Nakupa mfano rahisi.
Wewe una shamba lako ambalo lilikuwa halijalimwa wala kupandwa zao lolote, na watu walikuwa wakipita katikati ya shamba lako kama njia ya mkato. Mwaka huu ukaamua ulime na kupanda mazao hivyo ukazungushia uzio ili watu wasikanyage mazao kwa mazoea ya kutumia ile njia ya mkato. Watu wakatafuta njia nyingine. Baadhi waliamua kutumia njia ndefu yenye usalama na baadhi waliamua wawe wanapita porini huko huko pembeni mwa shamba lako. Hapo pembeni mwa shamba lako kwa kuwa palikuwa hapatumiki kama njia, kulikuwa kumeota kichaka cha wastani. Matapeli wakagundua kuwa kuna watu wanatumia njia ile ya kichakani, nao wakaanza kuvizia wafanye utapeli. Siku moja wakati mtu mmoja akipita katika njia yenye kichaka, ghafla wakatokea matapeli wawili waliokuwa wamejificha kichakani. Wakamwambia wao ni walinzi wa ule msitu na hairuhusiwi mtu yeyote kupita pale. Wakamwamuru atoe fedha na mali zake za thamani alizokuwa nazo pale ili wamuache huru vinginevyo angepigwa. Aliposikia vitisho hivyo akapata hofu na kupoteza fahamu, akadondoka chini na bahati mbaya alidondokea jiwe, akapasuka sehemu ya kichwani na damu ikaanza kumvuja. Wale matapeli wakaona imeshakuwa ishu, wakakimbia na kumuacha akivuja damu nyingi bila msaada, hatimaye akapita mtu mwingine mwema akambeba na kumfikisha hospitali. Majeruhi anaendelea kutibiwa hadi sasa.
Katika mfano huu, nani alaumiwe kutokana na majeraha ya mgonjwa;
1. Ni mwenye shamba aliyelima na kuweka uzio na kusababisha majeruhi apite kichakani?
2. Ni majeruhi mwenyewe kwa kuwa aliona uvivu kupita njia ndefu lakini yenye usalama?
3. Ni matapeli waliomtolea vitisho kichakani?
4. Ni hela na mali alizohofia kupoteza?
Endeleaaa!