Dr. Slaa hatimaye aibuka

Dr. Slaa hatimaye aibuka

Tuna imani na media zetu, au leo hii hauliamini tena gazeti la Nipashe? Lingekuwa limeamdika Uhuru labda mngesingizia kuwa ni la CCM. au Wambea unaozungumzia ni akina Mbowe, Mnyika na Yeriko Nyerere?

Mabadiliko hayawezi kusubiri mtu, ukawa ndiyo habari ya mujini.
 
Katika kupinga mafisadi tupo pamoja na dr slaa kwenye kupinga mafisadi kama wewe fisadi.

Nenda akuweke ndani, habari ya mujini kwa sasa ni kuondoa mfumo ulioshindwa wa ccm na kuweka UKAWA, mengine baadaye
 
Magufuli atakuwa mwenyekiti wa kwanza wa ccm ambaye hatakuwa raisi mjiandae kisakolojia maccm kukabithi nchi kwa amani kwa UKAWA

Kweli mkuu. Nadhani ndio maana wameamua kutuwekea wagombea wawili, mmoja CCM mngine CHADEMA. Uwezekano wa huyu wa CHADEMA kushinda ni mkubwa sana. Kwa hiyo huyu walietuletea CHADEMA akiwa Rais, yule waliyemuweka CCM atakuwa Mwenyekiti wa chama - Hilo nadhani ndo linaitwa Bao la mkono.
 
CHANZO: NIPASHE


Mytake: Kauli hizi za Dr. Slaa zinazidi kuonesha namna gani baadhi ya viongozi na wasemaji wa CHADEMA wanavyojribu kuwahadaa Watanzania kuhusu Sakata la Mwanasiasa huyu tegemeo kabisa katika CHADEMA. Sote tunaothamini mchango wa Dr. Katika kukijenga chama hatuna budi sasa tuachane na habari za hawa watu na tusubiri kauli ya Dr. Slaa mwenyewe.

Kauli ya Dr. Slaa imekuja wakati tayari zilishatolewa taarifa mbalimbali na viongozi na wasemaji wa Chadema kuhusiana na sakata hili, taarifa ambazo kwa kauli hii ya Slaa ni wazi zilikuwa ni za kuwahadaa watanzania. Kauli hizo ni pamoja na:

1. Dr. Slaa ameamua kupmzika, akiwa tayari atajiunga nasi-FREEMAN MBOWE

2. Dr. Slaa kukutana na Secretarieti ili kupanga mikakati ya ushindi ya UKAWA-YERIKO NYERERE

3. DR. SLAA atazindua Kampeni za UKAWA-JOHN MNYIKA n.k

Mbona unashindwa kuitendea haki MY TAKE? Au ume claim?
 
Nikatibu anae lipwa mshahala mkubwa sawa na mbunge...ni katibu aliye jikopesha ruzuku ya chama, ni katibu aliye mpa mchumba wake cheo makao makuu ya chama

Ni Katibu aliyepaisha ruzuku ya Chadema kutoka Mil. 50 kwa mwaka hadi Bil. 1.2 kwa mwaka.
Ni Katibu aliyepelekea Chama kupewa Nafasi 25 za wabunge viti maalum...
Kwa nini tunakosa Shukurani?
Kwa nini tunakuwa wapofu?
Kwa nini tunashindwa kuutambua mchango wake:......?
Siku laana ikiikumba Chadema,, sijui.
 
Kweli mkuu. Nadhani ndio maana wameamua kutuwekea wagombea wawili, mmoja CCM mngine CHADEMA. Uwezekano wa huyu wa CHADEMA kushinda ni mkubwa sana. Kwa hiyo huyu walietuletea CHADEMA akiwa Rais, yule waliyemuweka CCM atakuwa Mwenyekiti wa chama - Hilo nadhani ndo linaitwa Bao la mkono.

Mmebaki kujifariji tu, ccm lazima ife kama KANU baada ya october
 
Ni Katibu aliyepaisha ruzuku ya Chadema kutoka Mil. 50 kwa mwaka hadi Bil. 1.2 kwa mwaka.
Ni Katibu aliyepelekea Chama kupewa Nafasi 25 za wabunge viti maalum...
Kwa nini tunakosa Shukurani?
Kwa nini tunakuwa wapofu?
Kwa nini tunashindwa kuutambua mchango wake:......?
Siku laana ikiikumba Chadema,, sijui.

Mabadiliko hayawezi kumsubiri mtu
 
Jamani, unajua chadema wana akili kuliko slaa. Kitendo cha slaa kupumzika tayari wameshatoa sumu yake. Hata leo akitangaza kujiondoa impact yake itakuwa ndogo kwani watu hawamfeel tena. Bora aondoke mapema tujenge chama na viongozi waliopo
 
hahahaha jamaa alikuwa anataka kugombea urais walijipitisha yeye na lipumba
 
Apumzike tu huyo mzee, hiyo ndiyo demokrasia hata akiamua kuzungumza kwa sasa hakuna impact yoyote...na ameona Lipumba jinsi alivyopuuzwa...

Slaa hahangaiki na Chadema, ila Chadema ndio wanaohangaika kumrudisha Slaa kwenye Chama.

Jiulize toka Slaa amekaa pembeni ni viongozi wangapi wa Chadema wamemfuata kuzungumza nae.

Anachofanya Slaa ni kukanusha propaganda za viongozi na wafuasi wa Chadema.

Alichokifanya Mbowe ni uhuni, wengi hatuipendi ccm lakini huwezi kusema tuitoe kwa gharama yoyote ile.

Mwacheni Dr.Slaa apumzike..... wenye kuamini kuhusu misingi na Demokrasia ya Chadema tumekaa pembeni tunawaangalia mnavyojikaanga wenyewe.

Hoja zote zilizoipa Chadema Umaarufu zimetupwa kampuni, sasa hivi hoja kuu ya Chadema ni Lowassa....Lowassa amekuwa kama mgombea binafsi ndani ya Chadema.
 
Mbowe ni moja ya wenyeviti wa kuiga hapa nchini,aligombea uraisi mara moja tu na akamuachia Slaa sasa maskini huyu mzee alivyo na tamaa😱😱

Katika historia yake, Dr Slaa hajawahi kuukamia uongozi.
 
Dr. Slaa, asicheze na nguvu ya UMMA...!!

Akienda against UKAWA, atakuwa ktk hali mbaya sana...i hope kashaisoma namba...!!

He is NOT SPECIAL...period..!!!

Slaa sio MAARUFU kuliko Lowassa....!!!

Slaa hata angegombea UKAWA, asingeshinda...hili nina uhakika 100%...!!!

Mbowe is very GENIUS POLITICIAN... he knows exactly upepo unavuma wapi... na historia ya nchi hii itamkumbuka MBOWE milele... anajua siasa, Dr. Slaa kama alidhania siasa ni DINI arudi kanisani...kapotea...!!! Alishagombea urais akashindwa vibaya...aache uchu wa madaraka...anakera sana sasa, anajiona mtakatifu...? kwa lipi..?

Mtu anasusa kama demu...tupa kuleeeeeeee, hafai kwa ukombozi...tupa kuleeeeeeee...arudi upadre...!!
 
Mara waliongea nae kwa njia ya simu,
Mara hakupokea simu,
Mara alijibu ujumbe mfupi wa maneno waiii..
Mie nikishaona habari inakauongouongo huwa siiamini hata kidogo
 
Kama Magufuli alivyo fisadi

We! siku hizi hilo neno hatulipendi kabisa ndani ya chama chetu, Hivi unakumbuka mara ya mwisho Mh Mbowe kulitaja hilo nenoilikuwa lini? We umeingia juzi tu BAVICHA umeshaanza kukiuka misingi mipya ya chama? tutakutimua!
 
Back
Top Bottom