoza hii ni wabaguzi mno.
'out of context' hawa ni wanasiasa wawili tofauti kabisa, kuwa fair pambanisha ccm vs cdm, au kama nipashe watoke chama kimoja, vinginevyo panua wigo mbowe, mbatia, lipumba, dk shein, nk.
Dr.SLAA -SI MWIZI
Usitake kulisha watu ----- huna unachokijua kuhusu TEC,hizi propaganda zilishajibiwa na aliekuwa Rais wa TEC Muhashamu Askofu Thadeus Ruaichi askofu wa Mwanza...Usikurupuke na hoja unafahamu kilichowafanya baraza la Maskofu TEC wamtimue?