Usilalamike tu humu baada ya 25 October.
Nnakukumbusha tu, usione vinaelea vimeundwa.
Sijapata kuona watu waovu wanoweza kuwalaghai Watanzania kama chadomo...
Siku moja, uanachama, siku moja mgombe urais, siku moja maarufu kuliko chadema nzima. Na huyo hyo ndiyo alikuwa "fisadi" wa miaka yote!
Hivi chadomo inasema nini katiba yao kuhusu hilo? au ndiyo inabadilika apendavyo Mbowe na Mkwewe Mtei?
Maana nnakumbuka mtu mmoja tajiri kuliko Lowasa CCM ilimtema alipotaka kugombea ubunge kupitia CCM kwa mara ya kwanza kwa kuwa alikuwa hajatimiza miaka 5 ndani ya CCM, unamkumbuka ni na huyo? au ulikuwa bado kichinchiri?
Hiyo ndiyo CCM, hatujali fedha tunajali utu na katiba.
Sasa hivi sizioni hata zile hadithi za Lowasa kukataliwa na Nyerere! Mmezisahau?