Dr. Slaa hatimaye aibuka

TataMadiba

JF-Expert Member
Feb 7, 2014
9,866
5,742

Slaa-13August2015.jpg

Wakati kukiwa na hali ya sintofahamu kuhusu msimamo halisi wa kisiasa wa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibroad Slaa, mwenyewe ameibuka na kusema ataweka kila kitu hadharani muda wowote kuanzia sasa.

Katika siku za karibuni, Dk. Slaa amekuwa gumzo kutokana na kutoonekana katika shughuli mbalimbali za chama hicho pamoja na mikutano muhimu inayoitishwa na vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).

Akizungumza na NIPASHE kwa njia ya simu jana, Dk. Slaa alisema kuna mambo mengi yanayozungumzwa juu yake ambayo hayana ukweli wowote na kwamba hivi karibuni atazungumza na kuweka hadharani kila kitu.

Hata hivyo, Dk. Slaa hakusema ni mambo gani yasiyo ya kweli yanayozungumzwa juu yake na wala hakuwa tayari kuweka wazi siku atakayoweka hadharani yale aliyoyahifadhi moyoni mwake.

Alipoulizwa kuhusu taarifa kuwa atashiriki uzinduzi wa kampeni za uchaguzi mkuu ujao, Dk. Slaa alisema hakuna ukweli wowote kuhusiana na jambo hilo na zaidi, akasisitiza kuwa pawe na subira kwani mambo yote yatajulikana siku atakapozungumza.

"Hakuna ukweli baba... sijui kwa nini watu wanapenda kutoa kauli za namna hiyo. Ukweli utajulikana tu ndani ya muda mfupi," alisema Dk. Slaa kupitia ujumbe mfupi alioutuma kwa namba ya simu yake ya kiganjani jana.

Awali, Dk. Slaa alipigiwa simu na Nipashe simu yake ya mkononi ikawa inaita muda mrefu bila kupokelewa, lakini baadaye alipotumiwa maswali kupitia ujumbe mfupi wa maneno alijibu haraka na kukanusha taarifa zilizodai kuwa atashiriki uzinduzi wa kampeni za uchaguzi mkuu zitakazoanza Agosti 22.

Swali jingine aliloulizwa ni sababu za yeye kuwa kimya na haonekani katika shughuli za kisiasa za chama chake na Ukawa unaoundwa pia na washirika wa Chadema; Chama cha Wananchi (CUF), NCCR-Mageuzi na NLD.

Hivi karibuni, Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika, alikaririwa akisema kuwa amewasiliana na Dk. Slaa na kwamba (Dk. Slaa) amekubali kushiriki uzinduzi wa kampeni za Ukawa kwenye jimbo la Kibamba.
Mnyika aliwaambia wanachama wa Chadema wa matawi ya kata ya Goba muda mfupi kabla ya kufanyika kura za maoni kumchagua mgombea wao wa udiwani katika eneo hilo.

"Dk. Slaa yupo mapumzikoni na nilizungumza naye kwa kirefu na aliniambia bado anapumzika, lakini atakuja kushiriki kampeni za chama Jimbo la Kibamba ambalo mimi nagombea ubunge," alisema Mnyika.

KIKAO KIZITO
Kauli ya Dk. Slaa inakuja huku kukiwa na juhudi kadhaa za kumshawishi mwanasiasa huyo kujiunga na Ukawa kabla ya kuanza kwa kampeni mwezi huu.

Mathalan, chanzo kimoja kimeiambia Nipashe kuwa Jumanne wiki hii, Dk. Slaa alifanya mkutano wa faragha na Mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila, kwa takriban saa tano.

Inaelezwa kuwa Kafulila alikuwa akijaribu kumshawishi Dk. Slaa kubadili msimamo wake ili Ukawa waweze kufanya kampeni wakiwa na umoja.

Kwa mujibu wa chanzo chetu, Dk. Slaa anadai Mwenyekiti wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe, aliwaburuza wenzake katika hatua za mwisho za kumkubali Lowassa kuhamia chama hicho na hatimaye kuwa mgombea wa urais.

Dk. Slaa pia anahisi kupuuzwa na wenzake hasa kwa kuzingatia mchango wake wa kukijenga chama hicho tangu mwaka 2010 alipogombea urais.

Alipoulizwa na Nipashe kuhusiana na taarifa kuwa alikutana na Dk. Slaa, Kafulila alikiri kufanya hivyo lakini akakataa kuzungumza kiundani juu ya kile kilichojiri kwa maelezo kuwa ni masuala ya faragha.

"Tuliongea kweli, ni mambo mazito lakini siyo ya kuweka hadharani maana ulikuwa mkutano wa faragha," alisema Kafulila.

Kwa muda mrefu sasa kumekuwa na hofu iliyotanda ndani ya Chadema na wananchi kwa ujumla kutokana na kutoonekana kwa Dk. Slaa katika matukio mawili makubwa ya kisiasa yanayohusu mustakabali wa chama hicho.

Dk. Slaa hakuonekana siku Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa, alipotangaza kujivua uanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) na kujiunga Chadema.

Kadhalika, Dk. Slaa hakuonekana wakati Lowassa alipofika kuchukua fomu ya kuwania urais kupitia chama hicho akitarajiwa kuwakilisha Umoja wa Kutetea Katiba ya Wananchi (Ukawa).

Pia hakuonekana katika mkutano mkuu wa Chadema wa kumchagua mgombea urais na mgombea mwenza na pia katika maandamano ya kumsindikiza Lowassa yaliyovutia maelfu ya wananchi Jumatatu wakati akienda kuchukua fomu za kuwania urais kwenye ofisi za Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec).
CHANZO: NIPASHE


Mytake: Kauli hizi za Dr. Slaa zinazidi kuonesha namna gani baadhi ya viongozi na wasemaji wa CHADEMA wanavyojribu kuwahadaa Watanzania kuhusu Sakata la Mwanasiasa huyu tegemeo kabisa katika CHADEMA. Sote tunaothamini mchango wa Dr. Katika kukijenga chama hatuna budi sasa tuachane na habari za hawa watu na tusubiri kauli ya Dr. Slaa mwenyewe.

Kauli ya Dr. Slaa imekuja wakati tayari zilishatolewa taarifa mbalimbali na viongozi na wasemaji wa Chadema kuhusiana na sakata hili, taarifa ambazo kwa kauli hii ya Slaa ni wazi zilikuwa ni za kuwahadaa watanzania. Kauli hizo ni pamoja na:

1. Dr. Slaa ameamua kupmzika, akiwa tayari atajiunga nasi-FREEMAN MBOWE

2. Dr. Slaa kukutana na Secretarieti ili kupanga mikakati ya ushindi ya UKAWA-YERIKO NYERERE

3. DR. SLAA atazindua Kampeni za UKAWA-JOHN MNYIKA n.k
 
Tusha choka Kauli za Dr kila siku atasema, mara natishiwa maisha nikiwa tayari nitazungumza na waandishi Daaaaaa!
Hivi hakuna habari nyingine mpya zaidi ya Slaa. Kwanini wasisubiri mpaka aitishe press ndio waje na habari zake kamili kila kukicha Slaa tumechoka
 
Dr s. Anamaadili na anajitambua..... Kama 2010 mbowe na wabunge wa chadema walitoka bungeni wakidai dr silaa alishinda uchaguzi ila akaibiwa kuraa kwanini safariii hiii asiweze kushindaaa amaa walitudanganyaaa au deal la billion 10 ni la ukweli kwa kamanda wa angaa. Mzee wa mabisinessss
 
Namshauri Dr. APUMZIKE TU.......NI FAIDA KUBWA KWAKE AU AJE BILA MASHARTI
 
Hatutaki unafiki wala umbea tunasubiri kauli yake mwenyewe rasmi hivi mkimwona Dr.Slaa anazindua kampeni za uraisi mtaficha wapi nyuso zenu?
Tuna imani na media zetu, au leo hii hauliamini tena gazeti la Nipashe? Lingekuwa limeamdika Uhuru labda mngesingizia kuwa ni la CCM. au Wambea unaozungumzia ni akina Mbowe, Mnyika na Yeriko Nyerere?
 
Back
Top Bottom