Dr. Slaa amtembelea Gwajima TMJ hospital

Dr. Slaa amtembelea Gwajima TMJ hospital

Unajua watu wasomi huwa wanaweka mambo yanakuwa bayana kabisa. Ndugu karumbeta, nakuomba sana utusaidie kwa hili, tena nadhani halitakugharimu muda wako. Naomba uniandikie hapa kuwa kuwepo hospitali kwa Gwajima kumesababishwaje na Pengo. Bahati mbaya sana kila niliyemuuliza hakunijibu swali hili, labda wewe utanijibu, na utakuwa umejijengea heshima humu kwa kujibu hoja kwa hoja bayana.

Naam Jabulani,
Kwanza niseme tu kwamba, swali lako ni jepesi hivyo sitofikiri sana kulijibu humu ndani,

Pengo baada ya kwenda kinyume na makubaliano ya TEC na kuwasaliti maaskofu kwa kutoka povu jingi sana huku akiumia kuona wenzake wanasema pigeni kura ya HAPANA , ndipo Gwajima alipomkemea kwa bahati mbaya ulimi wa Gwajima ukakoleza chumvi ujumbe wake mzuri ukawa umemezwa na maneno uliyoyasikia.

Kwa mantic hiyo basi, polisi wakamtia misuko suko akapata mshituko ukampelekea kukimbizwa hospitali mpaka leo kalazwa.

Pengo asingeongelea lile tamko la maaskofu Gwajima angekuwa mzima na polisi wasingemhoji kitu chochote.
 
Sion ulichojibu maana na wewe pia umeshindwa uvumilivu unaoataka mwenzio awe nao. Wewe kama kweli muumini mbona unamuukumu mwenzio? Hata wewe kama ni kibanzi ungepashwa kuondoa boriti uliyo nayo. Ni kweli tumekwazika sisi kama Wakatoliki na tamshi la Baba Askofu Mkuu. Hatuwezi kunyamaza uku tukiumia maana husiposema nayo ni dhambi.
Nadhani ndugu unakoelekea unatumia zaidi jazba badala ya kufikiri. Kwanza siyo sahihi kutumia maoni yako kuwaseemea wakatoliki wote.
Ni aibu kujitambulisha kuwa wewe ni muumini wa dhehebu fulani alafu hapohapo unsashindwa mtihani mdogo tu wa kuwavumilia wengine na kuheshimu maoni yao hata kama hukupendezwa nayo!

Kwani kama ni kupiga kura ya HAPANA kwenye katiba mpya, wewe mwenyewe kwa utashi wako huwezi kufanya hivyo mpaka unasubiri Kadinali Pengo ndio akuambie? Achana na umasikini wa kifikra, kuwa mtu huru unaweza kufikiri na kuamua na siyo kuburuzwa kama gogo!
 
Ubinadamu kwanza mambo mengine baadae! Hata Pinda anatakiwa afike kwa Gwajima apate upako.
 
Mkuu hata kama unamchukia Gwajima kwa maneno makali dhidi ya Pengo kitu ambacho sikubaliani naye pia, lakini kwenye hili la afya ni vema kumjulia hali kwani uhai kwanza mambo mengine baadae. Slaa ameonesha upendo wa hali ya juu sana.

Mkuu ukiwa ccm unakuwa unatumikia matamko siyo ubinadamu
 
Tatizo Gwajima akiona macho ya misukule yake anajiona kama anahutubia dunia,haya mahojiano ya polisi sukari,presha,machozi na kupumua mfululizo kumempata.Nadhani akitoka itakuwa fundisho na atamuogopa mungu na hatojiita NABII tena!

Hivi ICC iko nchi gani vile?
 
Hongera prof.Lipumba kwa kumjulia hali kiongozi wa kiroho hakika umeonesha ubinadamu wa hali ya juu sanaaaa!!
 

Attachments

  • 1427726701652.jpg
    1427726701652.jpg
    18.1 KB · Views: 78
Nadhani ndugu unakoelekea unatumia zaidi jazba badala ya kufikiri. Kwanza siyo sahihi kutumia maoni yako kuwaseemea wakatoliki wote.
Ni aibu kujitambulisha kuwa wewe ni muumini wa dhehebu fulani alafu hapohapo unsashindwa mtihani mdogo tu wa kuwavumilia wengine na kuheshimu maoni yao hata kama hukupendezwa nayo!

Kwani kama ni kupiga kura ya HAPANA kwenye katiba mpya, wewe mwenyewe kwa utashi wako huwezi kufanya hivyo mpaka unasubiri Kadinali Pengo ndio akuambie? Achana na umasikini wa kifikra, kuwa mtu huru unaweza kufikiri na kuamua na siyo kuburuzwa kama gogo!

wewe unaonekana sio mkristo au kama ni mkristo hujui hata hiyo biblia inasema tufanyeje! watumishi wa Mungu wanajua na Mimi na wewe ukiacha husda unajua kilichotokea, kwamba marehemu akin a Sitta waliwapigisha kura, waliohija akina Sitta waliwapigisha kura etc. Kwa ukristo wako unadhani hao watumishi wa Mungu waseme hewala? biblia inasema ndio na iwe ndio na hapana na iwe hapana zaidi ya hapo ni Kitoka kwa shetani na ndicho walichokifanya akin a Sutta hapo hamna suala la utashi ni suala la uelewa na uamuzi,
 
Dr slaa ni tumaini la wanyonge! Nakwambia nilikuwa maeneo yale shughuli zilisimama kila mtu anataka kumshika Dr slaa mkono, kwa kuwa makachero wanaomlinda Gwajima na Makachero wa Dr Slaa walikutana kona moja ikawa ngumu lakini nimeamini Dr slaa anapendwa.

Dr slaa ni rais wa watanzania upende au laa
 
Gwajima analindwa na wanadamu huku akiwahubiria waumini wake kulindwa na Mungu! Maajabu haya. Hospitali anafuata nini wakati yeye anawaombea wagonjwa wanapona bila dawa, anaahidi kuwafufua wafu lakini yeye anakimbilia hospitali au alienda kuwaombea wagonjwa?

Mganga hajigangi
 
Back
Top Bottom