Dr. Slaa amtembelea Gwajima TMJ hospital

Dr. Slaa amtembelea Gwajima TMJ hospital

Weka picha

Sioni Kosa la Gwajima maana yeye alimkosoa Pengo na wale waliokuwa wakipotosha Mada kwamba wanaopinga Mahakama ya Kadhi ni Wakatoliki Pekee.Gwajima aliweka wazi kwamba wanaopinga MAHAKAMA YA KADHI ni Wakristo wote kupitia Tamko la Jukwaa la Wakristo.
 
HIvi Mtumishi wa Mungu na kiongozi anae dhubutu kunena kile kilicho moyoni mwake kwa wakati na siyo kujaza vidonda vya rohoni amedhurika na nini? Hii habari nimeisoma gazeti la Mtanzania la March 27,2015. Nilibaki nikitafakari nisipate jibu maana jana nilimsikia akitamka kuwa amekwenda polisi mwenyewe kutoa ufafanuzi wa kile alichotamka na hasa kufuatia wito wa Polisi kwa njia ya vyombo vya habari,mwenye kuujua ukweli tafadhali anipe mrejesho.
 
Dr slaa ni tumaini la wanyonge! Nakwambia nilikuwa maeneo yale shughuli zilisimama kila mtu anataka kumshika Dr slaa mkono, kwa kuwa makachero wanaomlinda Gwajima na Makachero wa Dr Slaa walikutana kona moja ikawa ngumu lakini nimeamini Dr slaa anapendwa.
Gwajima analindwa na wanadamu huku akiwahubiria waumini wake kulindwa na Mungu! Maajabu haya. Hospitali anafuata nini wakati yeye anawaombea wagonjwa wanapona bila dawa, anaahidi kuwafufua wafu lakini yeye anakimbilia hospitali au alienda kuwaombea wagonjwa?
 
Upande gani? Ule unaomtakia kifo mtu. Mauti na uzima uu mikononi mwa aliyemuumba. Dr. Silaa ameonesha upendo.

Mmesahau mlivyoshangilia maradhi ya kikwete? Unakumbuka kifo cha komba? Bavicha hamtaki kabisa kuguswa
 
mmnmmmmmm!!''!''!!!!!!!!!
Mungu ndiye anayejua zaidi. ila kila mmoja atakuja kutoa hesabu ya matendo yake mbele za bwn, maana hatujuui ukweli kama sisi ndio tinastahili kutoa hukumu.
 
Gwajima unavuka maji sio size yako ,Gwajima ni professional wa waimba kwaya wake tu
 
kitendo cha ngwajima kumtukana kadinali wa kanisa catolic,kimemskitisha sana pope fransis na ametaka sheria ifuate mkondo wake.
 
Kwani Gwajima kapatwa na nini hadi kawa hospitali??
attachment.php
 
Dr.Slaa alimtembelea hata Shekh Ponda baada ya kupigwa Risasi ya Bega.Huyu Jamaa ni Mkombozi na Kipenzi cha watanzania wanaonyanyasika.

Alipomtembelea Shekh Ponda hamkuleta taarifa, leo kamtembelea Gwajima basi tena hadi wengine mayowe..ohoo atakosa kura za upande wa pili. Kweli sisi tunaonewa jamani Mungu tusaidie
 
Unamsumbua askofu mwenza kwa jambo ambalo mlikuwa mmekubaliana tena kwa maandishi,hii ni aibu kwa kanisa. Waamini tunakushangaa.

Waumini gani wanaoshangaa? Labda wewe peke yako na hilo lilikuwa tamko la maaskofu sio waumini. Waumini tutaangalia ni nini tunataka, kupiga kura ya ndio au hapana linatuhusu sisi waumini sio maaskofu watuamulie pigeni kula ya hapana.

Mpaka nimefikia umri huu nafanya maamuzi mimi mwenyewe sio askofu anisurutishe, jamani Tanzania yetu ni ya demokrasia.
 
Gwajima analindwa na wanadamu huku akiwahubiria waumini wake kulindwa na Mungu! Maajabu haya. Hospitali anafuata nini wakati yeye anawaombea wagonjwa wanapona bila dawa, anaahidi kuwafufua wafu lakini yeye anakimbilia hospitali au alienda kuwaombea wagonjwa?

Mganga hajigangi ndugu.
 
Ni wasaa mzuri wa mwadhama polycarp cardinal pengo kumtembelea hosp na kumjulia hali na kutuonyesha ukomavu wa imani yake kwa kumsamehe askofu gwajima kwa kutokujua alitendalo.
Itategemea ratiba zake, ukizingatia hili ni juma Kuu. Hawezi kuacha kwenda kutoa sakramenti za kipaimara kwa waumini kibao just kwa ajili ya kumtembelea Gwajima
 
Asalaam aleykum !
Dr slaa ameonesha upendo wa hali ya juu sana alipomtembelea mtumishi wa bwana askofu Gwajima, hali ilikuwa shwari utulivu wa hali ya juu na ulinzi ukiwa umeimarishwa mara dufu.

Nimejaribu kudadisi afya ya Gwajima inaonekana inaendelea vema na baadae tutajulishwa zaidi akipata nafuu na kuruhusiwa. Makachero wanamlinda Gwajima ila kivutio ulikuwa ujio wa Dr Slaa shughuli zilisimama na wagonjwa wakapata nafuu nakusema yuko wapi Rais wa mioyo ya watu tumshike mkono!
Kwani nani hajui kama slaa anamtumia gwajima kwa malengo ya kisiasa?
 
Back
Top Bottom