Omulangira
JF-Expert Member
- Apr 2, 2012
- 230
- 29
Wapendwa wana JF, nimebahatika kutembelea nchi ya Rwanda kwa siku tatu kuanzia tarehe 2/8/2013- 5/8/2013. Nikiwa kwenye ziara yangu nilibahatika kufika miji ya Nyakarambi, Ruchira, Gituku, Kibungo, Kabarondo, Kayonza na Rwamagana.
Nikiwa huko nimeweza kujifunza kuwa wanyarwanda wanamchukia sana Kikwete lakini wanawapenda sana watanzania. Nilibahatika kuongea na watu tofauti wakiwemo raia wa kawaida, viongozi na wanajeshi.
Nilichogundua ni kwamba kila nyarwanda hata aliyeko kijijini anataarifa kuhusu mgogoro wa Kagame na kikwete kwani baada ya kujua mimi ni mtanzania walianza kurusha shutuma kwa Kikwete alivyo mjinga kuingilia masuala ya Rwanda na kujikomba Umoja wa mataifa bila kwanza kumshirikisha kagame mwenyewe au Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Kwa upande wa raia wanadai wanaipenda sana Tanzania na watanzania wote isipokuwa wanamchukia Kikwete kwa tabia ya kupenda kujipendekeza kwa mataifa ya magharibi tofauti na ilivyokuwa enzi za mwalimu. Wanasema Kikete hakuwa na haja ya kuyaongelea masuala ya Rwanda akiwa Ethiopia badala yake angetumia busara hizo kwanza kukaa na kagame akamshauru wakiwa wawil au angetumia jumuiya ya Affrika masharikia kutoa ushauri wake.
Kwa upande wa viongozi wa serikari niliobahatika kuongea nao wanadai kitendo alichokifanya kikwete akiwa Ethopia hakikuwa cha kiungwana kwani kule hakukuwa sehemu muafaka ya kuongelea jambo hilo na wanaongeza kuwa wanaimani kuwa hayo hayakuwa mawazo ya watanzania bali yalikuwa mawazo ya Kikwete binafsi na hawawezi kuwacghukia watanzania wote kwa sababu ya kikwete.
Tukiwa kwenye burudani tunapata kalinya nilibahatika kuongea na Mwanajeshi mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Mbalanga, ambaye pia hakuwa tofauti sana na raia pamoja na viongozi wa serikali. Yeye alisema Kikwete hawataki wanyarwanda na wanyarwanda hawamtaki kikwete lakini wanajua watanzania wanawapenda sana wanyarwandwa hivyo uhususiano baina ya watanzania na wanyarwanda hauwezi kuvunjika kwa mtazamo wa mtu mmoja, Ingawa kitu kilichonishtua ni pale aliposema tumajenga kwa kasi sana bandari yetu ya nchi kavu pale Rusumo kwa ajili ya kuweka vifaa vya kujilinda na kweli pale Rusumo upande wa Rwanda wanajenga bandari kubwa ya nchi kavu. Mwanajeshi huyo haukuishia hapo alisema pamoja na hayo Presdent ameshatwambia tukae tayari kwa lolote na tunajua udhaifu wa watanzania. Tunaweza kuwa ni rahisi kuwagawa na kutumia udhaifu huo kuwapiga.
Mwisho nilimalizia Benako kituo kodogo cha magari makubwa kilichoko kilometer 15 kutoka mpakani ambapo nilifanikiwa kuongea na nyarwanda wa ngara mwenye uraia wa Tanzania.
Mama huyo alisema baada ya agizo la kikwete la kuwataka wahamiaji wote haramu aidha warudi kwao au watumie taratibu za kupata uraia, serikali yake imetumia nafasi hiyo kuwanyanyasa na kuwatishia kwani hata kama mtu una uraia wa Tanzania ulioupata kihalali miaka zaidi ya ishirini iliyopita unaambiwa wewe ni mhamiaji halamu, Hivyo unalazimishwa kutoa rushwa vunginevyo unaorodheshwa kama mkimbizi au mhamiaji halamu.
Nawasilisha
Nikiwa huko nimeweza kujifunza kuwa wanyarwanda wanamchukia sana Kikwete lakini wanawapenda sana watanzania. Nilibahatika kuongea na watu tofauti wakiwemo raia wa kawaida, viongozi na wanajeshi.
Nilichogundua ni kwamba kila nyarwanda hata aliyeko kijijini anataarifa kuhusu mgogoro wa Kagame na kikwete kwani baada ya kujua mimi ni mtanzania walianza kurusha shutuma kwa Kikwete alivyo mjinga kuingilia masuala ya Rwanda na kujikomba Umoja wa mataifa bila kwanza kumshirikisha kagame mwenyewe au Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Kwa upande wa raia wanadai wanaipenda sana Tanzania na watanzania wote isipokuwa wanamchukia Kikwete kwa tabia ya kupenda kujipendekeza kwa mataifa ya magharibi tofauti na ilivyokuwa enzi za mwalimu. Wanasema Kikete hakuwa na haja ya kuyaongelea masuala ya Rwanda akiwa Ethiopia badala yake angetumia busara hizo kwanza kukaa na kagame akamshauru wakiwa wawil au angetumia jumuiya ya Affrika masharikia kutoa ushauri wake.
Kwa upande wa viongozi wa serikari niliobahatika kuongea nao wanadai kitendo alichokifanya kikwete akiwa Ethopia hakikuwa cha kiungwana kwani kule hakukuwa sehemu muafaka ya kuongelea jambo hilo na wanaongeza kuwa wanaimani kuwa hayo hayakuwa mawazo ya watanzania bali yalikuwa mawazo ya Kikwete binafsi na hawawezi kuwacghukia watanzania wote kwa sababu ya kikwete.
Tukiwa kwenye burudani tunapata kalinya nilibahatika kuongea na Mwanajeshi mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Mbalanga, ambaye pia hakuwa tofauti sana na raia pamoja na viongozi wa serikali. Yeye alisema Kikwete hawataki wanyarwanda na wanyarwanda hawamtaki kikwete lakini wanajua watanzania wanawapenda sana wanyarwandwa hivyo uhususiano baina ya watanzania na wanyarwanda hauwezi kuvunjika kwa mtazamo wa mtu mmoja, Ingawa kitu kilichonishtua ni pale aliposema tumajenga kwa kasi sana bandari yetu ya nchi kavu pale Rusumo kwa ajili ya kuweka vifaa vya kujilinda na kweli pale Rusumo upande wa Rwanda wanajenga bandari kubwa ya nchi kavu. Mwanajeshi huyo haukuishia hapo alisema pamoja na hayo Presdent ameshatwambia tukae tayari kwa lolote na tunajua udhaifu wa watanzania. Tunaweza kuwa ni rahisi kuwagawa na kutumia udhaifu huo kuwapiga.
Mwisho nilimalizia Benako kituo kodogo cha magari makubwa kilichoko kilometer 15 kutoka mpakani ambapo nilifanikiwa kuongea na nyarwanda wa ngara mwenye uraia wa Tanzania.
Mama huyo alisema baada ya agizo la kikwete la kuwataka wahamiaji wote haramu aidha warudi kwao au watumie taratibu za kupata uraia, serikali yake imetumia nafasi hiyo kuwanyanyasa na kuwatishia kwani hata kama mtu una uraia wa Tanzania ulioupata kihalali miaka zaidi ya ishirini iliyopita unaambiwa wewe ni mhamiaji halamu, Hivyo unalazimishwa kutoa rushwa vunginevyo unaorodheshwa kama mkimbizi au mhamiaji halamu.
Nawasilisha