Tutapambana na nyie mamluki mliomwagwa hapa kwa fujo na kila siku mnachonga IDs chungu nzima ili kuvuruga mijadala muhimu. Miaka ya nyuma kulipokuwa na wanachama wachache kulikuwa na kuheshimiana sana hata kama watu hawakubaliani, lakini tangu nyie mamluki wa buku 7 kuja hapa uwepo wenu umechangia sana kushusha viwango vya mijadala maana mkiona mjadala muhimu tu dhidi ya Serikali au CCM basi mtashuka hapa na IDs zenu 50 50 ili kuandika kejeli, kashfa na hata matusi ili tu kuvuruga mijadala kiasi ambacho baadhi ya wanachama wasiku nyingi kutotaka tena kuingia kuchangia lolote lile. Kwa taarifa yenu tumechoshwa na vitendo vyenu vya kukubali kutumika kama mamluki kwa ujira mdogo sana ili kuvuruga majadiliano muhimu hapa. Serikali na vyombo vyake vya dola itunyanyase na nyinyi mamluki hapa JF mtunyanyase na kuvuruga mijadala. Kama hamna cha maana cha kuandika zaidi ya kashfa, matusi na kejeli basi kaeni kimya vinginevyo tutapambana nanyi ili kuhakikisha JF inaendelea kuwa na hadhi na heshima yake kama miaka ya nyuma. Nyie wote wote akina Ritz, chama, scramble, Faiza Foxy, Bukyanandi, wabuyaga, Hamida, Utaifa kwanza, Zemarcopolo, lizaboni, leomimi na mambulula wengine wa buku 7 mnaochonga IDs mpya kutwa kucha ni sumu kali sana ya future ya JF. Kama hamuwezi kuandika cha maana zaidi ya pumba zenu basi tafuteni sehemu nyingine ya kuandika pumba zenu hapa tumezichoka zinatuharibia ukumbi wetu. Inawezekana kabisa kuwa na wanachama hata milioni na bado watu kuandika bila kashfa, kejeli au matusi. Habari ndiyo hiyo na kwa taarifa yako si kila mtu anataka vyeo vya kubabatizwa kama unavyodhani.