Apumzike tu huyo mzee, hiyo ndiyo demokrasia hata akiamua kuzungumza kwa sasa hakuna impact yoyote...na ameona Lipumba jinsi alivyopuuzwa...
kuwa mpole basi wewe mujahidina gani unapelekwa na mihemuko ivo ata mkisema nini Slaa amewadharau wewe na mwenyekiti wenu kwa tamaa zenu za hovyo
Kwanini hapokei simu? Bali anajibu sms tu, tena haraka. Huyo si Dr. Slaa.
Mabadiliko hayawezi kumsubiri mtu
kama hili ndo bao la mkono basi naliunga mkono.
Hawa watu wa suti nyeusi ni wakuangalia sana;
Inawezekana naye ameshapokea 3.5b/=.
........... Mpinzani aliyebaki kwa sasa ni Mbowe tu;tutaenda naye tu.
Hatutaki unafiki wala umbea tunasubiri kauli yake mwenyewe rasmi hivi mkimwona Dr.Slaa anazindua kampeni za uraisi mtaficha wapi nyuso zenu?
Kura zimepigwa lini ?Magufuli hafai akiwa waziri aliuza nyumba za serikali je akiwa raisi mtauzwa mpaka nyie majinga mnaoishabikia ccm
Mbowe anajua kusoma nyakati. Dr. Slaa ni MTU muhimu sana ila hajui kucheza na pyschologia ya watu wanataka nini nje.
Watu wengi tumeanza kumsahau Dr, tumeanza kumuona ni msaliti wa mabadiliko, hajui kucheza na muda. Mimi sina chama ila napenda CCM itoke.
Wanachama wa CCM humu wanamsifia Dr. Slaa hii inatuongezea chuki juu yake na akijichanganya katika kauli atazotoa hataamini reaction yake.
chanzo: nipashe
mytake: Kauli hizi za dr. Slaa zinazidi kuonesha namna gani baadhi ya viongozi na wasemaji wa chadema wanavyojribu kuwahadaa watanzania kuhusu sakata la mwanasiasa huyu tegemeo kabisa katika chadema. Sote tunaothamini mchango wa dr. Katika kukijenga chama hatuna budi sasa tuachane na habari za hawa watu na tusubiri kauli ya dr. Slaa mwenyewe.
Kauli ya dr. Slaa imekuja wakati tayari zilishatolewa taarifa mbalimbali na viongozi na wasemaji wa chadema kuhusiana na sakata hili, taarifa ambazo kwa kauli hii ya slaa ni wazi zilikuwa ni za kuwahadaa watanzania. Kauli hizo ni pamoja na:
1. Dr. Slaa ameamua kupmzika, akiwa tayari atajiunga nasi-freeman mbowe
2. Dr. Slaa kukutana na secretarieti ili kupanga mikakati ya ushindi ya ukawa-yeriko nyerere
3. Dr. Slaa atazindua kampeni za ukawa-john mnyika n.k